Friday, February 21, 2014

Tanzania na Misri kuimarisha ushirikiano


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Mhe. Nabil Fahmy  wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu  ziara ya siku tatu ya Mhe. Fahmy hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014. Mhe. Fahmy yupo nchini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususan katika nyanja za afya, elimu, uwekezaji na siasa. 
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwasikiza Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani) walipozungumza nao

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana (kushoto waliokaa)  na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga wakinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani) wakati wa Mkutano wao na Waandishi wa Habari. 
Mhe. Fahmy nae akizungumza wakati wa mkutano huo.
Waandishi na Maafisa kazini.

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil  Fahmy (hayupo pichani) katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) Jijini Dar es Salaam. Mhe. Fahmy yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014. Wakati wa mazungumzo hayo masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususan katika nyanja za elimu, afya na uwekezaji. Kulia kwa Mhe. Membe ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana.
Mhe. Fahmy (wa nne kutoka kushoto) kwa pamoja na ujumbe wake  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mkutano wao.
Mhe. Membe akizungumza.
Mhe. Fahmy akieleza jambo wakati wa mazungumzo.
Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Fahmy (hayupo pichani)
Ujumbe wa Tanzania wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani)
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani).

Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Vincent Kibwana (kushoto) akiwa na Balozi wa Misri hapa nchini, Mhe. Hossam Moharam wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakisubiri kumpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil Fahmy ambaye anatarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil Fahmy (kulia) akiongozana na Mhe. Balozi Moharam mara baada ya kuwasili nchini.
Mhe. Fahmy akisalimiana na Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri waliopo hapa nchini

Mhe. Fahmy akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili nchini.
Mhe. Fahmy akimsikiliza Balozi Kibwana wakati akifafanua jambo kwake mara baada ya kuwasili nchini
Mhe. Fahmy akizungumza na Balozi Moharam
Balozi Moharam akijadili jambo na Balozi Kibwana mara baada ya kumpokea Mhe. Fahmy.

Thursday, February 20, 2014

Waziri Membe azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari ( hawapo pichani) juu ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kiamataifa katika Ofisi za Idara ya Habari (Maelezo). Wakati wa Mkutano huo Mhe. Membe alizungumzia masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutetea suala la Uraia wa Nchi mbili kwa Watanzania waishio ughaibuni kupitia Bunge Maalum la Katiba, Kuchaguliwa tena kwa Tanzania kwenye Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, Nafasi ya Tanzania katika Ulinzi wa Amani duniani na kuendelea kudumisha  Uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Rwanda. Wengine katika ni  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajabu Gamaha (wa pili kutoka kushoto), Balozi Simba Yahya (wa kwanza kushoto),  Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati na Bw. Assah Mwambene Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo).

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (wa kwanza kushoto) akisikiliza kwa makini mkutano kati ya Mhe. Waziri Membe na Waandishi wa Habari (hawapo pichani). Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya  Habari, Bi Zamaradi Kawawa na  Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasilano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga.
Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati yao na Mhe. Membe.
Mhe. Waziri Membe akisikiliza maswali kutoka kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) alipozungumza nao. Mkurugenzi wa Afrika, Balozi Vincent Kibwana (wa pili kulia) na Bibi Rosemary Jairo (wa kwanza kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora wakati wa mkutano huo.


Picha na Reginald Kisaka 

Naibu Katibu Mkuu ashiriki maadhimisho ya mwaka mpya wa China

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza kwenye halfa ya kuadhimisha mwaka mpya wa China, iliyoandaliwa na Benki ya Standard Chartered na kufanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro, Dar es Salaam. Wakati wa hafla hiyo Balozi Gamaha aliupongeza Ubalozi wa China katika kusaidia na kuchangia maendeleo ya Tanzania. Pia Balozi Gamaha aliipongeza Benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na Ubalozi wa China nchini katika kurahisisha  biashara kati ya Tanzania na China. 
Balozi wa  Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe. Lv Youqing akitoa neno la shukrani kwa Benki ya Standard Chartered kwa kuandaa hafla hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Lizzy Lloyd akizungumza wakati wa hafla hiyo.

Wageni waalikwa walioshiriki hafla hiyo.
Balozi Gamaha (kulia) akimsikiliza Bw. Nathaniel Kaaya,  Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa hafla hiyo. Wengine wanaosikiliza  kutoka kushoto ni Bw. Iman Njalikai na Bw. Emmanuel Luangisa, Maafisa Mambo ya Nje.
Balozi Gamaha akizungumza na Waandishi wa Habari.




Picha na Reginald Kisaka

Wednesday, February 19, 2014

Makatibu Wakuu Zanzibar wapigwa msasa kuhusu mchakato wa uanzishwaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Balozi Celestine Mushy (wa kwanza kushoto kwa waliokaa), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika picha ya Pamoja na Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu wa Serikali ya Zanzibar baada ya kikao cha IMTC. Balozi Mushy alitumia kikao hicho kuwasilisha mada kuhusu mchakato wa uanzishwaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa ambayo yatachukuwa nafasi ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia


Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Zanzibar (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mushy (kulia) na Balozi Silima Haji, Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar mara baada ya kukamilika kikao cha IMTC.


Monday, February 10, 2014

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inapenda kukanusha taarifa za uvumi zinaosambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na vyombo vya habari kuwa kuna Watanzania wapatao 160 wamenyongwa nchini China kwa kosa la kusafirisha madawa ya kulevya.

