Friday, June 7, 2024

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CANADA AKUTANA NA MABALOZI WA AFRIKA

Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Melanie Joly akisalimiana na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Canada, Bw. Charles Faini wakati wa Mkutano kati yake na Mabalozi wa Afrika  uliofanyika hivi karibuni jijini Ottawa

Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Melanie Joly akizungumza na Mabalozi wa Afrika waliopo nchini humo uliofanyika hivi karibuni jijini Ottawa



 

Monday, June 3, 2024

MKUTANO WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI LINALOSHUGHULIKIA MASUALA YA EAC NA MIPANGO WAANZA ARUSHA


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Benjamini Mwesiga akichangia hoja kwenye Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha

Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango umeanza leo tarehe 3 Juni 2024 jijini Arusha.

Mkutano huo wa siku tano kuanzia Juni 3-7, 2024 umeanza kwa Ngazi ya Wataalam na na baadaye utafuatiwa na Ngazi ya Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 6 Juni 2024 na kuhitimishwa na Mkutano Ngazi ya Mawaziri ukaofanyika tarehe 7 Juni 2024. 

Mkutano huo katika Ngazi ya Wataalam pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili mapendekezo na taarifa mbalimbali za Jumuiya ikiwemo: Utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya; Mapendekezo ya kuhuisha Mipango ya Jumuiya na Mipango ya Nchi Wanachama; Taarifa ya Wakurugenzi wa Masuala ya Kazi kuhusu Ukamilishaji wa Rasimu Iliyorekebishwa ya Sera ya Uhamiaji ya Wafanyakazi wa Jumuiya.

Masuala mengine yatakayo jadiliwa ni pamoja na taratibu za Uanzishwaji wa Jukwaa la Mashauriano kuhusu Uhamaji katika Jumuiya ya Afrika Mashariki; Kuidhinisha Sera na Mkakati wa Pili wa Mawasiliano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki; na Kuidhinisha Kalenda ya Shughuli za Jumuiya kwa kipindi cha Julai – Desemba 2024.

Akifungua mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya forodha, biashara na fedha Bi. Annette Ssemuwemba amehimiza kuhusu umuhimu wa mkutano huo katika kusimamia utekelezaji na ufanisi wa sera na mipango ya Jumuiya ili kukidhi matarajio ya Wananchi. 

“Mtakumbuka kuwa takriban miaka miwili sasa hakupata fursa ya kufanya mkutano huu, kwa sababu hiyo kwa umoja wetu tutumie fura hii hadhimu kujadili na kutafuta majawabu yatakayotupa uelekeo mpya na sahihi wa kutekeleza na kusimamia kwa ufanisi sekta mbalimbali ikiwemo bishara na fedha kwa maendeleo ya Jumuiya yetu” Alieleza Bi. Annette Ssemuwemba

Vilevile mkutano huo unatarajiwa kufanya tathimini ya hatua iliyofikiwa kwenye utekelezaji wa masuala mbalimbali yaliyoamuliwa kwenye mikutano iliyopita ikiwemo mpango wa Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) na Uondoaji wa Vikwazo vya Biashara visivyokuwa vya kikodi,.

Mkutano huo umehudhuriwa na nchi zote Wanachama wa Jumuiya, huku ujumbe wa Tanzania ukijumuisha Mkurugenzi wa Mawasiliano Balozi Mindi Kasiga, Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka, na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Benjamini Mwesiga ambaye pia ni kiongozi wa ujumbe huo, wote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mkutano ukiendelea
Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga akifuatilia Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha
Mkutano ukiendelea
Meza kuu wakiongoza Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha

KAMATI YA BUNGE YA NUU YASISITIZA UWAJIBIKAJI


Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) imeisisitiza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi yake kwa wakati iliyo katika hatua mbalimbali.

 

Msisitizo huo umetolewa katika kikao cha ufuatiliaji kati ya kamati hiyo na Menejimenti ya Wizara kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma, tarehe 3 Juni 2024.

