Monday, June 25, 2018

Washindi wa TBL watembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi

Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Simon Mumwi amekutana na Washindi wa shindano la Tanzania Breweries Ltd. kupitia bia rasmi ya Kombe la Dunia - Kilimanjaro Premium Lager siku chache mara baada ya kuwasili jijini Moscow Urusi, kwa ajili ya kushuhudia Mechi za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini humo.

 Pichani katikati ni Balozi Mumwi, 
watatu kutoka kulia ni Bw. Charles John, wa pili kutoka kulia ni Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi Dkt. Mkama, na wa kwanza kulia ni Joel Terry. 
Wa kwanza kushoto ni Bw. Leodigard Isack,  Bw. Kironde Mwijage (wa pili kushoto), Bi. Mary Mushi (wa tatu kutoka kushoto),  wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili ubalozini hapo.
Balozi Mumwi akifanya mazungumzo na washindi hao.
Balozi Mumwi akipokea zawadi ya Majani ya Chai yanayotengenezwa nchini Tanzania kutoka kwa mmoja wa washindi wa shindano hilo Bw. Leodigard Isack kwa niaba ya Kundi la Washindi wa Shindano la TBL kupitia bia ya Kilimanjaro Premium Lager, ambapo washindi hao walidhaminiwa safari ya Urusi kushuhudia mojawapo ya Mashindano ya Kombe la Dunia yanayoendelea nchini humo.

Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa kufanyika jijini Arusha

Mhandisi Abdillah Mataka Mkurugenzi Msaidizi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Kijamii kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akichangia jambo kwenye mkutano wa  15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa unaoendelea jijini Arusha. Mkutano huu unafanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo katika Ofisi za Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.



Mkutano huu unaofanyika kila mwaka, mwaka huu pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili taarifa za utelelezaji wa mapendekezo, maagizo na maamuzi mbalimbali yaliyofikiwa na kuamuliwa katika mikutano ya ngazi mbalimbali na vyombo vya kisera vya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Sekta zinazotarajiwa kujadiliwa katika mkutano huu ni pamoja na sekta ya miundombinu ya uchukuzi inayojumuisha aridhi, anga na maji, mawasiliano na hali ya hewa. 

Utelezaji wa maagizo, mapendekezo na maamuzi mbalimbali yaliyotolewa ili kuboresha maeneo haya unatarajiwa kuleta mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii katika nchi wanachama za Jumuiya Afrika Mashariki.

Mkutano huu unaoendelea jijini Arusha na kuhudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi zote wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki utafanyika katika ngazi tatu ambazo ni; ngazi ya Wataalam, ngazi ya Makatibu Wakuu na hatimaye ngazi ya Mawaziri.
Meza kuu wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulipokuwa ukiimbwa na wajumbe kabla ya kuanza kwa mkutano.
Sehemu ya wajumbe kutoka Tanzania wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kabla ya kuanza kwa mkutano. Kushoto ni Mhandisi Abdillah Mataka Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Kijamii, Mhandisi Julius Chambo (katika) Mkurugenzi Sekta ya Ujenzi kutoka  Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Bw. Moses Malipula kutoka Wizara ya Fedha na Mipango

Meza kuu ikiongoza majadiliano wakati wa mkutano

Sehemu ya wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa.

Bibi Edna Chuku (wa kwanza kulia) Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia mkutano uliokuwa unaendelea.

Friday, June 22, 2018

MINISTER MAHIGA’S DAY VISIT TO ROMANIA; SIGNS AN MOU FOR BILATERAL CONSULTATIONS

   






