Friday, November 16, 2012

Minister Membe hosts EU-Tanzania Political Dialogue


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation in brief talks with H.E. Filiberto Cerian Sebregondi, Ambassador and Head of European Union Delegation in Tanzania.  Hon. Membe hosted the political dialogue the European Union delegation in Tanzania that was held today at Karimjee Hall in Dar es Salaam.


Hon. Membe (right) opens a political dialogue meeting between Tanzania-European Union.  Left is H.E. Filiberto Cerian Sebregondi, Ambassador and Head of the European Union Delegation in Tanzania during the Tanzania-EU political dialogue held today in Karimjee Hall in Dar es Salaam.


A Political Dialogue between Tanzania-EU in session at Karimjee Hall in Dar es Salaam.

 
H.E. Mrs. Diane Corner, the British High Commissioner to the United Republic of Tanzania gives her comments on recent events of religious demonstrations in Tanzania Mainland and Zanzibar.  Left is H.E. Johnny Flento, Ambassador of Denmark to the United Republic of Tanzania.


Some of the delegates from both Tanzania and EU during the political dialogue.


Other Tanzania delegates that included Ministry of Transport and Ministry of Home Affairs.


Delegation from Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.


A group photo of Hon. Bernard K. Membe (MP) (2nd right- front), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation together with H.E. Filiberto Cerian Sebregondi (3rd left-front), Ambassador and Head of European Union and EU Ambassadors to Tanzania.   


Hon. Membe thanks H.E. Ambassador Segregondi for his cooperation during the political dialogue which he hosted today at Karimjee Hall in Dar es Salaam.


Minister Membe hosts EU-Tanzania
Political Dialogue

By TAGIE DAISY MWAKAWAGO

The Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard K. Membe (MP) today met with the European Union Delegation in Tanzania led by H.E. Ambassador Filiberto Cerian Sebregondi in an annual political dialogue at Karimjee Hall in Dar es Salaam.
The meeting derived from an agreement between Tanzania and European Union, known as Cotonou Agreement.  In that Agreement both parties agreed to conduct a political dialogue by exchanging information, assess areas of concerns such as human rights, democratic principles, rule of law, good governance and formulate cooperative strategies to promote peace and democratic stability.
During their meeting, Ambassador Sebregondi raised concerns of recent events that took place in respect to religious demonstration both in Tanzania Mainland and Zanzibar, which some of them led to attacks on churches in Zanzibar by group called “UAMSHO”.  Also, the EU wanted to discuss issue of freedom of press and its infringement such as the killing of one reporter named Mr. David Mwangosi in Iringa and the ongoing constitutional review process.
In furtherance, the European Union delegation also wanted a dialogue on the update in respect to the situation in Eastern part of Democratic Republic of Congo, the presidential election in Zimbabwe, the crisis in Madagascar, the piracy incidents and the border dispute between Malawi and Tanzania.   
In his response, the Minister shared the Government views and stand on the religious demonstration that took place in Mainland and in Zanzibar.  He said that the Government is in control of the situation and it will not, under no circumstances allow such situations to escalate and cause any tension to our peaceful country. 
 “We have managed to have zero tolerance in respect to any religious demonstrations,” said the Minister, adding that all the accused persons involved in burning of churches in Zanzibar “have already been brought before the court of law and the situation is under control.”
In respect to the freedom of press, Hon. Membe said that the Government does indeed supports the freedom of press so long as it does not infringe the law set forth by the constitution.  In other regard, the Minister appealed to the EU delegation to provide training programs and education for the media personnel.      
On Tanzania and Malawi border issue, the Minister said that the two countries have been in talks amicably and diplomatically, to resolve the matter.  In fact, there is an ongoing three-day meeting on Lake Nyasa border dispute hosted by Tanzania from 15 through 17 November, 2012 at Serena Hotel in Dar es Salaam.
“The dispute derived from the 1890 Anglo-German Treaty known as ‘The Heligoland Treaty’ and in essence it is a triple-heritage of nature,” said Hon. Membe.  He added that the "triple-heritage is a water-body shared by Tanzania, Mozambique and Malawi and that nobody can claim that the whole Lake belongs to one."  
On his part, the Head of European Union delegation said that they support all the initiatives that both Tanzania and Malawi have taken in making sure that the Lake Nyasa border dispute will be resolved amicably.
In respect to the update on the EU economic and financial crisis, Ambassador Sebregondi said that the crisis does not have significant impact to the developing countries that include Tanzania.  He further said that they have a roadmap proposal in place to explore and address any long-term issues that may arise in respect to the EU single monetary union.   

