Monday, May 12, 2014

Mhe. Membe amwakilisha Mhe. Rais Kikwete kushuhudia uwekaji saini mkataba wa ujenzi wa Reli kati ya Kenya na China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) wa tatu kutoka kushoto waliosimama) kwa pamoja na viongozi wengine   akiwemo Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, Waziri Mkuu wa China, Mhe. Li Keqiang, Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta, Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni na Rais wa Sudan Kusini, Mhe. Salva Kiir wakishuhudia kusainiwa kwa Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya kisasa  Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Kenya na China. Mhe. Membe alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Membe wakati wa mkutano kabla ya mkataba kusainiwa.

Waziri Membe akimsikiliza Waziri Mkuu wa China, Mhe. Li Keqiang wakati wa mazungumzo.

Mkutano wa viongozi ukiendelea.

Rais Museveni akiongea kwa niaba ya viongozi waalikwa waliohudhuria uwekaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Reli kati ya Serikali ya China na Kenya.

Sunday, May 11, 2014

TANZIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa John M. Haule akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Juu ya Kifo cha aliyekuwa Balozi wa Mwalawi nchini Tanzania Hayati Mhe. Flossie Chidyaonga kilichotokea kwenye Hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa Tarehe 09 Mei 2014.

Bwa. John M. Haule akiendelea kuzungumza huku Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Vicent Kibwana (kushoto) akiyafuatilia kwa makini mazungumzo hayo na waandishi wa Habari (hawapo pichani)

Mazungumzo yakiendelea kati ya waandishi wa habari na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Picha na Reginald Philip



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali  imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Mhe. Flossie Gomile Chidyaonga kilichotokea juzi Ijumaa tarehe 09 Mei, 2014. Balozi Chidyaonga alifariki akiwa njiani kupelekwa hospitali ya Aga Khan ya hapa Dar es Salaam.

 Balozi Flossie Chidyaonga alizaliwa tarehe 16 Juni, 1960 huko Blantyre nchini Malawi. Balozi Chidyaonga aliitumikia Serikali ya Malawi katika nyadhifa mbalimbali.  Kati ya mwaka 2006 hadi 2010 alikuwa Naibu Balozi wa Malawi nchini Uingereza na baadaye Kaimu Balozi hadi alipoteuliwa kuwa Balozi wa Malawi hapa Tanzanaia.

Siku ya Jumatatu, tarehe 05 Mei, 2014, Balozi Flossie Chidyaonga alishinda vizuri na kufanya shughuli zake kama kawaida. Hata hivyo, ilipofika usiku,  alijisikia vibaya na kupelekwa hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam ambapo alipatiwa Matibabu na kuwekwa mapunziko kuanzia saa 6 usiku hadi saa 12 asubuhi aliporuhusiwa na kupewa dawa za kutumia nyumbani. Balozi Chidyaonga aliendelea kutumia dawa hizo na hali kuonekana kuimarika hadi siku hiyo ya ijumaa, tarehe 09 Mei, 2014. Siku hiyo, aliamka vizuri hadi ilipofika majira ya saa 6 mchana, hali yake ilipobadilika na kukimbizwa tena hospitali ya Aga Khan ambapo alipokelewa Daktari alisema amekwishafariki. Sasa hivi, Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Uchunguzi wa madaktari umeonesha kuwa marehemu amefariki kutokana na Mshipa Mkuu wa AORTA kuvimba na kupasuka kulikosababisha damu kukusanyika kwenye mfuko wa moyo na hivyo kufanya moyo ushindwe kufanya kazi yake.

Kesho tarehe 12 Mei, 2014 mwili wa Marehemu utachukuliwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kupelekwa kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere ambapo kutafanyika misa ya kumuombea Marehemu na kutoa heshima za mwisho kuanzia saa 4 asubuhi. Mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwenda Blantyre, Malawi siku ya Jumanne tarehe 13 Mei, 2014 na mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano tarehe 14 Mei 2014 huko Blantyer, Malawi.

