Thursday, May 26, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika
Tanzania inaungana na nchi nyingine za Bara la Afrika kusherehekea Siku ya Afrika inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Mei.
Sherehe hizo hufanyika kuadhimisha siku ya kuundwa  kwa Muungano wa Nchi za Afrika (OAU) Mwaka 1963 na baadaye Umoja wa Afrika (AU) mwaka 2002 pamoja na maendeleo ya demokrasia, amani na utulivu wa kisiasa, uchumi na kijamii yaliyopatikana tokea kuanzishwa kwa umoja huo.
Wakati wa kuadhimisha miaka 50 ya kuzaliwa kwa Umoja huo tarehe 25 Mei 2013 mjini Addis Ababa, Ethiopia Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika katika tamko lao waliahidi kumaliza kabisa vita ifikapo mwaka 2020 (Silencing the Guns by 2020).
Aidha, Umoja wa Afrika ulipitisha Agenda 2063 yenye kutaka Afrika yenye Amani, Maendeleo na utangamano (Afrika tunayoitaka ifikapo 2063 -Africa we want - 2063). Katika kutekeleza Agenda hiyo Umoja wa Afrika umeandaa mpamgo wa kwanza wa miaka kumi ya utekelezaji wa miradi ya kwanza muhimu iliyojikita kwenye sekta za nishati, usafirishaji, usafiri wa anga, sayansi na teknolojia pamoja na kukuza utangamano barani Afrika.
Kwa muktadha huo, Tanzania inatumia siku hii kuuhakikishia Umoja wa Afrika na Bara la Afrika kwa ujumla kuwa, itaendelea kuwa mwanachama mwaminifu na kuendelea kushirikiana na nchi nyingine katika kutekeleza malengo yake makubwa hususan Dira ya Maendeleo ya Afrika hususani Agenda 2063 na mpango wake huo wa kumaliza vita Barani Afrika ifikapo mwaka 2020.
Itakumbukwa kwamba, Tanzania imechangia kwa kiasi kikubwa kupigania uhuru wa nchi za Afrika, hususan Kusini mwa Afrika pamoja na kuendelea kutatua migogoro iliyopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudan Kusini, Darfur, Sudan na Burundi. Hivyo, kuadhimishwa kwa siku hii kunatoa fursa nzuri kama nchi kupitia upya nafasi yake katika Bara la Afrika na duniani kwa ujumla.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 25 Mei, 2016.



Tuesday, May 24, 2016

Press Release

PRESS RELEASE

JOB OPPORTUNITY AT ITU HEADQUARTERS-GENEVA

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy announcement from the International Telecommunication Union (ITU) inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Web Developer.
 
Application details can be found on ITU website: http://www.itu.int/employment/Recruitment/index.html Closing date for application is 20th June, 2016.

“The Ministry encourages qualified Tanzanians to apply”.


Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, Dar es Salaam.

24th May, 2016

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mipango wa Korea Kusini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Mipango na Uratibu kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Korea, Mhe. Balozi Paik Ji-ah. Mazungumzo yao yalijikita katika kukuza mahusiano baina ya Tanzania na Korea Kusini katika nyanja za   miundombinu, biashara na afya. Waziri Mahiga alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi Paik kwa ushirikiano wanaouendeleza katika kuisaidia Tanzania ikiwemo mchango wao kwenye ujenzi wa Daraja la Malagarasi huko Kigoma na miradi mingine ya barabara.Mhe. Balozi Ji-ah yupo nchini kwa ziara ya siku tatu.
Ujumbe ulioambatana na Mhe. Balozi Paik Ji-ah nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi  Ji-ah. Kulia ni Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum-young.
Balozi Ji-ah akiendelea kuelezea jambo huku Waziri Mahiga akimsikiliza kwa makini.
Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum-young (kulia) akichangia jambo katika mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Naibu Balozi Mhe. Paik Ji-ah kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Korea Kusini
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) pamoja na Afisa Mambo Nje Bi. Bertha Makilagi nao wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.
Waziri Mahiga akiagana na mgeni wake Balozi Paik Ji-ah mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Dkt. Mahiga akiagana na Balozi Geum-young.
Dkt. Mahiga na wageni wake wakiwa katika picha ya pamoja.