End. 



Tanzania na Malawi zaendelea na majadiliano kuhusu Ziwa Nyasa

 Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. John Haule kufungua kikao cha Pamoja  cha Maafisa Waandamizi kutoka Tanzania na Malawi kuendelea na majadiliano kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa. Majadiliano hayo yanafanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (mwenye kipaza sauti) akisoma agenda za kikao hicho wakati wa majadiliano. Wengine katika picha ni Mhe. Patrick Tsere (kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Balozi Kasyanju (kulia) na wajumbe wengine kutoka Tanzania.
Wajumbe kutoka Malawi wakimsikiliza Bw. Haule (hayupo pichani) wakati wa majadiliano hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Malawi, Bw. Patrick Kabambe (wa tatu kutoka kushoto) akichangia maoni yake wakati wa majadiliano hayo. Wengine katika picha ni wajumbe aliofuatana nao kutoka Malawi.
Wajumbe kutoka Tanzania wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Malawi (hayupo pichani) wakati wa majadiliano hayo.
Wajumbe wa pande zote mbili wakati wa majadiliano hayo.

Thursday, November 15, 2012

Tanzania na Malawi zakutana kujadili mpaka kwenye Ziwa Nyasa


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule akizungumza na Mhe. Flosie Gomile Chiyaonga, Balozi wa Malawi hapa nchini kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Timu ya Pamoja ya Wataalam wa Tanzania na Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa.

Bw. Abdallah Mtibora, Afisa kutoka Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kufungua mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akifungua Mkutano wa Timu ya Pamoja ya Wataalam kati ya Tanzania na Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa. Mkutano huo uliowahusisha wataalam kutoka Wizara na Idara mbalimbali za Serikali za Tanzania na Malawi unafanyika  Jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Malawi wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
Bw. Julius Chisi, Naibu Mpimaji Ardhi Mkuu kutoka Malawi  akizungumza machache wakati wa mkutano huo.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania akiwemo Mhe. Balozi Patrick Tsere (wa pili kutoka kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Malawi na Balozi Irene Kasyanju (kushoto) wakimsikiliza Bw. Chisi (hayupo pichani) wakati wa akizungumza.

Baadhi ya Wajumbe wengine kutoka Malawi akiwemo Mhe. Chiyaonga (kulia), Balozi wa Malawi hapa nchini.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.

 
Mkutano kati ya Tanzania na Malawi kujadili suluhu ya mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa umeanza katika ngazi ya Wataalamu jijini Dar es Salaam tarehe 15 Novemba, 2012.

Mkutano huo unaowahusisha wataalam kutoka Wizara na Idara mbalimbali za Serikali za Tanzania na Malawi unafanyika Jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena.

Akifungua Mkutano huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule alisisitiza umuhimu wa wajumbe kutoka nchi zote mbili kujadili na kupendekeza njia zitakazosaidia kupata suluhisho la kudumu la mgogoro huo.

Aidha, Bw. Haule aliweka bayana kuwa Serikali ya Tanzania ina dhamira ya dhati kufanya kazi pamoja na Serikali ya Malawi kutafuta suluhu ya mgogoro huo jambo ambalo pia lilisisitizwa na Bw. Julius Chisi, Kiongozi wa Ujumbe wa Malawi.

Mkutano huo ambao utafanyika kwa siku tatu hadi tarehe 17 Novemba, 2012 umeanza na Kikao cha Wataalamu ambacho kitafuatiwa na kikao cha Maafisa Waandamizi na kuhitimishwa na kikao cha Mawaziri tarehe 17 Novemba, 2012.

Wednesday, November 14, 2012

Congratulatory message on the occassion of the Belgium National Day


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty King Albert II, King of the Belgians following the occasion of the National Day of the Kingdom of Belgium on 15th November, 2012.
The message reads as follows;

“His Majesty King Albert II,
 King of the Belgians,
 Brussels,
 BELGIUM.

Your Majesty,

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and on my own behalf, it gives me great pleasure to congratulate you most sincerely on the occasion of the National Day of the Kingdom of Belgium.

              Belgium and Tanzania have over the years enjoyed good bilateral relations. The celebration of your country’s National Day offers me yet another opportunity to reaffirm our commitment to continue working closely with you in further consolidating and strengthening the ties of friendship, cooperation and partnership between the Kingdom of Belgium and the United Republic of Tanzania.