Katika kipindi chote alichokuwa mwakilishi wa Malawi hapa nchini, Balozi Chidyaonga alifanya kazi yake ya kukuza na kuendeleza ushirikiano kati ya nchi zetu mbili kwa umahiri wa hali ya juu. Siku zote alikuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa Serikali na Mabalozi wenzake wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania.

Mungu aiweke roho ya marehemu Balozi Flossie Chidyaonga, mahali pema peponi.

AMEN

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
 Dar Es Salaam, Tarehe 11 Mei, 2014

Saturday, May 10, 2014

Mikutano ya Waziri Membe na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki na Wafanyabiashara




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wa kwanza kulia na ujumbe wake akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki hayupo pichani jijini Istambul siku ya Ijumaa tarehe 09 Mei, 2014. Mhe. Membe aliliomba Shirika hilo liingie ubia na Shirika la Ndege la Tanzania. Ombi ambalo Mkurugenzi Mtendaji aliahidi kulifanyia kazi ambapo wiki ijayo atatuma timu ya wataalamu ili kuongea na timu ya wataalamu ya ATCL kutathmini namna mashiraka hayo yatakavyoweza kushirikiana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki wa katikati pamoja na timu yake ikimsikiliza kwa makini Waziri Membe hayupo pichani.

Ujumbe wa Tanzania na wa Shirika la Ndege la Uturuki wakiendelea na mazungumzo

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki akifanya power point presentation kuhusu utendaji wa shirika lake na matarajio ya kibiashara katika Bara la Afrika na ulimwengu wote kwa ujumla. Alitaja Bara la Afrika kuwa ni bora zaidi kibiashara katika siku zijazo kutokana na ukuaji wa uchumi wa kasi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (kulia) akimkabidhi zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki
Waziri Membe kushoto naye anapokea zawadi yake kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki
zawadi kwa Waziri Membe.



 Mkutano wa Waziri Membe na Wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (kati) akiwaeleza wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki (baadhi yao wanaonekana katika picha ya chini) fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini Tanzania. Aliwahamasisha waje kuwekeza Tanzania hususan, katika sekta zitakazoongeza ajira kwa wingi kama vile viwanda vya nguo na kilimo. Wafanyabiashara hao walionesha dhamira ya dhati kuja nchini kuangalia fursa walizotangaziwa.

Baadhi ya Wafanyabiashara wa Uturuki na ujumbe wa Tanzania.

Waziri Membe akibadilishana kadi za mawasiliano na Wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki.

Uchaguzi Afrika Kusini ulikuwa huru na wa haki:SADC

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.)-kushoto  akiwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Lesotho na Namibia pamoja na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Dkt. Stergomena Tax (Kulia) wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini. SADC ilikuwa ni miongoni mwa Vyombo vya kikanda na kimataifa vilivyosimamia uchaguzi huo. Katika taarifa yake Waangalizi wa SADC walisema kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru wa haki na uwazi pia amani na utulivu vilitawala.

Baadhi ya Wageni waalikwa na Waandishi wa Habari wakati wa mkutano huo.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Tax.

Friday, May 9, 2014

Naibu Katibu Mkuu akutana na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Afrika nchini Thailand

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza na Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Asia ya Kusini, Mashariki ya Kati na Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Thailand.Bwa. Manopchai Vongpakdi. Bw. Katibu Mkuu huyo anaongoza Ujumbe wa watu tisa  ambao upo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania.
Bwa. Vongpakdi nae akichangia jambo wakati wa akizungumza na
Balozi Rajabu Gamaha.

Mazungumzo yakiendelea huku wajumbe wengine wakifuatilia.
Bw. Manopchai Vongpakdi akimkabidhi Balozi Gamaha zawadi ya michoro mashuhuri nchini Thailand mara baada ya mazungumzo yao.