 

Akiwasilisha taarifa ya miradi ya ujenzi iliyo chini ya Wizara, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.), kwa niaba ya Mhe. January Makamba (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ameeleza kuwa, Wizara imewekeza nguvu kubwa katika kuhakikisha mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi ya Wizara lililopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma na jengo la mihadhara la Kituo cha Uhusiano cha Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim kilichopo Kurasini, jijini Dar es Salaam yanakamilika kwa wakati.

 

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya NUU na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mhe. Vita Kawawa (Mb.) alieleza juu ya umuhimu wa Wizara kushirikiana na Kamati hiyo katika kutekeleza majukumu yake.

 

Aidha, wajumbe wa Kamati wamepongeza jitihada zilizofanywa na Wizara katika utekelezaji wa miradi na wamesisitiza weledi katika usimamizi wa matumizi ya kifedha na mikataba ya miradi ya ujenzi.

 

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amewashukuru wajumbe wa Kamati ya NUU kwa kuendelea kuwa chachu katika usimamizi wa miradi inayotekelezwa na Wizara. Pia, amewaalika Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu unaotekelezwa katika eneo la Lakilaki, Arusha.

========================================

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mhe. Vita Kawawa (Mb.) akifungua kikao cha kamati yake na Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kilichofanyika tarehe 3 Juni, 2024 Bungeni, jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akiwasilisha taarifa ya Wizara ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi kwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama tarehe 3 Juni, 2024 Bungeni, jijini Dodoma.

Mhe. Byabato akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Dkt. Samwel Shelukindo (Kulia) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Eng. John Kiswaga (kati).

Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kikao.

Sehemu ya Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikifuatilia kikao.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikifuatilia kikao.

Kikao kikiendelea.


Friday, May 31, 2024

MAWAZIRI WA BIASHARA ,VIWANDA, FEDHA NA UWEKEZAJI WA EAC WAAZMIA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA

Picha ya pamoja kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Mawaziri wanaosimamia sekta ya Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa pamoja wamekubaliana kuendelea kuboresha ya mazingira ya biashara katika Jumuiya, huku wakitilia mkazo katika kuondoa vikwazo visivyo vya kodi, kurahisisha uvushaji wa mizigo mipakani, na kuimarisha utendaji wa miundombinu ya kusaidia biashara ikiwemo Vituo vya kutoa Huduma Pamoja Mpakani (OSBP). 

Vilevile wamekubaliana mapendekezo ya viwango mbalimbali vya ushuru wa forodha vitakavyo tumika katika mwaka wa fedha 2024/25 ambavyo vitachochea ukuaji wa uchumi wa nchi wanachama.

Azma hiyo imefikiwa leo tarehe 31 Mei 2024 kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Akizungumzia kuhusu azma hiyo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ameeleza kuwa hatua hiyo imefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ya kuwataka Watendaji na Viongozi walipo chini yao kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na kuondoa vikwazo vya kibiashara katika Jumuiya.

Waziri Nchemba aliongeza kutaja maeneo yaliyofanyiwa maboresho katika mkutano huo kuwa ni pamoja makubaliano kuhusu viwango vya tozo za barabara kwa Nchi Wanachama kutoka Dola za Marekani 16 hadi 10. 

Eneo jingine ni makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa Himaya Moja ya Forodha (Single Customs Territory) hasa kwa upande wa Tanzania na Kenya, ambapo Tanzania ilishaanza utelezaji wake. 

Jamhuri ya Kenya imeahidi kuanza kupitisha bidhaa za Tanzania katika mfumo wa himaya moja ya forodha mara moja na kufikia mwenzi Julai 2024, na kuleta wafanyakazi wake wa mamlaka ya forodha kwa ajili ya kuwezesha ukaguzi kabla mzigo haujaanza kuondoka ili mzigo usisimame mpakani. Hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano, usumbufu na upotevu wa mapato kwa Serikali na wasafirishaji wa bidhaa kati ya Tanzani na Kenya.

“Tanzania tumekuwa tukikabiliwa na tatizo la msongamano wa maroli katika mipaka yetu ikiwemo Namanga, Sirari, Holili na Hororo, hii imechangiwa na kuto kuwepo kwa maafisa wa KRA upande wa Tanzania ambao wangesaidia kufanyia kazi nyaraka za kupitisha mzigo mpakani kabla gari husika halijafika mpakani tofauti na ilivyo sasa, utelezaji wa ahadi hii itasaidia kutatua tatizo hili lililo tusumbua kwa muda mrefu” Alisema Nchemba. 

