Tuesday, September 4, 2012

Statement by Hon. Membe on SADC Electoral Observer Mission


  


SADC ELECTORAL OBSERVER MISSION
TO THE REPUBLIC OF ANGOLA

  
PRELIMINARY STATEMENT

BY


HON. BERNARD KAMILLIUS MEMBE (MP), MINISTER FOR FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

AND

HEAD OF SADC ELECTORAL OBSERVATION MISSION

TO THE

GENERAL ELECTIONS TO THE REPUBLIC OF ANGOLA,
 HELD ON 31ST AUGUST 2012



·         The National Electoral Commission of Angola (CNE);
·         Esteemed Leaders of the Political Parties;
·         Your Excellencies, Heads of Diplomatic Missions;
·         Members of the Diplomatic Corps;
·         Religious Leaders;
·         Members of Civil Society;
·         Esteemed Members of the various Observer Missions;
·         Esteemed Members of the Media;
·         Distinguished Guests;
·         Ladies and Gentlemen.

It is indeed an honour and pleasure to welcome you all to this important event, the presentation of the Southern African Development Community Electoral Observation Mission (SEOM) Preliminary Statement on the election process in the Republic of Angola.

1.         INTRODUCTION

The 31st August 2012 General Elections in the Republic of Angola follows the enactment of numerous election related legislations and notably the Constitution of 5th February 2010. Consequently and in line with the Southern African Development Community (SADC) Principles and Guidelines Governing Democratic Elections, the National Electoral Commission of the Republic of Angola invited SADC to observe its General Elections.

To this end, the Chairperson of the SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania, constituted the SEOM to the Republic of Angola and mandated the SADC Executive Secretary, Dr Tomáz Salomão to facilitate the administrative and logistical support for the Mission.

In His capacity as the Chairperson of the SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation,  His Excellency President Kikwete appointed me, Bernard Kamillius Membe, Minister for Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania to head the Mission which was officially launched on 20th  August 2012.

In terms of coordination of its activities, the SEOM’s Operations Centre was based here, at the Talatona Convention Hotel in Luanda, Angola. The Operations Centre was staffed with officials from the Troika of the Organ and the SADC Secretariat.

Your Excellencies, Ladies and Gentlemen, this Statement is therefore a preliminary view on the outcome of the SEOM’s observation of the electoral process in Angola. A final report in line with the Principles and Guidelines Governing Democratic Elections shall be released within thirty (30) days after the announcement of the election results.

THE ROLE OF THE SADC ELECTION OBSERVATION MISSION (SEOM)

In line with the mandate of the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections, the Mission was guided by the various electoral legal instruments of the Republic of Angola.

As I stated during the launch of the SEOM on 20 August 2012, the scope of observation would include among others, providing an analysis on the pre-electoral phase, polling day and post electoral period.

The SEOM most importantly sought to determine the existence of the following benchmarks as guided by Article 4 of the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections:

(i)         Constitutional and legal guarantees of freedoms and rights of citizens;
(ii)        Conducive environment for free, fair and peaceful elections;
(iii)       Non-discrimination in voters’ registration;
(iv)       Existence of an updated and accessible voters’ roll;
(v)        Timeous announcement of the election date;
(vi)       Where applicable, transparent funding of political parties based on the agreed threshold in accordance with the laws of the land;
(vii)      Neutral location of polling stations;
(viii)     Establishment of the mechanism for assisting the planning and deployment of electoral observation missions; and
(ix)       Counting of the votes at polling stations.

The SEOM in Angola as part of its electoral observation preparation undertook two (2) days refresher training that included briefings on country specific electoral process, held from 17 to 18 August 2012. The training covered the following areas:

(i)         SADC’s Role in Election Observations;
(ii)        Election Observation Methodology;
(iii)       Code of Conduct for Election Observers;
(iv)       International and Regional Election Observation Benchmarks; and
(v)        Understanding the electoral- political landscape of Angola.

During the launch of the SEOM on 20 August 2012, Observers were urged to adhere to the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections in the performance of their duties. Emphasis was placed on the following:

·         that the observers must comply with the laws and regulations of  the Republic of Angola;

·         that they should maintain strict impartiality in the conduct of their duties;

·         that  they will base all reports and conclusions on well documented, factual and verifiable evidence from a multiple number of credible sources as well as their own eye-witness accounts; and

·         that they should work harmoniously with each other and other observer missions/organisations in their areas of deployment.


DEPLOYMENT OF SEOM OBSERVERS

The SEOM constituted twenty (20) teams comprised of one hundred (100) observers drawn from the SADC Member States.  The SEOM included Members of Parliament, political and electoral experts, senior government officials and members of civil society in compliance with SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections relating to representation and gender balance.

Accordingly, the SEOM arrived in the Republic of Angola on 16 August 2012 in line with the provisions of the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections which stipulates that the SEOM should be deployed at least two weeks before the polling day.

Regrettably, the SEOM was unable to fully engage with the electoral process for at least two weeks before polling day as required by the above stated Article due to late accreditation. The late accreditation of the SEOM had therefore denied the fulfilment of the requirements for the assessment of the pre- election phase.

Notwithstanding the late accreditation, the SEOM deployed teams to the following provinces: Benguela, Bengo, Bie, Cabinda, Cuando Cubango, Cuanza Norte, Cuanza Sul, Huambo, Huila, Luanda, Malanje, Namibe and Uige.

CONSULTATIONS WITH STAKEHOLDERS

In discharging its duties, the SEOM interacted with various stakeholders in order to gather information on various aspects of the electoral process. With the limited period of observation from the time of accreditation, the SEOM could not engage with most of the relevant stakeholders to this election, however, the mission managed to consult with following stakeholders:

      i.        The CNE
    ii.        Political parties;
   iii.        SADC Ambassadors accredited to Angola;
   iv.        Secretary of State for External Relations;
    v.        Ministry of Territorial Administration;
   vi.        Ministry of Interior Affairs;
  vii.        National Police;
viii.        Youth Council of Angola;
   ix.        Confederation  of Trade Unions of Angola (UNTA); and
    x.        Observer Missions from the African Union (AU), Electoral Commissions Forum (ECF) of SADC Countries , Economic Community of Central African States (ECCAS),  International Conference of the Great Lakes Region (ICGLR), Community for Portuguese Speaking Countries (CPLP), the Council of Russian Federation (Senate),

These interactions though limited were sufficient to assist the SEOM to understand the prevailing electoral environment in Angola.