Picha na Reginald Philip

Matukio mbalimbali ya ziara ya kikazi ya Mhe. Membe nchini Uturuki


Waziri Mkuu wa Uturuki, Mhe. Recep Tayyip Erdogan (kulia) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe (Mb). mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu mjini Ankara, Uturuki tarehe 08 Mei, 2014.
Mazungumzo yanaendelea kati ya Waziri Mkuu wa Uturuki (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania. Mwingine katika picha ni Bibi Victoria Mwakasege, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Waziri Membe kulia akishikana mkono na Waziri Mkuu wa Uturuki mara baada ya viongozi hao kumaliza mazungumzo. 

Mazungumzo kati ya Waziri Membe na Waziri na Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki 

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa aliyevaa shati la njano kulia ukiwa katika mazungumzo na ujumbe wa Uturuki unaongozwa na Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler wa tatu kutoka kushoto. 

Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernard K. Membe akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki
Waziri Membe naye akimpa zawadi ya kinyago Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki 
Mhe. Membe na Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki wakijadili suala baada ya zoezi la kukabidhiana zawadi kukamilika


Mazungumzo ya Waziri Membe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe wa tatu kutoka kushoto na ujumbe wakijadili masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano na Uutruki na ujumbe wa Uturuki unaonekana katika picha ya chini.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu wa pili kutoka kulia akiwa na ujumbe wake wakati wa mazungumzo na Mhe. Membe.

Mkutano na Waandishi wa Habari


Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe akihutubia Mkutano wa Waandishi wa Habari huku akimshika mkono Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu
Waziri Membe akiendelea kuwahutubia waandishi wa habari hawapo pichani


Mapokezi ya Mhe. Membe nchini Uturuki


Waziri Membe akipeana mikono na watu waliofika Uwanja wa Ndege wa Ankara kumpokea
Waziri Membe kushoto akibadilishana mawazo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania katika Chumba cha Wageni Maalum kwenye Uwanja wa Ndege wa Ankara
Waziri Membe akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia ambaye pia anawakilisha Uturuki aliyekaa kushoto pamoja na Bw. Salvator Mbilinyi, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia aliyechutama wakibadilishana machache katika Chumba cha Wageni Maalum ndani ya Uwanja wa Ndege wa Ankara.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana na Naibu Meya wa jiji la Ankara ambaye naye alikuja Uwanja wa Ndege kumlaki


Naibu Meya wa jiji la Ankara aliyeketi kushoto akibadilishana mawazo na Mhe. Membe kabala ya kuondoka kutoka katika kiwanja hicho

Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, Bw. Frank Muhina akiwa kazini kunukuu mambo mbalimbali kutoka kwa Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki. 



