Saturday, January 10, 2015

Deputy Minister Presents Work Certificates to India, Oman Consuls

The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Maadhi Juma Maalim presents exequatur to the Consul General of India in Zanzibar, Mr. Satendar Kumar (Left).
Dr. Mahadhi exchanges views with Mr Kumar after the presentation ceremony.
The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr. Mahadhi Juma Maalim, presents exequatur to the Consul General of Oman in Zanzibar,  Mr. Ali Abdullah Al Rashdi (Left).
Dr. Mahadhi and Mr. Al Rashid in discussions after presentation of exequatur.

The Deputy Minister listens to the Oman Consul General (not in picture) as the minister's Personal Assistant, Mr. Adam Isara (Right) takes notes. 


Photo By: Reginald Philip



Deputy Minister Presents Work Certificates to India, Oman Consuls

The Deputy Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Dr Mahadhi Juma Maalim today presented work certificates (Exequatur) to the Indian Consul General in Zanzibar, Mr Satendar Kumar and the Consul General of Oman, Mr Ali Abdullah Sulaiman Al Rashid, in separate ceremonies at the ministry headquarters in Dar es Salaam.

Mr. Kumar informed the Deputy Minister that his government was financing construction of a vocational training centre in Zanzibar while preparations were underway for implementation of other development projects.
Dr Mahadhi commended India for the assistance, saying Tanzania and the Asian country had very strong relations.

The Oman Consul General told Dr Mahadhi that his country was preparing an international donor conference to marshal financial resources for the development of Zanzibar to be held this year. The Deputy Minister said Prime Minister Mizengo Pinda was made aware of the plan during his recent visit to the Sultanate of Oman and that the union government fully supported the idea.

Dr Mahadhi said Zanzibar and Oman had deep-rooted historical ties. "The history of Zanzibar is not complete without Oman and the history of Oman is not complete without Zanzibar," he explained.

Friday, January 9, 2015

Katibu mkuu Mambo ya Nje akutana na Mabalozi waliopanda mlima Kilimanjaro

Katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Mataifa Bw. John Haule (Wa tatu kulia) akizungumza na baadhi ya waheshimiwa Mabalozi waliopanda mlima Kilimanjaro mwezi uliopita.
Baadhi ya waheshimiwa Mabalozi waliopanda mlima Kilimanjaro wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Haule.
Picha na Reuben Mchome.

PRESS RELEASE

François Hollande

President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete has sent the condolence message to H.E. François Hollande, President of the Republic of France following a shooting attack at the Charlie Hebdo offices in Paris which occurred on 7th January, 2015.

The message reads as follows:

‘‘H.E. François Hollande,
President of the Republic of France,
Paris,
FRANCE

Your Excellency,

I have received with great sadness and dismay the devastating news of the tragic attack at the Charlie Hebdo offices in Paris which has claimed the lives of 12 people and injured several others. On behalf of the Government and the People of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I wish to convey to you our heartfelt condolences and through you to the bereaved families who have been robbed of their loved ones by this heinous act.

France and Tanzania enjoy good relations through which we have worked hand in hand to tackle the most pressing security challenges of our time. To this end, I condemn this senseless attack which aimed at bringing fear and insecurity among the French people and the world at large. We are convinced that under your able leadership, the Government of France will leave no stone unturned in bringing the perpetrators to justice.

       While wishing all the victims fortitude in this difficult time, please accept, Your Excellency, renewed assurances of my highest consideration.


Issued by: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

8 January 2015


Thursday, January 8, 2015

Wadau wajadili sera ya Taifa ya Mtangamano ya Afrika Mashariki


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akifungua kikao cha wadau cha kujadili Sera ya Taifa ya Mtangamano wa Afrika Mashariki, katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba yahaya akiwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Said Seif Mzee  wakifuatilia hotuba
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Irene Kasyanju pamoja na Mkuu wa Kitengo cha TEHEMA Bwa. Isack Kalumuna wakisikiliza Hotuba ya ufunguzi. 
Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje Bw. James Lugaganya akitoa mada kwa wadau kuhusu mambo muhimu yaliyozingatiwa katika Sera ya Taifa ya Mtangamano ya Afrika Mashariki

Wadau wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Bw. Lugaganya
Sehemu nyingine wadau
Balozi Mstaafu Vincenti Kibwana akichangia jambo katika kikao hicho
Mdau, Bi. Grace Naburi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi naye akitoa mchango wake kuhusi sera hiyo


Mdau, Bw. Justin Moshi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria
Mdau, Bi. Mindi Kasiga kutoka Wizara ya Mambo ya Nje nae akichangia mada
Wadau mbali mbali wakiwa katika kikao.
Kikao kikiendelea





Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akiwa katika Picha ya pamoja na wadau.


Picha na Reginald Philip 

Wednesday, January 7, 2015

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Balozi wa Syria

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Maadhi Juma Maalimu (Mb) akimkaribisha Balozi wa Syria Nchini Mhe. Abdulmonem Annan, alipokuja kumtembelea na kumweleza kuhusu hali ya kisiasa inavyoendelea nchini Syria 
Balozi Abdulmonem Annan akizungumza na Mhe. Maadhi Juma Maalim
Mazungumzo yakiendelea.


