Tuesday, October 17, 2017

Taarifa kuhusu kuzingatia sheria katika katika kuingiza au kutoa mifugo nchini kwa ajili ya malisho na maji.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

TAARIFA KUHUSU KUZINGATIA SHERIA KATIKA KUINGIZA AU KUTOA  MIFUGO NCHINI KWA AJILI YA MALISHO NA MAJI

Hivi karibuni, tumeshuhudia kuibuka kwa wimbi kubwa la uungizaji wa mifugo kutoka nchi jirani kuingia nchini kwa ajili ya malisho na maji bila kufuata sheria za nchi. Uingizaji wa mifugo kutoka nchi moja kwenda nyingine una madhara mengi, ikiwemo kiusalama, uharibifu wa mazingira na kueneza magonjwa ya mifugo.

Ikumbukwe kuwa tarehe 13 Oktoba, 2017, Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa agizo la kuondoa mifugo yote iliyo nchini kinyume cha sheria ndani ya  siku saba (7). Kutofanya hivyo kutapelekea mifugo hiyo kutaifishwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kufuatia agizo hilo, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  inatoa wito kwa Watanzania wote wenye mifugo nchi jirani wafuate taratibu za kisheria na kama kuna mifugo kwenye malisho nje ya Tanzania waiondoe mara moja ili kuepusha hasara na usumbufu.

Aidha,  wizara inatoa wito kwa Watanzania hususan wanaoishi Mikoa iliyopakana na nchi jirani kuwa wazalendo kwa kutokushirikiana na raia wa nchi za kigeni kuvunja sheria mbalimbali za nchi.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje Na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dar es Salaam
17 Oktoba, 2017

Monday, October 16, 2017

Meli ya Mfame wa Oman yawasili Jijini Dar es Salam kwa ziara


Meli ya Mfalme wa Oman " Fulk Al Salaam" imewasili leo Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya siku sita inayotarajiwa kumalizika tarehe 21 Oktoba, 2017. Meli hiyo imewasili na Mjumbe Maalum wa Mfalme, Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman, Mhe. Dkt. Hamad Al Rumphy Mahammed ambaye ameambatana na watu zaidi ya mia tatu (300)  kutoka katika sekta mbalimbali.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akisalimiana na  Mhe. Dkt. Hamad Al Rumhy Mahammed mara baada ya kuwasili katika Bandari ya Dar es Salaam. Pembeni ya Waziri Mwinyi ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Mhe. Hashimu Mgandila.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisalimiana na Waziri Mahammed katika sherehe za mapokezi zilizofanyika Bandarini Dar es Salaam. Pembeni yake ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Dkt. Aziz Mlima akisalimiana na Mhe. Dkt. Mahammed.

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima akisalimiana na Waziri Mahammed. Pembeni yake ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Felix Lyaniva.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Ayoub Mndeme akisalimiana na Waziri Mahammed.

Mhe. Waziri Mwinyi akikaribishwa ndani ya Meli na Mhe. Waziri Mahammed.

Mhe. Waziri Mwinyi pamoja na Dkt. Kolimba wakiwa katika mazunguzo na Mhe. Waziri Mohammed mara baada ya kuingia ndani ya meli.

Balozi Dkt. Mlima akifatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea  baina ya Mawaziri Mwinyi na Waziri Mahammed. Kushoto kwake ni Balozi wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Al-Mahruqi.

Viongozi waandamizi kutoka Serikali ya Tanzania na Oman wakijadiliana ndani ya Meli. 

Vikundi vya ngoma vikitumbuiza katika viwanja vya bandari mara baada ya Meli kuwasili.

Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wakifuatilia hafla ya mapokezi ya Meli ya Mfalme wa Oman.

Waziri Mwijage akutana na Balozi wa India nchini


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb.) akizungumza na Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya kuhusu kuimarisha ushirikiano kwenye masuala ya biashara, viwanda na uwekezaji kati ya Tanzania na India. Mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Oktoba, 2017. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.), Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Magabilo Murobi (hawapo pichani).

