Monday, June 17, 2019

Call to Design Corporate Logo for the EAC 20 Anniversary


East African Community

Consultancy ON DESIGN OF THE EAC 20TH ANNIVERSARY CORPORATE LOGO

1.0 Introduction

The EAC is set to mark its 20th Anniversary with various activities and events culminating into EAC Day on 30th November, 2019, the date of the 21st Ordinary Summit of the EAC Heads of State.

2.0 Objective

For purposes of publicity and branding, the Community requires a logo to brand its 20th Anniversary celebrations. The EAC Secretariat intends to engage a creative artist or graphic designer to come up with a logo for the anniversary.

The graphic designer will be required to provide the following:

i)   Three designs of the proposed 20th Anniversary Logo from which the Secretariat can select;
ii)  Three soft copies of the proposed 20th Anniversary Logo from which one will be selected for use during the 20th Anniversary;
iii) Three hard copies of the proposed logo; and
iv) Designs that are usable in multimedia channels (print, electronic, social media, etc.)

4.0 Qualification / Competencies required

(a)  A Senior Expert/Design Firm who has at least 10 years previous experience in graphics design, new brand creation and logos development
(b)  A Senior Expert/Design Firm who has directed or supported at least two re branding activities
(c)  A Senior Expert/Design Firm who has strong experience in creating visual campaigns 
(d)  Bachelor’s Degree in Graphics design, brand development, business administration or other relevant fields. A Master’s Degree will be preferred but is not mandatory. 
(e)  Must be an East African national/East African based Brand Design Firm

5.0 Submission Requirements

(a)  Application Letter/Expression of Interest
(b)  CV of key experts to be involved with references for previous assignments
(c)  Previous design portfolio (new logo/brand design development, not more than 20 pages)
(d)  Proof of minimum two previous similar assignments undertaken.

Interested Brand Design Experts/Firms should submit Technical and Financial proposals by email to Procurement@eachq.org not later than 26th June, 2019.

Wamiliki wa Hoteli wakutana na Prof. Kabudi Kuhusu SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akihutubia kwenye mkutano wa wamiliki na wafanyabiashara wa hoteli (hawapo pichani) Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.
  Baadhi ya Wafanyabiashara na Wamiliki wa Hoteli wakifuatilia kwa ukaribu mkutano baina yao na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)(hayupo pichani) Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Faraji Mnyepe akifafanua jambo wakati wa mkutano wa wamiliki na wafanyabiashara wa hoteli (hawapo pichani) Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Faraji Mnyepe wakati wa Mkutano wa wamiliki na wafanyabiashara wa hoteli (hawapo pichani) Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiendelea kuhutubia kwenye mkutano wa wamiliki na wafanyabiashara wa hoteli (hawapo pichani) Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.
 Sehemu ya Wafanyabiashara na Wamiliki wa Hoteli waliohudhuria mkutano wa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)(hayupo pichani). Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019. 
Baadhi ya Wafanyabiashara na Wamiliki wa Hoteli wakisubiri kupiga picha ya pamoja  na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)(hayupo pichani) baada ya kumalizika kwa mkutano baina yao katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na wamiliki na wafanyabiashara wa hoteli baada ya kumalizika mkutano baina yao uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.  Kushoto ni Katibu Mkuu wa wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Mnyepe na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Bi. Agnes Kayola. 
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na baadhi ya wamiliki na wafanyabiashara wa Hoteli baada ya kumalizika mkutano baina yao katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. June 15, 2019.

Friday, June 14, 2019

Prof. Kabudi amuaga Balozi wa India

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na Balozi wa India anayemaliza muda wa uwakilishi nchini, Mhe. Sandeep Arya (wa pili baada ya aliyevaa tai nyekundu) jijini Dar Es Salaam. Mhe. Waziri alimuandalia chakula cha jioni kwa ajili ya kumuaga Mhe. Balozi. Katika chakula hicho, Prof. Kabudi alishukuru misaada ya maendeleo inayotolewa na Serikali ya India katika sekta mbalimbali zikiwemo za maji, elimu, nishati na afya. Mhe. Waziri pia alimuhakikishia Mhe. Balozi kuwa Serikali itatoa ushirikiano kwa Balozi mpya atakayekuja kuchukua nafasi yake nchini.
Balozi wa India anayemaliza muda wa uwakilishi nchini (wa pili kutoka kulia) akiwa na ujumbe wake wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Prof. Kabudi akiwa na ujumbe wake wakati wa chakula cha jioni kwa ajili ya kumuaga Balozi wa India anayemaliza muda wa uwakilishi nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimpa zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro na Mbuga ya Wanyama Balozi wa India anayemaliza muda wa uwakilishi nchini, Mhe. Sandeep Arya.

TANGAZO KUHUSU USHIRIKI WA WIZARA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA


TANGAZO

            MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuwatangazia wananchi wote kuwa, itashiriki Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kuanzia tarehe 17 hadi 22 Juni 2019. Maadhimisho haya ni kwa mujibu wa kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kushiriki shughuli mbalimbali zinazohusu Utumishi wa Umma.

