Wednesday, December 12, 2012

Naibu Waziri akutana na ujumbe wa Kampuni ya Labiofam kutoka Cuba

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (katikati),  akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Jose Antonio Fraga Castro (kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya LABIOFAM ya Cuba na Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo (kulia), Balozi wa Cuba hapa nchini mara  baada ya kuzungumza nao kuhusu kampuni hiyo. Kampuni ya Labiofam inajenga kiwanda cha kutengeneza madawa ya kuulia vimelea vya malaria huko Kibaha.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (katikati),  akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Jose Antonio Fraga Castro (kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya LABIOFAM ya Cuba na Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo (wa kwanza kulia), Balozi wa Cuba hapa nchini na wajumbe wengine waliofuatana nao kutoka Cuba . Kushoto ni Bi. Upendo Mwasha, Afisa Mambo ya Nje.

Saturday, December 8, 2012

Finland National Day Celebrations

Deputy Minister for Constitutional and Legal Affairs, Hon. Angellah Kairuki (MP) delivering remarks on behalf of Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation at the Reception to celebrate Finland National Day.
Hon. Angellah Kairuki(left) preparing to toast with Ambassador Sinikka Antila of Finland during Finnish National Day.
Hon. Angellah Kairuki sharing a light moment with Finnish Ambassador H.E.Ambassador Sinikka Antila (left) and the Director for Europe and the Americas Department in the  Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Ambassador Dora Msechu during Finland National Day reception.

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC waanza

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Dkt. Tomaz Augusto Salomao akiwakaribisha wajumbe (hawapo pichani) kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo uliofanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Desemba, 2012.

Rais wa Msumbiji na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Armando Guebuza akifungua rasmi Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo uliofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Desemba, 2012. Wengine katika picha ni Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kutoka kushoto), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Yoweri Museveni (kulia), Rais wa Uganda na Mwenyekiti wa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) na Dkt. Salomao (kushoto), Katibu Mtendaji wa SADC.

Baadhi ya Wajumbe kwenye mkutano wa SADC wakisiliza hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo kutoka kwa Mhe. Rais Guebuza (hayupo pichani).

Mhe. Yoweri Museve (Kulia), Rais wa Uganda na Mwenyekiti wa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu  (ICGLR) akihutubia mkutano wa Wakuu wa Nchi wa SADC. Wengine katika picha wanaosikiliza ni Mhe. Rais Kikwete (wa pili kutoka kushoto), Mhe. Rais Guebuza (wa pili kutoka kulia) na Dkt. Salamao (kushoto).


Rais Guebuza (kushoto) ambaye ni Mwenyekiti wa SADC akiteta jambo na Mhe. Rais  Museveni (kulia) ambaye pia ni Mwenyekiti wa ICGLR wakati wa mkutano wa SADC.

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (wa pili kushoto), Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na wajumbe wengine wakati wa mkutano wa SADC.

Mhe. Rais Kikwete (kushoto) akishauriana jambo na Mhe. Bernard K. Membe (Mb) (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa mara baada ya ufunguzi rasmi wa  mkutano wa SADC.

Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano huo kufunguliwa rasmi katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Desemba, 2012.


Wakuu wa Nchi za SADC washiriki hafal ya chakula cha jioni

kwa
Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwakaribisha Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kwenye Hafla ya Chakula cha Jioni aliyoiandaa kwa heshima yao iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Jijiji Dar es Salaam tarehe 7 Desemba, 2012. Wakuu hao wa nchi wapo nchini kuhudhuria mkutano wa SADC utakaojadili masuala mbalimbali ya kikanda.
Wakuu wa Nchi za SADC wakiwa na mwenyeji wao Mhe. Rais Kikwete wakati wa Hafla ya Chakula cha Jioni.
Wakuu wa Nchi za SADC wakiwa katika ukumbi wa Serena walipofika kwa ajili ya hafla ya chakula cha jioni jana. Kutoka kushoto ni Mhe. Jacob Zuma, Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Joseph Kabila, Rais wa DRC, Mhe. Armando Guebuza, Rais wa Msumbiji na Mhe. Hifikepunye Pohamba, Rais wa Namibia.

