Tuesday, March 12, 2019

Prof. Kabudi na Dkt. Mahiga wakabidhiana ofisi

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye awali alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akikabidhi Taarifa ya Makabidhiano ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.  Prof. Palamagamba Kabudi ambaye awali alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Makabidhiano hayo yalifanyika jijini Dodoma tarehe 12 Machi 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi (kushoto) akimkabidhi Taarifa ya Makabidhiano ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akiweka saini Kitabu cha mahudhurio mara baada ya kukabidhiwa ofisi jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi mara baada ya makabidhiano ya ofisi.
Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakishuhudia makabidhiano ya ofisi kati ya Waziri wa Katiba na Sheria na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akiongea na Wakuu wa Idara na Vitengo (hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa ofisi na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga.
Wakuu wa Idara na Vitengo wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hayupo pichani).
Wakuu wa Idara na Vitengo wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiongea na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi Savera Kazaura akitoa maelezo kwa  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Waziri wa Katiba na Sheria kabla zoezi la makabidhiano kuanza.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana na baadhi ya watumishi mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Anayemkaribisha  ni mmoja wa watumishi hao, Bw. Shaban Mtambo.
Bi. Chiku Kiguhe akisalimiana na Mhe. Prof. Kabudi.
Bw. Habibu Ibrahim akisalimiana na Mhe. Waziri.
Bw. Maulidi Mkenda akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiongea na baadhi ya watumishi waliojitokeza kumpokea mara alipowasili kwa mara ya kwanza katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje jijini Dodoma.
Bw. Caesar Waitara akisalimiana na Mhe. Prof. Kabudi



Monday, March 11, 2019

Balozi wa Tanzania nchini India awasilisha Hati za Utambulisho nchini Bangladesh

Balozi wa Tanzania nchini India anayewakilisha pia nchini Bangladesh, Mhe. Baraka Luvanda akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Bangladesh, Mhe. Md. Abdul Hamid katika hafla iliyofanyika hivi karibuni katika Ikulu ya nchi hiyo jijini Dhaka.
Mhe. Balozi Luvanda akizungumza na Mhe. Rais Md. Abdul Hamid mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais huyo
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Rais Md. Abdul Hamid mara baada ya mazungumzo baina yao
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Rais Md. Abdul Hamid mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho. Kushoto ni Dkt. Kheri Goloka, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania ambaye alifuatana na Balozi Luvanda kwenye hafla hiyo

Mhe. Balozi Luvanda akiwa mbele ya gwaride la heshima mara baada ya kuwasili Ikulu ya Dhaka,  Bangladesh

Mhe. Balozi Luvanda akipita katikati ya gwaride la heshima mara baada ya kuwasilis Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha hati za utambulisho

Sunday, March 10, 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Hakuna Mtanzania aliyepoteza maisha kwenye ajali ya ndege iliyotokea Ethiopia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea kwa masikitiko makubwa, taarifa kuhusu ajali ya ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la Ethiopia, iliyotokea tarehe 10 Machi 2019 nchini Ethiopia na kusababisha vifo vya watu wote 157 waliokuwemo kwenye ndege hiyo.

Ndege hiyo ya abiria, aina ya  Boeing 737 yenye namba za usajili ET 302 iliyokuwa inafanya safari zake za kawaida kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole, mjini Addis Ababa, Ethiopia kuelekea mjini Nairobi, Kenya, ilikuwa imebeba abiria 149 kutoka mataifa mbalimbali na wafanyakazi wa kwenye ndege wapatao 8.

Kwa mujibu wa taarifa kuhusu ajali hiyo, iliyotolewa kwa waandishi wa habari na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la Ethiopia, ikiwemo orodha ya abiria na mataifa wanayotoka, hakuna Mtanzania aliyekuwemo kwenye ndege hiyo.