Wizara inapenda kuujulisha Umma kuwa hakuna Mtanzania yeyote aliyenyongwa kama inavyodaiwa kwenye mitandao na vyombo vya habari.

Aidha, taarifa hiyo ya uvumi imedai kuwa ndugu wa mmoja wa Watanzania hao ambaye kwa jina anajulikana kama Bw. Rajab Mohamed Ismail Mapusa wamekaa matanga kuomboleza kifo chake.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Serikali ya China, Bw. Mapusa yupo hai gerezani akitumikia kifungo cha maisha kwa kosa la kuingiza madawa ya kulevya nchini humo, na hivi karibuni alishiriki kuandaa maonyesho ya utamaduni wa Kiafrika wakati wa kuadhimisha sherehe za Mwaka Mpya wa China.

Wizara inapenda kuwakumbusha Wanahabari kuandika taarifa ambazo ni sahihi zisizopotosha Umma kwa kuzingatia weledi, maadili na ukweli kutoka mamlaka zote husika.

 

Imetolewa na: Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam

10 Februari, 2014

Friday, February 7, 2014

Wizara kutengeneza Database ya Diaspora kwa kushirikiana na IOM

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akizungumza wakati wa kikao kuhusu uundwaji wa Database na Tovuti kuhusu masuala ya Diaspora. Kikao hicho kiliwashirikisha Wajumbe kutoka Ofisi ya Rais Zanzibar, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uhamiaji na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji hapa nchini (IOM).
Wajumbe kutoka IOM, Ofisi ya Rais Zanzibar na Uhamiaji wakimsikiliza Bibi Jairo (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho
Mwakilishi kutoka IOM, Bi. Mia Immelback akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Bibi Jairo (wa pili kulia) akiwa na Wajumbe wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Mwakilishi wa IOM (hayupo pichani). Kutoka kushoto ni Bw. Mkumbwa Ally, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasialiano katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Kalumuna, Mkuu wa Kitengo cha ICT, Wizara ya Mambo ya Nje na Bi. Susan kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.
Bw. Kalumuna akichangia jambo wakati wa kikao hicho.

Picha na Reginald Kisaka.


Mkataba kuhusu Ujenzi wa Taasisi ya kuweka kumbukumbu za kazi za iliyokuwa Mahakama ya ICTR wasainiwa.

        Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha (kulia) pamoja na Katibu Mkuu Msaidizi wa masuala ya Sheria katika Umoja wa Mataifa, Bw. Stephen Mathias (kushoto) wakisaini Mkataba kuhusu  "Suplementary Agreement to the Agreement between the United Republic of Tanzania and the United Nations concerning the Headquarters of the International Residual Mechanism for Tribunals". Taasisi hii ya Kimataifa itajengwa Jijini Arusha eneo la Lakilaki kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya kazi za iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR).

     Balozi Gamaha akibadilishana Mkataba huo na Bw. Mathias mara baada ya kuusaini

Balozi Gmaha akizungumza mara baada ya kusaini mkataba. Kulia ni Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Tanzania kwenye Uwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa, New York, Marekani

Bw. Mathias kutoka Umoja wa Mataifa naye akizungumza mara baada ya kusaini Mkataba

Wajumbe waliokuwepo wakati wa kusainiwa Mkataba huo


Picha na Reginald Kisaka

Thursday, February 6, 2014

Mhe. Rais Kikwete alipokutana na Waziri wa Maendeleo wa Canada

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada, Mhe. Christian Paradis mara baada ya Waziri huyo kuwasili Ikulu. Mhe. Paradis alitembelea Tanzania hivi karibuni kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchini hizi mbili.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Alexandre Leveque.
Mhe. Rais Kikwete katika mazungumzo na Mhe. Paradis.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Paradis pamoja na Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (wa kwanza kulia), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb.), (wa pili kulia), Waziri wa Fedha, Balozi wa Canada hapa nchini, Mhe. Leveque (wa kwanza kushoto) na Wajumbe wengine.

Picha na Reginald Kisaka.

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiaano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada, Mhe. Christian Paradis walipokutana kwa mazungumzo rasmi katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb.). Mhe. Paradis alifanya ziara hapa nchi hivi karibuni kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya Tanazania na Canada.
Mhe. Membe katika mazungumzo na Mhe. Paradis.


Mhe. Membe na Mhe. Mkuya na wajumbe wengine wakati wa mazungumzo na Mhe. Paradis (hayupo pichani) . Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu.

Mhe. Paradis na Ujumbe wake akiwemo Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Alexandre Leveque (wa nne kutoka kushoto) wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)

Mhe. Mkuya akiagana na Mhe. Paradis mara baada ya mazungumzo huku Mhe. Membe akishuhudia.

Picha na Reginald Kisaka

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada atembelea Tanzania


 Waziri wa  Maendeleo  ya Kimataifa wa Canada, Mhe. Christian Paradis' (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya  Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu mara baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya siku mbili kuanzia tarehe  3-4 Februari, 2014. Akiwa nchini Mhe. Paradis atashiriki Kongamano kuhusu Afya ya Mama na Mtoto.
Mhe. Waziri   Paradis' (kulia) akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Benno Ndulu mara baada ya kuwasili nchini.
Balozi Msechu akibadilishana mawazo na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Alexandre Leveque
Balozi Msechu skizungumza na Mhe. Paradis mara baada ya kumokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Picha na Reginald Kisaka