Tuesday, September 5, 2017

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wahitimu mafunzo ya JKT

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa wamejipanga kusubiri sherehe za mahafali ya kumaliza mafunzo ya JKT kuanza. Mafunzo hayo yalifanyika Kambi ya JKT ya Oljoro mkoani Arusha kwa kipindi cha wiki sita kuanzia tarehe 24 Julai hadi 04 Septemba 2017.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima ambaye alikuwa Mgeni Rasmi wa mahafali hayo akiwa katika jukwaa kwa ajili ya kupokea heshima kutoka kikosi cha Vijana cha Operesheni Viwanda (hakipo pichani) ambacho kimejumuisha watumishi 30 wa Wizara ya Mambo ya Nje.

Mgeni Rasmi, Balozi Mlima akikagua gwaride maalum lililoandaliwa kwa heshima yake na kikosi kilichohitimu mafunzo ya JKT ambacho kilijumuisha watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje
 Mgeni Rasmi, Balozi Aziz Mlima wakiwa wamesimama pamoja na Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (kulia) na Kamanda wa Kambi ya Oljoro kwa ajili kuangalia vikosi vikipita mbele yao katika mwendo wa pole na kasi
Kikosi kikipita mbele ya Mgeni Rasmi kwa mwendo wa pole

Kikosi kikipita mbele ya Mgeni Rasmi kwa mwendo wa kasi

Mgeni Rasmi akikabidhi zawadi kwa waliofanya vizuri zaidi. 



Bi. Khadija Othman akipokea zawadi yake

Bw. Graison Ishengoma akipokea zawadi yake kutoka kwa Mgeni Rasmi

Bw. Edward Komba akipokea zawadi yake.

Wahitimu wa mafunzo ya JKT kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakila kiapo cha utii

Risala kwa Mgeni Rasmi. katika risala hiyo waliahidi kuyafanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata watakaporejea katika kituo chao cha kazi. Walijifunza uzalendo, utii, ustahamilivu, ukakamavu na mengine mengi.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ambao nao washapitia mafunzo hayo katika awamu ya kwanza wakiwashuhudia wenzao wakihitimu mafunzo ya JKT katika awamu ya pili.

Burdani ilikuwepo siku ya mahafali. Hapo bendi ya Jeshi ikitumbwiza.

Onesho la Makamandoo hapo mmoja wao amebeba ndoo za maji kwa kutumia meno yake.

Mkuu wa Kambi ya Oljoro akiongea machache kabla ya kumkaribisha Mwakilishi wa Mkuu wa JKT ili amkaribishe Mgeni Rasmi

Mwakilishi wa Mkuu wa JKT akimkaribisha Mgeni Rasmi atoe hotuba ya kufunga mafunzo hayo. Kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi alisisitiza umuhimu wa taasisi nyingine za umma kuiga Wizara ya Mambo ya Nje kwa kupeleka watumishi wao ili kupata mafunzo ya JKT ambayo ni muhimu kwa kujenga uzalendo, nidhamu na umoja.

Mgeni Rasmi akisoma hotuba yake. Alitoa ushuhuda kuwa watumishi walioshiriki mafunzo hayo katika awamu ya kwanza wameonesha umahiri mkubwa katika kutekeleza majukumu yao na ndio sababu amepeleka kundi lingine katika awamu ya pili. Aliahidi atawapeleka watumishi wa Wizara yake wenye sifa ikiwemo ya umri (chini ya miaka 40) hatua kwa hatua hadi watakapomalizika.

Wahitimu wa mafunzo ya JKT wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi
 Baadhi ya wageni waliohudhuria mahafali hayo. Hapo afande anateta na Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Bw. Othman Rashid.
Mkurugenzi wa Utawala katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Nigel Msangi akimpongeza Bw. Wambura kwa kuhitimu mafunzo ya JKT.
Tumemaliza salama, shukran kwa Wizara kwa kutuandalia mafunzo haya yenye tija kubwa kwetu.

Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala; Bi. Ngusekela Nyerere na Mwalimu wa somo la Uzalendo ambaye alikuwa Msadizi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere.

Furaha tumemaliza mafunzo, Kutoka kushoto ni Felista Rugambwa, Teodos Komba na Rose Mbilinyi.


Wanaimba nyimbo za jeshi.

Picha ya pamoja kati ya Mgeni Rasmi na wahitimu wa JKT.

Thursday, August 31, 2017

Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yapungua nchini, Dr. Zekeng

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Suzan Kolimba (Mb) akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI (UNAIDS), Bw. Dr. Leo Zekeng ofisini kwake jijini Dar Es Salaam leo. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Zekeng alisifu jitihada zinazofanywa na Tanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ambazo zimesaidia kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 25 na pia idadi ya watoto wanaozaliwa na virusi vya ukimwi imepungua kwa kiasi kikubwa. Dkt. Zekeng alisema kuwa kutokana na mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Bi Michel Sidibe anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini mwezi Oktoba 2017

Dkt. Zekeng akionesha takwimu zilizopo katika ripoti ya UNAIDS zinazoonesha namna maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI yalivyopungua nchini Tanzania.

Mazungumzo yanaendelea

Mhe. Naibu Waziri akiagana na Dkt. Zekeng baada ya kukamilisha mazungumzo yao

Picha ya pamoja

Wednesday, August 30, 2017

Libya yaipatia Zanzibar Msaada wa Matrekta

Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid (kulia) akiwa katika mazungumzo na Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania, Bw. Saleh Kusa  Mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam leo. Wawili hao walijadili namna ya kukamilisha taratibu za kukabidhi msaada wa matrekta 10 yenye thamani ya zaidi ya milioni 250 za Tanzania kutoka Libya kwa ajili ya Serikali ya Zanzibar. Matrekta hayo yashawasili jijini Dar es Salaam na wiki ijayo yanatarajiwa kukabidhiwa Serikali ya Zanzibar. Aidha, Kaimu Balozi alisema kuwa Libya imetenga Dola Bilioni 20 kupitia Mfuko wa "Libyan-Africa Investment Portfolio" kwa ajili ya nchi za Afrika. Aliahidi kuwa atahakikisha kuwa sehemu kubwa ya fedha hizo zinaletwa Tanzania.

Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika, Bw. Suleiman Saleh  na Afisa Dawati wa Libya, Bw. Nicolas wakifuatilia mazungumzo

Kulia ni Mkalimani wa Kaimu Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ya Serikali ya Zanzibar wakifuatilia mazungumzo hayo

Nazungumzo yanaendelea

Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania, Bw. Saleh Kusa  akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje
Mhe. Waziri na Kaimu Balozi wakiagana huku Katibu Mkuu, Dkt. Aziz Mlima akishuhudia
Picha ya pamoja

Thursday, August 24, 2017

Watumishi wa umma Zanzibar wapigwa msasa kutekeleza Mipango ya Serikali



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Watumishi wa umma Zanzibar wapigwa msasa kutekeleza Mipango ya Serikali

Taasisi za Umma zimeshauriwa kujikita zaidi katika utekelezaji wa mipango iliyojiwekea badala ya kutumia muda mwingi kupanga mipango isiyotekelezwa.
Ushauri huo umetolewa leo kwenye warsha ya kuwajengea uwezo watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuingiza Mpango kazi wa utelezaji wa APRM kwenye mipango ya maendeleo ya nchi kama vile Dira ya Zanzibar 2020, MKUZA III na Mipango ya Matumizi ya Muda wa Kati. 