Orodha ya nchi na idadi ya raia (kwenye mabano) waliokuwa kwenye ndege hiyo  ni kama ifuatavyo: Kenya (32), Canada (18), Ethiopia (9), China (8), Italia (8), Marekani (8), Ufaransa (7), Uingereza (7), Misri (6), Ujerumani (5), India (4), Slovakia (4), Austria (3), Urusi (3), Sweden (3), Hispania (2), Israel (2), Morocco (2) na Poland (2).

Nchi zingine ni Ubelgiji (1), Djibouti (1), Indonesia (1), Ireland (1), Msumbiji (1), Norway (1), Rwanda (1), Saudi Arabia (1), Sudan (1), Somalia (1), Serbia (1), Togo (1), Uganda (1), Yemen (1), Nepal (1), Nigeria (1) na raia aliyekuwa na hati ya kusafiria ya Umoja wa Mataifa (1).

Mamlaka husika zimeanza uchunguzi ili kujua  chanzo cha ajali hiyo.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaungana na wote walioguswa na msiba huu mzito kutoa pole kwa mataifa yote yaliyopoteza raia wake kwenye ajali hiyo.



Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dodoma.

10 Machi 2019


Saturday, March 9, 2019

Serikali ya awamu ya tano haichukii wawekezaji, Dkt. Magufuli

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali ya awamu ya tano haichukii wawekezaji, Dkt. Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amesema Serikali ya awamu ya tano anayoiongoza inathamini wawekezaji, tofauti na dhana ya baadhi ya watu kuwa wawekezaji katika awamu ya tano wanaonekana kuwa ni maadui.

Mhe. Rais Magufuli alisema hayo wakati wa sherehe ya kufungua mwaka 2019 ya wanadiplomasia (sherry party) iliyofanyika Ikulu jijini Dar Es Salaam tarehe 08 Machi 2019, na kuhudhuriwa na Mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yaliyopo hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli alisema uamuzi aliochukua hivi karibuni wa kuunda Wizara maalum ya uwekezaji ni ishara ya wazi kuwa Serikali ya awamu ya tano inathamini wawekezaji, na kuwasihi wanadiplomasia kuitumia wizara hiyo na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo ameifanyia mabadiliko.

Rais Magufuli alisema, Serikali yake imeshaanza mpango kabambe wa kuboresha mazingira ya uwekezaji na kutoa wito kwa wale wenye dhamira ya dhati ya kuwekeza nchini, waende mamlaka husika ili wahudumiwe.  “Mwenye dhamira ya dhati ya kuwekeza nchini, aende Wizara ya Uwekezaji au Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akikwamishwa huko aje kwangu ili nimkwamue huyo aliyekwamisha”, Rais Magufuli alisema.

Wanadiplomasia walioshiriki hafla hiyo, walisisitizwa kuhamasisha wawekezaji kuja kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali zikiwemo za kilimo, mifugo, uvuvi, utalii, madini na viwanda vya nguo. “Serikali inahimiza uwekezaji katika sekta zinazotumia malighafi zinazopatikana nchini na zitakazotoa ajira za kutosha kwa vijana wa kitanzania kwa madhumuni ya kukuza uchumi wa nchi”.  Rais Magufuli alisema.

Kuhusu utalii, Rais Magufuli alieleza kuwa, Tanzania ina vivutio vingi vya utalii, zikiwemo fukwe, uoto wa asili, malikale, mbuga za Wanyama na kwamba Serikali imejipanga kutangaza vivutio hivyo, hususan, vile vinavyopatikana kanda ya kusini. Mhe.  Rais aliitumia fursa hiyo kulipongeza Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa uamuzi wake wa kuanzisha channel maalum ya kutangaza vivutio vya utalii.

Kwa upande wa sekta ya madini, Serikali imejipanga kudhibiti wizi, biashara ya magendo, kuanzisha masoko ya kuuza madini na kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya kuchakata madini, ili sekta hiyo iwe na mchango mkubwa katika kuchangia uchumi wa nchi.