CONCERNS RAISED BY THE STAKEHOLDERS

While sharing views and consulting with the stakeholders, some expressed concerns on the electoral process which included inter alia:
              i.        Accreditation of party agents;
            ii.        Late start of the observation exercise;
           iii.        Lack of impartiality of the CNE;
           iv.        Accessibility and discrepancies in the voters’ roll;
            v.        Media coverage;
           vi.        Lack of consultation with the political parties on the voters roll;
          vii.        Incitement of electoral violence; and
        viii.        Transportation of ballot papers and transmission of election results.

In conducting its observation, the SEOM strived to pursue these concerns and sought clarity from the relevant stakeholders, however as a result of late accreditation, the SEOM could not engage systematically with CNE to confirm some of the above raised issues. The SEOM however noted the following responses provided by the CNE in its media briefings:

(i)            Accreditation of party agents
According to CNE the Political Parties submitted the Party Agents lists late and coupled with duplication of names in the submissions that required CNE to clear the lists in a limited timeframe.

However, CNE recognises that the timeframe provided in the law for the accreditation of party agents is not adequate to facilitate for the exercise.

(ii)          Lack of impartiality of the CNE
The political parties alleged that their concerns regarding the electoral process leading up to the election were not addressed by the CNE.
The SEOM observed that the CNE in its Media briefings addressed most issues of concern including the question of impartiality.

(iii)         Access to the voters’ roll
According to CNE, the voters roll was availed to the electoral stakeholders even though later than the period prescribed by the Electoral Act.
 
(iv)          Discrepancies in the voters’ roll
Some political parties presented to the SEOM that there were discrepancies in the actual number of voters that could not be substantiated due to lack of an updated national population database.

In the meeting with the Ministry of Territorial Administration, the SEOM was informed that the Country did not have an updated population database and the first ever national census since independence for the Republic of Angola will be undertaken in 2013.

(v)          Media coverage
The Electoral Law makes provision for equitable broadcasting time of contestants on State Owned Media. The SEOM learnt that during the campaign period, each party/coalition is entitled to ten (10) minutes free of public radio airtime daily and five (5) minutes of free public TV airtime daily.

However, some stakeholders alleged that the allocation of airtime was in favour of the ruling party.





(vi)         Lack of consultation with the political parties on the voters roll

The SEOM noted the complaint that the registration of the voters was previously conducted by the Ministry of Territorial Administration. The Ministry of Territorial Administration however handed over the mandate of registration of voters to CNE in line with the Amended Electoral Act of December 2011.

(vii)       Inciting electoral violence
The Ruling Party informed the SEOM that opposition parties conduct their campaigns based on hate speech targeting the political leadership, particularly the Presidential candidate of the ruling party.

(viii)      Transmission of election results
The political parties claimed lack of access to the process of transmission of results data. The parties submitted that some polling stations lacked INATEL network.

Regarding this concern, the Territorial Administration informed the SEOM that the INATEL network was functional and covered the entire Country.

(ix)         Late start of the observation exercise

The political parties were of the view that the election observation Missions should have commenced the activities earlier for an in depth coverage.


PRE – ELECTION PHASE

The SEOM observed that the pre-election phase was characterized by generally high levels of voter enthusiasm, notwithstanding a generally peaceful political atmosphere. Political parties were generally free to do their campaigning without any hindrance.

Moreover, the SEOM observed that law enforcement agencies were ready to respond to any threat or disruption of the peaceful electoral process.

POLLING PROCESS

The SEOM observed that on Election Day, most polling stations opened at the official time of 7am and closed at 7.30pm in the presence of security and party agents.
However the SEOM also noted that some polling stations opened very late and raised unease amongst the electorates. The polling stations that opened later than the official time had their closing time extended.
The SEOM observed that special arrangement was made for voters with special needs such as the elderly, people living with disabilities, expectant mothers among others. The SEOM observed the professionalism of the electoral staff.  

In some polling stations, the SEOM observed that some party agents were dressed in their party regalia and colours in contravention of the Electoral law that bars political propaganda within 250 metres of the polling stations.


COUNTING AND TALLYING OF RESULTS

Generally, the SEOM observed that counting of the votes at the polling stations began immediately after the closing of the polls and was conducted procedurally.  Equally, the SEOM observed instances where counting did not take place at some voting stations in line with the stipulated electoral regulation. One notable factor that led to this inconsistency was the misinterpretation of the regulation by the electoral staff deployed at the stations.

The SEOM also observed in the polling stations sampled that party agents, electoral officers, international observers witnessed and followed closely the counting of votes together with the electoral officials without any hindrance.

After the counting, the SEOM observed that electoral officers as well as party agents signed for the results in the presence of everybody and the agents for each candidate received a copy of the results.

BEST PRACTICES

In the course of observing the General Elections in the Republic of Angola, the SEOM noted that over and above, there was general adherence to some of the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections. The following best democratic practices and lessons were observed:

      i.        use of mobile smart technology to confirm voter’s registration;

    ii.        use of short messaging service (sms) to confirm and remind the voters of  their respective voting stations;

   iii.        Orderly layout of polling streams facilitated for smooth and speedy voting process;
   iv.        An impressive voter turn-out across the population spectrum which signifies civic commitment of the citizens;

    v.        Adherence to Electoral regulation for the provision of priority to elderly, physically disabled and pregnant voters in the voting process;

   vi.        High political tolerance under which the Angolan people exercised their voting rights;

  vii.        Use of indelible ink and translucent ballot boxes; and

viii.        The provision of the equitable party funding by the Government.


SADC ELECTORAL OBSERVATION MISSION (SEOM) RECOMMENDATIONS

Upon completion of the observation exercise, the SEOM has the following recommendations for the people of Angola and the electoral authorities:

(i)            Timely accreditation
To enhance the credibility of the electoral process, SEOM wishes to urge the CNE to facilitate accreditation at the earliest arrival of the observation missions in compliance with Article 4.1.10 of the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections.

(ii)          Deployment of observers
The SEOM urges CNE to consider the harmonisation and alignment of the Electoral Laws of the Republic of Angola with the SADC Principles and Guidelines Governing Democratic Elections and allow a degree of flexibility on the part of the SEOM to determine its deployment plan.




CONCLUSIONS
The SEOM is of the opinion that although some of the concerns raised are pertinent, they are nevertheless not of such magnitude as to affect the credibility of the overall electoral process.

In line with SADC principles and Guidelines Governing Democratic Elections and Electoral Laws of Angola, the SEOM urges all political parties and candidates to respect the will of the people of the Republic of Angola and any grievances that may arise from this election should be pursued in line with the relevant law of the Republic of Angola.

Therefore, on behalf of the Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania and on behalf of the entire SADC family, I wish to heartily congratulate the people of Angola for holding credible, peaceful and transparent general elections on 31 August 2012. This is a valuable contribution to the consolidation of democracy and political stability, not only in the Republic of Angola but in the SADC region as a whole.


Thank you for your attention.

Monday, September 3, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo jioni Jumatatu, 3 Agosti, 2012 amempokea Rais wa Msumbiji  Mheshimiwa Armando Emilio Guebuza ambaye pia ni Mwenyekiti wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika(SADC).
Rais Guebuza amefika nchini kuhudhuria kikao cha siku moja cha nchi tatu ambazo zinaunda Chombo cha Siasa, Ulinzi na Usalama cha SADC (TROIKA) kinachofanyika jijini Dar-Es-Salaam, kesho tarehe 4 Septemba, 2012, chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria ni Rais Jacob Zuma wa Afrika  Kusini, Rais Hifikepunye  Pohamba wa Namibia ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Troika na Rais Joseph Kabila wa DRC.
Hiki ni kikao cha kwanza tangu Tanzania ichaguliwe kushika nafasi ya uenyekiti wa TROIKA katika Kikao cha Wakuu wa Nchi za SADC kilichofanyika tarehe 16 -17 Agosti, 2012  nchini Msumbiji.
Nchi tatu za TROIKA ni Afrika Kusini, Namibia na Tanzania, ambaye ndiye Mwenyekiti.
Kikao hiki ni cha mpango kazi wa TROIKA kwa mwaka mzima wa uenyekiti wa Tanzania.
Miongoni mwa masuala yatakayojadiliwa katika mpango kazi huo na ambayo Tanzania imerithi kutoka kamati iliyomaliza muda wake  ni pamoja na mgogoro wa Mashariki ya Congo DRC, mchakato wa Katiba na Uchaguzi wa Zimbabwe na suala la Madagascar.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu – Dar-Es-Salaam
3 Septemba, 2012

Sunday, September 2, 2012

Vote Tanzania for 7 Natural Wonders of Africa


Please click below link to vote:   http://sevennaturalwonders.org/category/africa/



(Mt. Kilimanjaro)

Recently, a new competition has been launched for the public to vote for entries into the list of new SEVEN NATURAL WONDERS OF AFRICA. The competition is conducted via the Website, http://sevennaturalwonders.org involving twelve (12) tourist attraction sites on the African continent. Tanzania is the only blessed country with most entries in the list: these are Mount Kilimanjaro (top photo), the Ngorongoro Crater (center photo), and the Serengeti National Park (bottom photo).  All Tanzanians and the world at large are sensitized to vote for these three attraction sites.


(Ngorongoro Crater)

In order to ease the voting process, the Tanzania Tourist Board (TTB) has requested the organizers to establish a special website http://sevennaturalwonders.org/tanzania/ which will direct participants to submit their entries via e-mail vote@sevennaturalwonders.org, bearing the subject title “TANZANIA,” listing the names of the three entries. The competition also allows participants to propose not more than four other tourist attractions which they deem fit for inclusion in the list of the SEVEN NATURAL WONDERS of Africa.


(The Serengeti National Park)

This competition will provide yet another opportunity for Tanzania to identify herself and educate the rest of the world that Mt. Kilimanjaro, the highest mountain in Africa; the Serengeti Park, famous for the annual spectacular animal migration; and the Ngorongoro Crater, the natural and cultural World Heritage Site; are all located in Tanzania.

Seize this opportunity and vote for the entry of all the Tanzania tourist attractions into the list of the NEW SEVEN NATURAL WONDERS OF AFRICA.
For more information on Tanzania’s tourist attractions visit:  www.tanzaniatourism.go.tz

Angola's ruling party leads in early results


(CNN) -- Angola's ruling party held a big lead Saturday as the southern African nation posted preliminary results in its benchmark national election.

With almost 70% of the vote counted, the Popular Movement for the Liberation of Angola (MPLA) had almost 75% of the vote.

Friday's election was only Angola's third since it gained independence from Portugal in 1975.

Under the terms of a constitution approved in 2010, the leader of the party that wins Friday's parliamentary vote will automatically become Angola's president.

President Jose Eduardo dos Santos, who has held power since 1979, had been widely expected to retain the top spot as the head of the MPLA.

After independence, Angola suffered through 27 years of civil war. Friday's election were widely viewed as an indicator of the country's progress after a decade of peace.

Elections in 1992 were abandoned midway and led to an outbreak of further violence. The MPLA won the 2008 parliamentary vote with a landslide 82%.

It appeared from early results that the MPLA was headed for another comfortable victory.

The main opposition party and a former civil war enemy of the MPLA, the National Union for the Total Independence of Angola (UNITA), is among the nine political parties and coalitions contesting the election for 220 members of the National Assembly.

UNITA won about 18% of the vote in the preliminary results. Seven other parties split up the rest of the vote.

UNITA has alleged fraud in previous elections and again voiced concerns about apparent irregularities in election campaigning this time around. But on Saturday, spokesman Alcides Sakala said the party would recognize the election results, the official Angola News Agency reported.


Source:  www.cnn.com


Saturday, September 1, 2012

Hotuba ya Rais Kikwete ya mwisho wa mwezi Agosti 2012






HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 AGOSTI, 2012

Utangulizi
Ndugu Wananchi;
          Kila mwisho wa mwezi nimekuwa nazungumza na taifa kuhusu masuala mbalimbali muhimu kwa taifa letu na watu wake.  Leo nina mambo mawili ya kuzungumza nanyi.  Lakini, kama ilivyo mazoea yetu hatuna budi kwanza tumshukuru Mwenyezi Mungu, muumba wetu, kwa kutujaalia baraka zake, za uhai na uzima na kutuwezesha kuwasiliana leo tarehe 31 Agosti, 2012.