Picha na Reginald Philip

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia akutana na Balozi wa China nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki akizungumza na Balozi wa China nchini Mhe. Lu Youqing, alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara na kuzungumza naye juu ya kuendelea kuimrisha ushirikiano ili kukuza fursa za kiuchumi zilizopo hususan katika kuboresha miundombinu na kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya viwanda sambamba na kuinua maisha ya wananchi
Maafisa kutoka Ubalozi wa China walioambatana na Mhe. Lu Youqing wakifuatilia mazungumzo
Mhe. Lu Youqing akijadili jambo na Balozi Kairuki mara baada ya mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea

Wanafunzi kutoka Chuo cha Kijeshi cha India watembelea Wizara ya Mambo ya Nje

      Afisa Mwandamizi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Luangisa akiongoea na wanafunzi kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu wa Jeshi nchini India (hawapo pichani) ambao jana walitembelea katika Ofisi za Wizara Jijini Dare es Salaam  kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali kuhusu Sera ya Mambo ya Nje. Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Maji nchini India, Admiral D. M. Sudan.Wanajeshi hao watakuwa na ziara ya siku tano nchini Tanzania ambayo inatarajiwa kukamilika tarehe 26 Mei, 2016.
Sehemu ya wanajeshi wakifuatilia na kuchangia mazungumzo

 Sehemu nyingine ya wanajeshi hao wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikiwasilishwa na Bw. Luangisa

Monday, May 23, 2016

Utaratibu wa matumizi ya Wimbo na Bendera ya Afrika Mashariki

TAARIFA KWA UMMA


Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kutoa utaratibu wa matumizi ya Bendera na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  kama ilivyotangazwa hivi karibuni.

Utaratibu huo ni kwamba  Bendera ya Taifa itaanza kupeperushwa ikifuatiwa na Bendera ya  Jumuiya ya Afrika Mashariki, vivyo hivyo Wimbo wa Taifa utaanza kupigwa ukifuatiwa na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Itakumbukwa kuwa hivi karibuni, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilitatangaza kuhusu matumizi ya Bendera na Wimbo wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Wizara, Idara, Mashirika na Taasisi mbalimbali za Serikali pamoja na Taasisi Binafsi.

Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unapatikana katika tovuti ya Wizara ambayo ni www.foreign.go.tz.

Aidha, kwa mujibu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki  vipimo maalum vya kutengeneza Bendera hiyo ni kama vinavyoonekana hapa chini.






Imetolewa na,
 Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 23 Mei, 2016.

Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki






Balozi wa Kuwait atembelea Wizara ya Mambo ya Nje.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (kulia) akimkaribisha Balozi wa Kuwait nchini, Mhe. Jasem Alnajem alipomtembelea Ofisini kwake na kufanya mazungumzo yaliyojikita katika kukuza Mahusiano kati ya Tanzania na Kuwait katika sekta ya Elimu na Uchumi. 

Friday, May 20, 2016

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akutana na Balozi wa Chad nchini humo

Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akizungumza na Mhe. Ali Ahmed Aghabache, Balozi wa Chad nchini Kuwait alipomtembelea Ofisini kwake hivi karibuni. Katika mazungumzo yao Mhe. Maalim alimweleza Balozi Aghabache kuhusu ushiriki wa Tanzania katika maadhimisho ya Siku ya Afrika ambayo huadhimishwa tarehe 25 Mei ya kila mwaka. Chad ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kuanzia Januari 2016.  

===============================================
 
Maadhimisho ya Siku ya Afrika huvuta hadhira ya viongozi mbalimbali wa Serikali, waandishi wa habari, mifuko ya fedha na uwekezaji na taasisi zinazojihusisha na masuala ya kibinadamu na hutumiwa na Mabalozi wa nchi za Afrika waliopo Kuwait  kama jukwaa la kutangaza fursa  za uwekezaji, biashara na vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo.

Mtanzania achaguliwa Katibu Mkuu Jumuiya ya Sheria ya Afrika na Asia


Profesa Kennedy Gastorn, Katibu Mkuu mpya AALCO














































































TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Mtanzania achaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya masuala ya Kisheria katika Nchi za Asia na Afrika (AALCO)

Mkurugenzi wa masuala ya Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,  Profesa Kennedy Gastorn amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Mashauriano ya Masuala ya Kisheria katika nchi za Asia na Afrika-‘Asian-African Legal Consultative Organisation-AALCO’.

Profesa Gastorn alichaguliwa kwa kauli moja wakati wa Mkutano wa 55 wa Jumuiya hiyo yenye jumla ya nchi wanachama 47 uliofanyika Mjini New Delhi, India tarehe 17 Mei, 2016 na kuhudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Baraka Luvanda.

Aidha, Profesa Gastorn ambaye alikuwa ni mgombea pekee wa nafasi hiyo baada ya kupendekezwa na Tanzania na kupitishwa na Umoja wa Afrika, anachukua nafasi ya Katibu Mkuu anayemaliza muda wake  Profesa Rahmat Mohamad wa Malaysia ambaye muda wake unamalizika rasmi ifikapo mwezi Agosti, 2016 na Profesa Gastorn anatarajia kukabidhiwa madaraka hayo mwanzoni mwa mwezi Agosti, 2016.

Mkutano wa Jumuiya ya AALCO ulifanyika kuanzia tarehe 16 Mei na kumalizika tarehe 20 Mei, 2016.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 20 Mei, 2016.