Wakati wa maadhimisho hayo, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeandaa madawati maalum ya kutoa huduma kwa wananchi katika Ofisi za Wizara zilizopo Kata ya Mtumba jijini Dodoma na zile zilizopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Huduma zitakazotolewa ni pamoja na kusikiliza na kutoa ufafafanuzi wa hoja mbalimbali za wananchi kuhusu Wizara pamoja na kutoa elimu kuhusu majukumu yanayotekelezwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika.

Madawati hayo yatakuwa wazi kuanzia saa 1.30 asubuhi hadi saa 10.00 jioni.


NYOTE MNAKARIBISHWA.


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
14 Juni 2019




Kampuni 11 za Uturuki zatafuta fursa za Uwekezaji

Dodoma, 14 Juni 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kampuni 11 za Uturuki zatafuta fursa za Uwekezaji 

Ujumbe wa kampuni 11  kutoka Uturuki upo nchini kwa ajili ya kuangalia fursa mbalimbali za uwekezaji, hususan kwenye sekta ya viwanda vya dawa za binadamu, vifaa vya maabara, vyombo vya ndani,  vifaa vya umeme, ujenzi pamoja na ununuzi wa korosho.

Ziara hiyo imetokana na uratibu wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uturuki kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Ujumbe huo ambao uliwasili nchini tarehe 10 Juni 2019 ulishiriki mkutano (B2B) uliondaliwa na TPSF tarehe 11 Juni 2019. Katika mkutano huo pamoja na mambo mengine,  wawakilishi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Ukanda  wa Uwekezaji (EPZA) na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade) walitoa maelezo kuhusu kanuni, taratibu na mazingira ya kufanya biashara hapa nchini.

Ujumbe huo utatembelea Zanzibar tarehe 13 Juni 2019 na baadaye Dodoma kwa ajili ya kuangalia maonyesho ya masuala ya ujenzi. Ujumbe huo utaondoka nchini tarehe 16 Juni 2019 kurejea Uturuki.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Majadiliano baina ya wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki yakiendelea katika ukumbi wa TPSF. Aliyesimama ni Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe Ali Davutoglu ambaye anatoa ufafanuzi kuhusu mazingira ya biashara Tanzania.

Mwenyekiti wa TPSF, Bw. Salum Shamte (katikati) akipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa kampuni hizo za Uturuki, Bw. Ali Engiz. Wengine ni Bw. Godfrey Simbeye (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF na Mhe. Ali Davutoglu, Balozi wa Uturuki hapa nchini.

Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Hassani Mwamweta (kushoto) katika picha ya pamoja na viongozi wa wafanyabiashara wa Uturuki na Tanzania.


Thursday, June 13, 2019

Prof. Kabudi afanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Rwanda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akisalimiana na mgeni wake ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Mukabalisa Donatille alipowasili katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 12 Juni 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Mukabalisa Donatille. Mazungumzo yao yalifanyika  katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 12 Juni 2019
Mazungumzo kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.)  na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Mukabalisa Donatille yakiendelea. Kushoto kwa Mhe. Kabudi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe. Mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 12 Juni 2019
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiagana na mgeni wake ambaye ni  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Mukabalisa Donatille mara baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 12 Juni 2019
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Mukabalisa Donatille (kulia) akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe mara baada ya kuwasili  katika Ofisi ndogo za Wizara  zilizopo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazungumzo na  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi yaliyofanyika tarehe 12 Juni 2019.


Wednesday, June 12, 2019

Prof. Kabudi aviomba vyombo ya habari kuelimisha umma kuhusu SADC




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akizungumza na Wamiliki na  Wakuu wa Vyombo vya Habari nchini katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere leo. Prof. Kabudi aliwaeleza Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari kuhusu Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika nchini mwezi Agosti 2019. Prof. Kabudi aliwasihi Wakuu hao kushirikiana na Serikali hususan katika kueleimisha umma kuhusu SADC pamoja na kutoa elimu kwa wafanaybiashara na wananchi kwa ujumla kuhusu fursa za mkutano huo za zile zinazopatikana katika nchi wanachama wa SADC. 

Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbas akitoa neno katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha Prof. Kabudi azungumze na Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari nchini. Dkt. Abbas alimuhakikishia Mhe. Waziri kuwa namna anavyovijua vyombo vya habari vya hapa nchini vinavyofanya kazi hana shaka yoyote kuhusu kutoa ushirikiano wao.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akisisitiza jambo kwa Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari.
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda akiongea na Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari nchini. Mhe. Makonda alisema kuwa mkoa wa Dar Es Salam umejipanga kupokea ugeni mkubwa wa mkutano wa SADC ambao unakadiriwa utahudhuriwa na watu zaidi ya 1000 kutoka nchi 16 wanachama wa SADC.
Meza Kuu kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini, Bw. Henry Mwanika, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Agnes Kayola, Waziri Prof. Kabudi, na Dkt. Abbas.
Baadhi ya Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari nchini walioshiriki katika kikao cha Waziri. Mwenye tai nyekundu ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania, Dkt. Ayoub Rioba.
Mkutano wa Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya habari na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ukiendelea
Wakongwe wa tasnia ya Habari nchini ambao walikuwa walimu wa Mhe. Waziri katika fani hiyo.
Picha ya Pamoja kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wamiliki na Wakuu wa Vyombo vya Habari nchini.



VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE COMMONWEALTH SECRETARIAT


PRESS RELEASE


VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE COMMONWEALTH SECRETARIAT

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the Commonwealth Secretariat inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Adviser, Service Delivery and Reporting.

Application details can be found through the Secretariat’s website, http://thecommonwealth.org/jobs. Closing date for application is Tuesday 18th June 2019.

“The Ministry encourages qualified Tanzanians to apply”.

Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
12th June 2019.


Tuesday, June 11, 2019

ZOEZI LA KUPIMA UTAYARI KUKABILI MAGONJWA YA MLIPUKO MIPAKANI LA ZINDULIWA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim (katikati), Waziri wa Viwanda wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Adan Abdulla Mohammed pamoja na Mhe. Cristophe Bazivambo kwa pamoja wakionyesha vitabu vinavyoelezea Umuhimu wa kufungua zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani. Uzinduzi huo umefanyika Namanga Mpakani mwa Tanzania na Kenya tarehe 11 Juni, 2019  
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim akihutubia kwenye ufunguzi wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, ambapo amesisitiza umuhimu wa Sekta za Afya kutumia Dhana ya Afya moja, wakati  akifungua zoezi hilo.  

 

Sehemu ya Viongozi kutoka Upande wa Kenya wakimsikili kwa makini Mhe. Mwalim
Waziri wa Viwanda wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Adan Abdulla Mohammed naye akihutubia kwenye ufunguzi huo. 


 Juu na chini ni wageni walio hudhuria ufunguzi wa zoezi hilo

Mhe. Mwalim, Mhe. Mohammed pamoja na Mhe. Ulega wakitiza na kupama maelezo kutoka kwa mtaalamu wa kukabiliana na Magonjwa ya Mlipuko


 Juu na Chini Mawaziri hao walitembelea vituo vya Kutolea Huduma kwa pamoja (OSBP) vilivyopo Namanga mpakani mwa Tanzania na Kenya.

Prof. Kabudi afanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda na masuala ya Afrika Mashariki wa Sudan Kusini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Waziri wa Viwanda, Biashara na masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhe. Paul Mayom Akech kabla ya kuanza mazungumzo yao. Mazungumzo hayo yamefanyika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam tarehe 11 Juni 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mazungumzo kati yake na Waziri wa Viwanda, Biashara na masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhe. Paul Mayom Akech (kushoto). Mazungumzo hayo yamefanyika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  tarehe 11 Juni 2019.
Waziri wa Viwanda, Biashara na masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Paul Mayom Akech, akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) baada ya mazungumzo kati yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Profesa Palamagamba John Kabudi. Mazungumzo hayo yamefanyika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam tarehe 11 Juni 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Profesa Palamagamba John Kabudi (katikati) akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mazungumzo kati yake na  Waziri wa Viwanda, Biashara na Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Paul Mayom Akech (kushoto). Kulia Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam tarehe 11 Juni  2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.  Profesa Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Mhe. Paul Mayom Akech,Waziri wa Viwanda,Biashara na Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Sudan Kusini. Kushoto kwa Profesa Kabudi ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe. Mazungumzo ya viongozi hao yalifanyika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam tarehe 11 Juni 2019.

Washiriki wa Mafunzo kutoka NDC wafanya ziara ya mafunzo nchini India

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (kushoto) akimkaribisha Ubalozini Brig. Jenerali Chestino Msola, Kiongozi wa Ujumbe wa Washiriki wa Mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea ubalozini hapo wakati wa ziara yao ya mafunzo ya siku tano nchini humo iliyoanza tarehe 10 Juni 2019.
Mhe. Balozi Luvanda (kushoto) akizungumza na Brid. Jenerali Msola (mwenye sare za jeshi za rangi ya kijani) pamoja  na viongozi wengine wa ujumbe wa washiriki wa mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India wakati wa ziara yao ya mafunzo nchini humo. Kulia ni Comodore Michael Mumanga na Dkt. Lucy Shule, Mkurugenzi wa  Mafunzo wa NDC.
Mhe. Balozi Luvanda akizungumza na ujumbe wa washiriki wa mafunzo (hawapo pichani) kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India wakati wa ziara yao ya mafunzo nchini humo. 
Mhe. Balozi Luvanda akiendelea na mazungumzo na ujumbe huo kutoka NDC
Mhe. Balozi Luvanda akipokea zawadi ya ukumbusho (memento) kutoka kwa Brig. Jenerali Msola
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ujumbe wa washiriki wa mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India wakati wa ziara yao ya mafunzo nchini humo. 
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wote.