Saturday, May 24, 2014

Maadmisho ya Siku ya Afrika kufanyika Jumapili


Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vicent Kibwana akiwa katika mkutano na waandishi wa Habari kuelezea maadhimisho ya Siku ya Afrika yatakayofanyika katika Viwanja vya Karimjee siku ya Jumapili tarehe 25 Mei, 2014. wengine katika picha ni Mhe. Meja Gen. Edzai Chimonyo (kushoto), Kaimu Mkuu wa Mabalozi wa nchi za Afrrika ambaye pia ni Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania na Balozi wa DRC nchini Tanzania, Mhe. Juma Mpango (kulia). kaulimbiu ya mwaka huu ya siku ya Afrika ni Kilimo na Usalama wa Chakula ambapo Waheshimiwa Mabalozi walisisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kutoa kipaumbele katika sekta ya kilimo kwa kutengeneza sera nzuri za umiliki wa ardhi ili itumike kama dhamana katika taasisi za fedha. 

Balozi wa kenya nchini Tanzania akichangia mada kuhusu kaulimbiu ya Siku ya Afrika.

Waheshimiwa Mabalozi wa Nchi za Afrika nchini Tanzania na wana habari wakiendelea na mkutano.

Thursday, May 22, 2014

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Marekani nchini



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Marekani nchini, Mhe. Mark Childress IKULU, Dar es Salaam tarehe 22 Mei, 2014.
Mhe. Childress akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili IKULU.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Childress  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Childress  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Victoria Mwakasege
Balozi Childress akisalimiana na Afisa Dawati la Ulaya na Amerika  katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Redemptor Tibaigana.


Mhe. Rais Kikwete katika mazungumzo na Balozi Childress
Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Balozi Childress
Picha ya Pamoja
Brass Band ikipiga wimbo wa Taifa la Marekani mara baada ya Balozi wa Marekani kuwasili IKULU kwa ajili ya kuwasilisha Hati zake za utambulisho kwa Rais.


Picha na Reginald Philip 















Monday, May 19, 2014

Mfanyakazi Hodari wa Wizara na Wafanyakazi Bora wapokea vyeti vyao

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Dushhood Mndeme akijiandaa kutaja majina ya Wafanyakazi Bora wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwemo Mfanyakazi Hodari  wakati wa Kikao cha 8 cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Waliokaa ni Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. John Haule (mwenye miwani), Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha (wa kwanza kulia), Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Cosato Chumi (mwenye tai nyekundu) na Naibu Katibu wa Baraza la Wafanyakazi na Bi. Asya Hamdani.
Baadhi ya Wafanyakazi Bora wakiwa na nyuso za furaha.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Haule akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Hodari wa Wizara Bw. Bujiku Sakila kutoka Idara ya Afrika.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Ally Kondo.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Bi. Asya Hamdani.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Sera na Mipango,  Bw. Elly Chuma.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya DIASPORA, Bw. Seif Kamtunda.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Bw. Ibrahim Mamboya.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Gloria Mboya.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Batholomeo Jungu.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Rose Kitandula.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi wa Kada ya Makatibu Muhtasi , Bi. Faith Masaka.
Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Kada ya Wahudumu, Bi. Hadija Mwichande.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakifuatilia tukio la utoaji vyeti kwa Wafanayakazi Bora wa Wizara
Bw. Iman Njalikai, Mwenyekiti wa TUGHE wa Wizara akizungumza mara baada ya utoaji vyeti kwa Wafanyakazi Bora wa Wizara.

Katibu Mkuu akibadilishana neno na baadhi ya Wajumbe mara baada ya kikao.

Friday, May 16, 2014

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Vietnam awasili nchini kwa ziara ya kikazi



Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Vietnam, Mhe. Nguyen Phuong Nga mara baada ya kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Mhe. Nguyen yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tano.




Mhe. Dkt. Maalim na Mhe. Nguyen wakizungumza huku Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Vo Thanh Nam (kushoto), Bw. Nathaniel Kaaya (kulia), Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Asia na Australasia na Bw.Emmanuel Ruangisa, Afisa Mambo ya Nje  wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mhe. Nguyen akimkabidhi zawadi Dkt. Maalim mara baada ya mazungumzo yao.


Press Release

PRESS RELEASE
H.E President Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.M. King Harald V of Norway on the occasion to celebrate 200 years Anniversary of the Norwegian Constitution on 17th May, 2014.