Aidha, Rais Magufuli alitumia hafla hiyo kuwaeleza wanadiplomasia, mafanikio ya Serikali ya mwaka 2018, mafanikio hayo ni Pamoja na Serikali kuendelea kulinda na kudumisha amani ya nchi; kukuza uchumi wa nchi ambapo katika nusu ya kwanza ya mwaka 2018, Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi tano barani Afrika, uchumi wake umekua kwa kasi ikizidiwa na Ethiopia pekee.

Tanzania pia iliweza kudhibiti mfumuko wa bei na iliongoza katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuvutia uwekezaji wa Dola za Marekani bilioni 1.18.

Mafanikio mengine ni Pamoja na ujenzi wa Miundombinu ikiwemo: ujenzi unaondelea wa reli ya kiwango cha Kimataifa kutoka Dar Es Salaam hadi Dodoma; ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme wa Mega Watts 2100 katika Mto Rufiji; ujenzi na upanuzi wa barabara mbalimbali nchini; ujenzi wa meli mpya katika Ziwa Victoria; upanuzi wa bandari za Dar Es Salaam, Mtwara na Tanga na kuboresha viwanja vya ndege mbalimbali nchini ikiwemo ujenzi wa Terminal 3 kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Serikali pia imepiga hatua katika kuboresha utoaji wa huduma za kijamii katika sekta ya afya, elimu na maji. Kwa upande wa afya, bajeti ya sekta hiyo imeongezeka kutoka bilioni 31 hadi kufikia bilioni 270 ambapo ujenzi wa vituo vya afya 305 umekamilika na ujenzi wa hospitali 67 za Wilaya unaendelea, ukilenga kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Kuhusu elimu, Serikali imeendelea na mpango wake wa kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari na kuongeza bajeti ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Aidha, Miundombinu ya maji imeimarishwa ambapo upatikanaji wa maji kwa maeneo ya mijini umefikia asilimia 80 na asilimia 65 kwa maneo ya vijijini.
Rais Magufuli alieleza kuwa mafanikio ambayo Serikali ya awamu ya tano inaendelea kuyapata yanatokana na Ushirikiano na mchango mkubwa kutoka kwa wanadiplomasia, na kuahidi kuwa Serikali yake itaendelea kudumisha Ushirikiano huo.

Alihitimisha hotuba yake kwa kueleza kuwa, watumishi wengi wa Serikali walishahamia Makao Makuu ya Serikali jijini Dodoma na kuelezea matumaini yake kuwa, baadhi ya Balozi zitakuwa zimeshaanza mchakato wa kuhamia Dodoma, ukizingatia kuwa Serikali imetoa viwanja bure kwa ofisi zote za balozi.  
  
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar Es Salaam, Tanzania

09 Machi 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na Mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yaliyopo nchini katika Sherehe za kufungua Mwaka 2019 (sherry party) zilizofanyika Ikulu, Dar Es Salaam jana. Sherehe hizo zimehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na Wakuu wa Idara na Vitengo.
Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiendelea kuzungumza wakati wa sherehe hizo.
Mabalozi wakimpongeza Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 
Rais Magufuli akiendelea kuzungumza na wanadiplomasia

Kiongozi wa Mabalozi ambaye ni Balozi wa Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed naye akizungumza kwa niaba ya Jumuiya ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa.
Sehemu ya Mabalozi pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (kulia)
Mshereheshaji kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Bertha Makilagi akisherehesha kwenye Shughuli hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana na Balozi wa Namibia, Mhe.Theresa Samaria mara baada ya kumalizika kwa sherehe hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana na Balozi wa Oman hapa nchini, Mhe. Ali A. Al Mahruqi mara baada ya kumalizika kwa sherehe hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Sarah Cooke mara baada ya kumalizika kwa sherehe hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisalimiana na Balozi wa India hapa nchini, Mhe. Sandeep Arya mara baada ya kumalizika kwa sherehe hizo.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kulia) akisalimiana na Balozi wa Ufaranza nchini, Mhe. Frederic Clavier mara baada ya kumalizika kwa sherehe za mwaka 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoziwakilisha nchni zao hapa nchini, mara baada ya kumalizika kwa Sherehe za kufungua Mwaka 2019 (Diplomatic Sherry Party).




Friday, March 8, 2019

Sakata la Chuo cha Diplomasia lahamia Takukuru

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe (kulia) akikabidhi ripoti za ukaguzi za Chuo cha Diplomasia, kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (PCCB), Bw. Diwani Athumani kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa tuhuma za ubadhilifu wa fedha uliofanywa na baadhi ya viongozi wa chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika leo kwenye Ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar Es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia, Balozi Ombeni Sefue akishuhudia makabidhiano ya ripoti za ukaguzi ambazo zimeainisha ubadhilifu wa fedha katika Chuo cha Diplomasia.
Balozi Sefue (kushoto), Dkt. Mnyepe na Bw. Diwani wakibadilishana mawazo kuhusu utendaji kazi wa Chuo cha Diplomasia. 
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Diwani Athumani akiagana na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia, Balozi Ombeni Sefue.




Thursday, March 7, 2019

Prof. Kabudi akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Richard Sezibera. Katika mazungumzo yao, Mhe. Sezibera alimpongeza Mhe. Kabudi kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ernest Mangu na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo. Mhe. Sezibera yupo nchini kwa ajili ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame. 
Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Mhe. Eugene Kayihura (kulia) na Afisa Ubalozi wa Rwanda wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Prof. Kabudi na Mhe. Dkt. Sezibera (hawapo pichani). 
Mhe. Prof. Kabudi akimwelezea jambo Mhe. Dkt. Sezibera wakati wa mazungumzo hayo.
Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ernest Mangu pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw. Wilbroad Kayombo wakiwa kwenye Mazungumzo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (katikati) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Richard Sezibera (wapili kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ernest Mangu (wa kwanza kulia) na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Mhe. Eugene Kayihura (wa kwanza kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.




ZIARA YA KIKAZI YA RAIS KAGAME WA RWANDA NCHINI TANZANIA


Rais Kagame awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (kulia) akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ziara ya siku mbili. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi akitembea na Rais Kagame kuelekea katika chumba cha wageni maalum.
Rais Kagame akiwapungia mkono wananchi waliofika uwanja wa ndege kwa ajili ya kumpokea.
Prof. Kabudi na Rais Kagame wakiingia kwenye gari kwa ajili ya kuelekea Ikulu jijini Dar Es Salaam.




Wednesday, March 6, 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taarifa kuhusu ziara ya Mhe. Paul Kagame, Rais wa Jamhuri ya Rwanda

Mhe. Paul Kagame, Rais wa Jamhuri ya Rwanda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, atawasili nchini tarehe 7 Machi 2019 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Ziara hiyo inafanyika kufuatia mwaliko wa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Ziara hii itatoa fursa kwa viongozi hao wawili kujadiliana masuala mbalimbali kuhusu uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizi mbili. Aidha, Viongozi hao wanatarajia kuzungumzia masuala mbalimbali ya mtangamano katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe. Kagame, Rais wa Jamhuri ya Rwanda, atawasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere saa Tisa Alasiri tarehe 7 Machi 2019 na kupokelewa na mwenyeji wake, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Rais Kagame anatarajia kuondoka nchini tarehe 8 Machi, 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
6 Machi 2019


Tuesday, March 5, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI WAWILI, BALOZI MMOJA PAMOJA NA KUSHUHUDIA UAPISHWAJI WA MAOFISA WATANO WA JESHI LA POLISI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Yahya Simba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambia Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya pamoja na Makamishna watano kutoka jeshi la Polisi, Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Palamagamba Kabudi, pamoja na Balozi Yahya Simba mara baada ya hafla ya Uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.