Monday, November 25, 2013

Minister Membe holds talks with the UN Special Envoy for the Great Lakes Region


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation in a photo with Ms. Mary Robinson, Special Envoy of the United Nations Secretary General for the Great Lakes Region during their meeting at his office today.

Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation holds talks with Ms. Mary Robinson, Special Envoy of the United Nations Secretary General for the Great Lakes Region who had paid a courtesy visit today in his office in Dar es Salaam.  During their discussion, Ms. Robinson praised Tanzania for her role in securing peace and security in the Eastern Democratic Republic of Congo –DRC.


Minister Membe and Ms. Robinson, who is also a former President of the Republic of Ireland, continue with discussion about the latest developments and the ongoing efforts to implement peace, security and cooperation (PSC) framework for the Eastern Democratic Republic of Congo –DRC and the region. 

Minister Membe's delegation included Hon. Mahadhi Juma Maalim (MP) (left), Deputy Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Ambassador Dora Msechu (center), Acting Permanent Secretary and the Director of the Department of Europe and Americas and Mr. Miyaye, Acting Director of the Department of Regional Cooperation in the Ministry of Foreign Affairs. 

Listening on are Ms. Robinson's delegation that included Mr. Modibo Toure, Senior Advisor to the Special Envoy of the UNSG for the Great Lakes Region, Dr. Alberic Kacou (center), the UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, and Mr. Fode Said Conde, Special Assistant to the Special Envoy of the UNSG for the Great Lakes Region.  

Hon. Minister Membe (center), in a group photo with Ms. Robinson (2nd left), Hon. Maalim (2nd right), Dr. Kacou (left) and Mr. Toure (left).



All photos by Tagie Daisy Mwakawago 



Sunday, November 24, 2013

H.E. President Kikwete meets with the Crown Prince of Abu Dhabi


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete (left), President of the United Republic of Tanzania gets welcomed by the Crown Prince of Abu Dhabi in the United Arab Emirates His Highness Shaikh Gen. Mohamed bin Zayed Al Nahyan.  President Kikwete had paid a courtesy visit to the Bahr Palace in Abu Dhabi on the 18th of November, 2013. 

H.E. President Kikwete (right) in a discussion with the Crown Prince of Abu Dhabi His Highness Shaikh Gen. Mohamed bin Zayed during their meeting. 

The Crown Prince of Abu Dhabi His Highness Shaikh Gen. Mohamed bin Zayed Al Nahyan (center), escorted out H.E. Jakaya Mrisho Kikwete (right), President of the United Republic of Tanzania after they finished their meeting at the Bahr Palace in Abu Dhabi.  Also in the photo is H.E. Mbarouk Nassor Mbarouk (left), Ambassador of the United Republic of Tanzania to the United Arab Emirates. 



All photos courtesy of the Protocol Department  


Thursday, November 21, 2013

Naibu Waziri azungumza na Balozi wa Finland hapa nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akimkaribisha Ofisi kwake Balozi wa Finland hapa nchini Mhe. Sinikka Antila alipofika kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya nchi yake na Tanzania. Tanzania na Finland zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu katika masuala mbalimbali ya kiuchumi, kijamii na utawala bora.

Mhe. Dkt. Maalim akimweleza jambo Mhe. Antila wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Antila naye akifafanua jambo kwa Mhe. Dkt. Maalim wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bibi Victoria Mwakasege (kulia mwenye nguo ya njano), Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Ulaya na Amerika akifuatiwa na Bi. Upendo Mwasha, Afisa Mambo ya Nje. Kushoto ni Bw.Jussi Nummelin, Afisa katika Ubalozi wa Finland hapa nchini.


Wednesday, November 20, 2013

AfroChamber Team visits Tanzania Embassy in Brasilia


Mr. David Mwakanjuki (center), Minister Plenipotentiary of the Embassy of the United Republic of Tanzania in Brasilia in a group photo with the AfroChamber Team, when they visited the Embassy on 14th of November, 2013.  The AfroChamber Team is an organization conjoined by both African and Brazilian groups.   Others in the photo are Mr. Antônio Lúcio (left), Vice President, Mr. Rui Mucaje (2nd left), Director, Mr. Abel Domingos (2nd right), President and Mr. Jader de Oliveira Nicolai, Jr. (right), Director General.


