Saturday, December 6, 2014

Waziri Membe aanzisha Mfuko Maalum kusaidia Wanafunzi Elimu ya Juu

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba  wakati wa Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu cha Bagamoyo yaliyofanyika katika Viwanja vya Hoteli ya Kiromo iliyopo Bagamoyo. Wahitimu 99 katika fani mbalimbali walitunukiwa shahada zao. Pembeni yake ni Prof.  Costa Ricky Mahalu, Makamu Mkuu wa Chuo hicho.

=======================


WAZIRI MEMBE AANZISHA MFUKO KUSAIDIA WANAFUNZI ELIMU YA JUU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) ameanzisha Mfuko Maalum wa kuwasaidia Wanafunzi wenye Ulemavu na Mahitaji Maalum kwa Ngazi ya Elimu ya Juu ambao utajulikana kama The Bernard Membe Scholarship Fund.

Waziri Membe aliutangaza Mfuko huo wakati akihutubia katika Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu cha Bagamoyo yaliyofanyika katika Viwanja vya Hoteli ya Kiromo mjini Bagamoyo hivi karibuni.

Mhe. Membe alisema kuwa Mfuko huo ambao utakuwa chini ya usimamizi wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo unalenga kuwasaidia Wanafunzi nchini kote wenye mahitaji maalum na wenye nia ya kufikia elimu ya juu lakini hawana uwezo wa kifedha katika kutimiza malengo yao.

“Wakati umefika kwa Watanzania wenye uwezo kusaidia na kuchangia elimu nchini. Ni imani yangu kuwa kwa kushirikiana na wafadhili mbalimbali na pia kwa kutumia harambee mfuko huu utatunishwa na malengo yatatimia kama ilivyokusudiwa,” alisema Waziri Membe.

Aidha, Mhe. Membe alitumia fursa hiyo pia kuwaasa Wahitimu katika Kozi mbalimbali zinazotolewa na Chuo hicho kutumia vizuri elimu waliyoipata katika kudumisha amani, kufikia mafanikio na kuondoa umaskini katika jamii. Pia aliwaonya kujiepusha kabisa na vitendo vyovyote vya rushwa katika maisha yao na kuwataka kuwa raia wanaoishi kwa kufuata sheria za nchi.

Mhe. Membe ambaye pia alipata fursa ya kuwatunuku shahada mbalimbali Wahitimu hao kwa niaba ya Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Mstaafu, Dkt. Elinaza Sendoro ambaye hakuweza kuhudhuria kwa sababu za kiafya, alizipongeza  jitihada za Chuo katika kutoa Taaluma mbalimbali ambazo kwa kiasi kikubwa zinalenga kuwawezesha Wahitimu hao kujiajiri  na  kupata kazi sehemu yoyote duniani ikiwemo Mashirika ya Kikanda na Kimataifa.

“Ninaupongeza Uongozi wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo kwa kuweka mkazo katika  masomo ya Sayansi na Teknolojia, pia kwa ubunifu wa kuwafundisha vijana namna ya kutengeneza ajira na si kutafuta ajira ili kutoa suluhisho kwa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu  nchini,” alisisitiza Mhe. Membe.

Awali akizungumza wakati wa mahafali hayo, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Costa Ricky Mahalu alisema kuwa Chuo kimedhamiria kuwawezesha wanafunzi kuchangia Taifa katika vita dhidi ya maradhi, ujinga na umaskini na kutoa wataalam wenye uwezo wa hali ya juu katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazotokana na utandawazi.

Chuo Kikuu cha Bagamoyo kilianzishwa mwaka 2011 kwa lengo la kutoa elimu ya juu kwa ngazi ya Shahada, Shahada ya Uzamili, Stashahada na Cheti katika kozi zinazohusu Sheria, Sayansi na Teknolojia,  Elimu, Utawala, Biashara, Usuluhishi wa Migogoro na Utunzaji wa Amani.
Sehemu ya Wahitimu hao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe (hayupo pichani)
Baadhi ya wahitimu wa fani mbalimbali wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo wakiwa wamekaa kwa utulivu huku wakimsikiliza Mhe. Membe wakati wa sherehe za mahafali yao. 
Waziri Membe akiwatunuku  Shahada mbalimbali Wahitimu hao kwa niaba ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Askofu Mstaafu, Dkt. Elinaza Sendoro


Wahitimu wakiwa wamesimama kupokea shahada zao.
Wahitimu wa Stashahada


Sehemu ya Wageni Waalikwa
Waziri Membe akiendelea na hotuba
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria mahafali hayo wakifuatilia hatua kwa hatua kile kinachoendelea katika sherehe hizo.
Meza Kuu wakiwa wamesimama kwa heshima ya  kumkumbuka Dkt.Edmund Senghondo Mvungi,  mmoja wa waanzilishi wa chuo hicho ambaye alifariki dunia mapema mwaka huu.
Waziri Membe akipokea zawadi kutoka kwa Bi. Happyness Katabazi kwa niaba ya Uongozi wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo wakati wa mahafali hayo.
 Waziri Membe akikata keki iliyoandaliwa na Wahitimu hao kama ishara ya kuwapongeza  huku akishirikiana na   Prof. Mahalu na mwakilishi wa Wahitimu hao Bi. Pamela Twalangeti 
waziri Membe na Prof. Mahalu kwapamoja wakifurahia burudani iliyokuwa ikitolewa na kikundi cha ngoma kutoka Chuo cha Utamaduni cha Bagamoyo (hakipo pichani)  
Kikundi cha ngoma kutoka Chuo cha Sanaa cha Bagamoyo kikitumbuiza
Picha ya Pamoja na Wahitimu na Viongoiz wa Chuo

Waziri Membe akizungumza na Waandishi wa Habari



........................Matukio mengine kabla ya Mahafali kuanza

Msafara wa Waziri Membe ukiwasili
Akipokelewa na Prof. Mahalu
Akilakiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Chuo hicho, Prof. Paramagamba Kabudi


Akisalimiana na Wakufunzi wa Chuo hicho


Maandamano kuelekea kwenye Mahafali
Brass band ikiwaongoza wahitimu kuelekea kwenye sherehe za mahafali. Picha na Reginald Philip






President Museveni to send Observer to Arusha talks

President of Uganda, H.E. Yoweri Museveni in a meeting with Special Envoys of President Jakaya Kikwete,  Hon. Bernard Membe, Minister for Foreign Affairs and International Coopertion of Tanzania and CCM Secretary General Abdulrahman Kinana at the State House in Entebbe of recent. 

Hon. Bernard K. Membe (Centre), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation of Tanzania, exchange views with Hon.Okello Oryem, Minister for Foreign Affairs of Uganda together with Mr. Abdulrahman Kinana (left) Secretary General of CCM.


===============================

President Museveni to send Observer to Arusha Talks

Uganda President Yoweri Museveni has joined his Sudan and Kenya counterparts in endorsing the Arusha dialogue to reunite the warring factions of the Sudanese People’s Liberation Movement (SPLM), brokered by Tanzania’s ruling party, CCM.
President Museveni told the Minister for Foreign Affairs and International Coopertion, Hon. Bernard Membe and CCM Secretary General Abdulrahman Kinana, Special Envoys of President Jakaya Kikwete at State House in Entebbe on Thursday, that he would send an observer to the talks scheduled to resume on December 11.
“There is no alternative to reuniting SPLM . CCM must continue the effort and achieve full or even part SPLM unity , short of which South Sudan  will disintegrate into sectarian groups,” said President Museveni.
The Special envoys called on the Uganda President in the last leg of a mission ordered by President Kikwete to brief leaders of countries neighbouring South Sudan on progress of the Arusha dialogue and reassure them that it would not undermine the peace process taking place in Addis Ababa under the Inter-Governmental Authority on Development (IGAD). They also solicited for assistance in conducting the talks.
Hon. Membe and Mr. Kinana earlier consulted Presidents Omar Al-Bashir in Khartoum and Uhuru Kenyatta in Nairobi, who declared their full support for the Arusha dialogue, which started last September at the request of South Sudan President Salva Kiir Mayardit.
They also held talks with President Kiir in Juba, who pledged full commitment to the Arusha talks and  that he would implement the decisions to be agreed.
The regional leaders have condemned the killing of thousands of civilians and displacement of hundreds others in the civil war in South Sudan caused by a power struggle in SPLM. IGAD has given the warring parties ultimatum to cease fire or face sanctions.

Hon. Membe described their mission as highly successful. He said the IGAD process involved all the 10 parties to the conflict in South Sudan while the CCM-brokered dialogue concentrated on the differences among the three SPLM factions. 
The mission has allayed suspicion that the Arusha dialogue was competing with the IGAD process and won the support of regional leaders, who agree that reuniting the SPLM factions was a surer way to resolve the South Sudan crisis.

Ends

Friday, December 5, 2014

Press Release

H.E. Sauli Niinisto, President of Finland

PRESS RELEASE

H.E President Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Sauli Niinisto, the President of the Republic of Finland on the occasion of the 97th Anniversary of Finland’s Independence on              6th December, 2014.

“His Excellency Sauli Niinisto,
   The President of the Republic of Finland,
   Helsinki,
   FINLAND.

It is my pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to extend to you and through you to the people of Finland my heartfelt congratulations on the occasion of the 97th Anniversary of your Country’s Independence.  
The celebration of your Independence Day offers us yet another opportunity to reaffirm our commitment to continue working together towards our shared aspirations in further strengthening the healthy relations that happily exist between our two countries and peoples. I am confident that the bonds of friendship and co-operation that our two countries enjoy will continue to soar to greater heights for our mutual benefit.
Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of Finland".

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International

Co-operation, Dar es Salaam. 

05th December, 2014





Naibu Katibu Mkuu afungua Mkutano wa Kamati ya Ukaguzi ya Nchi za Maziwa Makuu

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Rajabu Gamaha akifungua Mkutano wa 6 wa Kamati ya Ukaguzi kwa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu unaofanyika katika Hoteli Harbour View, Jijini Dar es Salaam. Kamati hiyo pamoja na mambo mengine inalenga kudhibiti uvunaji haramu wa maliasili ikiwemo madini ambao kwa kiasi kikubwa umekuwa kichocheo cha vikundi vya uasi na migogoro katika Eneo la Maziwa Mkuu hususan katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Sehemu ya Wajumbe  wakimsikiliza Balozi Gamaha alipokuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo. Wajumbe hao wanahusisha Maafisa kutoka nchi wananchi, Vyama vya Kiraia na Wafanyabiashara.
Wajumbe wengine wakiwemo Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mkurugenzi wa Idara ya Demokrasia na Utawala Bora katika Sekretarieti ya Maziwa Makuu, Balozi Ambeyi Ligabo akizungumza wakati wa mkutano wa 6 wa Kamati ya Ukaguzi ya Nchi Wanachama wa Maziwa Makuu.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. Peter Karasila nae akisema jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano huo
Kaimu Mkuugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent Shiyo akiwakaribisha Wajumbe kwenye mkutano
Mkutano ukiendelea
Balozi Gamaha (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Mkutano wa Kamati ya Ukaguzi ya Nchi za Maziwa Makuu

................Matukio kabla ya mkutano

Balozi Gamaha akisalimiana na Balozi Ligabo alipofika Wizarani kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa 6 wa Kamati ya Ukaguzi ya Nchi za Maziwa Makuu.
Balozi Gamaha akizungumza na Balozi Ligabo alipofika Wizarani
Ujumbe uliofuatana na Balozi Ligabo walipofika Wizarani akiwemo Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ya Nchi za Maziwa Makuu, Bw. Peter Karasila (mwenye tai nyekundu)
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent Shiyo (kushoto) akiwa na Maafisa Mambo ya Nje, Bi. Upendo Mwasha na Bw. Amos Tengu wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Gamaha na Balozi Ligabo (hawapo pichani).


Picha na Reginald Philip



Thursday, December 4, 2014

Hon. Membe, Kinana on special mission over South Sudan

H.E. Uhuru Kenyatta (Centre), President of Kenya in a group photo with Hon. Bernard K. Membe (2nd from left), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation of Tanzania, Hon. Amina Mohammed (left), Kenyan Minister for Foreign Affairs, Mr. Abdulrahman Kinana (2nd from right), Secretary General of CCM, and Amb. Batilda S. Burian (right),   Tanzanian ambassador to Kenya. The Tanzania Special Envoys are on a mission to reassure IGAD leaders that the Arusha initiative to resolve the South Sudan crisis is not in conflict with the separate peace negotiations in Addis Ababa spearheaded by the regional grouping.


Membe, Kinana on special mission over South Sudan
Sudan and Kenya have endorsed Tanzania’s efforts to reunite factions of the Sudan People’s Liberation Movement (SPLM), whose antagonism is central to the civil war in South Sudan.
Presidents Omar Al-Bashir and Uhuru Kenyatta said separatey during meetings with Special envoys of President Kikwete-- the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard Membe, and CCM Secretary General Abdulrahman Kinana, that the CCM-brokered mediation in Arusha had great potential to resolve the South Sudan crisis.
“It will be a difficult process, but if Arusha does not succeed there may be no peace in South Sudan,” declared President Al-Bashir, when the Special envoys called on him at the State House in Khartoum on Tuesday evening.
But the two leaders emphasized that the Arusha dialogue should be complementary to the South Sudan peace talks being conducted by the Inter-Governmental Authority for Development (IGAD). 
Hon. Membe and the CCM Secretary General are on a mission to reassure IGAD leaders that the Arusha initiative, which was requested by South Sudan President Salva Kiir last September, is not in conflict with the separate peace negotiations in Addis Ababa spearheaded by the regional grouping.
Mr. Kinana reassured the Sudan and Kenya leaders that the Arusha mediation conducted October 12-20 and set to resume next week, was not competing against the IGAD process. 
Hon. Membe told reporters in Khartoum that while the peace talks under IGAD conducted at the AU Headquarters in Addis Ababa involved 10 parties to the conflict in South Sudan, Arusha was focused on the SPLM factions led by President Kiir, his fired deputy Riek Machar and Ex-detainees. The bloody conflict has seen thousands of people killed and hundreds others displaced.
During the meeting with President Kenyatta at the State House in Nairobi yesterday, the Kenyan leader told the Special Envoys that the warring parties in South Sudan must not take advantage of the new initiative in Arusha to ignore the decisions reached at IGAD.
One of the decisions is that the killing of civilians should stop immediately. “They must not hide under the Arusha dialogue and continue the killings,” President Kenyatta warned. 
The two leaders agreed that CCM could use its experience spanning  over 50 years to reconcile the warring factions in SPLM, seen as the core of the conflict in Juba. Tanzania hosted the liberation movements of Angola, Mozambique, Namibia, Zimbabwe and South Africa.
The Special Envoys yesterday held talks with South Sudan President Kiir in Juba. The President reaffirmed his commitment to the dialogue in Arusha and assured CCM and the Tanzania government that he will respect and fully implement the decisions to be taken.
The Special Envoys are scheduled to wind up their mission today after consulting Uganda President Yoweri Museveni in Entebbe.
Ends

Makala ya Rais ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Nchini Vietnam Oktoba 2014

Wednesday, December 3, 2014

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar afanya ziara nchini Comoro

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Seif Sharif Hamad akilakiwa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Prince Said Ibrahim Hahaya nchini Comoro kwa ziara binafsi uanzia tarehe 1 hadi 4 Desemba, 2014.
Mhe. Hamad akisalimiana na Mhe. Muhammad Ali Soilihi, Makamu wa Rais wa Comoro. Kushoto ni Mhe. Chabaka Kilumanga, Balozi wa Tanzania nchini Comoro na kulia Dkt. Ahamada Albadaoui Fakih, Balozi wa Comoro nchini Tanzania.
Mhe. Hamad akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima Haji
Mhe. Hamad akiwa na baadhi ya Masheikh na Viongozi aliofutana nao
================================================



Mhe. Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amefanya ziara binafsi visiwani Comoro kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 4 Desemba 2014. Madhumuni ya ziara hii yalikuwa ni kushiriki katika maadhimisho ya miaka arobaini (40) tangu kufariki kwa Marehemu Sheikh Alhabib Omar bin Sumeti, mwanazuoni mashuhuri katika eneo la 
Bahari ya Hindi, ambaye aliwahi kuishi, kujifunza na kutoa elimu Visiwani Zanzibar.

Akiwa nchini Comoro, Mhe. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar alipata pia fursa ya kuonana na Mhe. Dkt. Ikililou Dhoinine, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro, na Mhe. Muhammad Ali Soilihi, Makamu wa Rais wa Comoro. Katika mazungumzo yake na viongozi hao, Mhe. Makamu wa Rais alisifia juhudi zinazochukuliwa kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Comoro. Alibainisha kuwa zipo fursa nyingi za ushirikiano ambazo endapo zitafanyiwa kazi, zitazinufaisha zaidi pande hizi mbili. Aidha, Mhe. Seif Sharif Hamad alikutana na Jumuiya ya Watanzania wanaishi Nchini Comoro na kuzungumza nao.


Monday, December 1, 2014

Waziri wa Mambo ya Nje amuaga Balozi wa Australia


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb.) ameagana na Balozi wa Australia nchini Tanzania Mhe Geoffrey Tooth ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi nchini. 
 Waziri Membe akizungumza na Balozi Tooth na kumweleza kuwa wakati wa kipindi chake cha uwakilishi, uhusiano baina ya nchi hizi mbili umeimarika. Mhe. Membe pia amemshukuiru Balozi Tooth kwa ushirikiano mzuri alioutoa katika kipindi chote na kusisitiza kuwa Tanzania ni nyumbani kwake sasa na asisite kurudi nchini kutembea au kwa mapumziko mara apatapo fursa ya kufanya hivyo.
Mazungumzo yakiendelea kushoto wa kwanza ni Katibu wa Tatu wa Ubalozi huo Bi. Freya Carlton.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akizungumza na Balozi wa Australia ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini.



Picha na Reginald Philip
==========================================

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa leo ameagana na Mhe.Geoffrey Tooth Balozi wa Australia nchini Tanzania ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi nchini. Katika mazungumzo yao. Waziri Membe alimueleza Balozi Tooth kuwa wakati wa kipindi chake cha uwakilishi, uhusiano baina ya nchi hizi mbili umeimarika. Mhe. Membe pia amemshukuiru Balozi Tooth kwa ushirikiano mzuri alioutoa katika kipindi chote na kusisitiza kuwa Tanzania ni nyumbani kwake sasa na asisite kurudi nchini kutembea au kwa mapumziko mara apatapo fursa ya kufanya hivyo.

Kwa upande wake, Balozi Tooth ambaye amekuwa akiiwakilisha nchi yake hapa Tanzania kutokea Nairobi Kenya, kuanzia Desemba 2010 amemshukuru Mhe. Membe, uongozi wa Wizara na wafanyakazi wote kwa ushirikiano mzuri alioupata wakati wote. Alisifu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuleta maendeleo na kukuza mahusiano baina ya Tanzania na nchi nyingine.

Balozi Tooth aliyeongozana na Bi. Freya Carlton, Katibu wa Tatu wa Ubalozi huo, anatarajiwa kuondoka nchini wiki hii kurejea Australia ambapo atakuwa mshauri wa Serikali kwenye masuala ya mazingira na mabadiliko wa tabia nchi. 

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA 3 WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI (EAC) KUHUSU MIUNDOMBINU JIJINI NAIROBI, KENYA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza katika mkutano wa 3 
tatu wa wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu miundombinu, uliofanyika katika ukumbi wa KICC jijini Nairobi jana 
Novemba 29, 2014
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wa tatu kutoka (kushoto) Makamu wa Rais 

wa Kenya, William Ruto, (kushoto kwake) Makamu wa Rais kwanza wa Burundi, (kulia kwake) wakijumuika kwa pamoja na viongozi 


wengine wakionyesha Taarifa ya pamoja waliyoisaini kuhusu majadiliano ya kuimarisha Miundombinu kwa nchi wanachama wa 
Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Miundombinu, uliofanyika 
kwenye Ukumbi wa KICC, jijini Nairobi jana Novemba 29, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wakati 

wakitoka kwenye Ukumbi wa mikutano wa KICC, baada ya kushiriki katika mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki 
(EAC) kuhusu Miundombinu 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi 

wengine walioshiriki katika mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia jambo na Makamu wa Rais wa 

Kenya William Ruto na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, wakati wakiondoka katika viwanja vya Ukumbi wa mikutano wa 

KICC, baada ya kushiriki kwenye mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Miundombinu, uliofanyika 

jijini Nairobi, Kenya jana Novemba 29, 2014.
 (Picha na OMR)

==========================================

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MHESHIMIWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI (EAC) KUHUSU MIUNDOMBINU JIJINI NAIROBI, KENYA
Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal jana Novemba 29, 2014 aliiwakilisha Tanzania katika mkutano wa siku moja wa Wakuu wa Nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Nairobi, Kenya. Mkutano huo, kwa mujibu wa utaratibu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unafanyika kila baada ya miaka miwili na lengo lake kuu ni kufanya tathmini juu ya miradi ya miundombinu inayoshirikisha nchi washirika, sambamba na kutazama fursa ya kutanua miundombinu mipya katika nchi hizi kwa lengo la kukuza uchumi wa pamoja kwa nchi za Afrika Mashariki.
Tathmini hii ya Miundombinu inafanyika kwa kuwa mataifa ya Afrika Mashariki yanatambua umuhimu wa kuwa na miundombinu bora katika nchi hizi ili kuharakisha ukuaji wa uchumi, sambamba na kutanua mtengamano wa nchi hizi na hivyo kuwafanya wananchi wanaoishi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuzidi kuwa wamoja.
Mkutano wa jana uliongozwa na Kaimu Rais wa Kenya Mheshimiwa William Ruto na kuhudhuriwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais Dkt. Bilal, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, Waziri Mkuu wa Rwanda pamoja na Waziri wa Afrika Mashariki wa Uganda. Viongozi wengine waliopata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo ni pamoja na Mheshimiwa Balozi Richard Sezibera, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Waziri wa Wizara hiyo kutoka Tanzania, Mheshimkiwa Samwel Sitta, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Dkt. Donald Kaberuka, Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Ukanda wa Afrika, Bwana Makhtar Diop, Katibu Mtendaji wa UNCTAD, Dkt. Mukhisa Kituyi na Baalozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania Balozi Filiberto Sebregondi. Pia mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa nchi za China, Marekani, Japan na nyinginezo ambazo ni wadau wakubwa wa ujenzi wa miundombinu katika nchi za Afrika Mashariki.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Kaimu Rais wa Kenya, William Ruto alifafanua juu ya umuhimu wa kuhakikisha Afrika Mashariki inaunganishwa kwa miundombinu imara ili kukuza uchumi na akapongeza jitihada mbalimbali zinazofanyika katika kufanikisha azma hiyo huku pia akiomba nchi wanachama wa Afrika Mashariki kuendelea kuungana katika kutekeleza miradi ya miundombinu na kujitahidi kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo.
Mkutano huu pia uliambatana na kupokea ripoti ya utekelezaji wa maagizo ya Wakuu wa Nchi za EAC kuhusu Miundombinu kutoka kwa Mawaziri wa Nchi za Jumuiya.  Wakuu wa Nchi katika Mkutano huu walipokea taarifa ya utekelezaji wa maagizo waliyoyatoa katika mkutano wa pili uliofanyika mwezi Novemba, 2012 na kuidhinisha miradi 72 ya miundombinu ya kipaumbele ya Barabara, Reli, Nishati na Bandari.
Kwa upande wa utekelezaji; miradi 16 imekamilika, 39 inaendelea kutekelezwa na 17 ipo katika hatua za awali za kutafutiwa fedha kwa ajili ya utekelezaji wake.
Kwa upande wa Tanzania miradi minne imekamilika ambayo ni Umeme katika mji wa Kibondo, mradi wa barabara ya Mbezi-Shule-Tangibovu-Makutano ya Nelson Mandela na barabara ya Tabata. Barabara nyingine iliyokamilika ni Nyangunge – Musoma – Sirari na sehemu ya Simiyu - Musoma inayounganisha Kenya na Tanzania huko ujenzi unaendelea.
Akizungumza katika Mkutano huo Makamu wa Rais amezitaka nchi wanachama kuharakisha utekelezaji wa miradi ya Miundombinu ili kusaidia utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja, ambayo inalenga kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na abiria. “Tusiishie kubakiza mipango hii katika karatasi, tusiishie kuzungumza tu bali huu ni wakati wa kuhakikisha tunarahisisha ufanyaji biashara katika nchi zetu na kupunguza vikwazo visivyo vya lazima,” alisema Mheshimiwa Makamu wa Rais.
Katika mkutano huo, Mheshimiwa Makamu wa Rais pia aliambatana na Mheshimiwa Dkt. Mahadhi J. Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara wa Zanzibar, Mheshimiwa Nassor Ahmed Mazrui. Mheshimiwa Makamu wa Rais na msafara wake tayari wamerejea nyumbani Tanzania ambapo kesho anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, maadhimisho yanayofanyika Kitaifa Mkoani Njombe.
Imetolewa na: Ofisi ya Makamu wa Rais
Novemba 30, 2014