Ndugu Wananchi;
          Jambo la kwanza ninalotaka kuzungumzia leo ni zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lililoanza tarehe 26 Agosti, 2012 ambalo linatarajiwa kumalizika tarehe 01 Septemba, 2012.  Mtakumbuka kuwa tarehe 25 Agosti, 2012 nilizungumza nanyi na kuwaomba mjitokeze kwa wingi na muwape ushirikiano unaostahili Makarani wa Sensa watakapopita majumbani mwenu kutekekeza wajibu wao.  Tumebakisha siku moja kufikia kilele cha sehemu ya kwanza ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.

           Napenda kuwashukuru kwa dhati Watanzania wenzangu wote kwa kujitokeza kwa wingi kuhesabiwa.  Mpaka sasa mwelekeo ni mzuri na ugumu ulioonekana kuwepo pale mwanzoni uliendelea kupungua siku hadi siku kadri utekelezaji wa zoezi ulivyokuwa unaendelea.  Kwa mwenendo huu nina matumaini makubwa kuwa Sensa ya mwaka huu itakuwa na mafanikio mazuri.

Ndugu Wananchi; 
          Napenda kutumia nafasi hii kutoa wito kwa wale wote ambao hawajahesabiwa wafanye hivyo. Naomba waitumie siku moja iliyosalia yaani tarehe 1 Septemba, 2012 kufanya hivyo.  Aidha, namuomba Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi Kuu ya Takwimu ya Serikali ya Muungano na Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhakikisha kuwa kasoro zo zote zilizopo mahali po pote zinatafutiwa ufumbuzi ili mambo yakamilike bila upungufu wowote.

Ndugu Wananchi;
          Baada ya kazi ya Makarani wa Sensa kuhesabu watu kufikia kilele chake, tarehe 2 Septemba, 2012, linaanza zoezi la kuwashughulikia wale ndugu zetu ambao watakuwa bado hawajahesabiwa.  Itakuwepo fursa ya siku saba kwa watu hao kuhesabiwa.  Watatakiwa wao wenyewe kupeleka taarifa zao kwa Wenyeviti wao wa Serikali za Mitaa au Vijiji.  Taarifa hizo zitafikishwa kwa Kamishna wa Sensa kwa ajili ya kujumuishwa.  Baada ya muda huo kwisha, zoezi la kuhesabu watu litakuwa limefika mwisho.  Yule ambaye atakuwa hakutumia fursa hizo mbili atakuwa amekosa kuingizwa katika hesabu ya Watanzania ya mwaka 2012.  Napenda kuwasihi ndugu zangu, Watanzania wenzangu kutumia siku ya tarehe 1 Septemba, 2012  kuhesabiwa na kama hapana budi basi tumia fursa ya kupeleka taarifa zako kwa Mwenyekiti wako wa Mtaa au Kijiji katika siku saba zinazofuatia siku hiyo ili nawe ujumuishwe.

Ndugu Wananchi;
          Baada ya kazi ya kuhesabu watu kwa namna zote mbili kufikia mwisho, itaanza kazi ya uchambuzi na kuunganisha takwimu na taarifa zilizokusanywa.  Kazi hiyo ni muhimu na ni kubwa hivyo inahitaji umakini na uangalifu wa hali ya juu sana, kwani ikikosewa zoezi zima la Sensa litaingia dosari.  Nafarijika kuhakikishiwa na Viongozi wa Sensa na Wakuu wa Idara za Takwimu za Serikali zetu mbili, kwamba wanatambua ukweli huo na wajibu wao.  Wameniarifu kwamba kama mambo yatakwenda kama ilivyopangwa, matokeo ya awali ya Sensa ya Watu na Makazi kuhusu idadi ya watu na jinsia zao yatatolewa mwishoni mwa mwaka huu. Taarifa nyingine zitafuata baadaye.  Narejea kuwasihi Watanzania wenzangu kuwapa nafasi wataalamu wetu wafanye kazi yao kwa ufanisi ili tupate matokeo yaliyo sahihi.

Mpaka na Malawi
Ndugu Wananchi;
          Jambo la pili ninalotaka kuzungumza nanyi leo ni kuhusu mpaka baina ya Tanzania na Malawi katika Ziwa Nyasa.  Kama mjuavyo, kwa miaka mingi nchi zetu mbili zinatofautiana kuhusu wapi hasa mpaka uwe.  Sisi, Tanzania, tunasema mpaka upo katikati ya ziwa wakati wenzetu wa Malawi wanasema upo kwenye ufukwe wa ziwa upande wa Tanzania.  Kwa maneno mengine wanasema ziwa lote ni mali ya nchi yao. 

Utata kuhusu mpaka wetu katika Ziwa Nyasa haujaanza leo.  Ulikuwepo tangu wakati nchi zetu mbili zikiwa bado zinatawaliwa na wakoloni na kuendelea baada ya Uhuru wa nchi zetu mpaka sasa.  Jambo kubwa lililo tofauti na jipya ni kwamba hivi sasa, nchi zetu mbili zimeamua kukaa mezani na tunalizungumza suala hilo.


Chimbuko la Mzozo

Ndugu Wananchi;
Chimbuko la mzozo wa mpaka uliopo sasa, baina ya nchi zetu mbili jirani, rafiki na ambazo watu wake ni ndugu, ni makubaliano baina ya Waingereza na Wajerumani kuhusu mpaka baina ya nchi zetu yaliyofanywa tarehe 1 Julai, 1890.  Makubaliano hayo yajulikanayo kama Mkataba wa Heligoland, (The Anglo-Germany Heligoland Treaty) yalitiwa saini kule Berlin, nchini Ujerumani baina ya Waingereza na Wajerumani.  Wakoloni hao walikubaliana kuhusu mipaka baina ya makoloni yao na baina yao na wakoloni wengine waliopakana nao.  Kwetu sisi hayo ndiyo makubaliano yaliyoweka mipaka ya Tanganyika na ile ya Zanzibar na majirani zake.  Kwa upande wa Ziwa Nyasa, Waingereza na Wajerumani walikubaliana kuwa mpaka uwe kwenye ufukwe wa nchi yetu.  Kwa maana hiyo ziwa lote likapewa nchi ya Malawi.  Kwa upande wa Mto Songwe mpaka ulikuwa ufukweni upande wa Malawi kwa maana hiyo mto wote ukawa upande wa Tanzania.