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.) (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (wa pili kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Magabilo Murobi (wa kwanza kulia) wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Mwijage na Balozi wa India nchini (hawapo pichani).
Mhe. Dkt. Kolimba akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Mwijage na Balozi Arya.
Mazungumzo yakiendelea

Saturday, October 14, 2017

Taarifa kuhusu ziara ya meli ya Kifalme kutoka Oman nchini

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taarifa kuhusu ziara ya meli ya Kifalme kutoka Oman nchini

Meli ya Kifalme ya FULK AS SALAAM ya Mfalme Qaboos Bin Said Al Said wa Oman iliyo katika ziara ya kirafiki katika Pwani ya Afrika Mashariki itatia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ziara ya siku sita kuanzia tarehe 16 hadi 21 Oktoba, 2017. Lengo kuu la ziara hiyo ni kueneza ujumbe wa amani, upendo na kuimarisha urafiki uliodumu kwa muda mrefu kati ya Oman na Tanzania. 

Meli hiyo ambayo imeanzia Zanzibar tarehe 12 hadi 15, 2017 inatarajiwa kuja na ujumbe wa zaidi ya watu mia tatu (300) ukiongozwa na Mhe. Mohammed bin Hamad Al Rumhy, Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman ambaye ataongozana na Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Umma ya Kukuza Uwekezaji nchini Oman, Dkt. Salim Al Nasser Ismaily na Mhe. Maitha Al Mahrouqi, Katibu Mkuu wa Utalii. 

Mara baada ya kuwasili katika Bandari ya Dar es Salaam, Meli hiyo itapokelewa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Hussein Ali Mwinyi (Mb.) na viongozi mbalimbali wa Serikali. 

Aidha, tarehe 17 Oktoba, 2017 kutakuwa na hafla maalum ya chakula cha mchana ndani ya Meli hiyo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan. 

Tarehe 18 Oktoba, 2017 kutakuwa na tukio la Muziki wa Kitamaduni utakaopigwa mubashara na Bendi kutoka Oman katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. 

Pia tarehe 19 Oktoba, 2017 wananchi wakiwemo wanafunzi wataruhusiwa kufanya ziara ya kutembelea Meli hiyo kwa utaratibu maalum. Pamoja na kutembelea Tanzania, Kenya ni nchi nyingine iliyopewa nafasi ya kutembelewa na Meli hiyo ya Kifalme. 

Meli hiyo itaondoka Bandari ya Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2017 kuelekea Mombasa, Kenya. 

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dar es Salaam
14 Oktoba, 2017

Thursday, October 12, 2017

Balozi wa Hispania atembelea Wizara

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Hispania nchini Tanzania Filex Costales, katika mazungumzo yao walizungumzia masuala mbalimbali ya mahusiano kati ya Tanzania na Hispania hususani suala la jimbo la Catalonia kutaka kujitenga na Hispania
Mazungumzo yakiendelea.

Wednesday, October 11, 2017

Tanzania na Cuba kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo,alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Mkutano ukiendelea
Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe.Prof. Polledo, wa pili kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Amerika na Ulaya Bi. Mary Matare, na wa kwanza kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bi. Lilian Kimaro na kushoto ni afisa wa Ubalozi wa Cuba hapa nchini.

=======================================



Serikali ya Tanzania na Cuba zimeahidi kuendelea kuweka mikakati madhubuti kwaajili ya kuimarisha ushirikiano wa siku nyingi ulioasisiwa na viongozi wakuu wa Mataifa hayo Hayati Baba wa Taifa  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Fidel Castor.

Hayo yamesemwa leo katika mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo walipokutana katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wa Mhe. Kolimba alieleza Cuba imekuwa mdau wa Maendeleo nchini tangu enzi za ukoloni ambapo ilishiriki katika kupigania Ukombozi wa Tanzania na Afrika kwa ujumla na hivyo kuleta undugu baina ya watu wa mataifa hayo mawili.

Aidha, aliongeza kwa kusema “Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua jitihada na mchango wa Serikali ya  Cuba katika Sekta  ya Afya kwa kuleta madakatari kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Hospitali ya Taifa Muhimbili, Pia ujenzi wa kiwanda cha viuadudu kilichopo Kibaha ni sehemu ya jitihada za kuwasaidia Watanzania katika kuhakikisha wanakuwa na Afya bora ili kuweza kumudu majukumu yao ya kila siku katika kuliletea Taifa maendeleo” alisema Dkt. Kolimba.