PRESS RELEASE
Tanzania’s foreign minister Hon. Dr. Augustine Mahiga, and his Romanian counterpart Hon. Teodor Melescanu have signed a Memorandum of Understanding, redefining bilateral relations that exist between Tanzania and Romania. 
The two leaders held extensive talks prior to the signing ceremony which was held at Ministry of Foreign Affairs in Bucharest in front of members of the press. The timely signing came at a time when the two parties are working to establish strong economic ties, with different nations around the world.  
The signed MoU between the two countries’ Foreign Ministries provides a platform to hold regular strategic consultations on political, economic, commercial, scientific, technical and cultural aspects of bilateral relations, regional and international matters.
The platform is envisaged to further develop and strengthen friendly relations while increase mutual understanding and cooperation between Tanzania and Romania.
“During the liberation struggle of Africa, many Tanzanian students came to Romania to study medicine and pharmaceutical. With the signing of this MoU, now Romania and Tanzania are strategic partners. We anticipate diversification in the area of training and capacity building to include new sectors such as agronomy for Tanzanian students” Hon. Mahiga remarked. 
Hon. Melescanu explained that ever since the new Government of Romania came into leadership one year ago, the focus has been to re establish relations and partnerships with countries outside Europe. 
“But Tanzania and Romania have been friends for the longest time, and we witnessed many of your colleagues receiving education in Romania. The number kept decreasing year after year due to the closing of our embassy in the 90’s. I believe now things will be better, for our people” announced Foreign Minister Melescanu. 
Diplomatic relations between the two countries were established on 5th May 1964. The relations were very active until 18th November, 1999, when the government of Romania closed its embassy in Dar es Salaam, due to financial difficulties. The relations were mainly based on education particularly scholarship to Tanzania students. 
The platform for political discussions will provide an opportunity to discuss both priority issues, including migration issues, business opportunities, investments, various development projects, capacity building and tourism promotion.
Hon. Mahiga and his delegation, made a one-day visit to Bucharest on their way back to Tanzania after concluding another working visit in the region. Permanent Secretary of Romania Foreign Ministry is also expected to visit Tanzania as a follow up of this signed MoU within the coming month. 

ENDS

Issued by:
Government Communication Unit, 
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, 
Bucharest, Romania June 21 2018

African envoys plug business on the continent

Ambassadors and diplomats from Sierra Leone, Tunisia, Kenya, Tanzania, Ethiopia, Nigeria, Sudan, Ghana, Angola, Rwanda, Egypt, Gabon, Senegal, Morocco, the Ivory Coast and Zambia; and Korean lawmakers and investors attend the Africa Business Seminar at the FKI Tower in western Seoul on Wednesday. 

Africa is changing and Korea should get on board, ambassadors of African nations said at a forum in Seoul on Wednesday to celebrate Africa Day.

“Currently, six of the world’s 10 fastest growing economies are in Africa,” said Albino Malungo, ambassador of Angola and dean of the African Group of Ambassadors. “The African train has already left the station. The message to our Korean business partners is that Africa is the new global growth pole and the next market.”

The Korea-Africa Foundation, African Diplomatic Corps in Korea and Federation of Korean Industries hosted the Africa Business Seminar at the FKI Tower in western Seoul, on Wednesday. Organizers highlighted the African Continental Free Trade Area, which includes 44 countries and intends to pool together African goods and services into a single market with free movement of people and investment.

The free trade area “is aware that there are other economic communities in the regions where it will [have] impact,” said Rwandan Ambassador Emma-Francoise Isumbingabo, who chaired the preparation committee for this year’s Africa Day celebration in Korea. “[The free trade area] will work closely with existing communities, aligning itself with their goals and objectives, and ensuring that cooperation with foreign and outside investment in the African market is made easy and approachable.”

Investors noted budding Korean interest in the African market.

“Korea’s Ministry of Foreign Affairs has what’s called the Country Partnership Strategy for each recipient country of its funds,” said Jun Woo-hyung, director of trade information at the Korea Trade-Investment Promotion Agency, “which in Africa are Ethiopia, Ghana, Mozambique, Uganda, Rwanda, Senegal and Tanzania. There is budding interest in the African market here. Recall that the African Development Bank held its annual meeting in Busan this past May.”

Some ambassadors said Korean companies can do more in Africa.

“We all think there is a huge potential that is underutilized,” said Egyptian Ambassador Hazem Fahmy. “Korea is leading in high technology and the fourth industrial revolution, and I think it could make huge profits by investing in Africa in these areas.”