            Please accept, Your Majesty, my best wishes for your personal good health and prosperity for the people of Belgium”.


ISSUED BY: MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION,
DAR ES SALAAM.
14TH NOVEMBER, 2012.


Katibu Mkuu akutana na Mjumbe Maalum kutoka Argentina

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akipokea Ujumbe Maalum kutoka Serikali ya Argentina kwa niaba ya Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka kwa Balozi Bibiana Jones. Balozi Jones ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika anayeshughulikia nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Argentina.

Bw. Haule akizungumza na Balozi Jones mara baada ya kupokea Ujumbe Maalum.

Balozi Jones akifafanua jambo kwa Bw. Haule wakati wa mazungumzo yao.

Katibu Mkuu, Bw. Haule akiendelea na mazungumzo na Balozi Jones kuhusu ushirikiano baina ya Tanzania na Argentina. Mwingine katika picha ni Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Katibu Mkuu akimsikiliza Balozi Jones wakati wa mazungumzo yao huku Balozi Msechu na Bi. Upendo Mwasha, Afisa katika Idara ya Ulaya na Amerika wakishuhudia.

Saturday, November 10, 2012

Ushirikiano kati ya Tanzania na China wazidi kuimarika: Wizara ya Mambo ya Nje na Tume ya Mipango zajadili miradi na Serikali ya China

Kaimu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bw. Longinus Rutasitara (katikati) akifafanua jambo wakati wa mkutano na Wajumbe kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na wadau wengine (hawapo pichani) kujadili misaada ya Serikali ya China katika kuisadia Tanzania kutekeleza miradi mikubwa katika sekta kama vile Kilimo, Miundombinu na Umeme. Wengine katika picha ni Maafisa Waandamizi kutoka Tume hiyo.

Balozi Mbelwa Kairuki (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akitoa mchango wake wakati wa majadiliano na ujumbe kutoka Serikali ya China kuhusu kuisaidia Tanzania kutekeleza miradi yake mikubwa. Wengine katika picha ni Bw. Lin Zhiyong (katikati) Mwakilishi Mkuu katika masuala ya Uchumi na Biashara wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China hapa nchini na Bi. Fang Wang, Afisa kutoka Ofisi hiyo.

Bw. Lin Zhiyong akitoa maoni yake wakati wa majadiliano hayo.

Balozi Kairuki na wajumbe kutoka China wakimsikiliza Kaimu Katibu Mtendaji, Bw. Rutasitara (hayupo pichani) wakati wa majadiliano. Wengine katika picha ni Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Tume ya Mipango walioshiriki mkutano huo.

Bw. Rutasitara na Maafisa wengine wakimsikiliza Bw. Li wakati wa majadiliano hayo.

Thursday, November 8, 2012

Ushirikiano kati ya Tanzania na China wazidi kukua; Rais Kikwete azinduzia bomba la gesi asilia



Rais Kikwete azindua Ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa bomba la gesi asilia linalotoka Mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam katika maeneo ya Kinyerezi, leo jijini Dar es Salaam.  Akishuhudia uzinduzi huo (kushoto) ni Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal.  


Rais Kikwete, Makamu wa Rais Dkt. Bilal na viongozi wengine wakimsikiliza Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (Mb), Waziri wa Nishati na Madini ambaye alikuwa akielezea kuhusu miundombinu ya bomba la gesi la asilia. 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa kampuni inayojenga bomba la gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, Benki ya Exim ya China na viongozi waandamizi wa Serikali akiwemo Balozi Dkt. Philip S. Marmo (wa pili kulia - mstari wa mbele), Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China.  Rais Kikwete aliwakaribisha Ikulu kwa mazungumzo baada ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa bomba hilo maeneo ya Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.



Picha zote kwa hisani ya      www.issamichuzi.blogspot.com







Wednesday, November 7, 2012

Rais Kikwete ametuma salamu za pongezi kwa Rais Obama


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameeleza furaha na shangwe yake kufuatia ushindi wa jana, Jumanne, Novemba 6, 2012 wa Rais Barack Obama wa Marekani katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo.