Na Ally Kondo, Uturuki

 WATURUKI WAHIMIZWA KUWEKEZA TANZANIA

Waturuki wenye mitaji wamehimizwa kuja Tanzania kuchangamkia fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Uturuki tarehe 08 na 09 Mei, 2014.
Katika ziara hiyo, Waziri Membe aliweza kuonana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Kitaifa wa Serikali ya Uturuki akiwemo Waziri Mkuu, Mhe. Recep Tayyip Erdogan; Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler; Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Ahmet Dovutoglu na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Lutfi Elgan.
Aidha, Mhe. Waziri na mwenyeji wake, Mhe. Dovutoglu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi habari pamoja na kushiriki chakula cha mchana na wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki.  
Mhe. Waziri alieleza kuwa Tanzania ina fursa nyingi za uwekezaji ambazo hazijatumiwa ipasavyo, hivyo ni muda muafaka kwa Waturuki kuwekeza mitaji yao nchini Tanzania kwa faida ya pande zote.
Baadhi ya maeneo ambayo yatakuwa na faida kubwa endapo yatapata wawekezaji ni pamoja na sekta ya usafiri wa anga. Hivyo,  Mhe. Waziri alilihamasisha Shirika la Ndege la Uturuki kuangalia uwezekano wa kuingia ubia na Shirika la Ndege la Tanzania. “Endapo Shirika la Ndege la Tanzania litapata mwekezaji, likawa na ndege za kutosha na kwa sababu Tanzania imezunguukwa na nchi nyingi, wasafiri wengi wa nchi hizo, watatumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuunganisha safari zao kwenda nchi za Ulaya”. Mhe. Membe alisikika akiwambia Viongozi wa Uturuki pamoja na wafanyabiashara wakubwa
Waziri Membe pia aliwahahakishia wawekezaji wa Uturuki watakaokuwa na dhamira ya kuwekeza nchini, kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) itatoa eneo maalum ili wawekezaji hao waweze kujenga viwanda vya uzalishaji. Alisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika viwanda vya nguo, mbolea, gesi, zana za kilimo, miundombinu ya umwagiliaji, umwagiliaji wa matone  pamoja na viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, nyama na maziwa. Alisema endapo sekta hizo zitafanyiwa kazi ipasavyo basi ukuaji wa uchumi utaenda sambamba na ustawi wa maisha ya watu wa kawaida, kwa sababu sekta hizo zitaongeza ajira kwa maelfu ya vijana wa Tanzania.
Aliendelea kueleza kuwa ili ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki uendelee kuimarika, Serikali itatimiza ahadi yake ya kufungua Ubalozi nchini Uturuki katika mwaka wa Fedha 2014/2015.
Kwa upande wao, Viongozi wa Uturuki walimuhakikishia Mhe. Membe kuwa watawahamasisha wafanyabiashara wa Uturuki kuja kuwekeza Tanzania. Walisema kazi hiyo kwao ni nyepesi na wanahakika itapokelewa vizuri na jumuiya ya wafanyabiashara kwa sababu Tanzania mbali na kuwa na fursa nyingi, pia  ina utulivu wa kisiasa ambao ni kigezo muhimu katika uwekezaji. 
Katika hatua nyingine, Mhe. Membe aliishukuru Serikali ya Uturuki kwa kitendo chake cha kukubali wanamichezo 10 wa Tanzania kuweka kambi ya mafunzo kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Scotland mwezi wa Julai, 2014.
Sanjari na shukrani hizo, alimshukuru pia Balozi wa Uturuki nchini Tanzania na Mke wake kwa jitihada zao za kunusuru maisha ya watu wenye ualbino. Alisema uamuzi wao wa kujenga kijiji ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchukuwa watu wenye ualbino 500 kwa ajili ya kuwapa elimu na stadi nyingine za maisha ni mfano wa kuigwa na jamii ya wasamalia wema.  
Vile vile, Mhe. Waziri aliishukuru Uturuki kwa kulisaidia Shirika la Utangazaji la Taifa Tanzania (TBC)  kwa kulipa vifaa na teknolojia ya kisasa. Alisema kabla  ya msaada huo, TBC ilikuwa inafanya kazi katika mazingira magumu.


Thursday, May 8, 2014

Naibu Waziri aongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye uchaguzi Afrika Kusini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya wakielekea kwenye moja ya Vituo vya kupigia kura wakati wa  Uchaguzi Mkuu wa Rais nchini humo uliofanyika tarehe 7 Mei, 2014. Mhe. Dkt. Maalim anaongoza ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi  kutoka Tanzania kama nchi mwanachama wa SADC na pia  mjumbe wa Asasi ya Ulinzi, Siasa na Usalama ya SADC. 


Mhe. Dkt. Maalim akiwa na Waangalizi wengine kwenye moja ya vituo vya kupigia kura mjini Pretoria kabla ya zoezi la upigaji kura kuanza.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waangalizi wa Uchaguzi kwenye Kituo cha Taifa cha Kuratibu Matokeo. Kwa nyuma ni screen zinazoonesha matokeo kutoka sehemu mbalimbali za nchi yanavyoingia.

Press Release

H.E. Vladimir Putin, President of the Russian Federation.