Africa Day is celebrated on May 25 annually and commemorates the foundation of the Organization of African Unity in 1963. In addition to the business forum, embassies of African nations hosted a food and culture fair in central Seoul’s Cheonggye Plaza.

There was injera (sourdough flatbread) made with teff flour; baked goods from the Algerian embassy, including semolina-stuffed makrout and date-filled kaak cookies; figurines from Ghana in traditional dress; handwoven baskets from Sudan and Rwanda; and stone animals from Tanzania.

“Before I knew it, Korea has become my home,” said Audrey Aduol, a 28-year-old Kenyan studying at Seoul National University, who was helping out at the Kenyan booth. “The other time I went home, I felt like a guest in my own country. It’s bittersweet how that happens.”

BY ESTHER CHUNG [chung.juhee@joongang.co.kr]

Naibu Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Kuwait


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani M.Mwinyi akisalimiana na Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al-Najem, alipomtembelea Wizarani tarehe 22 Juni,2018, Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine walizungumzia kuhusu jinsi ya kuboresha mahusiano yaliyopo katika kati ya Tanzania na Kuwait, nchi ya Kuwait imekuwa ni kati ya wadau muhimu wa Maendeleo hapa nchini kupitia mradi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait(Kuwait Fund).

            Mhe. Al-Najem akifafanua jambo katika mazungumzo hayo.

 Balozi Mwinyi akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.
 Mazungumzo yakiendelea, wanaofuatilia kulia kwa Balozi Mwinyi ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Bw. Suleiman Salehe, Bw. Hangi Mgaka na Bw. Fidelis Odilo Maafisa wa Mambo ya Nje, wakifuatilia mazungumzo hayo.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.


Thursday, June 21, 2018

WAZIRI MAHIGA AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI NORWAY


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI MAHIGA AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI NORWAY ASISITIZA UWEKEZAJI WENYE TIJA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amehitimisha ziara yake ya kikazi nchini Norway kwa mazungumzo na wafanyabiashara huku akiwapa ujumbe mkuu wa kuwekeza Tanzania ambapo tayari kuna mazingira mazuri ya uwekezaji.

Kwenye hotuba yake kwa wanachama wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Norway na Afrika (NABA), Mhe. Mahiga ameelezea ushirikiano uliopo kati ya Serikali za Norway na Afrika kwa ujumla hususan Tanzania, ambapo Norway inasaidiana na nchi nyingi za kiafrika  ikiwemo Tanzania katika kutekeleza miradi ya maendeleo. Hii ni ishara nzuri kwa ukuaji wa biashara na mahusiano.

Akitolea mfano wa Tanzania, Mhe. Mahiga alisema kuwa miaka ya hivi karibuni Serikali ya Norway imebadilisha ushirikiano wake na Tanzania kutoka kwenye kutoa misaada kwenda kwenye udhamini wa pamoja wa miradi mbalimbali ya maendeleo yenye lengo la kuinua uchumi.

“Ushiriki wa Serikali ya Norway nchini kwetu ni wa kipekee, kwani unazingatia vipaumbele na sera za Tanzania na pale wanaongeza nguvu kwa kudhamini mafunzo na hatimaye ujenzi wa mifumo sahihi ya utekelezaji wa sera hizo” Waziri Mahiga alisema.

Waziri Mahiga aliongeza kuwa, kwenye awamu ya tano ya uongozi nchini Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mambo mengine, amejenga mifumo bora ya ukusanyaji kodi, usimamizi wa rasilimali za umma pamoja na uendelezwaji wa rasilimali ya mafuta kwa maendeleo. “Serikali ya Norway inadhamini maeneo yote hayo na mengine mengi, kama mdau wa maendeleo ya Watanzania. Hivyo ni vyema na nyie wafanyabiashara muwekeze pale ambapo Serikali yenu ipo. Kwa sababu hapo ndio mahali salama kwa uwekezaji wenye tija” alihimiza Mhe. Mahiga.

Mkutano huo uliojumuisha taasisi takriban 25, ulifanyika chini ya mwamvuli wa Norfund, Taasisi inayojenga uwezo kwa wafanyabiashara kuendesha biashara kwenye nchi zinazoendelea.

Akielezea mikakati ya taasisi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wake, Bw. Kjell Roland alisema Norfund inajikita zaidi kwenye nchi ambazo upatikanaji wa mitaji ni mgumu kutokana na uchanga wa sekta binafsi.

Kwa upande wake, Mratibu wa umoja huo wa Wafanyabiashara wa NABA, amesema kuwa wapo kwenye maandalizi ya ziara ya biashara Tanzania kabla ya mwisho wa mwaka huu.

Waziri Mahiga alitumia fursa ya mkutano huo kumtambulisha Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa ambaye anatarajiwa kukabidhi hati zake  za utambulisho tarehe 21 Juni, 2018.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 21 Juni, 2018


Wednesday, June 20, 2018

MINISTER MAHIGA COMMENDS RELATIONS BETWEEN TANZANIA AND NORWAY



    PRESS RELEASE


MINISTER MAHIGA SPEAKS ABOUT FIVE DECADE-LONG THRIVING RELATIONS BETWEEN TANZANIA AND NORWAY
       
Tanzania Foreign Minister Hon. Dr. Augustine Mahiga has told his Norwegian counterpart Hon. Ine Eriksen Soreide today that the strength behind flourishing Tanzania-Norway bilateral relations has been the distinctive cooperation and strategic assistance that exist for over five decades now between these two traditional partners. The two leaders held talks at the Government Guest House to kick start the first-ever political and diplomatic consultations meeting aimed at strengthening their relations.  

Minister Mahiga who is in Oslo for a three-day working visit told the Norwegian delegation that besides diplomatic relations that Tanzania enjoys, the Norwegian government has been in the forefront in providing substantial amount of development assistance to Tanzania with a plus, throughout all the leadership phases in the country.

“Our bilateral relations with you, our friends, date back before the independence of Tanganyika whereby Norwegian teachers, doctors, nurses and engineers, came to the country to provide social services to the people of Tanzania particularly in rural areas” Hon. Mahiga said. This is a testimony that the two countries have long-standing relations, adding that “shortly after independence in 1960’s and 1970’s the Norwegian and Tanzanian governments participated in joint Nordic Projects like the Kibaha Education Centre and the Uyole Agricultural Research Centre, in line with policies and principles of an independent Tanganyika. This demonstrates that Norwegian cooperation is strategically aligned with our country’s vision” Minister Mahiga complemented.

Responding to this, Hon. Ine Eriksen Soreide said that her government has over the years enjoyed the relations with Tanzania and as a Foreign Minister; she will strive to continue this trend. Norwegian government has selected Tanzania to be among its recipients of development assistance and her duty is to make sure that this is implemented swiftly.

“Norway and Tanzania see eye to eye in many global issues of concern such as global peace, improving multilateral trading system, international order as well as world efforts in prevention of conflicts. In all this we view Tanzania as a key and credible player in the African region and our partner in development” Hon. Soreide emphasized. She added that she looks forward to continue with the commenced political consultations annually, for mutual benefits in those issues.  Hon. Mahiga assured Minister Soreide that Tanzania will reciprocate hosting the consultations next year, which will be held in Dodoma, the capital city of Tanzania.

Under the political and diplomatic consultations framework,  Hon. Mahiga and his delegation also held talks with the Norwegian Development Minister Hon. Nikolai Astrup at the Ministry of Foreign Affairs. In their consultations, Minister Mahiga reiterated Norwegian strategic assistance for development to Tanzania which is key for economic growth and alleviation of poverty.

“Given the historical ties between us, your government has always provided support to projects that are much beneficial in rural areas example rural electrification. Norway’s support to energy sector is key given the role of the sector in supporting our economic growth”, said Amb. Mahiga.

Other areas in Tanzania that receive Norwegian assistance are; management of public recourses as well as tax collection. The Government of Norway through the assistance programs of Oil for Development and Tax for Development contribute to build capacity of Tanzania’s institutions responsible management of resources, management of public revenues and environment protection.

The maiden Political and Diplomatic Consultations comes as a result of the MoU signed in 2017 in Dar es Salaam between the Ministries of Foreign Affairs of Tanzania and Norway, which enable the two ministries to discuss issues of mutual concern in order to enhance further bilateral ties. Next round of consultations of this nature are envisaged to take place next year in Dodoma, Tanzania.

-ENDS-

Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Oslo Norway, June 20 2018

Tuesday, June 19, 2018

Ziara ya Waziri Mahiga katika picha

KIKAO CHA KAZI CHA UJUMBE WA WAZIRI MAHIGA NA MHE. DKT. WILBROAD SLAA, BALOZI WA TANZANIA NCHINI NORWAY MWENYE MAKAZI YAKE NCHINI SWEDEN

Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akipokea taarifa ya kazi kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake Stockholm Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa, katika Hoteli ya Grand Oslo iliyopo kwenye mji wa Oslo, Norway.  


Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akiwa kwenye kikao cha kazi na ujumbe wake mara baada ya kuwasili Mjini Oslo, Norway kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Kwenye ziara hiyo Waziri Mahiga ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara Prof. Adolf Mkenda (kulia kwa Waziri), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Marekani Bw. Jestus Nyamanga, Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati Bw. Adamu Zuberi, pamoja na maafisa waandamizi wa Mambo ya Nje. 



KIKAO CHA KAZI CHA UJUMBE WA WAZIRI MAHIGA KWENYE KAMPUNI YA STATOIL (EQUINOR) NA WATENDAJI WA KAMPUNI HIYO YENYE MAKAO YAKE MAKUU MJINI OSLO, NORWAY.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akisalimiana na Makamu wa Rais Mtendaji wa STATOIL Bw. Lars Christian Bacher mara baada ya ujumbe wa Waziri Mahiga kuwasili kwenye makao makuu ya kampuni hiyo Oslo, Norway. Wengine kwenye picha ni Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa, Balozi wa Tanzania nchini humo, na Bw. Adamu Zuberi, mtaalam wa Wizara ya Nishati.

Balozi wa Tanzania nchini Norway, Mhe. Dkt. Slaa akisalimiana na Watanzania wawili Nyarobi na Eunice, wanaofanya mafunzo ya vitendo kwenye kampuni hiyo, baada ya kumaliza mafunzo ya shahada ya uzamili kwenye Chuo Kikuu Norway. 

Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Hanne Marie Kaarstad akizungumza kwenye kikao hicho kilichofanyika kwenye ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo. Pichani chini Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho. 


Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje akipokea zawadi kutoka kwa Bw. Lars Christian Bacher, Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni ya Statoil. Pichani chini, Mkurugenzi Bacher akimkabidhi zawadi Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa, Balozi wa Tanzania nchini Norway baada ya kikao hicho kumalizika kwa mafanikio makubwa. 


Picha ya pamoja 
Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa kwenye picha na Mtanzania Nyarobi aayefanya mafunzo ya vitendo kwenye kampuni ya Statoil akiwa na mmoja wa Wakurugenzi watendaji wa kampuni hiyo.



Waheshimiwa Balozi Dkt. Slaa na mwenzake Balozi Kaarstad wanaowakilisha nchi zao Tanzania na Norway wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa kitanzania Eunice na Nyarobi walionufaika na ufadhili wa kampuni ya Statoil kwenye masomo ya shahada ya uzamili ambao wanaendelea kupata mafunzo ya vitendo.


KIKAO CHA KAZI CHA UJUMBE WA WAZIRI MAHIGA NA UONGOZI WA SHIRIKA LA MAENDELEO LA NORWAY, NORAD MJINI OSLO NORWAY

Ujumbe wa Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ukiwa kwenye kikao cha kazi na Ujumbe wa Mkurugenzi wa Norad Bw. Jon Lamoy. Norad ni Shirika la Maendeleo ya Norway linalofadhili miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Norway. Shirika hilo lipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo. 


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Marekani kwenye Wizara ya Mambo ya Nje Tanzania Bw. Jestus Nyamanga akiwa na ujumbe wa Mhe. Waziri Mahiga, wakati wa kikao cha kazi na Shirika la Maendeleo la Norad la Serikali ya Norway.


WAZIRI MAHIGA ZIARANI NCHINI NORWAY

Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akipokea taarifa ya kazi kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake Stockholm Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa, katika Hoteli ya Grand Oslo iliyopo kwenye mji wa Oslo, Norway. 




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ZIARA YA WAZIRI MAHIGA NCHINI NORWAY

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeihakikishia Serikali ya Norway kuwa inaendelea kuelekeza nguvu zake kwenye kuweka mikakati sahihi ya kuvutia uwekezaji kutoka nje ya nchi, ikiwemo nchi ya Norway, ili kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania alipokutana na Bw. Jon Lamoy, Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Norway lijulikanalo kwa kifupi kama NORAD mwanzoni mwa ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mjini Oslo, makao makuu ya Norway.

Katika mazungumzo yao, Mkurugenzi Lamoy alimueleza Waziri Mahiga kuwa shirika hilo limekuwa na uhusiano wa karibu na wa kindugu kwa zaidi ya miongo mitano na nchi ya Tanzania. Yeye binafsi na washirika wengi wa Tanzania nchini humo wanasifu utendaji kazi wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli hususan kwenye mapambano dhidi ya rushwa. Rushwa inarudisha nyuma maendeleo kwa kuikosesha nchi mapato, hivyo jitihada za Tanzania za kupambana na rushwa, hususan kwenye ukusanyaji kodi, zitawawezesha wananchi wa Tanzania kunufaika na huduma za kijamii na hatimaye kupata maendeleo kwa haraka.

Hata hivyo mkurugenzi huyo alitoa angalizo kuwa nia nzuri ya Serikali ya Tanzania ya kuweka mifumo thabiti ya uwekezaji wenye faida  ukiwemo ule wa sekta ya madini, ni muhimu ikakamilika mapema ili kutoa fursa kwa wawekezaji wapya kuwekeza kwenye sekta hiyo kwa wakati.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Mahiga alielezea kuwa suala hilo tayari linafanyiwa kazi ambapo pamoja na Serikali kuweka mazingira rafiki  kwa wawekezaji, uwekezaji huo ni lazima uwe na faida kwa Watanzania na kwa maendeleo ya nchi.

“Serikali ya Rais Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa kati unaoongozwa na sekta ya viwanda. Katika kutekeleza hilo, Serikali imepitia na kurekebisha baadhi ya sheria na mikataba ambayo ilikua inanufaisha upande mmoja. Marekebisho yanayofanyika sasa yanalenga kwenye kuleta faida kwa pande zote mbili yaani win win situation”alisisitiza Dkt. Mahiga.

Kwenye mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Balozi wa Tanzania nchini Norway, Dkt. Wilbroad Slaa mwenye makazi yake nchini Sweden kwa pamoja walielezea kuwa marekebisho hayo, yatakapokamilika, yatarutubisha mazingira ya uwekezaji Tanzania ikiwemo mikataba itakayoridhiwa na Bunge ambayo italeta manufaa kwa pande zote mbili kama zifanyavyo nchi nyingi duniani, ikiwemo Norway.

Awali kabla ya mkutano huo, Mheshimiwa Mahiga alikutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Kampuni ya STATOIL yenye makao yake makuu Mjini Oslo, ambayo kwa sasa nchini humo inajulikana kama Equinor. Kampuni ya STATOIL Tanzania ni mshirika mkubwa nchini Tanzania kwenye shughuli za utafutaji na upatikanaji wa gesi.

Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni ya Statoil Bw. Lars Christian Bacher alielezea shughuli za kampuni hiyo Tanzania ikiwemo kujenga uwezo wa ndani ya nchi kwa Watanzania kuijua na kuendesha sekta hiyo muhimu kwa ukuaji wa uchumi. Kwa sasa kampuni hiyo inatoa ufadhili wa masomo ya shahada ya uzamili kwa Watanzania kumi kila mwaka kwenye eneo la mafuta na gesi.

Bw. Bacher pia alieleza kuwa uwekezaji wa kampuni hiyo kwenye masuala ya gesi ni wa muda mrefu, na matunda yake yanachukua muda kuonekana. Lakini yakishatoka yataongeza mara mbili upatikanaji wa nishati ya umeme nchini Tanzania, ambapo itaongeza uzalishaji wa viwanda pamoja na faida nyingine nyingi za kiuchumi.

Ujumbe wa Waziri Mahiga ulisifu jitihada za kujenga uwezo kwa Watanzania na kuelezea kuwa hatua hiyo itasadia sana kwenye kutoa elimu kwa Watanzania ili wawe na matarajio sahihi ya matokeo ya shuguli za uwekezaji wa kampuni hiyo nchini Tanzania. Waziri Mahiga aliwasihi kuendelea kujenga uwezo wa kada ya kati ya wataalam wa gesi kwa kushirikiana pia na vyuo vya ndani ya nchi ili utaalamu huo uendelezwe nchi nzima.

Waziri Mahiga yupo nchini Norway kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 18 hadi 20 Juni 2018, kufuatia mualiko wa mwenyeji wake Mhe. Ine Eriksen Soreide, Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway. Ziara hiyo imekuja baada ya Tanzania na Norway kusaini makubaliano ya ushirikiano mwaka 2017.
Mbali na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, Mheshimiwa Mahiga na ujumbe wake wanatarajiwa kukutana na makampuni ya Norway yanayowekeza Tanzania pamoja na kuzungumza kwenye Jukwaa la Oslo kuhusu uthabiti wa amani kwenye Eneo la Maziwa Makuu na mchango wa nchi jirani.

Jukwaa la Oslo linakutanisha watu mashuhuri duniani wanaoshughulika na utatuzi wa migogoro duniani akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Mkutano huu hufanyika mara moja kila mwaka kujadili masuala ya utatuzi wa migogoro duniani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 19 Juni, 2018


Wednesday, June 13, 2018

Waziri afanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Maziwa Makuu Mhe. Said Djinnit alipomtembelea Wizarani terehe 13 Juni 2018, Dar es Salaam. Anayeshuhudia kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez.

Mjumbe huyo alifika Wizarani kwa lengo la kuzungumzia hali ya usalama na amani katika nchi za Maziwa Makuu.Aidha, mjumbe huyo alimuomba Mhe. Waziri kufikisha shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa mchango mkubwa wa Tanzania katika kusaidia kutunza amani ya nchi za Maziwa Makuu.

 Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Mhe.Djinnit.
Mkutano ukiendelea, wanaoshuhudia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw. Salvatory Mbilinyi(wa kwanza kulia kwa Waziri), Bw. Ally Ubwa Afisa Mambo ya Nje na Bw. Magabilo Murobi Katibu wa Waziri na kushoto ni Ujumbe wa Mhe. Djinnit alioongozana nao.

Tuesday, June 12, 2018

Naibu Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Mabalozi wa Uturuki, Algeria, Kuwait na Palestina.

Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhan M. Mwinyi( wa kwanza kushoto) akiwasikiliza Mabalozi wa Uturuki, Palestina, Algeria na Kuwait ( hawapo pichani) walipomtembelea Wizarani tarehe 12 Juni,2018,Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Bw. Suleiman Saleh na Mwisho ni Afisa Mambo ya Nje Bw. Fidelis Odiro wakifuatilia mazungumzo hayo. 
Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili namna ya kuendelea kuboresha mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na nchi hizo. Pia walizungumzia kuhusu azimio la Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa Palestine.
Balozi wa Algeria Mhe. Saad Belabeb(wa kwanza kushoto), Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al Najem, Balozi wa Palestine nchini Mhe.Hazem Shabat na mwisho ni Balozi wa Uturuki nchini Mhe.Ali Davutaglu wakimsikiliza Balozi Mwinyi (hayuko pichani) katika mazungumzo hayo.

Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.