Ndugu Wananchi;
Katika kipengele cha Sita (Article VI) cha Mkataba huo, wakoloni hao walikubaliana kufanya marekebisho ya mpaka mahali popote kama itakuwa ni lazima kufanya hivyo, kulingana na mazingira na hali halisi ya mahali hapo.  Kwa mujibu wa kutekeleza matakwa ya kipengele hicho mwaka 1898 Tume ya Mipaka iliundwa.  Ilianzia kazi katika Mto Songwe kuhakiki mpaka baina ya nchi yetu na Malawi. Tume ilikubaliana kuhamisha mpaka kutoka ufukweni mwa Mto Songwe upande wa Malawi na kuwa katikati ya mto.  Baada ya uhakiki katika eneo hilo kukamilika, mwaka 1901 mkataba mpya ulisainiwa kuhusu mpaka huo.

Tume iliendelea na kazi yake katika Ziwa Tanganyika na kuhamisha mpaka kutoka ufukweni hadi katikati ya ziwa na mkataba mpya kusainiwa mwaka 1910.  Tume iliendelea katika ziwa Jipe ambapo mpaka ulihamishwa pia hadi katikati ya ziwa.

Ndugu Wananchi;
Bahati mbaya Tume hiyo haikufanikiwa kufanya uhakiki wa mpaka katika Ziwa Nyasa kutokana na kutokea kwa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia kati ya mwaka 1914 - 1918.  Kama tunavyokumbuka, Waingereza na Wajerumani waligeuka kuwa maadui na kupigana hata hapa nchini.  Baada ya vita hivyo na Ujerumani kushindwa, Baraza la Umoja wa Mataifa (The League of Nations) liliikabidhi Uingereza udhamini wa Tanganyika. Hivyo, Uingereza ikawa inatawala Malawi na Tanganyika. 

Ndugu Wananchi; 
Wakati Tume ya Uingereza na Ujerumani ilipokuwa imekufa, Tume ya Mipaka kati ya Uingereza na Ureno iliendelea na kazi.  Matokeo yake, mwaka 1954, Uingereza na Ureno zilitengua mkataba wao wa mwaka 1891 ulioweka mpaka wa Ziwa Nyasa katika ufukwe wa mashariki ya Ziwa, yaani kwenye ufukwe wa Msumbiji, na kuuhamishia katikati ya ziwa.

Ndugu Wananchi;
Jambo la kustaajabisha ni kuwa, Waingereza walioona umuhimu na busara ya kurekebisha mpaka kati ya Malawi na Msumbiji, hawakuona umuhimu wa kufanya hivyo kati ya nchi yetu na Malawi.  Inashangaza, kwa sababu wakati huo Uingereza ilikuwa mtawala wa nchi zetu mbili hivyo kazi ya marekebisho ingekuwa rahisi, lakini hawakufanya hivyo.  Na, baya zaidi ni kuwa  hata pale watu wa nchi yetu walipotaka kupatiwa ufafanuzi na kutaka ukweli uwekwe wazi kuhusu mpaka hawakusikilizwa.  Watu walitaka ufafanuzi kwa sababu inasemekana kati ya mwaka 1925 na 1938, taarifa ya Uingereza kwa Umoja wa Mataifa ziliweka mpaka katikati ya ziwa.  Lakini, kuanzia mwaka 1948 mpaka ukawekwa tena ufukweni. 

Ndugu Wananchi;
Mwaka 1959, 1960 na 1962, suala la mpaka wa Malawi lilijitokeza tena na kujadiliwa na Bunge la Tanganyika, wakati ule lilijulikana kuwa Baraza la Kutunga Sheria, (Legislative Council – LEGCO).  Hoja ya Wabunge wa Tanganyika ilikuwa kwamba mpaka kuwekwa kwenye ufukwe wetu kunawanyima wananchi wa Tanganyika wanaoishi kando kando ya ziwa haki yao ya msingi ya kutumia maji kwa kunywa, kuoga, kuvua samaki na kupata manufaa mengine yatokanayo na ziwa bila ya kuomba ridhaa ya Serikali ya Koloni la Nyasaland kama Malawi ilivyokuwa inajulikana wakati ule.  Hoja iliyotolewa ilikuwa kwamba Serikali ya Tanganyika ijadiliane na Serikali ya Nyasaland kupitia Serikali ya Malkia wa Uingereza ili ufumbuzi upatikane.  Wakoloni hawakujali na wala hakuna hatua zilizochukuliwa mpaka Tanganyika ikapata uhuru wake tarehe 9 Desemba, 1961 na Malawi kupata uhuru wake mwaka 1964.


Juhudi za Kubadili Mpaka wa Ziwa Nyasa Baada ya Uhuru

Ndugu Wananchi;
          Wakati tulipopata Uhuru mwaka 1961, mjadala kuhusu mpaka wa Tanganyika na Malawi uliendelea Bungeni, ambapo ilitolewa hoja kwamba zifanyike juhudi za makusudi za kuanzisha na kuendeleza mazungumzo ya kurekebisha mpaka huo kwa manufaa ya wananchi wote wanaoishi pembezoni mwa ziwa.  Iliamuliwa kwamba tusubiri mpaka wenzetu wa Malawi wapate uhuru ili yafanyike mazungumzo baina ya nchi mbili huru.  Kulijengeka matumaini kuwa mambo yangekuwa rahisi.  Bahati mbaya haikuwa hivyo na kwamba mambo yakageuka na kuwa magumu na ya uhasama.  Miaka mitatu baada ya Malawi kupata Uhuru wake (1964), kunako tarehe 3 Januari 1967, Serikali ya Tanzania iliandika barua kwa Serikali ya Malawi kuelezea tatizo la mpaka wa ziwani na kupendekeza nchi zetu mbili zizungumze na kulitafutia ufumbuzi. 

Ndugu Wananchi;
Bahati nzuri tarehe 24 Januari, 1967, Serikali ya Malawi ikajibu kukiri kupokea barua hiyo na kuahidi kuwa itatoa majibu baada ya muda si mrefu.  Hata hivyo, tarehe 27 Juni, 1967, Rais Kamuzu Banda akilihutubia Bunge la Malawi, alikataa maombi ya Tanzania.  Alisema hayana msingi na alidai kuwa kihistoria Songea, Mbeya na Njombe ni sehemu ya Malawi.  Hivyo basi, mazungumzo yakafa. 

