Tuesday, June 17, 2014

Balozi wa China nchini, Lu Youqing akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Li Yuanchao.

Balozi wa China nchini,Lu Youqing (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Watu wa China Mhe. Li Yuanchao katika ukumbi wa mikutano wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini China ,Luteni Jenerali Mstaafu Abdulrahman Shimbo .

Balozi wa China nchini,Lu Youqing(kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Watu wa China Mhe. Li Yuanchao katika ukumbi wa mikutano wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Balozi wa Tanzania nchini China ,Luteni Jenerali Mstaafu Abdulrahman Shimbo na wakwanza kutoka kushoto ni  Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiruikiano wa Kimataifa Balozi Mbelwa Kairuki.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Balozi wa China nchini,Lu Youqing (hayupo pichani).

Mazungumzo yakiendelea


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKUTANO WA KATIBU MKUU, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU ZIARA YA MHE. LI YUANCHAO, MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA WATU WA CHINA, NCHINI TANZANIA, DAR ES SALAAM
TAREHE 18 JUNI, 2014


·       Wakurugenzi wa Idara na Wakuu wa Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje,
·       Ndugu waandishi wa Habari wa vyombo vya habari vya umma na binafsi,
·       Mabibi na Mabwana,

Ndugu Waandishi,
Tumekutana hapa leo kwa lengo la kufahamishana kwa muhtasari kuhusu ziara ya Mheshimiwa, Li Yuanchao, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, nchini. Makamu huyo wa Rais wa China, anatarajiwa kufanya ziara rasmi nchini kuanzia tarehe 21 hadi 26 Juni 2014. Lengo la ziara hiyo, ni kuimarisha mahusiano ya karibu na ya kidugu kati ya nchi hizi mbili ambayo mwaka huu yamefikisha miaka hamsini tangu kuasisiwa rasmi mwaka 1964.



Ndugu Waandishi,
Mheshimiwa Li Yuanchao atawasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tarehe 21 Juni 2014 amnapo atatembelea vivutio vya utalii vilivyopo Mkoa wa Arusha hususan Bonde la Ngorongoro tarehe 22 Juni 2014 na jioni atawasili jijini Dar es Salaam kuendelea na ziara yake hiyo.

Ndugu Waandishi,
Kama mnavyofahamu, ziara hii inakuja wakati muafaka ambapo tunaelekea katika kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania. Kadhalika, huu ni mwendelezo wa ziara mbalimbali zinazofanywa na Viongozi wa ngazi za juu wa pande zote mbili ambazo zimekuwa ni chachu katika kufikiwa kwa makubaliano mbalimbali hususan ya kiuchumi kwa manufaa ya pande zote mbili. 

Ndugu Waandishi,
Akiwa jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Li Yuanchao, atakutana na kufanya mazungumzo na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa kati ya tarehe 23 na 26 Juni 2014 pamoja na kufungua Jukwaa la Kiuchumi kati ya Tanzania na China. Miongoni mwa Viongozi atakaokutana nao ni Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyeji wake Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vilevile, Mheshimiwa Li Yuanchao atatembelea Zanzibar tarehe 25 Juni 2014 ambapo atakutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Balozi Seif Idi, Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kurejea Dar es Salaam tarehe 26 Juni 2014 tayari kwa safari ya kuelekea nchini China.

Ndugu Waandishi,
Ikumbukwe kuwa, Tanzania na China si tu zimekuwa zikishirikiana katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi na kisiasa lakini wamekuwa ni marafiki wakati wa shida na wa raha. Hili linadhihirishwa na mikataba takribani 17 ambayo nchi hizi mbili zilikubaliana mwezi Machi 2013 wakati wa ziara ya Mhe. Xi Jinping, Rais wa Jamhuri ya Watu wa China nchini.

Hivyo, mazungumzo kati ya Mheshimiwa Li Yuanchao na viongozi wetu Wakuu wa Kitaifa yatajikita zaidi katika kuimarisha zaidi ushirikiano uliopo wa kiuchumi, kisiasa na kijamii kati ya nchi hizi mbili pamoja na kuibua maeneo mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya pande zote mbili.





Ndugu Waandishi,
Ni matumaini yangu mimi binafsi, Wizara pamoja na Serikali kwa ujumla kwamba wakati wote Mheshimiwa Li Yuanchao atakapokuwa nchini tutapata ushirikiano wa kutosha kutoka kwenu na wadau wengine.

Itoshe tu kusema kwamba Tanzania na China zitaendelea kufanya juhudi za pamoja katika kuimarisha ushirikiano wa kirafiki, katika sekta mbalimbali, na kuhimiza uhusiano na ushirikiano wa kiuchumi ili kunufaisha pande zote mbili.

Mwisho Ndugu Waandishi wa Habari, napenda kunukuu kauli ya Mwalimu Nyerere, Mwasisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba katika huu Ulimwengu tumekuwa na marafiki wengi sana lakini rafiki mmoja wa kweli ni Jamhuri ya Watu wa China.


……Ahsanteni Sana…


WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Juni 2014                                       Dar es Salaam.


mahojiano baina ya Bw. Omar Mjenga na Cloudstv.


mahojiano kati ya Bw.  Omar Mjenga Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai na CloudsTv yaliyofanyika wakati wa Mkutano wa uwekezaji tarehe 11 Juni 2014.

Thursday, June 12, 2014

Mhe. Membe akutana na Mhe. Mark Simmonds Waziri wa Uingereza anayeshughulikia maswala ya Afrika

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na

Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye mazungumzo na

Mhe. Mark Simmonds, Waziri wa Uimgereza

anayeshughulikia masuala ya Afrika kwenye Wizara ya

Mambo ya Nje ya Uingereza leo tarehe 11 Juni 2014.

Pamoja na mambo mengine, Mawaziri hao wamezungumzia

maazimio ya Mkutano wa Kimataifa kuhusu Ukomeshwaji

wa Udhalilishaji wa kijinsia kwenye maeneo yenye

Migogoro (''End Sexual Violence in Conflict") unaoendelea

mjini London, Uingereza. Tanzania inashiriki Mkutano huo

kufuatia mualiko wa Serikali ya Uingereza kutokana na

mchango mkubwa wa Tanzania katika kufanikisha kuwepo

kwa Tamko la Umoja wa Mataifa linalo husu suala hilo

(Declaration of Commitment to End Sexual Violence in

Conflict).  


Wednesday, June 11, 2014

Uteuzi wa Naibu Mabalozi



UTEUZI WA NAIBU MABALOZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Naibu Mabalozi wawili.

Walioteuliwa ni Bw. Robert Kahendaguza (pichani juu) anayekuwa Naibu Balozi, Ubalozi wa Kudumu kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi, na Bw. Msafiri Marwa (pichani chini) anayekuwa Naibu Balozi wa Tanzania London, Uingereza.

Kabla ya uteuzi huu, Bw. Kahendaguza alikuwa Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Marwa alikuwa Ofisa Mambo ya Nje Mkuu.

Uteuzi huu unaanza tarehe 25 Mei, 2014.

IMETOLEWA NA:
KATIBU MKUU
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM
JUNI 11, 2014




Misri yapata Rais Mpya



Na Ally Kondo, Cairo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) amemwakilisha Rais Kikwete katika sherehe za kumuapisha Mkuu wa Majeshi wa zamani, Field Marshal Abdel Fattah al Sisi kuwa Rais mpya wa Misri. Rais Sisi aliapishwa na Jaji Mkuu katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Misri siku ya Jumapili tarehe 08 Juni, 2014 ambayo ilitangazwa kuwa ni siku ya mapunziko.
Sherehe za uapisho zilihudhuriwa na Viongozi wa nchi mbalimbali duniani, hususan kutoka nchi za Kiarabu na Afrika. Nchi za Kiarabu ziliwakilishwa vizuri katika sherehe hizo kwa kutuma Viongozi wa ngazi ya Juu ukilinganisha na nchi za Afrika ambazo nyingi zilituma Mawaziri wa Mambo ya Nje isipokuwa chache kama vile Somalia, Chadi na Equatorial Guinea ambazo Marais wao walishiriki wenyewe.
Sherehe za uapisho zilipambwa na shughuli mbalimbali ikiwemo gwaride la kijeshi, hotuba za Rais anayengia madarakani na anayetoka na kila mwakilishi kupata fursa ya kusalimiana na kufanya mazungumzo ya muda mfupi na Rais Sisi.
Sherehe hizo ambazo zilifanyika huku kukiwa na ulinzi mkali zilishuhudiwa pia, wafuasi wa Rais Sisi wakizunguka katika mitaa ya jiji la Cairo wakiwa katika magari, pikipiki au kutembea kwa miguu wakiwa wamebeba bendera za nchi hiyo huku wakifyatua fataki, kupiga mayowe na honi.
Wachambuzi wa mambo walieleza kuwa Rais mpya wa Misri anatarajiwa kuituliza nchi hiyo ambayo imekuwa ikikumbwa na machafuko ya kisiasa ya mara kwa mara tangu mapinduzi ya wananchi yaliyomuondoa madarakani Rais Hosni Mubarak mwaka 2011.
Hata hivyo, walikiri kuwa Rais Sisi anakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufufua uchumi wa nchi hiyo ambao umedorora kwa kiasi kikubwa kutokana na machafuko hayo. Changamoto nyingine ambayo Rais Sisi anakabiliwa nayo ni kurejesha mshikamano na umoja wa wananchi wa Misri ambao kwa kiasi kikubwa wametofautiana mitazamo kutokana na hali ya mambo inavyokwenda katika nchi hiyo. 

Taswira ya Ushiriki wa Mhe. Membe katika Sherehe za Kumuapisha Rais wa Misri

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) (kulia) akiwa katiika Kiwanja cha Ndege cha Addis Ababa  akiwa njiani kuelekea Cairo, Misri katika sherehe za kumuapisha Rais Mteule, Mhe. Abdel Fattah al Sisi. Mwingine katika picha ni Bw, Shelukindo, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Waziri Membe (kushoto)  akiongea na Msaidizi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ambaye ana ngazi ya Ukurugenzi kwenye chumba cha Wageni Maalum katika Uwanja wa Ndege wa Cairo alipowasili kwa ajili ya kushiriki sherehe za kumuapisha Rais wa nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje (kulia) akipokea taarifa fupi kutoka kwa Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Misri, Bw. Jestas Nyamanga katika Hoteli aliyofikia Mhe. Waziri ya Fairmont.

Mhe. Waziri Membe mwenye miwani akiwa amesimama mbele ya Hoteli ili kuingia katika gari maalum kwa ajili ya kumpeleka eneo lililofanyika sherehe za uapisho. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana.


Balozi Kibwana (kushoto) akijadili jambo na Afisa wake, Bw. Celestine Kakere

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) kushoto akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil Fahmy.

Mhe. Membe na Mhe. Fahmy walifanya mazungumzo katika Hoteli aliyofikia Waziri Membe. Mazungumzo yao yalihusu kuimarisha ushirikiano, Misri kurejea katika Umoja wa Afrika na matumizi ya maji ya mto Nile.

Waziri Membe akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Mawaziri wenzake baada ya kushiriki katika chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yao na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri

Waziri Membe akibadilishana mawazo na watu mbalimbali kabla ya kupata Chakula cha Jioni.

Sehemu ya mto Nile ambapo kando yake ndiyo kuna Hoteli ambayo Waheshimiwa Mawaziri waliandaliwa chakula cha jioni. Angani ni helikopta ikiwa katika doria kuhakikisha kuwa hakuna mtu anadhurika.

Waziri Membe akiwa na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa Misri, Bi. Fatma. Bi. Fatma ambaye alishawahi kufanya kazi katika Ubalozi wa Misri nchini Tanzania ndio alikuwa Afisa Itifaki anayemuhudumia Mhe. Waziri na ujumbe wake.


Tuesday, June 10, 2014

Waziri Membe kushiriki Mkutano kuhusu Ukomeshaji Udhalilishaji wa Kijinsia mjini London

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali ya Uingereza imemwalika Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa kuhusu Ukomeshwaji wa Udhalilishaji wa Kijinsia kwenye Maeneo yenye Migogoro (“End Sexual Violence in Conflict”) utakaofanyika mjini London, Uingereza kuanzia tarehe 10 hadi13 Juni, 2014.

Mwaliko huo unakuja kufuatia mchango mkubwa wa Tanzania katika kufanikisha kuwepo kwa Tamko la Umoja wa Mataifa linalohusu suala hilo (Declaration of Commitment to End Sexual Violence in Conflict).Vile vile itakumbukwa kuwa, Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia vikosi vya kulinda amani katika maeneo yenye migogoro Barani Afrika ambayo pia yana wahanga wengi wa udhalilishwaji wa kijinsia.

Pamoja na masuala mengine, Mkutano huo utajadili hatua za kuchukua ili kumaliza tatizo la udhalilishaji wa kijinsia katika maeneo yenye migogoro; mchango au nafasi ya vijana katika kupambana na udhalilishaji wa kijinsia katika maeneo yenye migogoro; kiwango cha udhalilishaji wa kijinsia unatokea katika maeneo yenye migogoro na kuweka makubaliano ya kimataifa ya namna ya kutekeleza  mikakati iliyomo katika maazimio ya G8 na Umoja wa Mataifa; na kusikia matatizo na athari za udhalilishaji wa kijinsia katika migogoro moja kwa moja kutoka kwa Wahanga.

Pia washiriki watajadili changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na udhaifu unaotokana na kutoadhibiwa kwa wanaofanya vitendo hivyo.
Mkutano huo utazikutanisha nchi zilizoathiriwa na migogoro, nchi wahisani, Umoja wa Mataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mashirika ya Kimataifa na Taasisi za Kijamii na wadau wengine.

Aidha, wakati wa ziara hiyo, Mhe. Membe atakutana kwa mazungumzo na Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Mark Simmonds. Miongoni mwa masuala watakayozungumza ni kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Uingereza.

IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM
10 JUNI, 2014

Friday, June 6, 2014

PRESS RELEASE

King Carl XVI Gustav of Sweden


PRESS RELEASE
H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty, King Carl XVI Gustav of Sweden on the occasion to celebrate the Swedish National Day on 6th June, 2014.
 “Your Majesty King Carl XVI Gustav,
   The King of Sweden,
   Stockholm,
   SWEDEN.
It is my pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to extend to Your Majesty and through you to the people of Sweden my heartfelt congratulations on the occasion to celebrate the Swedish National Day.
The celebration of your National Day offers us yet another opportunity to reaffirm our commitment to continue working closely together in enhancing the existing bilateral ties between our two countries. I am confident that the bonds of friendship, co-operation and partnership that our two countries enjoy will continue to grow in greater heights for our mutual benefit.
Please accept, Your Majesty, my best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of Sweden”.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania,
Dar es Salaam.

06TH JUNE, 2014


Waziri Mwandamizi wa Mambo ya Nje na Ndani wa Singapore ziarani nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri Mwandamizi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ndani wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Masagos Zulkifli ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Katika mazungumzo yao walisisitiza kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo utalii, uchukuzi  na uwekezaji.
Mhe. Zulkifli naye akizungumza wakati wa mkutano wake na Mhe. Dkt. Maalim.

Balozi wa Tanzania nchini India anayewakilisha pia nchini Singapore, Mhe. John Kijazi (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Nathaniel Kaaya wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Maalim na Mhe. Zulkifli (hawapo pichani)
Bw. Adam Isara (kushoto), Katibu wa Naibu Waziri na Bw. Khatib Makenga, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo
Mhe. Dkt. Maalim akimsindikiza Mhe. Zulkifli na ujumbe wake mara baada ya mazungumzo yao
Mhe. Dkt. Maalim akiagana na Mhe. Zulkifli.



Thursday, June 5, 2014

Wizara ya Mambo ya Nje yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akipanda mti katika kuashiria kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani katika eneo la Kituo wa Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kilichopo jijini Dar es Salaam. Siku hiyo iliadhimishwa duniani kote tarehe 05 Juni, 2014.  
Afisa Mambo ya Nje, Bi. Naomi Zegezege akipanda mti kwa niaba ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani.
Bw. John Haule akiongozana na Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere  Bw. Deus Kulwa (kulia) baada ya kupanda miti katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani. Kushoto ni Bi Naomi Zegezege, Afisa Mambo ya Nje
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Wafanyakazi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (hawapo pichani) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.
Baadhi Wafanyakazi wa Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Katibu Mkuu  (hayupo pichani)
Katibu Mkuu, Bw. John Haule na Mkurugenzi wa JNICC, Bw. Kulwa katika picha ya pamoja.
Katibu Mkuu akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa baada ya Wizara kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kupanda miti.
Bw. John Haule akizungumza na waandishi wa habari



Picha na Habari na Reginald Philip

Wizara ya Mambo ya Nje yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule, amewataka wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na watanzania wote kwa ujumla kutumia nishati endelevu badala ya kuni na mkaa, kuunga mkono juhudi za serikali za kunusuru mazingira.

Akiongea katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyoandaliwa na wizara kwenye ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo, Bw. Haule alisema hatua nyingine za kutunza mazingira ni kupanda miti; kutolima kwenye miteremko ya milima; kupunguza matumizi makubwa ya mbolea na kuachana na matumizi ya mifuko ya plastiki isiyiteketezeka kwa urahisi.
Wawekezaji katika viwanda watumie teknolojia ya kisasa isiyoongeza gesi joto, alishauri.

Katika maadhimisho hayo chini ya kauli mbiu isemayo  “Sayari ya dunia ni kisiwa chetu wote kwa hivyo tuunganishe nguvu zetu kulinda kisiwa hiki,” Bw. Haule alipanda mti kuanzisha mpango wa wizara wa kupanda miti kutunza mazingira. Miti saba ilipandwa nje ya ukumbi wa Julius Nyerere leo kwa kuanzia.


Maadhimisho hayo pia yalishirikisha wafanyakazi wa AICC na ukumbi wa Julius Nyerere.

PRESS RELEASE

Queen Margrethe II

PRESS RELEASE

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.M Queen Margrethe II of Denmark on the occasion to celebrate the Constitution Day of Denmark on 5th June 2014.

“Your Majesty Queen Margrethe II,
   The Queen of Denmark,
   Copenhagen,
   DENMARK.
It is my pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to extend to Your Majesty and through you to the people of Denmark my heartfelt congratulations on the occasion to celebrate your Constitution Day.
The celebration of your Constitution Day offers me yet another opportunity to reiterate my personal commitment and that of my Government to working with you and your Government in strengthening further the close and historic relations that happily exist between our two countries and peoples.
Please accept, Your Majesty, my best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of Denmark.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania,
Dar es Salaam
05th June 2014  


Tuesday, June 3, 2014

Tanzania participates in the 17th NAM Ministerial Conference

Mr. Japhet Mwaisupule, Minister Plenipotentiary from the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation reading Tanzania's statement to the NAM Ministerial Conference on behalf of Dr. Mahadhi Juma Maalim, Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation. Behind him are Mr. Noel Kaganda, First Secretary (left) from the Tanzania 's Permanent Mission to the United Nations in New York and Ms. Eva Ng'itu, Second Secretary at the Ministry's Headquarters
TANZANIA PARTICIPATES IN THE 17TH NON-ALIGNED MINISTERIAL CONFERENCE

Tanzania participated in the 17th Non-Aligned Ministerial Conference, which ended in the Algerian capital, Algiers, on May 29.

The conference, which was opened by Algerian Prime Minister Abdelmalek Sellal on behalf of President Abdelaziz Bouteflika, adopted a final document asserting NAM’s position on global political, development and social issues, ranging from reform of the United Nations, peacekeeping operations, terrorism, disarmament, post-2015 development agenda to food security.

The ministers also adopted the Algiers Declaration and five other specific statements, including reaffirmation of support for Palestinian nationhood, nuclear non-proliferation and a vote of thanks to Algerian Foreign Minister Ramtane Lamamra and the host country.

The conference, which was held at the Palace of Nations, was attended by almost all the 120 members of the movement, many of whom made statements. Speaker after speaker reaffirmed the relevance and validity of NAM in bringing the members together to address emerging global challenges.

The Tanzanian statement was read by Mr. Japhet Mwaisupule, Minister Plenipotentiary, on behalf of the Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Mahadhi Juma Maalim.

Tanzania urged NAM to continue pressing for fair and just economic, financial and trading multilateral institutions. Reform of these institutions “will not be complete without involving the United Nations Security Council. We must stand together in calling for early reform of the Council so as to make it more effective and responsive to the aspirations of all members,” said the statement.

It also called for new trade and investment rules that work for the benefit of developing countries to facilitate implementation of the global development agenda.


The Ministerial Conference, which was preceded by a Senior Officials Meeting, was addressed by His Excellency Ivo Morales, President of Bolivia, in his capacity as Chairman of G-77 plus China.

Monday, June 2, 2014

Tanzania na Qatar zasaini Mkataba wa ushirikiano wa kazi na ajira

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar wakisaini Mkataba wa Kazi ambao unalenga kuwawezesha Watanzania hususan vijana wenye ujuzi/taaluma katika fani mbalimbali kupata fursa za ajira na kazi za staha, ujira stahiki, kujiunga na hifadhi za jamii nchini Qatar.  Mkataba huo pia unazingatia sheria na viwango vya kazi kulingana na Mikataba ya Kimaataifa ikiwemo ya Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar mara baada ya kusaini Mkataba wa Kazi kati ya nchi hizo mbili. Kulia ni Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo  ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mazungumzo yakiendelea.