PRESS RELEASE


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Vladimir Putin, President of the Russian Federation on the occasion of the National Day of Russia –Victory Day, on 9th May 2014. The message reads as follows:

“H.E. Vladimir Putin,
President of the Russian Federation,  
Moscow

RUSSIA


Your Excellency and Dear Colleague,

On the occasion of the celebration of your country’s National Day, I would like to convey to you and through you to the Government and people of Russia my most heartfelt congratulations.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries. On this historic day, I take this opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Russia”.


Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation,Dar es Salaam

08th May 2014








Wednesday, May 7, 2014

Press Release


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency MiloÅ¡ Zeman, President of the Czech Republic on the occasion of his country’s Liberation Day on the 8th May.

The message reads as follows;

“His Excellency MiloÅ¡ Zeman,
 President of the Czech Republic,
 Prague,

 CZECH REPUBLIC.


Your Excellency,

        On behalf of the people and government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I wish to convey my sincere congratulations to you, the people and the government of Czech Republic on the occasion of the Liberation Day of Czech Republic.

Tanzania values the close ties of friendship and co-operation and the warm and friendly relations between our two countries and the people.

I am confident that with the good will and understanding on both sides, the bilateral relations between Tanzania and Czech will continue to flourish as both countries pursue the shared ideas and objectives for the benefit of the two countries and peoples.

Please accept, your Excellency, my best wishes for your personal good health and peace and prosperity for the people of Czech Repulic”.

Issued by:  Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania, Dar es Salaam.

7th May, 2014


Tuesday, May 6, 2014

Waziri Membe Ziarani Uturuki



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



 Waziri wa Mambo   ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) atafanya ziara ya kikazi ya siku tatu nchini Uturuki kuanzia tarehe 07 – 09 Mei, 2014 kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Mhe. Ahmet Davutoglo. Madhumuni ya ziara hiyo ni kukuza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki ambao umedumu kwa kipindi kirefu sasa.

Aidha, katika ziara hiyo Mhe. Membe na mwenyeji wake watajadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki hususan, katika maeneo ya vipaumbele yaliyoainishwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Afrika na Uturuki uliofanyika mwaka 2008. 

Maeneo hayo ni pamoja na biashara, uwekezaji, kilimo, mawasiliano, afya, elimu pamoja na amani na usalama.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri ataonana na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa Uturuki akiwemo mwenyeji wake, Mhe. Davutoglo; Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler; Waziri wa Uchukuzi, Usafiri wa Majini na Mawasiliano, Mhe. Lutfi Elvan; Waziri wa Nishati na Maliasili, Mhe. Tarrer Yildiz pamoja na kuongea na wafanyabiashara wa Uturuki.

Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri atafuatana na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa; Wizara ya Viwanda na Biashara; Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika; Mamlaka ya Majengo Tanzania na Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA).

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es salaam.
 6 Mei 2014.
  

Friday, May 2, 2014

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje washiriki Sherehe za Mei Mosi

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakisheherekea Siku ya Wafanyakazi Duniani, iliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "UTAWALA BORA UTUMIKE KUTATUA KERO ZA WAFANYAKAZI"

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa kati maandamano
Maandamano yakiwa yameshika kasi
Maandamano yakiendelea
Rais wa Jamhuri ya Muungano akiwapungia mkono Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani) walipopita kwa heshima mbele yake.
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakiwa wamejawa na furaha na bashasha.





Picha na Reginald Philip

Press Release

PRESS RELEASE


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to to H.E. BronisÅ‚aw Komorowski, President of Poland on the occasion of the National Day of Poland –Constitutional Day, on 3rd May 2014. The message reads as follows:

President of Poland
Warsaw

POLAND


Your Excellency and Dear Colleague,

On behalf of the people of Tanzania and on my own behalf, I would like to extend to you and through you to the Government and people of Poland my heartfelt congratulations on the occasion of your country’s National Day.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries.  On this historic day, I take the opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Poland”.


Issued by: Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam.

02nd May 2014