Warsha hiyo ya siku mbili imeandaliwa na APRM Tanzania na inafanyika katika Hoteli ya Golden Tulip mjini Zanzibar tarehe 24 na 25 Agosti 2017.
Mgeni Rasmi kwenye warsha hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Kubingwa Mashaka Simba ambaye alimwakilisha Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Haroun Ali Suleiman aliwahakikishia washiriki kuwa Serikali ya Zanzibar imejipanga vema kutekeleza changamoto zote zilizobainishwa kwenye ripoti ya APRM iliyowasilishwa rasmi kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan mwanzoni mwa mwezi Agosti 2017.
Bw. Simba alieleza kuwa tayari Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilishachukua hatua za kuimarisha Utawala Bora ikiwemo kuunda taasisi za kusimamia suala hilo ambazo baadhi yao ni Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Tume ya Kupambana na Rushwa pamoja na ugatuzi wa madaraka.
Wadau wanaoshiriki warsha hiyo walibainisha kuwa changamoto kubwa katika taasisi za umma ni utekelezaji wa mipango iliyowekwa, Hivyo kuna umuhimu wa APRM kuangalia namna ya kujenga uwezo wa watumishi katika kutekeleza mipango ya Serikali kwa kuzingatia namna ya kupata rasilimali zinazohitajika na zenye uwezo wa kutekekeza mipango iliyopo pamoja na muda wa kutekeleza mipango hiyo.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa APRM, Tanzania, Bi. Rehema Twalibu alisema warsha hiyo ni muhimu kwa watumishi wa Serikali ya Zanzibar kwa kuwa itawapa uwezo wa kuandaa taarifa ya utekelezaji wa changamoto zilizoainishwa kwenye ripoti ya APRM iliyowasilishwa miaka mitano iliyopita kwa Wakuu wa Nchi zilizoridhia Mpango wa APRM. 

Taarifa ya utekelezaji itakayoandaliwa na Serikali ya Zanzibar itajumuishwa na taarifa ya Tanzania Bara ili kupata ripoti moja ambayo inatarajiwa kuwasilishwa na Mhe. Rais kwa Marais wenzake wanaounda APRM baadaye mwaka huu.


-Mwisho-

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Zanzibar, 24 Agosti 2017

Katibu Mtendaji wa Mpango wa Afrika wa Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) Tanzania, Bi. Rehema Twalib akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Kubingwa Mashaka Simba (hayupo pichani) kwenye ufunguzi wa Warsha ya kuunganisha mipango ya APRM na Mipango ya Serikali inayofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip, mjini Zanzibar. 
Naibu Katibu Mkuu, Bw. Kubingwa Mashaka Simba akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika ufunguzi wa Warsha ya ya kuunganisha mipango ya APRM na Mipango ya Serikali
Sehemu ya viongozi waliohudhuria kwenye Warsha hiyo wakimsikiliza kwa makini Mhe. Simba.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Bw. Kombo Abdulhamid Khamis (katikati), wa kwanza kushoto ni Mratibu wa Utawala APRM, na kulia ni Amani A.M. Shein nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Warsha  hiyo.
Mjumbe wa Jopo la Watu Mashuhuri na Kiongozi wa Mchakato wa Tanzania toka APRM, Mhe. Bridget Mabandla naye akizungumza kwenye ufunguzi huo.
Sehemu ya washiriki wa ufunguzi huo wakisikiliza kwa makini.
Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wa kwanza kulia ni Halima Salim Abdallah, na katikati ni Hamida Makame Juma.
Watumishi wa APRM Tanzania, Bi. Stella William (kushoto`) na Bi. Elizabeth Ngereza nao wasikiliza hotuba iliyokuwa ikiendelea kutolewa na mgeni rasmi (hayupo pichani).
Bw. Max Ochai kutoka (UNECA), akitoa mada ya kwanza mara baada ya kumalizika kwa zoezi la ufunguzi
Sehemu ya washiriki wakifuatilia kwa kumsikiliza Bw. Ochani (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mada ya kwanza.
Bw. Ochani akiendelea kutoa mada yake kwa washiriki
Picha ya pamoja mara baada ya kumaliza ufunguzi wa Warsha hiyo.