Picha na Reginald Philip

Mada kuhusu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia na athari zake kwa nchi yawasilishwa kwa maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje

Bw. Allan William mtaalamu wa sekta za kibenki nchini, akizungumza katika mhadhara na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa juu ya Mwenendo wa bei za mafuta duniani  na athari zake kwa nchi yetu, mhadhara huo umefanyika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa JNICC uliopo jijini Dar es Salaam mapema leo Asubuhi.
Balozi Simba Yahaya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati (wa kwanza kulia), Balozi Mbelwa Kairuki (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Austrasia na Bw. Togolani Mavura kwa pamoja wakimsikiliza kwa makini Bw. Allan William.
Maafisa wa Wizara wakisikiliza kwa makini 
Balozi Simba Akichangia mada katika muadhara huo.
Bw. Adam Elinawinga kutoka kampuni ya PUMA naye akiendelea kuelezea mwendendo mzima wa bei za mafuta duniani na athari zake kwa nchi yetu. 
Msaidizi wa Rais (hotuba) Bw. Togolani Mavura akichangia mada katika muhadhara huo
Maafisa wa Wizara.
Mhadhara ukiendelea.
Picha na Reginald Philip


Monday, January 5, 2015

MEMBE APONGEZA ANGLIKANA KUPINGA USHOGA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamillius Membe akizindua sherehe ya miaka 50 ya Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es salaam, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano, jijini Dar es salaam jana Jumapili, Januari 4, 2015, akishuhudiwa na  Dk. Valentine Mokiwa, Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam.
Waziri Membe akizungumza katika sherehe hiyo
Wachungaji wakimsikiliza Mheshimiwa Membe kwa makini wakati akiongea.
Masista nao wakifuatilia  
Askofu Mokiwa akitoa mahubiri katika ibada ya uzinduzi wa sherehe ya miaka 50 ya Diyosisi ya Dar es Salaam. .
Waziri Membe akisikiliza mahubiri yaliyokuwa yakitolewa na Askofu Valentino


Mahubiri yakiendelea.
Mwimbishaji kwaya akiwaimbisha nyimbo wanakwaya waliovalia majoho ya rangi ya blue na nyeupe.
Mcheza kinanda akisindikiza kwaya ya kanisa






Waziri Membe akikaribishwa na Askofu Mokiwa kwaajili ya utoaji wa vitabu vya kuchangishia fedha kwa ajili ya miradi ya Dayosisi
Waziri Membe aliaanza kumkabidhi kitabu cha Harambee Askofu Mokiwa
Ibada ikiendelea.

Picha na Reginald Philip

======================================

MEMBE APONGEZA ANGLIKANA KUPINGA USHOGA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, amelipongeza Kanisa la Anglikana Tanzania kwa kusimama kidete kupinga ndoa za jinsia moja, hata pale makanisa mengine ya Anglikana duniani yalipounga mkono suala hilo.
Akizindua sherehe za Miaka Hamsini tangu kuanzishwa kwa Dayosisi ya Dar es Salaam ya Kanisa hilo jana, Mhe. Membe alisema msimamo huo wa Kanisa na Watanzania uliipa serikali nguvu kukataa shinikizom kutoka nchi za Magharibi kwamba iidhinishe ushoga hapa nchini.
"Mlinitia nguvu sana pale niliposimama kidete kuwaambia rafiki zetu wa nje kuwa katika hilo la ndoa za jinsia moja, Tanzania tunaomba tukubaliane kutokukubaliana," alisema Mhe. Waziri, wakati wa uzinduzi huo uliofanyikia kwenye kanisa la Mtakatifu Albano, jijini Dar es Salaam. Sherehe za Miaka 50 ya Dayosisi ya Dar es Salaam zitafikia kilele Julai, mwaka huu.
Mhe. Membe alisema serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa la Anglikana na madhehebu mengine ya dini kuboresha maisha ya Watanzania. "Naomba muendelee kushirikiana na serikali katika kutoa huduma kwa wananchi," aliwaambia waumini na waalikwa wengine waliohudhuria misa maalum ya uzinduzi iliyoongozwa na Askofu Valentine Mokiwa.
Aliwataka viongozi wa dini kuombea nchi umoja na  amani, na kuhimiza waumini wao kushiriki kikamilifu katika matukio mawili muhimu yanayolikabili taifa mwaka huu -- Kura ya maoni ya Katiba inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge.
Uchaguzi wa Rais ni muhimu kwa sababu "Rais wa Awamu ya Tano atategemewa kuendeleza mema ya Awamu ya Nne na awamu zilizopita, na kutoa majawabu kwa changamoto za sasa na zijazo na kutusogeza karibu zaidi na Tanzania njema tunayoitamani, Tanzania yenye neema tele. Hatuko mbali na nchi yetu hiyo ya ahadi," alisema.

Mhe. Membe alishambulia rushwa na ifisadi kuwa ndivyo vinavyodidimiza nchi na kuongeza umasikini kwa wananchi licha ya Tanzania kuwa na rasilimali lukuki. "Tuchague viongozi waadilifu, wazalendo, wachapa kazi, wasio na uchu wa madaraka kwa ajili ya kujinufaisha wao binafsi na marafiki zao," alisema.
Alitaka vijana waandaliwe vyema kushiriki ujenzi na ulinzi wa taifa kwani ndio warithi. "Tukiwaandaa vyema,mustakabali wa taifa letu na watu wake utakuwa kwenye mikono salama. Tukishindwa leo, tutalia na kusaga meno kesho," alionya.