Halikadhalika Mhe. Prof. Polledo alisisitiza kuwa Cuba itaendeleza ushirikiano na Tanzania na kuzidi kuangalia maeneo mengine ya ushirikiano hususani upande wa michezo ambapo nchi hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika mchezo wa ngumi pamoja na walimu stadi wa mchezo huo ambao wamekuwa wakitoa mafunzo katika mataifa mengine ya Afrika.

Pia alieleza kutambua mchango wa Tanzania katika Kikao cha 72 cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kwa msimamo wake wa kutaka Cuba kuondolewe vikwazo vya kiuchumi ambavyo vimekuwa vikikwamisha na kurudisha nyuma jitihada za maendeleo ya Taifa hilo. “ ni wakati sasa Cuba na Tanzania zikaimarisha ushirikiano wake kwa kuhakikisha unakuwa na mafanikio  kiuchumi kwa manufaa ya mataifa hayo” alisema Prof. Polledo

Tuesday, October 10, 2017

TAARIFA KWA UMMA

TAARIFA KWA UMMA
Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya umeandaa Misa Maalum ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere itakayofanyika tarehe 14 Oktoba, 2017 katika Kanisa la Holy Family Basilica, Nairobi kuanzia saa 4.00 hadi saa 5.00 asubuhi.
Watanzania wote pamoja na ndugu, jamaa na marafiki mnakaribishwa kushiriki katika Misa hii. Kufika kwenu kwa wingi ndio kufanikisha shughuli yetu sote.

TUNATANGULIZA SHUKRANI ZETU ZA  DHATI.

IMETOLEWA NA:
UBALOZI WA TANZANIA
NAIROBI, KENYA
10 OKTOBA, 2017

Monday, October 9, 2017

African countries told to use FOCAC Opportunities, Kairuki

Ambassador of the United Republic of Tanzania to the People's Republic of China, H.E. Mbelwa Kairuki delivering a key note address at the youth Forum on China-Africa Youth Exchange Programme on Poverty Reduction and Development  which took place in Beijing, China  on 9th  October, 2017 at Beijin Convetion Centre.

The forum on progress.




========================================================================

 Ambassador of the United Republic of  Tanzania to the People’s Republic of China, His Excellency  Mbelwa Kairuki has urged African countries to cooperate in order to tap into opportunities provided by China under China-Africa Cooperation (FOCAC) which is an official Forum between China and Africa.

This has been addressed during the Youth Forum and 2nd  China – Africa Youth Exchange Programme on Poverty Reduction and Development which took place in Beijin, China  on 9th October 2017 at Beijing Convention Centre.

Ambassador Kairuki also expressed concern to the fact that Africa spends USD 35 Billion every year importing food from outside the continent while it is endowed with 60 percent of the World's arable land. He called on African governments to work together to implement regional  infrastructure projects that would unleash Africa's economic potential.

The forum was opened by the Deputy Prime Minister of China His Excellency WANG Yang. In his remarks Mr. Wang reported remarkable achievements made by China by lifting hundreds of millions or people out of poverty.

The forum was also attended by Mr. Tegegnework Gettu, the United Nations Under-Secretary General and  Associate Administrator of the United Nations Development Programme (UNDP) who represented the United Nations Secretary General to the Conference. In his message the United Nations Secretary General cautioned that globalization and technological progress have increased inequalities and left millions of people behind. He underscored that reducing and eradicating poverty is the key to improve lives and realizing the potential of hundreds of millions of people. 










Tuesday, October 3, 2017

Naibu Waziri afanya mazungumzo na Balozi wa Iran chini Tanzania


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dkt. Susan Kolimba akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran nchini Tanzania Mhe.Mousa Farhang. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara za Jijini Dar es Salaam yalijikita zaidi katika kujadili masuala mbalimbali yatakayo imarisha zaidi uhusino wa kidiplomasia uliodumu kwa kipindi cha takriban miaka 40 kati ya Mataifa hayo mawili ( Tanzania na Iran). 
Naibu Waziri Mhe. Dkt.Susan Kolimba akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran Mhe. Mousa Farhang walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mhe.Dkt. Kolimba na Balozi Mhe.Farhang wakiwa katika picha ya pamoja. Wapili kulia ni Balozi Innocent Shio, Afisa kutoka Wizarani Bw.Hangi Mgaka (wa kwanza kulia) na mjumbe kutoka Ubalozi wa Iran nchini (wa kwanza kushoto)