Katika hatua nyingine Waziri Nchemba kwenye mkutano huo amewa ongoza Mawaziri wenzake kuzindua mfumo mpya wa Kielektroniki wa masuala ya forodha unaolenga kuongeza ufanisi katika biashara kwa kuweka mazingira ya uwazi, uwajibikaji na hatimaye kuongeza mapato kwa Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya.

Mkutano huo wa Mawaziri ulitanguliwa na mkutano ngazi ya Wataalam uliofanyika tarehe 27 hadi 29 Mei 2024 na ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 30 Mei 2024. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifuatilia mkutano

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo umejumuisha Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ambaye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania, Mhe. Shariff Ali Shariff, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Kazi, Uchumi na Uwekezaji- Zanzibar, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud S. Kigahe.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akichangia jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya jijini Arusha.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato wakishirikishana jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.
Mawaziri Sekta ya Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Afrika Mashariki wakishuhudia uzinduzi wa mfumo mpya wa Kielektroniki wa masuala ya forodha unaolenga kuongeza ufanisi na mapato kwa Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud S. Kigahe wakifuatilia Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Benjamin Mwesiga wakifuatilia Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Shariff Ali Shariff (kushoto) akichangia jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya jijini Arusha.

TANZANIA KUJIIMARISHA KATIKA UKANDA WA IORA


Tanzania imeweka nia ya dhati ya kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika Jumuiya ya Nchi za Mwambao wa Bahari ya Hindi (IORA) kupitia uanachama wake kwenye Jumuiya hiyo. 


Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya hiyo uliofanyika kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dodoma na kuhitimishwa leo tarehe Mei 31, 2024.


Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao huku ujumbe wa Tanzania ukishiriki kutokea jijini Dodoma, Balozi Mussa amesema zipo fursa nyingi katika Jumuiya hiyo ambazo Tanzania ikijipanga itanufaika nazo ikiwemo utunzaji wa mazingira na rasilimali za bahari, ulinzi na usalama baharini, namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, uvuvi na utalii na kwamba wakati umefika sasa wa kuhakikisha wananchi wa Tanzania wananufaika kupitia jumuiya hiyo.


Aidha, kupitia mkutano huo Balozi Mussa amewasisitiza wajumbe wa mkutano waliotoka katika Taasisi, Wizara na Idara za Serikali kuendelea kuhakikisha maazimio mbalimbali yanayofikiwa kupitia Jumuiya hiyo yanatekelezwa kikamilifu ili kulinufaisha taifa kiuchumi na kijamii kwa ujumla.


“Ninawahimiza tuendelee kushirikiana ili taarifa za utekelezaji wa maazimio ya mkutano huu yaweze kufanyiwa kazi kwa haraka na kuiwezesha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kuratibu shughuli za kikanda na kimataifa kwa tija na maslahi mapana ya Nchi’’ alisema Balozi Mussa.


Kadhalika wakati wa Mkutano huo, Tanzania iliwasilisha pendekezo la Mradi kuhusu Ushirikishwaji wa Jamii za Pwani katika Utunzaji wa Rasilimali za Bahari za ukanda wa Pwani ambalo linalenga pamoja na mambo mengine kuzijengea uwezo jamii za Pwani kutunza rasilimali za bahari na kuibua fursa za kiuchumi zitakazowanufaisha na kuinua kipato cha wananchi wa ukanda wa Pwani.


Akiwasilisha pendekezo hilo, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Dkt. Saida Fundi amesema Chuo hicho kilikuja na wazo la kuandaa mradi huo baada ya kuona upo umuhimu mkubwa wa kuziwezesha jamii zilizopo kwenye mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi kunufaika na rasilimali zitokanazo na bahari.


Amesema pendekezo la mradi huo ambalo litahusisha Warsha itakayofanyika hapa nchini mwezi Oktoba 2024 na kuzihusisha nchi wanachama na wadau mbalimbali lina malengo mahsusi ikiwemo kuimarisha mtandao wa watumiaji wa rasilimali za bahari katika ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na kuzijengea uwezo jamii za ukanda wa Pwani ili kunufaika na fursa mbalimbali.


========================

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akichangia katika Mkutano  wa 26 wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Nchi za Mwambao wa Bahari ya Hindi (IORA) uliofanyika kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dodoma na kuhimishwa leo tarehe 31 Mei, 2024.

Balozi Mussa akijadili jambo na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Talha Waziri wakati wa mkutano wa 26 wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Nchi za Mwambao wa Bahari ya Hindi (IORA) uliofanyika kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dodoma na kuhitimishwa leo 31 Mei, 2024

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mkutano.

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania.



Mkutano ukiendelea.



UBALOZI WA TANZANIA NAMIBIA WARATIBU JUKWAA LA BIASHARA NA UWEKEZAJI

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

 

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi akizungumza



 

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar Bi. Fatma Mabrouk Khamis akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

 

Balozi wa Tanzania nchini Nambia Mheshimiwa Ceasar Waitara akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

 

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024

meza kuu katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa jukwaa hilo





Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia umeratibu na kushiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi,ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa hilo. 

Jukwaa hilo limejumuisha Sekta za Kilimo, Mifugo, Utalii, Biashara na Uwekezaji.





Thursday, May 30, 2024

MAKATIBU WAKUU SEKTA YA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE MAJI WA EAC WAKUTANA ARUSHA


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa Sita wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uvuvi na Ukuzaji Viumbe maji katika Ziwa Victoria la EAC kwa Ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika jijini Arusha. 

Mkutano wa Kawaida wa Sita wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uvuvi na Ukuzaji Viumbe maji katika Ziwa Victoria la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu umefanyika leo tarehe 30 Mei 2024 jijini Arusha.

Mkutano huo ulio ongozwa na Mwenyekiti wake Bi. Daisy Olyel Aciro ambaye pia ni Kamishna wa Uvuvi katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Uganda, umepokea na kujadili taarifa ya kikao cha Wataalam kilichofanyika kuanzia tarehe 27 hadi 29 Mei 2024, ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa Mawaziri wa Sekta hiyo utakaofanyika terehe 31 Mei 2024 jijini Arusha. 

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo Bi. Aciro ameeleza kuwa rasilimali za samaki na viumbe maji vimeendelea kuwa tegemeo kubwa la kiuchumi na chakula kwa wananchi wengi katika ukanda Afrika Mashariki, hivyo juhudi kubwa zinahitajika kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kustawi. 

Aliongeza kusema Baraza hilo kupitia Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) inaendelea kuweka mikakati madhubuti ya kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo ikiwemo kuweka mifumo ya usimazi endelevu wa rasilimali samaki na viumbe maji, mifumo ya uhifadhi na ufuatiliaji ili kuongeza tija zaidi. 

Vilevile Bi. Aciro ametoa wito kwa LVFO kuendelea kutumia fursa na nafasi iliyonayo kutafuta rasilimali fedha kutoka kwa wadau mbalimbali ili kuweza kutekeleza miradi mipya inayoibuliwa kwa manufaa ya Jumuiya. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ambaye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo, amehimiza kuhusu umuhimu wa Jumuiya na wadau kuendelea kuunganisha nguvu na kushirikiana katika kuendeleza rasilimali samaki na viumbe maji kufuatia mchango mkubwa wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa Jumuiya. 

Katika Mkutano huo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imewakilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka.

Katika hatua nyingine Uganda imekabidhi Uenyekiti wa Baraza hilo kwa Jamhuri ya Burundi ambayo itashika nafasi hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja. 
Picha ya pamoja
Kamishna wa Uvuvi katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Uganda Bi. Daisy Olyel Aciro akikabidhi Uenyekiti kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mazingira, Kilimo na Mifugo Bw. Emmanuel Niyungeko wa Burundi kwenye Mkutano wa Kawaida wa Sita wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uvuvi na Ukuzaji Viumbe maji katika Ziwa Victoria la EAC kwa Ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika jijini Arusha

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka akifuatilia Mkutano