Katika salamu zake za pongezi kwa kiongozi huyo wa Marekani ambaye amechaguliwa tena na wananchi wa nchi hiyo kwa kipindi cha pili, Rais Kikwete amesema mapema leo, Jumatano, Novemba 7, 2012:


Obama
Rais Barack Obama akisheherekea ushindi wake
dhidi ya mpinzani wake, Bw. Mitt Romney, na kuwa
Rais wa Marekani kwa kipindi cha pili.

“Nimepokea kwa furaha na shangwe habari za kuchaguliwa tena kwako kuwa Rais wa Marekani kwa kipindi cha pili. Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu mwenyewe, napenda kukutumia wewe na kupitia kwako Chama cha Democratic pongezi nyingi kwa ushindi wako wa maana sana.”




Ameongeza Rais kikwete katika salamu zake hizo: “Kuchaguliwa kwako tena kuendelea kuongoza nchi yako muhimu na wananchi wake, ni ishara ya wazi ya uaminifu na imani ambayo wananchi wa Marekani wanayo katika uongozi wako wa mfano.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Wakati unajiandaa kuchukua tena uongozi wa nchi hiyo katika kipindi chako kipya, napenda kukuhakikishia msimamo wangu binafsi na ule wa Serikali yangu kuwa tutaendelea kufanya kazi kwa karibu kabisa na wewe na Serikali yako ya kutukuka, ili kuendeleza uhusiano bora ulioko kati ya nchi zetu mbili ndugu.”



Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

7 Novemba, 2012

Tuesday, November 6, 2012

Rais Kikwete akagua miradi 19 katika wiki moja






THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais akagua miradi 19 katika wiki moja
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amerejea Dar es Salaam mchana wa leo, Jumanne, baada ya kumaliza ziara ya siku tisa katika mikoa minne ambako amekagua, kuanzisha ama kuzindua miradi 19 ya maendeleo na kutembea kiasi cha kilomita 2,770.
Rais Kikwete amewasili Dar es Salaam akitokea Dodoma ambako amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili baada ya kumaliza ziara katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida.
          Katika Mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete alianzia ziara yake Oktoba 28, mwaka huu, miongoni mwa mambo mengine alikagua nyumba za wahanga wa maporomoko ya mwaka 2006 kwenye kijiji cha Goha na akafungua Kiwanda cha Kusindika Tangawizi kilichoko Mamba Miamba, Wilaya ya Same, na akafungua Shule ya Sekondari ya Kata ya Asha Rose Mingiro iliyoko mjini Mwanga.
Miradi mingine aliyoifungua Rais Kikwete katika Mkoa wa Kilimanjaro ni uzinduzi wa barabara za Rombo Mkuu-Tarakea na Kwasadallah-Masama na akafungua Ofisi ya Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (NAO) mjini Moshi.
Katika Mkoa wa Arusha, Rais Kikwete alizindua Hospitali ya Wilaya ya Arusha ya Olturumet, akazindua Mradi Mkubwa wa Uboreshaji wa Miji kwa kufungua barabara za Jiji la Arusha, akazindua Jiji la Arusha, akafungua rasmi Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela na akatembelea Kiwanda cha Nguo cha A-Z.
Kabla ya kuondoka Mkoani Arusha, Rais Kikwete alifungua Shule ya Msingi ya Sokoine na kuzindua ukarabati mkubwa wa Barabara ya Minjingu-Arusha.
Mkoani Manyara, Rais Kikwete alifungua rasmi Barabara ya Singida-Minjingu-Arusha, akazindua mradi mkubwa wa maji wa Mji wa Babati na akaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Babati-Bonga.
Mkoani Singida, Rais Kikwete alizindua mradi mkubwa wa maji wa Mwankoko kwa ajili ya Mji wa Singida, akaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Manyoni-itigi-Chaya na akafungua Barabara ya Issuna-Manyoni.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Novemba, 2012


Monday, November 5, 2012

Sherehe za Mwenge za Kuadhimisha Miaka 100 ya ANC



Mhe. Balozi Radhia Msuya, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini akisema machache wakati wa Sherehe za Mwenge za kuadhimisha Miaka 100 ya Chama Cha African National Congress (ANC) zilizofanyika hivi karibuni tarehe 30 Oktoba, 2012 kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania mjini Pretoria, Afrika Kusini.


 
Wanachama wa ANC wakisikiliza hotuba ya Mhe. Balozi Msuya.


Mjumbe wa Chama cha ANC, Bw. Sochayile Khanyile, naye akiongea machache wakati wa Sherehe hizo.