Photo and details from the Tanzania Embassy in Brasilia 


Kuwait kuzipatia nchi za Afrika mikopo ya masharti nafuu yenye thamani ya Dola bilioni moja, Amir


 
 
Na Ally Kondo, Kuwait

Serikali ya kuwait imetenga kiasi cha Dola za Marekani bilioni moja (1) kwa ajili ya kuzipatia nchi za Afrika mikopo ya masharti nafuu katika kipindi cha miaka mitano ijayo. Tangazo hilo lililotolewa na Amir wa Kuwait ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Tatu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Ushirikiano baina ya Nchi za Afrika na Kiarabu (Third Afro Arab Summit), Sheikh Sabah Al-Ahnad Al-Sabah wakati alipokuwa anatoa hotuba ya ufunguzi ya mkutano huo nchini Kuwait siku ya Jumanne tarehe 19 Novemba, 2013.

Sanjari na kiasi hicho cha fedha, Sheikh Al-Sabah alitangaza kiasi kingine cha Dola za Marekani milioni moja (1) kwa ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali za utafiti zenye lengo la kuibua fursa za maendeleo katika nchi za Afrika.

 
Sheikh Al- Sabah aliwambia wajumbe wa mkutano huo kuwa, Mkutano wa Tatu wa Afro Arab Summit unafanyika huku nchi nyingi za Afrika na Kiarabu zikikabiliwa na changamoto za kisiasa na kiuchumi ambazo bila kupatiwa ufumbuzi wa kudumu malengo yanaayowekwa katika mikutano hiyo hayatafikiwa. Alisisitiza nchi za Afrika na Kiarabu kuwekeza katika miradi itakayoimarisha ushirikiano wao akitolea mfano wa sekta ya kilimo. “Endapo usalama wa chakula hautakuwa wa kuaminika katika nchi za Afrika na Kiarabu, kutazifanya nchi hizo kuwa katika hali tete na hatimaye kushindwa kukidhi matarajio ya wananchi wao. Sheikh Al-Sabah alisikika akisema.

 
Aidha, Amir wa Kuwait aliwaomba Wakuu wa Nchi kutumia mkutano huo kutafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro unaoendelea nchini Syria ambao athari zake unaikumba kanda nzima ya Kiarabu. Alihitimisha hotuba yake kwa kulitolea wito Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuishinikiza Israel itekeleze Maazimio ya Umoja wa Mataifa kuhusu Mamlaka ya Palestina.

 
Kwa upande wake, Mwenyekiti mwenza wa mkutano huo, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Hailemariam Dessalegn alieleza kuwa nchi za Afrika haziwezi kufikia mapinduzi ya kijani endapo hakutawekwa mkazo katika sekta za nishati jadilifu, miundombinu na utalii. Hivyo, alisisitiza umuhimu wa mkutano huo kubuni mwongozo makini wa ushirikiano utakaowezesha kufikiwa kwa malengo hayo.  

 

Mhe. Dessalegn alizihimiza nchi za Afrika na Kiarabu kuongeza nguvu mara dufu katika mapambano dhidi ya uharifu wa mipakani, ugaidi, uharamia pamoja na uhamaji wa kinyume cha sheria. Aliweka angalizo kuhusu tatizo la uhamaji kwa kusema kuwa endapo halitafanyiwa kazi vizuri linaweza kudhoofisha ushirikiano huo. Hivyo, aliunga mkono pendekezo la kuunda Kamati ya Pamoja ya Wataalamu kutoka nchi za Afrika na Kiarabu ili kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.

 

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Nkosazana Dlamini-Zuma naye aliwahakikishia Wakuu wa Nchi katika mkutano huo kuwa, Afrika imejizatiti kutekeleza yale yote mazuri yatakayoafikiwa katika mkutano huo. Aidha, alihimiza umuhimu wa kuwekeza katika elimu ili idadi kubwa ya vijana ambao ndio nguvu kazi na wanawake ambao ni zaidi ya nusu katika nchi za Afrika wapate elimu bora inayoendana na madadiliko yanayotokea duniani hivi sasa.

 

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unaongozwa na Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais ambaye pia amepangiwa kutoa hotuba.

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal wa pili kutoka kushoto akisikiliza ahadi ya Amir wa Kuwait ya kuzikopesha  nchi za Afrika Dola za Marekani biliomni moja.


Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Prof. Abdillah Omar wa kwanza kushoto, Mbunge wa Wawi, Mhe. Ahmadi Rashidi na Mbunge wa Gando, Mhe. Khalifa Khalifa nao walishuhudia ahadi ya Amir wa Kuwait.


Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz mwenye ushungi mwekundu na kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Simba Yahya nao walikuwepo katika ukumbi wa mkutano wakati Amir wa Kuwait akitoa hotuba.

Tuesday, November 19, 2013

CHOGM 2013 Final Communique


H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete (see Tanzania national flag in the background) of the United Republic of Tanzania as he enters the Nelum Pokuna Mahinda Rajapaksa Theatre in Colombo City during the opening ceremony of the CHOGM 2013 in Colombo, Sri Lanka.  

Heads of State and Government of Commonwealth in a group photo before issuing a joint Final Communique for the CHOGM 2013. 



Monday, November 18, 2013

Dkt. Bilal kuongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Afro Arab Summit

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Mohamed Gharib Bilal akiongea na ujumbe wake {haupo pichani}wakati wa kikao cha maandalizi kwa ajili ya Mkutano wa Afro Arab Summit utakaofanyika nchini Kuwait tarehe 19 na 20 Novemba, 2013. kikao hicho kilifanyika katika moja ya kumbi za Jumba la Mfalme wa Kuwait.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe {Mb}, akitoa taarifa kwa Makamu wa Rais kuhusu masuala yatakayojadiliwa katika Mkutano wa Afro Arab Summit.


Mbunge wa Wawi, Mhe. Hamadi Rashidi naye akichangia jambo kuhusu maandalizi ya Mkutano wa Afro Arab Summit. Aliyevaa kofia ni Mbunge wa Gando, Mhe. Khalifa Khalifa.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz akichangia hoja katika kikao hicho.

Mhe. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa sita kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wake katika mkutano wa Afro Arab Summit.

Mkutano wa Mawaziri wa Afro Arab Summit umefunguliwa

 

Meza Kuu ikionesha baadhi ya Viongozi wa Mkutano wa Mawaziri wa Afro Arab Summit wakiwa wameketi.

Mwenyeki wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Nkosazana Dlamini-Zuma akihutubia Mkutano wa Mawaziri wa Afro Arab Summit.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Mhandisi Christopher Chiza {Mb}akifuatilia kwa makini mkutano wa Mawaziri.

Ujumbe wa Tanzania, kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Gregory Teu {Mb}, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Uledi Mussa, Mhe. Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Wajumbe kutoka nchi mbalimbali wakati wa mkutano huo.

Tanzania na Kuwait zasaini Mkataba wa Kulinda na Kukuza Vitega Uchumi pamoja na Mkataba wa Kushitrikiana katika Masuala ya Utalii

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe {Mb} aliye kushoto akiongea na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah kabla ya shughuli ya kusaini Mikataba kuanza.
 




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe {Mb} na Waziri mwenzake wa Kuwait wakisaini Mikataba ya Kukuza na Kulinda Vitega Uchumi; na Kushirikiana katika Masuala ya Utalii. Uwekaji saini huo ulifanyika nchini Kuwait siku ya Jumapili tarehe 17 Novemba, 2013.

Picha zaidi za uwekaji saini huku Maafisa kutoka Wizara za Mambo ya Nje za Tanzania na Kuwait wakishuhudia. kushoto ni Bw. Benedict Msuya kutoka Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe {Mb} na mwenzake wa Kuwait wakipongezana baada ya kukamilisha kazi ya kuweka saini Mikataba, Wanaopiga makofi ya furaha kutoka kushoto ni Mhe. Prof. Abdillah Omar, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia ambaye anawakilisha pia Kuwait na Qatar na anayefuata ni Mhe. Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Waheshimiwa Mawaziri wakibadilishana Mikataba mara baada ya kuisaini huku Balozi Yahya akipiga makofi kwa furaha.

Waheshimiwa Mawaziri wakiteta jambo baada ya kukamilisha kazi ya kusaini Mikataba.

Mhe. Membe akiongea na ujumbe wake, Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Clifford Tandari , Kamishna Msaidizi wa Wizara ya Fedha, Bw. Charles Samanyi, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia ambaye pia anashughulikia masuala ya Afro Arab, Mhe. Naimi Aziz na Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje.