Friday, January 23, 2015

Watanzania wahimizwa kuchangamkia fursa za ajira Emirates

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Simba Yahya  akizungumza na waandishi wa Habari katika ukumbi wa Habari-Maelezo. Balozi Yahya aliwaomba wanahabari hao kuwafikishia ujumbe Watanzania wote ili wachangamkie fursa za ajira katika Shirika la Ndege la Emirates. Wengine katika picha, kulia ni Konseli Mkuu wa Konseli ya Tanzania nchini Dubai Bw. Omar Mjenga na kushoto ni Kaimu Mkuu Mtendaji kutoka Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TAESA) Bw.  Boniface Chandaruba. Emirates ni moja ya Shirika la Ndege tajiri duniani.
Balozi Yahya akiendelea kuzungumza.
Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini mazungumzo kutoka kwa Balozi Yahya
Konseli Mkuu wa Tanzania nchini Dubai Bw. Omar Mjenga akitilia mkazo katika taarifa iliyo tolewa na Balozi Simba katika mkutano na waandishi wa Habari. Alisisitiza umuhimu wa Watanzania kuchangamkia ajira hizo ambazo awali zilitangazwa mwaka 2014  ambapo ni watanzania wachache tu ndio waliojitokeza kuomba nafasi hizo.


Mkutano ukiendelea.
Picha na Reginald Philip



TAARIFA FUPI KWA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU AJIRA KWA WATANZANIA KATIKA SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES KWA MWAKA 2015

  1. UTANGULIZI
Tarehe 22 Januari, 2015 kuanzia saa tano hadi sita mchana, Wizara ilizungumza na waandishi wa habari ili kuufahamisha umma wa Watanzania kuhusu fursa za ajira katika Shirika la Ndege la Emirates kuanzia mwaka 2015. Katika tukio ambalo lilifanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari-Maelezo. 

  1. TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI
Katika kutekeleza moja ya malengo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, hususan kuwatafutia ajira Watanzania nje ya nchi, Wizara kupitia Ubalozi Mdogo wa Tanzania ulioko Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) umefanikiwa kulishawishi Shirika la Ndege la Emirates kuajiri watanzania wengi zaidi kuanzia mwaka huu 2015.

Shirika hilo la Ndege limekubali kuajiri Watanzania katika kada mbalimbali ambapo maafisa wake wanaosimamia ajira watakuja Tanzania mwezi Machi 2015 kwa ajili ya kuwafanyia usaili Watanzania watakaoomba kazi hizo na kupata uteuzi wa awali.

Shirika la Emirates litaajiri kada mbalimbali kuanzia Maintenance Technicians/Mechanics, Planners-Ground Handling, Metal Workers, Customer Service Professionals na Cabin Crews.

Lengo kuu la kuongea na Waandishi wa Habari ni kuutangazia Umma wa Watanzania kuchangamkia ajira hizo ambazo awali zilitangazwa mwezi Julai 2014, lakini ni Watanzania wachache tu waliomba wakati huo na hivyo kutofikia lengo lililokusudiwa. Baada ya mazunguzo ya kina, Uongozi wa Shirika la Ndege hilo umekubali kuongeza muda wa kuzitangaza ajira hizo kwa mara nyingine, na kupanga kufanya usaili kama ilivyoelezwa hapo awali.

Serikali kwa kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ikishirikiana na Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Ajira inawatangazia Watanzania wote wenye sifa na vigezo vinavyotakiwa wachangamkie fursa hizi za ajira bila kukosa. 

Waombaji wanaweza kuwasilisha maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia anuani ya emirates.com/careers. Aidha, waombaji wanashauriwa kuuarifu Ubalozi Mdogo kwa barua pepe (tzconsdb@emirates.net.ae) mara baada ya kuwasilisha maombi yao ili kurahisisha ufuatiliaji. Mwisho wa kuwasilisha maomba ni tarehe 15 Machi, 2015, wakati usaili umepangwa kufanyika tarehe 29 Machi, 2015.

  1. HITIMISHO
Watanzania wote mnahimizwa kutumia fursa hii adhimu kuomba nafasi hizi kwa wale wenye sifa na vigezo stahiki, na pia kujiandaa vema katika usaili ili Tanzania iweze kufanya vizuri kama wenzetu wengine katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, ambao kwa sasa wameajiriwa kwa wingi sana katika soko la Ajira la UAE.

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

JANUARI, 2015

Balozi Dora Msechu awasilisha Hati za Utambulisho kwa Mfalme wa Norway

Balozi wa Tanzania kwenye Nchi za Nordic na Baltic, Mh. Dora Mmari Msechu (kulia) akisalimiana na Mfalme Harald V wa Norway wakati alipowasilisha Hati zake za Utambulisho tarehe 15 January, 2015.
Balozi wa Tanzania kwenye Nchi za Nordic na Baltic, Mh. Dora Mmari Msechu (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mfalme Harald V wa Norway wakati alipowasilisha Hati zake za Utambulisho tarehe 15 January, 2015.

Wednesday, January 21, 2015

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje akutana na Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Italia


Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha (kulia) akisalimiana na Kansela Raffaele De Benedictis kutoka Wizard ya Mambo ya Nje ya Italia ambaye alifuatana na Balozi wa Italia nchini Tanzania Mhe. Luigi Scotto walipotembelea Wizara ya Mambo ya Nje leo.

Balozi wa Italia (katikati) akimtambulisha Kansela Benedictis kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Italia kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Rajabu Gamaha walipomtembelea ofisini kwake leo.

Balozi Gamaha (kulia) akiwa katika mazungumzo na Kansela Benedictis kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Italia. Wawili hao walijadili masuala mbalimbali ikiwemo kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Italia, uwekezaji, usalama katika kanda pamoja na masuala ya kisiasa.

Mazungumzo yakiendelea. wengine katika mazungumzo hayo kutoka kushoto ni Balozi wa Italia, Mhe. Scotto, Kensela Benedictis, Balozi Gamaha, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bibi Victoria Mwakasege na Bibi Olivia Maboko, Afisa katika Wizara ya Mambo ya Nje.

Friday, January 16, 2015

Hon. Bernard Membe's Official Visit in Moscow


The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation Hon. Bernard K. Membe (L)  is in the joint press conference with Russian Foreign Minister, Hon. Sergey Lavrov in Moscow today Friday January 16, 2015.
 Hon. Bernard K. Membe (L) and his Russian counterpart Hon. Sergey Lavrov walking out of Press Briefing Room in Moscow today.

==================================

PRESS RELEASE

Today the governments of Tanzania and Russia have jointly agreed to speed up the process of establishing Tanzanian - Russian Intergovernmental Commission on Trade, Investment and Economic Cooperation to be signed during the first quarter of 2015. 

This was announced during the meeting between Hon. Bernard Membe, Tanzanian Minister for Foreign Affairs and International Cooperation and his Russian counterpart H.E. Sergey Lavrov in Moscow.

The commission aiming at expanding trade and investment between the two countries is expected to boost trade which at the moment is at the minimum.

"Although the volume of trade between our two countries has increased to reach 52 million USD for Tanzania and 60 million USD for Russia, it is not enough. We can do better" Minister Membe elaborated. 

On his part, Minister Lavrov said the last bilateral investment forum between the two countries was held in 2009. The Commission will provide the needed platform for the countries to conduct regular forums which in turn will increase trade and investment opportunities.The commission will also assist in promoting the fast-growing energy sector in Tanzania whereby a number of Russian companies have already expressed their interest investing in it.

Other areas that will benefit through the establishment of this commission are tourism and education sectors whereby strategies to attract more Russian tourists to Tanzania and to increase number of Tanzanian students in Russia will be implemented respectively.  

The two Ministers also agreed to strengthen the Military Technical Cooperation between their countries due to the crucial role they both play in conflict resolution and peace building in Africa. 

On peace building aspect, Hon. Membe thanked Russian Government for its continued support and assistance in resolution of conflicts in Somali, DRC and now South Sudan.

In turn, Minister Lavrov commended Tanzania for her unwavering historical role in promoting and sustaining peace in DRC, South Sudan and other areas in Africa.

In his response, Hon. Membe who is in Moscow following an invitation of his counterpart urged Russia to stay on course in promoting Africa's development agenda. 

"Time has now come for AU to implement its decision to open an office in Moscow to allow continuous discussions on this agenda. It is our hope that your government will facilitate the process for our mutual benefit" said Minister Membe.

The two ministers also agreed to take their countries bilateral relations to greater heights by promoting culture of both countries and people to people relations. 

While in Moscow, Hon. Membe also had an opportunity to brief African Ambassadors and diplomats based in Moscow on the on-going peace processes in DRC and South Sudan. 

Minister Membe's two-day official visit in Moscow will conclude with the meeting with Tanzanians students and professionals from Moscow and surrounding areas. 

Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation.
16.01.2015

Minister Membe's delegation during the joint press conference. (L-R) H.E. Lt.Gen. Wynjones Kisamba (rtd), Ambassador of the United Republic of Tanzania to the Russian Federation, Amb. Joseph Sokoine, Director of Europe and Americas, Ms. Mindi Kasiga, Head of Government Communication in the Ministry.  




Hon. Membe's Arrival Ceremony at the Domodedovo Airport in Moscow

Hon. Bernard K. Membe, Minister for Foreign Affairs and International Cooperation speaking with a group of African Ambassadors and their representatives upon his arrival at the Domodedovo Airport in Moscow, Russia.

Wednesday, January 14, 2015

Taarifa kwa Vyombo vya Habari



Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz
Tovuti : www.foreign.go.tz
Nukushi: 255-22-2116600
              

 

   20 KIVUKONI FRONT,
                 P.O. BOX 9000,
11466 DAR ES SALAAM,  
                          Tanzania.

 




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) ameondoka nchini tarehe 14 Januari 2015 kwenda Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Mhe. Sergey Lavrov.

Ziara hiyo ya kwanza ya kikazi ya Waziri Membe nchini Urusi, inalenga kwenye kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Urusi.

Akiwa nchini humo, Mhe. Membe anatarajiwa kutumia fursa hiyo kuhimiza ushirikiano wa kiuchumi na Urusi, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji na ubadilishanaji wa teknolojia. 

Tanzania inaweza kufaidika na utaalamu wa Urusi katika sekta za uzalishaji wa nishati, uvuvi, afya, kilimo na huduma za jamii. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

14.01.2015

Waziri Membe amuaga Balozi wa Algeria

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamiliusi Membe (Mb.) akimkabidhi zawadi ya picha yenye michoro ya Tembo  Balozi wa Algeria Mhe. Djelloul Tabel nchini Tanzania wakati wa hafla fupi ya kumuaga Balozi huyo ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Hyatt regency kempinski Hotel jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akitoa neno la shukrani kwa Balozi wa Algeria Mhe.Djelloul Tabel, kwenye Hafla ya Chakula cha Mchana iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje  kwa ajili ya kumuaga Balozi Tabel ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundara akizungumza katika ghafla ya kumwaga balozi wa Algeria.
Balozi Djelloul Tabel akitoa neno la shukrani, wakati wa hafla ambapo alitoa shukrani kwa Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano aliopata katika kipindi chote alichokuwepo hapa nchini na kuomba ushirikiano huo uendelee.
Balozi Tabel akiendelea kuongea
Wageni waalikwa wakimpongeza Balozi Tabell kwa kumpigia makofi
Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia wizara ya Mambo ya Nje Balozi Mbelwa Kairuki naye akimsikiliza Balozi Tabell wa Algeria 


Waziri Membe akimweleza jambo Mhe. Balozi.
Waziri Membe wakigonga Glasi (Cheers)
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Algeria Mhe Tabell.


Naibu Waziri Mambo ya Nje akutana na Mabalozi wa kundi la nchi nne.



Naibu waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akiwapokea wizarani mabalozi wa kundi la nchi nne (Ujerumani,Brazil,India na Japani)  kwa mazungumzo kuhusu mabadiliko ya muundo wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

 Balozi wa Brazil hapa nchini, Mhe.Fransisco Carlos Luiz akichangia jambo katika mazungumzo hayo,huku Naibu waziri Mhe.Mahadhi pamoja na maofisa wa wizara ya Mambo ya Nje Adam Isara (wa kwanza kulia) na Ramla Khamis wakimsikiliza kwa makini.
Majadiliano ya mabalozi na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Mhe.Mahadhi yakiendelea.
Balozi wa Japani, Mhe.Masaki Okada (kulia),Balozi wa India Mhe.Dednath Shaw (katikati) pamoja na Balozi wa Ujerumani Mhe.Egon Kochanke wakati wa mazungumzo hayo.

Tuesday, January 13, 2015

Balozi Kilumanga ashiriki Hafla ya kuwakumbuka Wahanga wa shambulizi la kigaidi Ufaransa



Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Chabaka Kilumanga akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo kuwakumbuka wahanga wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa katika Ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo, jijini Paris, Ufaransa. Kitabu cha maombolezo kimefunguliwa kwenye ubalozi wa Ufaransa nchini Comoro na kusainiwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Comoro, Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa pamoja na watu Mashuhuri. 
Balozi Chabaka Kilumanga, akisalimiana na viongozi wa Serikali ya Comoro katika maombolezo hayo.


Rais Kikwete awaandalia Sherry Party Wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini katika hafla ya kuwatakia heri ya mwaka mpya, iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, Januari 9, 2015.
Baadhi ya Mabalozi wakimsikiliza Mhe. Rais katika hafla hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Mhe.Bernard Kamillius Membe (wa kwanza kulia) akiwa pamoja na maofisa wa wizara hiyo wakimsikiliza Mhe. Rais.
Mmoja wa mabalozi waliohudhuria hafla ya mwanzo wa mwaka akisalimiana na Mhe. Rais
Mmoja wa mabalozi waliohudhuria hafla hiyo,akisalimiana na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa kimataifa Mhe.Bernard Kamillius Membe akiteta jambo na naibu wake, Mhe. Dkt.Mahadhi Juma Maalim na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Bw.John Haule (Kulia), wakisubiri kuanza kwa hafla ya mwanzo wa mwaka ya mabalozi.
Rais Kikwete (mstari wa mbele,katikati) akiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa mabalozi wa nchi mbalimbali aliowaandalia hafla ya kufungua mwaka. Kulia kwa Mhe. Rais ni waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Membe,na kushoto kwake ni Naibu waziri wa Mambo ya Nje, Mhe.Dkt.Mahadhi. 
(Picha na Reuben Mchome)

Deputy Minister Presents exequatur to New Zealand Consul

The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Maadhi Jima Maalim presents exequatur to the Honorary Consul of New Zealand in Tanzania, Mr. Hatim Karimjee (L).
Dr. Mahadhi exchanges views with Mr Karimjee after the presentation of exequatur.
 Personal Assistant to the Deputy minister, Mr. Adam Isara (left) and Miss. Berthar Makilagi takes notes of the meeting. 
Meeting is in progress

Photo by Reginald Philip.

Saturday, January 10, 2015

Deputy Minister Presents Work Certificates to India, Oman Consuls

The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Maadhi Juma Maalim presents exequatur to the Consul General of India in Zanzibar, Mr. Satendar Kumar (Left).
Dr. Mahadhi exchanges views with Mr Kumar after the presentation ceremony.
The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Mahadhi Juma Maalim, presents exequatur to the Consul General of Oman in Zanzibar,  Mr. Ali Abdullah Al Rashdi (Left).
Dr. Mahadhi and Mr. Al Rashid in discussions after presentation of exequatur.

The Deputy Minister listens to the Oman Consul General (not in picture) as the minister's Personal Assistant, Mr. Adam Isara (Right) takes notes. 


Photo By: Reginald Philip



Deputy Minister Presents Work Certificates to India, Oman Consuls

The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr Mahadhi Juma Maalim today presented work certificates (Exequatur) to the Indian Consul General in Zanzibar, Mr Satendar Kumar and the Consul General of Oman, Mr Ali Abdullah Sulaiman Al Rashid, in separate ceremonies at the ministry headquarters in Dar es Salaam.

Mr. Kumar informed the Deputy Minister that his government was financing construction of a vocational training centre in Zanzibar while preparations were underway for implementation of other development projects.
Dr Mahadhi commended India for the assistance, saying Tanzania and the Asian country had very strong relations.

The Oman Consul General told Dr Mahadhi that his country was preparing an international donor conference to marshal financial resources for the development of Zanzibar to be held this year. The Deputy Minister said Prime Minister Mizengo Pinda was made aware of the plan during his recent visit to the Sultanate of Oman and that the union government fully supported the idea.

Dr Mahadhi said Zanzibar and Oman had deep-rooted historical ties. "The history of Zanzibar is not complete without Oman and the history of Oman is not complete without Zanzibar," he explained.