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa Hotelini hapo kutekeleza majukumu ya kiitifaki ya kuhudumia wajumbe wa mkutano.


Friday, December 7, 2012

Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi wa SADC waanza kwa kikao cha Troika

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na Mhe. Jacob Zuma (katikati), Rais wa Afrika Kusini mara baada ya Mhe. Zuma  kuwasili Ikulu, Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudhuria Kikao cha Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Troika). Mwingine katika picha ni Dkt. Tomaz Augusto Salomao, Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo.Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC unaotarajiwa kufanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam tarehe 8 Desmba, 2012.
Mhe. Rais Kikwete (wa pili kutoka kulia) akifurahia jambo na Marais wenzake Mhe. Zuma (wa tatu kutoka kushoto) na Mhe. Hifikepunye Pohamba (kulia), Rais wa Namibia walipokuwa Ikulu, Dar es Salaam kabla ya Mkutano wa Troika kuanza.Wengine katika picha ni Mhe. Joaquim Chissano (wa pili kutoka kushoto), Rais Mstaafu wa Msumbiji na Msuluhishi wa Mgogoro wa kisiasa nchini Madagascar na Dkt. Salomao, Katibu Mtendaji wa SADC.
Mhe. Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) akiongoza kikao kujadili masuala mbalimbali ya kikanda. Kikao hicho kilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Mabalozi kabla ya mkutano wa Troika kuanza. Kutoka kushoto ni Balozi Liberata Mulamula, Msaidizi Mwandamizi wa Rais katika masuala ya Diplomasia, Balozi Shamim Nyanduga (wa tatu kutoka kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji na Balozi Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.
Balozi Naimi Aziz (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na baadhi ya wajumbe waliofika kuhudhuria mkutano wa Troika uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Thursday, December 6, 2012

Congratulatory message on the occasion of Finland's National Day


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, the President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Sauli Niinistö, the President of the Republic of Finland on the occasion of celebrating Finland's National Day on
6th December, 2012.
 
The message reads as follows;
President of the Republic of Finland,
Helsinki,
FINLAND

Your Excellency,

On behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania, and on my own behalf, I wish to extend my sincere greetings to you and through you to the Government and people of Finland on the occasion of your country’s National Day.

We in Tanzania cherish the close ties of friendship, cooperation and partnership that happily exist between our two countries. As you celebrate this important day of your country, I wish to seize this opportunity to reaffirm my personal commitment and that of my Government to continue working closely with you to further strengthen our cordial relations and cooperation for the mutual benefit of our people.

I wish, Your Excellency, personal good health and peace and prosperity for the people of Finland”.


ISSUED BY: MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

05TH DECEMBER, 2012


 

Wednesday, December 5, 2012

Mhe. Membe azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa SADC na Meli za Iran

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) alipokutana nao Wizarani jana. Mhe. Waziri alizungumza na Waandishi hao kuhusu Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) unotarajiwa kufanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam tarehe 7 na 8 Desemba, 2012 na pia alijibu tuhuma kuhusu Meli za Iran kusajaliwa na kupeperusha Bendera ya Tanzania. Wengine katika picha ni Balozi Rajab Gamaha (kulia), Kaimu Katibu Mkuu na Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Kimataifa
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifurahia jambo wakati wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao.
Mhe. Membe akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani)
Mhe. Membe akiendelea na mkutano na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) huku Balozi Gamaha akimsikiliza kwa makini.
Mhe. Waziri Membe akisisitiza jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) huku Balozi Msechu akitafakari.


Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kutoka kushoto ni Balozi Vincent Kibwana, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Balozi Irene Kasyanju, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria.
Baadhi ya Watendaji wengine wa Wizara ya Mambo ya Nje waliohudhuria mkutano huo wa Mhe. Membe na Waandishi wa Habari. Kutoka kushoto ni Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw.Joachim Otaru, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango na Bw. Gabriel Mwero, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani.

