Monday, November 13, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje afanya mazungumzo na Balozi China nchini


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba na Balozi wa China nchini Mhe. WANG Ke wakifuarahia jambo walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Mjini Dodoma.Naibu Waziri amemuhakikishia Mhe.Balozi WANG Ke kuwa Wizara na Serikali wataendelea kudumisha uhusiano wa kahistoria uliodumu kwa muda mrefu baina ya Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China. Pia Mhe. Dkt. Kolimba alitumia fursa hiyo  kuishukuru Serikali ya China kwa kufadhili miradi mbalimbali hapa nchini
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba na Balozi wa China nchini Mhe. WANG Ke wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa nchi wa Falme za Kiarabu nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Umoja wa nchi wa Falme za Kiarabu nchini Tanzania Mhe. Balozi Abdulla Ibrahim Alsuwaidi walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalikita katika kujadili masuala mbalimbali ya namna ya kudumisha na kukuza uhusiano baina ya pande mbili. (Tanzania na Umoja wa Nchi wa Falme za Kiarabu)  
Waziri Mhe.Balozi Dkt.Mahiga na Mhe. Balozi Alsuwaidi wakifurahia jambo wakati walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazunguzo
Waziri Mhe. Mahiga akimsikiliza Balozi wa Nchi wa Falme za Kiarabu nchini Mhe.Abdulla Ibrahim Alsuwaidi walipokutana kwa Mazungumzo Jijini Dar es Salaam

2018 SADC SECONDARY SCHOOL ESSAY COMPETITION





N:B All applicants are requested to send their applications to the following address:
    
         Permanent Secretary
         Ministry of Education,  Science and Technology
         Block 10,
         College of Business Studies and Law,
         University of Dodoma,
         P.O.Box 10
         DODOMA



















Friday, November 10, 2017

Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Ujumbe wa EU nchini

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Jestas Nyamanga akizungumza na Kaimu Kiongozi  wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Bw. Charlie Stuart alipofika Wizarani tarehe 10 Novemba, 2017 kwa ajaili ya kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu Umoja huo na masuala mengine ya Kimataifa.
Sehemu ya Ujumbe uliofuatana na Bw. Stuart wakifuatilia mazungumzo
Sehemu nyingine ya ujumbe kutoka EU na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki


Thursday, November 9, 2017

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Pro.Adolf Mkenda akiwa katika mzungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) inchini Bibi Abla Beuhammouche,Wizarani Jijini Dar es Salaam. Pamoja na masuala mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili njia bora zaidi za kutekeleza miradi ya kilimo na uhifadhi wa mazingira. IFAD inatekeleza miradi ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kwa wananchi na uhifadhi wa mazingira katika maeneo mbalimbali nchini.

Katibu Mkuu Prof. Adolf Mkenda akimsiliza Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini Tanzania  Bibi Abla Beuhammouche walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Prof. Adolf Mkenda na Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini Tanzania  Bibi Abla Beuhammouche wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Mhe. Balozi wa China Nchini

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akiwa katika mkutano na Balozi wa China Nchini Mhe. Wang Ke alipomtembelea Wizarani, tarehe 09 Novemba,2017.
 Katibu Mkuu Prof. Mkenda ( katikati), kushoto kwake ni Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke, wakiendelea na mazungumzo, wanaofutilia mazungumzo hayo ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia(wa kwanza kulia) Bi. Justa Nyange na anayefuata ni Afisa katika Idara hiyo Bw. Harmesh Lunyumbu.

Katibu Mkuu Prof. Mkenda akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa China Nchini Mhe. Wang Ke, baada ya mkutano

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Finland nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Adolf Mkenda akimkaribisha Wizarani Balozi wa Finland nchini, Mhe. Pekka Hukka alipofika kwa ajili ya kujitambulisha kwake kama Katibu Mkuu mpya na kuzungumzia jinsi ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Finland. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 09 Novemba,  2017.
Prof. Mkenda akimweleza jambo Balozi Hukka wakati wa mazungumzo yao. Pamoja na mambo mengine wlizungumzia kuimarisha ushirikiano katika masuala ya elimu, biashara na uwekezaji ambapo Prof. Mkenda alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi Hukka kwa msaada unaotolewa na Serikali yake kwa Taasisi ya Uongozi.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salvatory Mbilinyi kwa pamoja na Bi. Tunsume Mwangolombe wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Balozi Hukka (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea

Wednesday, November 8, 2017

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mjumbe Maalum kutoka Norway

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Mjumbe Maalum kutoka Serikali ya Norway kwa Serikali ya Tanzania, Balozi Arild Oyen ambaye alifika Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe maalum. Pamoja na mambo mengine walizungumzia namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Norway hususan katika sekta za Nishati, Elimu na Utamaduni. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 08 Novemba, 2017.
Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Balozi Oyen (hawapo pichani). Kutoka kushoto ni Bw. Jestas Nyamanga, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Salvatory Mbilinyi, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika na Bi. Ramla Hamis, Afisa Mambo ya  Nje.
Mazungumzo yakiendelea. Wa kwanza kushoto ni Balozi wa Norway nchini, Mhe. Hanne Marie Kaarstad.
Prof. Mkenda na Balozi Oyen wakimsikiliza Balozi Kaarstad mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao
Prof. Mkenda akiagana na Balozi Oyen

Katibu Mkuu Prof. Mkenda afanya Mazungumzo na Balozi wa Japan Nchini

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akiwa katika mkutano na Balozi wa Japan nchini Mheshimiwa Masaharu Yoshida alipomtembelea Wizarani leo tarehe 08 Novemba,2017. Katika Mkutano huu walizungumzia masuala mbalimbali yanoyohusu uhusiano kati ya Tanzania na Japan hasa katika eneo la uwekezaji.

 Prof.Mkenda akipokea zawadi ya Kalenda ya Mwaka 2018 kutoka kwa Mheshimiwa Balozi Yoshida, kalenda hiyo ni maalum yenye picha  zinazoelezea utamaduni wa Japan.

Katibu Mkuu Prof. Mkenda na Mhe. Balozi Yoshida pamoja na maafisa kutoka Wizarani na Ubalozi wa Japan wakiwa katika picha ya Pamoja baada ya Mkutano.

Waziri Mahiga amkaribisha rasmi Wizarani Katibu Mkuu mpya Prof.Mkenda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) wakati wa kikao rasmi cha kumkaribisha Katibu Mkuu mpya wa Wizara Prof. Adolf Mkenda (kulia). Kikao hicho kilifanyika hivi karibuni  katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu, Bw. Hamid Mbegu.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Waziri Mahiga (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia kikao
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akiwasalimia Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) mara baada ya kukaribishwa rasmi Wizarani.
Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya Watumishi wa Wizara

Watumishi wengine wa Wizara

Tuesday, November 7, 2017

Waziri Mahiga akutana na Kamishna wa Umoja wa Ulaya

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea na Kamishna wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Neven Mimica alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 6 Novemba, 2017. Bw. Mimica alikuwepo nchini kwa ziara ya siku sita (6) ambapo aliwasili nchini tarehe 1 Novemba 2017 na kukamilisha ziara hiyo kwa kukutana na Waziri Mahiga.
Mkuu wa mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Mhe. Roeland van de Geer pamoja na afisa wa Ubalozi huo wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Salvatory Mbilinyi na Afisa aliyeambatana na kamishna wakifuatilia mazungumzo.

Picha ya pamoja.
Mazungumzo yakiendelea.

Friday, November 3, 2017

Msichana wa Kitanzania kuiwakilisha nchi Mkutano wa Dunia wa Vijana

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Deusdedit Kaganda akimkabidhi Bendera ya Taifa, Bi Hilda Jacob Mwakatumbula ambaye amechaguliwa na Kamati ya Kimataifa ya Vijana kuiwakilisha Tanzania kwenye Mkutano wa Dunia wa Vijana utakaofanyika Belize, Amerika ya Kati kuanzia tarehe 6 hadi 9 Novemba, 2017. Bi. Mwakatumbula ambaye anachukua Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Waseda nchini Japan amepata ufadhili wa kushiriki Mkutano huo kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto). Akimkabidhi Bendera hiyo, Bw. Kaganda alimwomba Bi. Mwakatumbula kuwa Balozi mzuri wa Vijana wa Kitanzania kwenye mkutano huo hususan katika kutekeleza Malengo Endelevu ya Maendeleo.
Picha ya pamoja

Thursday, November 2, 2017

Balozi Mbarouk akabidhi Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran


Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk, mwenye Makazi yake Umoja wa nchi wa Falme za Kiarabu (U.A.E) akikabidhi Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mhe. Rais Hassan Rouhani. Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ikulu ya Rais, Mjini Tehran tarehe 28 Oktoba, 2017.

Mhe. Rais Hassan Rouhani akisoma hati za utambulisho alizokabidhiwa na

Mhe. Balozi Mbarouk, ambapo alitumia fursa hiyo kumkaribisha Mhe. Mbarouk na kuahidi kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake.
Mhe. Rais Hassan Rouhani akizungumza na Mhe. Balozi Mbarouk baada ya kukabidhi hati. Katika mazungumzo yao wameahidi kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano kwa lengo la kukuza uchumi wa mataifa yao. 


Wednesday, November 1, 2017

Naibu Waziri Mhe.Dkt Suzan Kolimba afanya mazungumzo na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Halotel Wizarani

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan Kolimba(Mb) akiwa katika mkutano na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya simu ya Halotel nchini Bw. Pham Dinh Quan alipomtembelea Wizarani jana tarehe 31 Oktoba,2017, Dar es salaam. 
Katika Mazungumzo yao Bw. Quan alisema kampuni ya halotel hadi sasa imewekeza katika eneo kubwa la Tanzania hasa vijijini, alisema hadi sasa Kampuni hiyo imewekeza asilimia 80 ya eneo la Tanzania na wana mpango wa kuongeza uwekezaji zaidi katika eneo ambalo halijafikiwa. Mhe. Dkt. Kolimba alipongeza kampuni ya Halotel kwa uwekezaji huo mkubwa ambao umesaidia kurahisisha mawasiliano nchini hasa Vijijini.

 

 Mkutano huo ukieendelea.
 Naibu Waziri Mhe.Dkt. Suzan Kolimba (Katikati), Naibu Mkurugenzi wa Halotel Bw. Pham Dinh Quan kushoto kwake na kulia ni  Bw. Emmanuel Luangisa Afisa Mambo ya Nje wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mkutano.