Konseli Mkuu wa Tanzania Dubai afanya mazungumzo na Konseli Mkuu wa Saudi Arabia Dubai

Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai, Bw. Omar Mjenga amekutana na Konseli Mkuu wa Saudi Arabia, Dubai, ambaye pia ndio Mkuu wa Makonseli Wakuu waliopo Dubai (Dean of Diplomatic Corps), Bw. Emad A. Madani katika ofisi za Koseli Kuu wa Saudi Arabia.
Konseli Mkuu Bw. Omar Mjenga akiwa katika picha ya pamoja na Konseli Mkuu  wa Saudi Arabia Dubai Bw. Bw. Emad A. Madani


Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai, Bw. Omar Mjenga amekutana na Konseli Mkuu wa Saudi Arabia, Dubai, ambaye pia ndio Mkuu Makonseli Wakuu waliopo Dubai (Dean of Diplomatic Corps), Mhe. Emad A. Madani katika ofisi za Koseli Kuu ya Saudi Arabia.

Bw. Mjenga alienda kumtembelea ili kuomba ushiriki wake pamoja na Makonseli Wakuu wote kwenye kongamano la uwekezaji kwenye sekta ya Utalii nchini Tanzania, litakalofanyika tarehe 17 Disemba 2014.

Bw. Emad Madani amesema atashiriki vikamlifu kwenye kongamano hilo huku akisema kuwa Tanzania na Saudi Arabia ni nchi rafiki wa siku nyingi, na hivyo basi wapo tayari kuomba taasisi ya utalii ya Saudi Arabia kushiriki pia.

Aliahidi kuwaomba Makonseli Wakuu wote washiriki.
Kongamano hilo limeandaliwa na Koseli Kuu ya Tanzania uliopo Dubai kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).