Tanzania haikukata tamaa.  Alipochaguliwa Rais wa Pili wa Malawi, Mheshimiwa Bakili Muluzi, juhudi zilifanyika lakini nazo hazikufika mbali. Bahati nzuri tarehe 9 Juni, 2005, Rais wa Tatu wa Malawi, Mheshimiwa Bingu Wa Mutharika, ambaye sasa ni marehemu, alimuandikia barua aliyekuwa Rais wa nchi yetu wakati ule, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kushauri nchi zetu zifanye mazungumzo kuhusu mpaka wa ziwani.  Alipendekeza iundwe Tume ya Pamoja itakayojumuisha Mawaziri na Wataalamu kutoka nchi zetu mbili.  Tume hiyo itatoa mapendekezo kwa Marais wa nchi zetu mbili ambayo yatakuwa msingi wa majadiliano baina yao.  Alisisitiza umuhimu wa kulipatia ufumbuzi suala hilo. 

Ndugu Wananchi;
Kwa kuwa ilikuwa kipindi cha mpito kuelekea kuchaguliwa Serikali ya Awamu ya Nne, Rais Benjamin Mkapa hakuwahi kuishughulikia barua hiyo. Nilipoletewa barua hiyo nikaijibu kukubali ushauri na mapendekezo yake.  Aidha, nilipendekeza Wizara na Idara zipi za Serikali zetu zishirikishwe katika Tume hiyo.  Bahati nzuri Rais wa Malawi alikubali mapendekezo yangu pamoja na lile la kwamba Malawi waitishe mkutano wa kwanza wa Tume hiyo.

Ndugu Wananchi;
Mpaka sasa mikutano mitatu ya Tume ya Pamoja imeshafanyika, wa kwanza ulifanyika tarehe 8 – 10 Septemba, 2010.  Mkutano wa pili ukafanyika tarehe 27 – 28 Julai, 2012 hapa Dar es Salaam na wa tatu ukafanyika Mzuzu na Lilongwe tarehe 20 – 27 Agosti, 2012. Hatua kadhaa zimepigwa lakini bado muafaka haujapatikana kwa maana ya madai yetu ya kutaka mpaka uwe katikati ya ziwa na madai yao kuwa mpaka ubaki ufukweni kwetu kama  ilivyo kwenye Mkataba wa Heligoland wa Julai 1, 1890.  Hoja ya wenzetu ni kuwa huo ndiyo mpaka tuliorithi wakati wa uhuru.  Wanataka tuthibitishe hivyo na kwamba tuzingatie kauli ya OAU ya kuheshimu mipaka tuliyorithi kwa wakoloni. Wananukuu kauli ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere akisisitiza hoja hiyo katika mkutano wa OAU mwaka 1963. 


Hoja za Msingi za Kutaka Mpaka Uwe Katikati ya Ziwa

Ndugu Wananchi;
Kwa upande wetu tumekuwa na hoja kadhaa za kutaka mpaka uwe katikati ya ziwa.  Ya msingi kabisa ni ukweli kwamba Mkataba wa Heligoland umekosewa kwa kuamua kuwanyima wananchi wa Tanzania wanaoishi ufukweni mwa ziwa haki yao ya msingi ya kutumia maji na rasilimali zilizomo katika Ziwa Nyasa.  Zipo sababu kadhaa kwa upande wetu kudai hivyo.  Mojawapo ni sheria ya kimataifa inayoelekeza kwamba popote kwenye maji ya asili kama vile ziwa na mito iliyopo kati ya nchi mbili mpaka huwa katikati.  Ndiyo utaratibu unaotumika duniani kote, na mifano iko tele.  Kwa nini iwe tofauti katika ziwa Nyasa na kwa upande wa Tanzania tu wakati kwa upande wa Msumbiji mpaka upo katikati ya ziwa?

Ndugu Wananchi; 
Kwa upande wa Mto Songwe, mpaka baina ya nchi zetu mbili upo katikati.  Iweje hapa kanuni hiyo itambulike na kuheshimiwa lakini isiwe hivyo ziwani?  Kama nilivyoeleza awali, mwanzoni Mto Songwe wote ulikuwa umewekwa upande wetu, lakini Tume ya Mipaka iliyoundwa mwaka 1898 ilifanya marekebisho na kuweka mpaka katikati ya mto.  Kama nilivyokwishagusia kwenye ziwa hilo hilo la Nyasa kwa upande wa Msumbiji mwaka 1954 mkataba wa mwaka 1891 ulioipa Malawi ziwa lote ulirekebishwa na mpaka kuwekwa katikati.  Kwa nini isifanyike hivyo hivyo kwa upande wa Tanzania?  Hivi hasa ni kipi ambacho wenzetu wa Msumbiji walichotuzidi na kustahili kupata haki yao ya msingi ya kumiliki na kutumia maji ya Ziwa Nyasa ambacho sisi Tanzania tumepungukiwa?

Ndugu Wananchi;
Maji ni zawadi ya Mwenyezi Mungu kwa wanadamu wake, waitumie kwa uhai na maendeleo yao.  Iweje leo, kwa watu wanaoishi pembeni mwa ziwa hilo hilo wengine wapewe na wengine wanyimwe haki ya kulimiliki na kulitumia? Kwa nini wanyimwe haki ya kunufaika na zawadi hiyo? Hivi kauli ya wakoloni waliokaa Berlin ya kusema fulani apate na fulani asipate inatosha?  Hivi kweli ni rahisi kiasi hicho? 

Mpaka wa kwenye maji ni tofauti na ule wa nchi kavu.  Huu una rasilimali ambayo huwezi kuamua kumnyima mwanadamu mwingine anayeishi pembeni yake kwa vile haina badala yake.  Unapowaambia watu wa Mbamba Bay, Liuli, Lituhi, Manda, Ngonga, Matema, Mwaya, Itungi na wengineo waishio kando ya ziwa kuwa maji hayo si yao bali ni mali ya Malawi hawakuelewi na watakushangaa sana.  Watadhani umechanganyikiwa kwani tangu waumbwe wamekuwepo hapo wanamiliki na kutumia maji ya Ziwa.  Unataka wafanyeje?  Waende Malawi kuomba kibali cha kuyatumia?   Wao watakuuliza swali moja tu “hivi hao wenzao wanaoishi ng’ambo ya pili wamewazidi nini katika ubinadamu wao hata wapewe maji yote na wao wanyimwe?”