Wanajeshi wakiwa wamejipanga kabla ya Sherehe rasmi za kuwasha Mwenge kuanza.  Kushoto ni Bw. Robert Kahendaguza, Mtawala Mkuu kwenye Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchi Afrika Kusini.


Mhe. Balozi Radhia Msuya, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini, akiwasha Mwenge, ikiwa ni ishara ya kuadhimisha Sherehe za Kitaifa za Kutimiza Miaka Mia Moja ya kuanzishwa kwa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini.  

Sherehe hizo zilianza katika vitongoji na miji kadhaa nchini Afrika Kusini tangu mwezi Januari 2012, ambapo viongozi mbalimbali wa Kitaifa walihudhuria, wakiwemo Mhe. Rais Jacob Zuma ambaye alikuwa mgeni rasmi, Rais mstaafu Mhe. Benjamin W. Mkapa, pamoja na marais na viongozi wa nchi mbali mbali.

Wakati huo huo, matamasha mbali mbali, mijadala, maonyesho na mbio za Mwenge zimekuwa zikiendelea nchini Afrika Kusini katika muendelezo wa Maadhimisho hayo ya Miaka 100 ya Chama Tawala.   Aidha, tarehe 31 Oktoba, 2012 Mbio za Mwenge za Maadhimisho hayo zilifanyika katika Balozi zaidi ya kumi za nchi marafiki, ikiwa ni sehemu ya kutoa ushirikiano katika harakati za Ukombozi wa Afrika Kusini. Nchi hizo zinaijumuisha Tanzania, Zimbabwe, Botswana, Namibia, Zambia, Angola, Palestina, Urusi, China, Cuba na nyingine nyingi. 

Saturday, November 3, 2012

President Kikwete sends a sympathy message to H.E. President Barack Obama of the United States of America


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, the President of the United Republic of Tanzania, has sent a sympathy message to H.E. Barack Obama, the President of the United States of America following the devastations from hurricane Sandy.

The message reads as follows: -

 “H.E. Barak Obama,
  President of the United States of America,

  Washington, DC

  USA.

Your Excellency,

I have learnt with deep sorrow and profound dismay about the sad news of the devastating hurricane Sandy which killed more than forty people, injuring many and leaving others homeless.

In the wake of this terrible tragedy, I would like on behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf to convey our most heartfelt condolences to Your Excellency, and through you, to the bereaved families, the government and people of the United States of America.

While wishing the affected families strength and fortitude during this moment of distress please accept, Your Excellency, the assurances of my highest consideration”.


ISSUED BY: MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION, DAR ES SALAAM.
3RD NOVEMBER, 2012




Naibu Waziri ashiriki Mkutano wa IOR na kukutana na baadhi ya Mawaziri kwa mazungumzo

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (kushoto) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Pierrot Jocelyn Rajaonarivelo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar. Mhe. Maalim na Mhe. Rajaonarivelo wapo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri kutoka Nchi Zinazopakana na Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim-IOR)

Mhe. Maalim akisalimiana na Mhe. Abu-Bakr Al-Qirbi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen wakati wa Mkutano wa Mawaziri kutoka Nchi Zinazopakana na Bahari ya Hindi unaoendelea nchini India

Mhe. Maalim akipata picha ya kumbukumbu  na Mhe. Jean-Paul Adam, Waziri wa Mambo ya Nje wa Shelisheli mara baada ya kumaliza mazungumzo yao. Mawaziri hao wapo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi.

Mhe. Maalim (katikati) katika picha ya pamoja na  Mhe. Jean-Paul Adam (wa pili kutoka kushoto), Waziri wa Mambo ya  Nje wa Shelisheli na Mhe John Kijazi (wa pili kutoka kulia), Balozi wa Tanzania nchini India  na wajumbe wengine wanaoshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi.

Thursday, November 1, 2012

Naibu Waziri atembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisaini Kitabu cha Wageni  alipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India. Anayeshuhudia pembeni ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini humo. Mhe. Maalim yupo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim).

Mhe. Maalim akimsikiliza Balozi Kijazi wakati akimkaribisha  kuzungumza na Watumishi wa Ubalozini. Wengine katika picha ni baadhi ya Watumishi wa Ubalozi huo.

Mhe. Maalim (mwenye tai ya bluu) akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Kijazi  (kulia kwake) na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania uliopo New Delhi nchini India mara baada ya kuwatembelea na kuzungumza nao.