Thursday, November 5, 2015

Magufuli Aapishwa kuwa Rais wa awamu ya Tano wa Tanzania Leo Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akila  kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Mh. Mohamed Chande Othman, katika  Sherehe za kuapishwa kwake, zilizofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam leo.Kushoto ni Rais aliemaliza muda wake, Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Makamu wake, Mh. Dkt. Mohamed Gharib  Bilal. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

Rais aliemaliza muda wake, Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davies Mwamunyange, wakati  akiwaaga wananchi mara tu alipowasili kwenye Uwanja wa Taifa, katika Sherehe za kuapishwa Rais Mpya wa awamu ya tano, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli, zilizofanyika leo jijini Dar es salaam. 

Rais aliemaliza muda wake, Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea salamu ya heshima ya kijeshi kabla ya kukabidhi madaraka kwa Rais Mpya wa awamu ya tano, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli.

Rais Mpya wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akionyesha Mkuki na Ngao aliokabidhiwa na Wazee wa kimila ikiwa ni ishara ya Uongozi wa Kitaifa, katika Sherehe za kuapishwa kwake, zilizofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam leo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride maalum la Jeshi la Ulinzi lenye Umbo la Alfa, ikiwa ni ishara ya kuanza kwa Serikali mpya ya awamu ya tano, katika Sherehe za kuapishwa kwake, zilizofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam leo. Sherehe hizo zimehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa sita kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Marais kutoka nchi mbalimbali walioudhuria katika Sherehe za Kumwapisha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa pili kutoka kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kutoka kulia), Mke wa Rais Magufuli Mama Janeth Magufuli (wa kwanza kulia) na Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja.

Marais 7 wawasili asubuhi ya leo kuwahi uapisho wa Dkt. Magufuli


Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame (kulia) akilakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushiriki sherehe za uapisho wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisindikizwa na Waziri wa Mambo ya Nje kwenda kukagua gwaride.
Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akikagua gwaride.
Mhe. Paul Kagame akikangalia kikundi cha wapiga tarumbeta
========================
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Hailemariam Desalegn (kulia) akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernard Membe alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushiriki sherehe za uapisho za Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
Waziri Mkuu wa Ethiopia akikagua gwaride

===========================
Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushuhudia sherehe za uapisho wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais Nyusi akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mhe. Shamimu Nyanduga.
Rais Nyusi akikagua gwaride

================================
Rais wa Zambia, Mhe. Edger Lungu akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushuhudia sherehe za uapisho wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Mhe. Lungu akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Grace Mujuma.
Rais wa Zambia akifurahia kikundi cha tarumbeta.

==========================
Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushuhudia sherehe za uapisho wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Kenya akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule.

===========================
Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kushuhudia sherehe za uapisho wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Mhe. Museveni akisalimiana na Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Ngusekera Nyerere.
Rais Museveni akikagua gwaride.


Picha na Reginald Philip

Viongozi mbalimbali waendelea kuwasili kwaajili ya sherehe za Uapisho wa Rais Mteule

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (kushoto) akimpokea Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma (anayeshuka kwenye ngazi), Rais Zuma amewasili nchini kwaajili ya kuudhuria sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  
Waziri Membe akisalimiana na Rais Zuma
Rais Zuma akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mhe. Radhia Msuya (wa kwanza kulia).
Rais Zuma akitizama kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitoa burudani.
Balozi wa Tanzania nchini UAE Mhe. Mbarouk Nassoro Mbarouk (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE.
Afisa Mambo ya Nje Bw. Hangi Mgaka naye akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE

Picha na Reginald Philip.

Wednesday, November 4, 2015

Viongozi wawasili nchini Kushuhudia Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe (katikati chini) akimsubiria Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe (katikati juu kwenye ngazi) alipokuwa akiteremka kwenye Ndege, Rais Mugabe amewasili nchini kwaajili ya kuhudhuria Sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

 Waziri Membe akimpokea Rais Mugabe (mwenye Ua Mkononi) mara tu baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mambo ya Nje Bi. Liliani Kimaro akisalimiana na Rais Mugabe.
 Rais Mugabe akikagua Gwaride la Heshima.
Rais Mugabe akiangalia kikundi cha wapiga Tarumbeta huku Waziri Membe akitoa ufafanuzi wa nyimbi iliyokuwa inachezwa.  


===============================

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (kushoto) akimlaki Naibu Waziri Mkuu wa Namibia Mhe. Netumbo Nandi - Ndaitwah mara baada ya kuwasili nchini kwa ajili ya kushuhudia Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Mhe. Netumbo Nandi - Ndaitwah (wa pili kutoka kulia) akifurahia kikundi cha ngoma kilichopo mbele yao.


================================

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini pia anayeiwakilisha Tanzania nchini Botswana Mhe. Radhia Msuya (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Rais wa Botswana Mhe. Olale Eric Mothibi alipo wasili nchini kwaajili ya kushiriki Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.


Picha na Reginald Philip

Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Msajili wa ICTR

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia), akisalimiana na Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda  (ICTR), Bw. Bongani C. Majola (kushoto) alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu utendaji wa Mahakama hiyo iliyopo Jijini Arusha. 

Bw. Majola akimweleza Balozi Mulamula majukumu na namna wanavyoendesha kesi katika mahakama hiyo .
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda ( kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga ( kulia) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mustafa Makame (katikati) nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo yaliyo kuwa yakiendelea kati ya Balozi Mulamula na Bw. Majola (hawapo pichani).
Balozi Mulamula kwa pamoja na Bw. Majola wakifurahia jambo wakati wa mazungumzo yao.
Mazungumzo yakiendelea


Picha ya Pamoja



Picha na Reginald Philip