Monday, December 3, 2012

Naibu Katibu Mkuu akutana na Msajili wa MICT

Mhe. Balozi Rajabu Gamaha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (kushoto) akiwa katika picha na Bw. John Hocking, (wa tatu kutoka kulia) Msajili wa Mahakama iliyorithi shughuli za ICTR (United Nation Mechanism for International Criminal Tribunals (MICT). Bw. Hocking alikuja Wizarani kwa madhumuni ya kufanya mazungumzo na uongozi wa Wizara kuhusu utendaji kazi wa Mahakama hiyo. Wengine katika picha ni watendaji wa Mahakama hiyo.

Mhe. Balozi Gamaha akifafanua jambo wakati alipofanya mazungumzo na Bw. Hocking (hayupo katika picha)

Bw. Hocking (kulia) pamoja na ujumbe wake wakimsikiliza kwa makini Naibu Katibu Mkuu wakati wa mazungumzo yao.

Msajili wa MICT akitoa maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati alipomtembelea ofisini kwake.

Naibu Katibu Mkuu, Mhe. Gamaha akimsikiliza kwa makini Bw. Hocking. (hayupo katika picha)

Balozi Irene Kasyanju, (kulia) Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa naye akifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Naibu Katibu Mkuu na Msajili wa MICT huku Afisa kutoka Kitengo chake, Bw. Benedict Msuya akinukuu mambo muhimu ya mazungumzo hayo.

Wajumbe wakimsikiliza kwa makini Mhe. Balozi Gamaha aliye katikati.

Friday, November 30, 2012

Hafla ya Kufungua Jengo Jipya la Makao Makuu ya EAC

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Serikali na wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika hafla ya ufunguzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha tarehe 28 Novemba, 2012

Mhe. Mwai Kibaki, Rais wa Kenya na Mwenyekiti wa EAC akiwasilisha hotuba yake wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mhe. Rais Kibaki akitoa cheti kwa mmoja wa Wahandisi waliofanikisha ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mwakilishi wa Serikali ya Ujerumani naye akitoa hotuba fupi katika hafla hiyo. Serikali ya Ujerumani ndiyo iliyodhamini ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC

Mhe. Rais Kikwete wa kwanza kushoto akiwa na baadhi ya viongozi wenziwe wa EAC wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya EAC.

Mhe. Rais Kikwete (katikati) na Viongozi wenziwe wa EAC wakiwa katika moja ya vyumba vya jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mhe. Rais Kikwete wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa EAC mjini Arusha.

Mwakilishi wa Serikali ya Ujerumani na wa EAC wakiweka saini Mkataba wa kushirikiana kiuchumi kati ya Ujerumani na EAC

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akibadilishana mawazo na Bw. Richard Sezibera, Katibu Mkuu wa EAC wakati wa hafla ya kufungua Jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Wanafunzi wa Shule ya Msingi wakitoa burdani wakati wa hafla ya kufungua jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Wednesday, November 28, 2012

Rais Kikwete ahutubia Mkutano wa Tatu wa Bunge la Afrika Mashariki

m

Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Margaret B. Ziwa akimkaribisha Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipowasili kwenye Makao Makuu ya Jumuiya hiyo kwa ajili ya kuwahutubia Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki mjini Arusha tarehe 27 Novemba, 2012.

Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Margaret Ziwa akitoa salamu za kumkaribisha Mhe. Rais Kikwete kuhutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Anayeoneka pembeni mwa Mhe. Ziwa ni Mhe. Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe.  Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisisitiza jambo wakati alipokuwa anawahutubia Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki mijini Arusha tarehe 27 Novemba,2012
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na wageni waalikwa wakimsikiliza Mhe. Rais Kikwete alipowahutubia.

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na  Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Ziwa mbele ya Jengo Jipya la Makao Makuu ya EAC.

Bw. David Mwakanjuk (katikati), Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha (kushoto) Mhe. Magesa Mulongo kabla ya kikao cha Bunge la EAC kuanza tarehe 27 Novemba, 2012. Mwingine katika picha ni Afisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.