Ndugu Wananchi;
Kwa maana halisi ya Mkataba wa Heligoland tangu tarehe 1 Julai, 1890, wananchi wa upande wa Tanzania wamekuwa wanakunywa, kuoga, kuvua samaki na kusafiri katika maji ya Ziwa yasiyokuwa yao bali ya nchi nyingine.  Na kwa kuwa wamekuwa wanafanya hivyo bila ya kupata kibali cha Malawi wamekuwa wanaiba maji na samaki wa Malawi na kusafiri isivyo halali katika nchi ya watu.  Jambo hili haliingii akilini hata kidogo.  Ndiyo maana tunadai haki yetu stahili.

Ndugu Wananchi;
 Na hiyo pia, ndiyo maana,  busara na hekima ya Sheria ya Kimataifa kuhusu mpaka wa kwenye maji kuwa katikati.  Sheria hii inazingatia hali halisi ya maisha ya jamii inayozunguka ziwa ambayo imekuwa inalitegemea maisha yao yote kwa shughuli zao za kuwapatia uhai na maendeleo yao.  Haiwezekani kuwatenganisha watu waishio kando ya Ziwa Nyasa kumiliki na kutumia maji hayo na rasilimali zake.  Hawataelewa wala kukubali kuambiwa kuwa wanatumia maji na rasilimali za ziwani  kwa hisani ya nchi ya Malawi. 

Kwa watu waliokuwepo tangu Mungu anawaumba wao na wenzao wa ng’ambo ya pili, siyo sawa na siyo haki hata kidogo kuwafanyia hivyo.  Kwe kweli ni unyanyasaji wa hali ya juu.  Ndiyo maana wazee wetu walidai suala hili liwekwe sawa wakati wa ukoloni, kabla na baada ya Uhuru.  Na ndiyo maana na sisi tunafuata nyayo zao katika madai haya ya haki.

Ndugu Wananchi; 
Kuna mambo mengine mawili ambayo yanatufanya tudai haki ya kumiliki na kutumia Ziwa Nyasa.  La kwanza ni ule ukweli kwamba mito mingi ya Tanzania nayo inachangia kujaza maji katika ziwa.  Iweje leo maji yanayojaza ziwa ni jambo jema, lakini yakishaingia ziwani, ziwa hilo si mali yao wenye mito hiyo tena na wakiyatumia wanaiba mali ya watu wengine.    Hivi kweli ndivyo wanavyostahili kufanyiwa watu wanaotunza vyanzo vya mito hiyo na kuruhusu maji yake kutiririka na kuingia ziwani? 

Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ni kwamba mpaka wa Tanzania na Malawi kuwa ufukweni kunafanya ukubwa wa nchi zetu kuwa haujulikani kwa uhakika.  Unategemea mabadiliko kutokana na  kujaa na kupungua kwa maji ziwani.  Kunafanya mpaka wa nchi kuwa hautabiriki na unaweza kuwa tatizo siku moja mbele ya safari.  Isitoshe kuwa na nchi isiyojulikana ukubwa wake nalo ni tatizo la aina yake.  Ndiyo maana mpaka kuwa katikati ya ziwa ni bora zaidi.

Ndugu Wananchi;
Kama nilivyokwishasema, chimbuko la mzozo huu ni mkataba wa Heligoland ambao umepanda mbegu ya fitina baina ya nchi zetu.  Bahati mbaya sana Tume ya Mipaka haikumaliza kazi ya kuhakiki mipaka yote ya nchi yetu na majirani zake kufuatia kuzuka kwa Vita Kuu ya Kwanza mwaka 1914.  Ujerumani ikashindwa vita na koloni lake kuwa sehemu ya himaya ya Uingereza.  Bahati mbaya kwetu Waingereza waliotawala nchi zetu mbili tangu 1918 hawakuchukua hatua za kurekebisha mpaka kabla ya uhuru wa nchi zetu.  Ni maoni yetu kuwa nchi zetu sasa zifanye kile ambacho hakikufanywa na Tume ya Mipaka ya wakoloni – Waingereza na Wajerumani.  Tukifanye sisi wenyewe kama nchi mbili huru kwa njia ya mazungumzo. 

Bahati mbaya majaribio ya mwaka 1967 hayakufanikiwa.  Bahati nzuri kufuatia uamuzi wa kijasiri wa marehemu Rais Bingu wa Mutharika nchi zetu sasa zinazungumza.  Bado hatujafikia muafaka kuhusu kurekebisha mpaka na huenda ikatuwia vigumu kufikia muafaka.  Jambo linaloleta faraja, hata hivyo, ni kuwa sote wawili tumekubaliana kuwa tutafute mtu wa kutusuluhisha. 

Ndugu Wananchi;
Hayo ndiyo matokeo ya mazungumzo ya Tume yetu ya pamoja tangu ngazi ya Wataalamu, Makatibu Wakuu mpaka kwa Mawaziri, katika vikao vya Mzuzu na Lilongwe kati ya tarehe 20 – 27 Agosti, 2012.  Katika mkutano wao wa tarehe 27 Agosti, 2012 Mawaziri husika wa nchi zetu chini ya uongozi wa pamoja wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mheshimiwa Ephraim Chiume na mwenzake wa Tanzania, Mheshimiwa Bernard Membe, wameafiki mapendekezo hayo.  Aidha, wamekubaliana kuwa pande zote mbili wakutane tena Dar es Salaam kati ya tarehe 10 – 15 Septemba, 2012 kukubaliana juu ya usuluhishi wa aina gani unafaa.

