Tuesday, November 13, 2018

Tanzania kupokea Watalii 10,000 kutoka Shanghai mwaka 2019


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania kupokea Watalii 10,000 kutoka Shanghai mwaka 2019

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imesaini makubaliano na kampuni ya Touchroad International Group ya China kwa ajili ya kusafirisha watalii 10,000 kutoka jiji la Shanghai kutembelea Tanzania mwaka 2019 kwa kutumia ndege Maalum (chartered flights).

Makubaliano hayo yalisainiwa sambamba na mikutano ya kutangaza utalii katika soko la China- Tourism Roadshow katika miji mitano ya China iliyoanza katika jiji la Shanghai tarehe 12 Novemba 2018.

Mikutano hiyo ni matokeo ya jitihada za Ubalozi wa Tanzania nchini China kwa kushirikiana na TTB ambapo katika mkutano wa kwanza uliofunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki, washiriki mbalimbali zaidi ya 200 walijitokeza wakiwemo makampuni ya utalii (tour operators), mawakala wa usafirishaji (travel agents), mashirika ya ndege (airlines), na vyombo vya habari.

 Katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii, Bi. Devotha Mdachi alitoa mada maalum kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo nchini Tanzania pamoja na fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii.

Aidha, makampuni ya utalii kutoka Tanzania yalipata fursa ya kuelezea packages zao za utalii mahsusi kwa soko la China. 

Kadhalika, Shirika la Ndege la Tanzania lilitumia fursa hiyo kutangaza juu ya mpango wake wa kuanza safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi China katika mji wa Guangzhou mwezi Februari 2019.

Mikutano ya kutangaza utalii itaendelea kufanyika katika miji mingine ikiwa ni pamoja na Guangzhou tarehe 14 Novemba 2018, Hong Kong tarehe 16 Novemba 2018, Chengdu tarehe 19 Novemba 2018 na Beijing tarehe 20 Novemba 2018.

                                                        -Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma, 13 Novemba 2018
Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki akitoa neno la ukaribisho katika mkutano wa kutangaza vivutio vya utalii uliofanyika Shaghai, China tarehe 12 Novemba 2018.


Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bi. Devotha Mdachi, Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania, Jaji Mstaafu, Thomas Mihayo na viongozi wa kampuni ya Touchroad International Group wakiwa katika furaha baada ya kukamilika uwekaji saini wa makubaliano ambapo kampuni hiyo italeta watalii 10,000 nchini Tanzania mwaka 2019.

Wajumbe wameshika shuka la kimasai ambalo linaonesha utamaduni wa kabila hilo maarufu kutoka Tanzania.

Baadhi ya Washiriki wakiwemo viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, TTB na Balozi wa Tanzania nchini China wakiwa katika mkutano huo.

Monday, November 12, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU FURSA ZA MASOMO NCHINI PAKISTAN

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

FURSA ZA UFADHILI WA MAFUNZO KWA WATANZANIA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili wa masomo ya muda mrefu kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Pakistan.

Mafunzo hayo ambayo ni kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili yatafanyika nchini Pakistan kwa kipindi cha mwaka 2018/2019.

Maelezo zaidi kuhusu mafunzo haya yanapatikana kupitia http://www.hee.gov.pk/english/scholarshipsgrants/ARL-FS

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 15 Novemba, 2018.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
12 Novemba, 2018


Fly Your Ideas Students Competition


PRESS RELEASE

Fly Your Ideas Students Competition

The United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) in collaboration with the Airbus have prepared 6th Fly Your Ideas (FYI) Competition.

The competition needs the students across the world to develop new ideas using the latest digital technologies to create smart solutions for a safer, cleaner and better connected world aimed at contributing to an eco-efficient aviation industry of the future.

The competition is open to students who studying bachelor, masters or PHD degree in any academic discipline.

The competition will involve several rounds concluding with live final where up to 6 finalist teams will present their ideas to a jury of experts for a chance to win a share of €45,000.

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation call upon students around the country to participate in the competition which its registration deadline is on 16th November 2018 and the final will be in May-June 2019.

For more information about the Competition, Please visit: https://www.airbus-fyi.com

For inquiries, you can contact Rovani Sigamoney, Engineering Specialist of the capacity-building in Science and Engineering Section (email: r.sigamoney@unesco.org; tel +33145682237).   


Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dar es Salaam.
12 November  2018.

Saturday, November 10, 2018

Ubalozi wa Poland waadhimisha miaka 100 ya Uhuru

Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisoma hotuba katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Poland iliyofanyika kwenye makazi ya Balozi jijini Dar Es Salaam tarehe 09 Novemba 2018.