“Your Majesty King Harald V,
   The King of Norway,
   Oslo,
   NORWAY.

It is my pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to extend to Your Majesty and through you to the people of Norway my heartfelt congratulations on the occasion to celebrate your Constitution Day.
The celebration of your Constitution Day offers me yet another opportunity to reiterate my personal commitment and that of my Government towards our shared aspirations in further strengthening the healthy relations that happily exist between our two countries and peoples. I am confident that the bonds of friendship and co-operation that our two countries enjoy will continue to grow in greater heights for our mutual benefit.
Please accept, Your Majesty, my best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of Norway.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International

Co-operation, Dar es Salaam



16th May 2014

Thursday, May 15, 2014

Balozi wa Tanzania nchini Urusi aapishwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha  Lt. Gen. Wynjones Mattew Kisamba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 15 Mei 2014.
Picha ya Pamoja
Mhe. Rais Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na Familia ya Balozi Kisamba

Balozi Kisamba akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Bibi Victoria Mwakasege mara baada ya kuapishwa.

Picha na Reginald Philip


VACANCY ANNOUNCEMENT - ICGLR


VACANCY ANNOUNCEMENT




SOUTHERN AFRICAN DEVELOPMENT COMMUNITY

VACANCY ANNOUNCEMENT


Background

The Southern African Development Community (SADC) currently has fifteen Member States with a population of approximately 250 million people and a combined GDP of USD 467.3 billion (2006). The overall objective of SADC is to achieve development and economic growth, which is to be attained through increased regional integration, built on democratic principles and equitable and sustainable development.

The Southern African Development Community (SADC) is made up of Angola, Botswana, Democratic Republic of the Congo, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Mozambique, Namibia, Seychelles, South Africa, Swaziland, Tanzania, Zambia, Zimbabwe

It is following this background that SADC Secretariat wishes to invite suitably qualified, experienced citizens of SADC to apply for the following positions tenable at its Headquarters in Gaborone, Botswana:

Position Job Grade
1. Programme Officer –Cereal Production 6
2. Programme Officer-Competition Policy 7

Remuneration

The SADC Secretariat offers a competitive package for all the positions listed below.

Job Grade Average Package Per Annum:
Job Grade 6 US$ 91,717
Job Grade 7 US$ 87,148

Submission of Applications
Applications must be submitted to the:

Permanent Secretary,
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation
Attn: SADC National Contact Point,
P. O. Box 9000,
DAR ES SALAAM.
Fax: + 255 222 116600 or
+ 255 222 120529
Email:nje@foreign.go.tz

Closing Date: Not later than 16th May 2014:

Your application should accompany the following: REF: SADC/2/3/3/3
a) a short covering letter stating the position that you want to be considered for and describe how your qualifications, experience and competencies are relevant to the position;
b) a detailed and updated curriculum vitae;
c) certified copies of your degree(s), Diploma(s) and Certificate(s); and
d) duly completed SADC Application Form.

Should you be shortlisted, you will be required to produce evidence of any educational and professional qualifications supporting your application, on the day of your interview.

Gender Mainstreaming
SADC is an equal opportunity employer and particularly encourages applications from female candidates.

If you are results oriented, you have a passion for the transformation and development of Southern Africa, and possess the required competencies, please submit your application.

Only applicants, who meet the requirements of the SADC Secretariat and being considered for interview, will be contacted. Should you not hear from the SADC Secretariat within four weeks after the closing date, kindly consider your application as unsuccessful.

For further details on the position that you want to apply for, job profiles and SADC Application Form, refer to the SADC Website: www.sadc.int

Details can also be obtained from the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation.

ISSUED BY THE MINISTRY OFBFOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM.

15TH MAY 2014

Waziri Membe afungua Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Mambo ya Nje


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)-katikati) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa tatu kutoka kushoto) na viongozi wengine wakiimba wimbo wa "Solidarity" wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Mei, 2014.
Mhe. Membe akitoa hotuba ya ufunguzi wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambapo alitoa rai kwa Wafanyakazi hao kujituma na kuongeza bidii katika utendaji kazi wao wa kila siku.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Waziri Membe alipofungua kikao cha Baraza hilo.
Katibu Mkuu, Bw. Haule nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo.