Ndugu Wananchi;
Mtakubaliana nami kuwa tumepiga hatua muhimu kuelekea kwenye kupata ufumbuzi wa kudumu wa suala hili.  Hata hivyo, bado safari ni ndefu na huenda ikawa na magumu mengi.  Maombi yangu kwa viongozi na wananchi wa Tanzania na Malawi ni kuendelea kuunga mkono jitihada hizi.  Tuwaunge mkono wataalamu na Mawaziri wetu ili wafanikishe vizuri jukumu lao.  Tuzingatie na kuheshimu walichokubaliana Lilongwe kuwa viongozi na wananchi wa nchi zetu wajiepushe na kutoa kauli au kufanya vitendo vinavyoweza kuchafua hali ya hewa, kuleta uchochezi na kuathiri majadiliano yanayoendelea. 

Nawasihi Watanzania wenzangu kuzingatia ushauri na rai hiyo ya Mawaziri na wataalamu wetu, ili kuwe na mazingira mazuri ya mazungumzo na kuwezesha mzozo huu kuisha kwa amani na kirafiki. 


Hitimisho

Ndugu Wananchi;
Kabla ya kumaliza hotuba yangu, napenda kusisitiza kuwa si makusudio yangu wala ya Serikali yetu kutafuta suluhisho la suala hili kwa nguvu ya kijeshi.  Nawahakikishia Watanzania wenzangu kuwa hatuko vitani na Malawi na wala hakuna maandalizi ya vita dhidi ya jirani zetu hawa kwa sababu ya mzozo wetu wa mpaka katika Ziwa.  Ondoeni hofu na endeleeni na shughuli zenu za ujenzi wa taifa letu kama kawaida. 

Nilimhakikishia hivyo Rais wa Malawi, Mheshimiwa Joyce Banda nilipokutana naye Maputo, Msumbiji tarehe 18 Agosti, 2012.  Tanzania haina mpango wa kuingia vitani na Malawi.  Mimi na wenzangu Serikalini tunaona kuwa fursa tuliyoitafuta miaka mingi ya kukaa na ndugu zetu Malawi kuzungumzia suala hili lenye maslahi kwetu sote sasa tumeipata.  Hatuna budi kuitumia ipasavyo.  Naamini, tukifanya hivyo, inaweza kutufikisha pale tunapopataka. Ni muhimu, kwa ajili hiyo kwa pande zetu mbili, kuipa fursa ya mazungumzo nafasi ya kuendelea bila ya vikwazo visivyokuwa vya lazima. 


Ndugu Wananchi;
          Kwa sababu hiyo basi, napenda kutumia nafasi hii kuwasihi ndugu zetu wa vyombo vya habari na wanasiasa wenzangu tuepuke kauli au matendo yatakayovuruga mazungumzo na kuchochea uhasama kati ya nchi zetu mbili jirani na rafiki.  Kuna manufaa makubwa ya kumaliza mzozo wetu kwa njia ya mazungumzo kuliko kwa njia ya vita.  Kufikiria sasa kutumia njia nyinginezo hasa za nguvu za kujeshi, si wakati wake muafaka.  Aidha, tukitumia njia ya vita, badala ya kuwa tumepata suluhisho inaweza kuwa ndiyo mwanzo wa mgogoro mpana zaidi.  Tuendelee kuwaunga mkono wawakilishi wetu katika Tume yetu ya pamoja.  Naahidi, Serikali itakuwa inawapa taarifa kadri mazungumzo yetu na wenzetu wa Malawi yatakavyokuwa yanaendelea.  Nina hakika tutamaliza salama.



Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika!
Asanteni kwa Kunisikiliza




Muda wa Sensa waongezwa


(picha na Aron Msigwa - Maelezo)



Na : Tiganya Vincent-  MAELEZO-Dar es salaam


Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imeongeza mbele tarehe za kumaliza kazi ya sensa ya watu na makazi hadi Jumamosi ya tarehe 8 septemba mwaka huu ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi aliyebaki anahesabiwa.

Kauli hiyo imetolewa leo(jana) na Kamishna wa Sensa kutoka NBS Hajjat Amina Mrisho Said wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu masuala mbalimbali yaliyohusu kazi nzima ya kuhesabu watu na makazi inaendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Alisema kuwa ni vema wananchi ambao hawajafikiwa na makarani wa sensa watoe taarifa katika Ofisi za Serikali za Mitaa au Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa ajili ya kuhesabiwa.

Hajjat Amina alisema taarifa zinazotakiwa ni pamoja na taarifa za wanakaya waliolala katika kaya yao usiku wa kuamkia tarehe 26 Agosti mwaka huu.

Alitoa wito kwa wale ambao hawajaandikishwa hadi hivi sasa wanatakiwa watume taarifa kwa namba 2122724, 0754583415, 2129622 ,0713335429,0713574622 na 0713312699 .

Hajjat aliongeza kuwa katika taarifa watakazopeleka ni vema wakaeleza mitaa au kijiji au kitongoji gani walipo ili iwe rahisi kwa NBS kutambua karani mhusika na kumwelekeza afanye kazi hiyo.

Aidha , Kamishna hiyo alisema kuwa malipo ya makarani yalishafanyika kwa awamu ya kwanza kulingana na mkataba na wanataraji kuwalipa awamu ya pili mara baada ya kazi zao kuhakikiwa na wasimamizi wao.

Aliongeza kuwa kwa wasimamizi watalipwa baada ya kazi zao kukamilika na kuhakikiwa na waratibu katika ngazi za wilaya.

Kuhusu malipo ya wenyeviti wa vijiji , vitongoji na mitaa ,alisema fedha zao wasishapelekwa siku nyingi na maelekezo ya namna ya kuzigawa yalipelekwa kwa waratibu wa Sensa wa mikoa na wilaya ambao walipaswa kuwa wameshalipa ili kuepuka manung’uniko.

Katika hatua nyingine Kamishna wa Sensa huyo amewaonya kuwa Karani yoyote atakayechakachua taarifa na ikathibitika hilo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria na kuongeza kuwa NBS inafuatilia taarifa kutoka Dodoma eneo la Kisasa kuwa kuna Karani amekwenda kwenye kaya lakini alikuwa haulizi maswali.

Wakati huo huo Kamishna wa Sensa Hajjat Amina alisema kuwa wale viongozi wengi waliokuwa wakiwa hamasisha wenzao wasihesabiwe , wamehesababiwa kwa hiari baada ya kutoa ushirikiano wa kutosha ikiwemo kuacha taarifa muhimu zilizohitajiwa ikiwemo zile zilihitajika katika madodoso. Kwa wale ambao hawakuwakuta waliweka alama maalum ili wawarudie mara ya pili.