Mhe. Krzysztof Buzalski, Balozi wa Poland nchini akisoma hotuba katika hafla ya kuadhimisha miaka 100 ya uhuru wa Poland

Baadhi ya wageni mbalimbali walioshiriki hafla hiyo wakisikiliza kwa makini hotuba za viongozi

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi alikuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za kutimiza miaka 100 ya Uhuru wa Taifa la Poland. Sherehe hizo zilifanyika katika makazi ya Balozi wa Poland, Mhe. Balozi Krzysztof Buzalski yaliyopo Oystberbay, Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Novemba 2018
.
Katika Sherehe hizo, Naibu katibu Mkuu pamoja na mambo mengine alifafanua kuwa uhusiano baina ya Poland na Tanzania ni wa kihistoria na kuwa unaimarika siku hadi siku.

Pamoja na kuishukuru Poland kwa uwekezaji katika maeneo mbalimbali ikiwemo kilimo, amemuomba Balozi Buzalski, kuongeza jitihada katika kuvutia wawekezaji zaidi wa Poland kuja kuwekeza hapa nchini na kusaidia kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania nchini Poland.

Naibu Katibu Mkuu amemhakikishia Balozi wa Poland kuwa Wizara na Serikali kwa jumla itampa ushirikiano wakati wowote atakapohitaji ili kufanikisha malengo kwa manufaa ya mataifa yote mawili.

Friday, November 9, 2018

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO TOKA KWA MABALOZI WAPYA WA UAE, CANADA NA SPAIN IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mazungumzo na  Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Canada nchini Mhe. Pamela O'Donnel  kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mazungumzo na  Balozi wa Canada nchini Mhe. Pamela O'Donnel mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Spain nchini Mhe. Maria Pedros Carrtero  kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018  
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mazungumzo na  Balozi wa Spain nchini Mhe. Maria Pedros Carrtero mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho kwenye sherehe iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 8, 2018




Taarifa kwa Vyombo vya Habari kuhusu fursa za ufadhili wa masomo



FURSA ZA UFADHILI WA MAFUNZO

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili wa masomo ya muda mfupi kutoka Serikali ya Singapore kupitia Programu ya Ushirikiano ya nchi hiyo (SCP) na Serikali ya Israel kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Israel (MASHAV).

Maelekezo ya kalenda ya kozi ambazo zimetolewa chini ya ufadhili wa Programu ya Ushirikiano ya Singapore inapatikana kupitia tovuti yao ya http://www.scp.gov.sg.

Taarifa ya kina kuhusu nafasi za masomo chini ya ufadhili wa MASHAV inapatikana kupitia tovuti ya https: //mfa.gov.il/MFA/mashav/Courses/Pages/default.aspx.

Sehemu ya kalenda ya kozi chini ya ufadhili wa Programu ya Ushirikiano ya Singaporekwa mwaka 2018 na 2019 ni kama inavyoonesha kwenye jedwali hapa chini.


Na.
JINA LA KOZI
MUDA WA KOZI KUANZA
MUDA WA KOZI KUMALIZIKA
1.
Maritime Public Leaders Programme
12/11/2018
16/11/2018
2.
Public Private Partnerships for Infrastructure Financing
19/11/2018
23/11/2018
3.
Smart Nation: Strategy to Implementation
26/11/2018
30/11/2018
4.
Green Climate Financing
03/12/2018
07/12/2018
5.
Integrated Cyber Security Management
10/12/2018
14/12/2018
6.
Investment Promotion and Free Trade Management-FTAs
17/12/2018
21/12/2018
7.
Strategic Foresight: From Insight to Action
14/01/2019
18/01/2019
8.
International Law of the Sea
21/01/2019
25/01/2019
9.
Aviation Security Auditing Techniques and Developing Security Manuals
21/01/2019
25/01/2019
10.
Competitive and Sustainable Ports
28/01/2019
01/02/2019
11.
Climate Change and Emerging Threats
18/02/2019
22/02/2019
12.
Aircraft Accident Investigation Management
18/02/2019
22/02/2019
13.
Strategies to Promote Active Ageing
25/02/2019
01/03/2019
14.
International Dispute Resolution
04/03/2019
08/03/2019
15.
Aviation Incident Investigation: Effective Safety Risk Management
11/03/2019
15/03/2019
16.
Aeronautical Information Services/Management-AIS-AIM
18/03/2019
22/03/2019

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
09 Novemba, 2018