Baadhi ya Wajumbe wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati akizungumza. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Dushhood Mndeme.
Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Bibi Naomi Zegezege nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo huku Mhe. Membe na Viongozi wengine wakimsikiliza.
Kikao kikiendelea.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Baloiz Vincent Kibwana akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo.
Katibu Mkuu, Bw. Haule, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha na Viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mambo ya Nje.
Waandishi wa Habari nao pia walikuwepo.
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mara baada ya kulifungua.

Picha na Reginald Philip



Press Release



H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania addressed to H.E. Abdullah Gül, President of the Republic of Turkey following the tragic mining disaster, which occurred in Soma, Turkey on 14th May, 2014. The message reads as follows:

His Excellency,
Abdullah Gül,
President of the Republic of Turkey,
ANKARA.

Your Excellency and Dear Brother,

I have received with profound sorrow and shock the sad news about the tragic accident caused by terrible explosion at a coal mine in Soma, Turkey and claimed ……lives of more than 200 people.

On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania, and indeed on my behalf, I wish at this difficult time, to express our deepest sympathies and condolences to you and through you express our deepest sympathies and condolences to you and through you to the bereaved families and relatives. We pray that the Almighty God give the families and relatives of the deceased strength and fortune to bear at this moment of agony distress.

May the Almighty God bring rapid and complete recovery to the injured and rest the souls of the deceased in eternal peace.

Please accept, Your Excellency and Dear Brother, the assurance of my highest consideration.





Jakaya Mrisho Kikwete
PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA



Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation






Wednesday, May 14, 2014

Mhe. Membe amuaga Marehemu Balozi Flossie nyumbani kwake Malawi




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisoma kwa majonzi Salamu za Pole za Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Rais wa Malawi, Mhe. Joyce Banda kufuatia kifo cha ghafla cha aliyekuwa Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Marehemu Flossie Gomile-Chidyaonga. Mhe. Waziri Membe alisoma salamu hizo wakati wa kumuaga Marehemu Balozi Flossie tukio hilo lilifanyika nyumbani kwa marehemu Kitongoji cha Limbe katika mji wa Blantyre nchini Malawi. Mhe. Membe alimwakilisha Rais Kikwete kwenye mazishi ya Balozi Flossie yaliyofanyika tarehe 14 Mei, 2014.
Mhe. Membe akiendelea kusoma salamu hizo huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Ephraim Chiume (mwanye tai nyeusi) na Mume wa Rais wa Malawi, Jaji Mkuu Mstaafu, Banda (wa kwanza kulia mstari wa kwanza) wakimsikiliza.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Mhe. Membe akimkabidhi Mhe. Chiume Salamu hizo mara baada ya kuzisoma.
Mhe. Chiume nae akisema machache wakati wa shughuli za kumuaga Balozi Flossie. Katika maelezo yake Mhe. Chiume kwa niaba ya Serikali ya Malawi alitoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa wakati wote wa msiba wa Marehemu Balozi Flossie.
Mhe. Chiume akimtambulisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule ambaye alikuwa miongoni mwa wajumbe waliofuatana na Mhe. Membe nchini Malawi.
Baba Mdogo wa Marehemu Balozi Flossie, Dkt. Joseph Gomile nae akitoa neno wakati wa shughuli hizo za kumuaga Marehemu Balozi Flossie. Dkt. Gomile ambaye   anaishi nchini Tanzania kwa kipindi kirefu sasa nae aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango mkubwa katika msiba huo mzito wa mtoto wake.
Mhe. Membe. Mhe. Chiume na Mhe.  Jaji Mstaafu Banda wakimsikiliza Dkt. Gomile (hayupo pichani)
Baadhi ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa nchini waliomsindikiza mwenzao Marehemu Balozi Flossie nao wakifuatilia matukio.
Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Baloz Flossie kama linavyoonekana katika eneo la nyumbani kwake likiwa limezungukwa na waombolezaji.
Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. PatrickTsere  (kushoto)  akiwa na Balozi Vincent Kibwana, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Malawi hapa nchini mara baada ya shughuli za kuaga mwili wa Marehemu Balozi Flossie kumalizika.
Baadhi ya viongozi wa dini waliokuwepo.
Viongozi mbalimbali walioshiriki kumuaga Balozi Flossie katika eneo la nyumbani kwake kabla ya mazishi.
Marafiki wa Marehemu Balozi Flossie wakiwa katika simanzi kufuatia kifo cha mpendwa wao.
Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Mabalozi aliofuatana nao nchini Malawi mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere.