Thursday, July 19, 2018

Ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea nchini Tanzania



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ZIARA YA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA KOREA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Lee Nak-yon atafanya ziara ya kikazi nchini kwa mwaliko wa mwenyeji wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), kuanzia tarehe 21 hadi 23 Julai 2018. Ziara hiyo itakuwa ya kwanza kufanywa na kiongozi wa ngazi ya juu kutoka Jamhuri ya Korea tangu nchi zetu mbili zianzishe mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1992. 

Madhumuni ya ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili na kufungua zaidi fursa za ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi katika ngazi na sekta mbalimbali. Mhe. Waziri Mkuu Lee atafuatana na ujumbe mzito wa maafisa wa Serikali, wabunge na wafanyabiashara wakubwa. Ujumbe wa wafanyabiashara utakaoongozana na Mhe. Lee unatarajiwa kukutana na wenzao wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Wafanyabiashara uliopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam tarehe 23 Julai 2018. Mkutano wa kwanza ambao ulikuwa na mafanikio makubwa ulifanyika Seoul mwezi Februari 2018.

Mhe. Lee Nak-yon atawasili nchini saa kumi na mbili na nusu jioni (12:30) ya tarehe 21 Julai 2018 na atapokelewa na mwenyeji wake Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku inayofuata, Waziri Mkuu Lee na mwenyeji wake Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), watafanya mazungumzo rasmi jijini Dar es Salaam na baadaye watashuhudia uwekaji saini wa mkataba wa kuondoa hitaji la visa kwa wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na za utumishi (diplomatic and official/service passport). Aidha, Mhe. Lee atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa ajili ya kusalimiana.

Jamhuri ya Korea ni mshirika mkubwa wa maendeleo wa Tanzania ambapo kupitia  Shirika la Kimataifa la Maendeleo (KOICA) na Mfuko wa Ushirikiano wa Uchumi na Maendeleo (EDCF) yamekuwa yakitoa misaada na mikopo mingi ya masharti nafuu kwa Tanzania ikiwemo misaada ya fedha katika bajeti, ujenzi wa miundombinu ya jamii, mafunzo ya muda mfupi na mrefu, wataalamu mbalimbali wa kujitolea, vifaa na mashine kwa ajili ya sekta mbalimbali ikiwemo ya afya.

Baadhi ya miradi ambayo imegharamiwa na Serikali ya Korea ni pamoja na Mradi wa kuboresha Huduma ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Chanika, Mradi wa Mfumo wa Usajili wa Meli na Mabaharia kwa Njia ya Mtandao Zanzibar, Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Taifa ya Taaluma na Tiba (MUHAS) kampasi ya Mloganzila na ujenzi wa daraja katika mto Malagarasi.

Vile vile, Korea ni mshirika mkubwa katika kusaidia maendeleo ya Bara la Afrika ambapo hivi karibuni katika mkutano wa Sita wa Jukwaa la Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na Africa (KOAFEC VI) uliofanyika mwezi Mei 2018, Busan, Korea ambapo Serikali ya Korea ilitangaza msaada wa Dola za Marekani bilioni 5 kwa ajili ya Bara la Afrika kwa kipindi cha mwaka 2018/2020. Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazonufaika na msaada huo.



Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
19 Julai 2018

Wednesday, July 18, 2018

Mabalozi wanne waagwa jijini Dar Es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) aliyesimama katikakti akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi waliomaliza muda wao wa uwakilishi nchiniTanzania. Mabalozi hao, wakwanza kutoka kushoto ni Balozi wa Norway, Mhe. Hanne-Marie Kaarstad, Balozi wa Malawi, Mhe. Hawa Olga Ndilowe, Balozi wa Sweden, Mhe. Katarina Rangnitt na Balozi wa Canada, Mhe. Ian Myles. Mhe. Dkt. Mahiga aliandaa hafla ya kuwaaga Mabalozi hao iliyofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 17 July 2018. Katika hafla hiyo, Dkt. Mahiga aliwashukuru Mababalozi hao kwa niaba ya Serikali zao kwa mchango mkubwa wanaotoa kuboresha sekta mbali mbali hapa nchni zikiwemo za Elimu, Afya, Biashara, Kilimo pamoja na Miundombinu. Aidha, Mabalozi pia walipata nafasi ya kutoa neno la shukrani kwa Wizara pamoja na watumishi wake kwa ujumla kwa kuwapa ushirikiano wa kutosha uliowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi hapa nchini.
Dkt. Mahiga akizungumza kwenye hafla ya kuwaaga Waheshimiwa Mabalozi walio maliza muda wao wa uwawakilishi nchini.

Sehemu ya Mabalozi walio hudhuria hafla hiyo wakisimsikiliza kwa makini Mhe. Dkt. Mahiga (hayupo pichani).
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya naAmerika, Bw. Jestas Nyamanga (kulia) pamoja na Balozi Rangnitt nao wakimsikiliza kwa makini Dkt. Mahiga.
Sehemu nyingine ya Mabalozi waliohudhuria hafla hiyo
Mabalozi walio maliza muda wa uwakilishi nchini wakigonga glasi na Waziri Mahiga ikiwa ni ishara ya kuwatakia Viongozi wa Nchi zao Afya njema na Baraka tele kwenye kufanikisha gurudumu la maendeleo.
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi wa Sweden picha ya mchoro wa Tembo wa Tatu pamoja na Mlima Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuikumbuka Tanzania pamoja na kuendelea kuvitangaza vivutio vinavyopatikana nchini. 
Balozi wa Malawi naye alipewa Picha yenye tembo wa Tatu na mlima Kilimanjaro
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi wa Norway picha inayofanana na wenzake isipokuwa yake ilikuwa na Michoro ya Wanyama aina ya Twiga, Tembo pamoja na Mlima Kilimanjaro.
Balozi wa Canada naye alipata zawadi ya picha yenye mchoro wa Tembo pamoja na Mlima Kilimanjaro, kwa pamoja Mabalozi hao walionyesha kuzifurahia zawadi hizo.
Dkt. Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi waliomaliza muda wa uwakilishi nchini pamoja na Mabalozi ambao bado wanaendelea kuziwakilisha nchi zao. 











Tuesday, July 17, 2018

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Kenya nchini

Balozi Mteule wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.). Mara baada ya kuwasilisha nakala hizo Mhe. Mahiga na Balozi Kazungu walipata fursa ya kuzungumza kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya hususan kwenye sekta za biashara, uchumi na elimu. Tukio hilo lilifanyika kwenye Ofisi Ndogo ya Wizara iliyopo Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Julai, 2018. 
Dkt. Mahiga akiendelea na mazungumzo na Balozi Mteule wa Kenya hapa nchini
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Mteule wa Kenya nchini. Kushoto ni Bibi Judica Nagunwa na Bw. Magabilo Murobi
Balozi Kazungu akimweleza jambo Dkt. Mahiga
Mazungumzo yakiendelea kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Kazungu
Picha ya pamoja.
Dkt. Mahiga akiagana na Balozi Mteule wa Kenya nchini Tanzania. 






Thursday, July 12, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU FURSA ZA MASOMO


TAARIFA KWA VYOMBO VY HABARI

FURSA ZA UFADHILI WA MASOMO
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili wa masomo katika kozi mbalimbali kutoka Serikali ya Saudi Arabia.

Mafunzo hayo yatatolewa katika Chuo Kikuu cha Imam Abdulrahman bin Faisal kilichopo Saudi Arabia. Taarifa kamili kuhusu ufadhili, kozi na taratibu zote za namna ya kuomba zinapatikana kupitia tovuti ya Chuo hicho www.iau.edu.sa
 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje Na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
12 Julai, 2018


Tuesday, July 10, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaendelea kutoa huduma kwenye maonesho ya sabasaba

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (wa pili kushoto) akifafanua jambo kwa mteja aliyetembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa yanayoenedelea jijini Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Rajab Luhwavi Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji (wa kwanza kulia) akizungumza na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya sabasaba.



Balozi Mohamed Haji Hamza Mkurugenzi wa ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje Zanzibar (kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia Bw. Shoo Innocent alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba 

Bw. Zakariyya Kera Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya sabasaba

Bw. Teodos Komba akifanunua jambo kwa mteja aliyembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Wanafunzi kutoka Dar es Salaam Islamic Secondary School wakipewa maelezo walipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya sabasaba


Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiangalia bidhaa kwenye maonesho ya sabasaba

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiangalia bidhaa kwenye maonesho ya sabasaba

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiangalia maonesho ya kazi ya ubunifu wa teknolojia kutoka kwa Wataalam wa Taasisi ya Mafunzo ya Ufundi Zanzibar

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akitoka kuangalia bidhaa kwenye jengo la Zanzibar katika maonesho ya sabasaba 

Sunday, July 8, 2018

Waziri Mahiga atembelea maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa (Sabasaba)



Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alipotembelea banda la Wizara.

Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akiwa katika mahojiano na wanahabari kwenye maonesho ya biashara kimataifa maarufa sabasaba yanayofanyika jijini Dar  es Salaam
Mhe.Waziri akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Mhe. Mahiga akisikiliza maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa ya sabasaba

Thursday, July 5, 2018

Naibu Waziri atembelea maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa (sabasaba)



Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

 Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga pamoja na watumishi wa Wizara. 

Dkt. Kolimba alifurahishwa na ushiriki wa Wizara  kwenye maonyesho ya sabasaba, ambapo aliwasisitiza watumishi wa Wizara kuendelea kutumia fursa hiyo kutoa elimu kwa umma kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara. 
 Mhe.Dkt. Kolimba akipata maelezo kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga

Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza na watumishi alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Mkurugenzi wa Masomo wa Chuo cha Diplomasia Prof. Watengere Kitojo  akizungumza na watumishi alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya sabasaba .
Wanafunzi kutoka Chuo cha Diplomasia wakipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara walipotembelea bandala kwenye maonesho ya saba.Wanafunzi hao walipata fursa ya kuelezwa kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kikanda na kimataifa sambamba na fursa na faida zinazopatikana.
Bw. Teodos Komba Afisa Mawasilino, akielezea jambo kwa wananchi waliojitokeza  kwenye banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Bw. Hassan Mnondwa akielezea jambo kwa wananchi waliotembelea banda la Wizara.

Mhe.Dkt. Susan Kolimba akiwa katika Picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara

Tuesday, July 3, 2018

Wananchi waendelea kujitokeza katika banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba


Mama Anna Mkapa Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa, akiangalia moja ya machapisho yanayopatikana katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya biashara ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Wananchi wengi wameendelea kujitokeza kwenye banda la Wizara ili kuongeza  uelewa  juu ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara, ikiwemo namna Wizara inavyosimamia na kuteleza sera ya mambo ya nje ya nchi,  faida  na hatua mbalimbali za mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lipo katika jengo la sabasaba hall.Wananchi  wote wanakaribishwa 
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto) wakizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye banda la Wizara (kulia)



Sehemu nyingine ya watumishi wa Wizara wakihudumia wananchi

Sehemu nyingine ya wananchi wakiuliza masuala mbalimbali kwa watumishi wa Wizara
Sehemu nyingine ya wananchi wakipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara

Sehemu nyingine ya wananchi wakipewa maelezo na mtumishi wa Wizara