Wednesday, July 24, 2019

Elewa Kuhusu SADC




Wadau waipongeza Serikali maandalizi ya Mkutano wa SADC

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Lugha Bashungwa amekutana na kufanya mazungumzo na Wadau mbalimbali kutoka Sekta binafsi na Serikali ikiwa ni muendelezo wa maandalizi ya Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe.

Katika kikao hicho wadau waliahidi kutoa ushirikiano unaohitajika ili kufanikisha maandalizi ya mkutano huo.


 
 Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam tarehe 24 Julai, 2019.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akieleza hatua ziizofikiwa katika maandalizi ya Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajiwa kufanyika nchini mwezi Agosti 2019.  
Wadau wa Sekta binafsi na Serikali wakimsikiliza kwa makini, Dkt. Mnyepe (hayupo pichani) alipokuwa akiongea.
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Bwana Laurean Bwanakunu akichangia jambo katika kikao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya sekta binafsi Tanzania (TPSF), Bw. Godfrey Simbeye akizungumza 
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Lugha Bashungwa (kulia) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe wakiwasikiliza wadau walipokuwa wakizungumza kwenye kikao hicho.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agness Kayola (wa kwanza kushoto), Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Sheria wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Caroline Chipeta wakiwa kwenye mkutano uliowakutanisha Sekta Binafsi na Serikali
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Kampuni ya SportPesa, Bw. Abbas Tarimba naye akichangia mada katika kikao hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bw. Albert Jonkergouw naye akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Juu na chini sehemu ya wadau kutoka Sekta Binafsi wakichangia mada kwenye Mkutano huo. 

Dkt. Mnyepe akiendelea kuzungumza kwenye Mkutano huo.






Monday, July 22, 2019

Prof. Kabudi afanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Bunge la jimbo la Zhejiang nchini China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wafanyabiashara katika jimbo la Zhejiang, China jimbo embalo ni la nne kwa uchumi miongoni mwa majimbo ya China.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiendelea kuzungumza na Mhe. Bi. GE Huijun pamoja na ujumbe alioambatana nao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akimkabidhi zawadi ya picha ya kuchora ya  Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro Bi. GE Huijun ambaye alionekana kuifurahia sana.



Friday, July 19, 2019

Wizara ya Mambo ya Nje yamuaga Balozi wa Switzerland na Denmark waliyomaliza muda wa kazi nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akimkabidhi Balozi wa Switzerland Mhe. Florence  Tinguely Mattli zawadi ya picha ya kuchora ya  Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro kama kumbukumbu yake ya vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akimkabidhi Balozi Jensen zawadi ya picha iliyochorwa  Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro kama kumbukumbu yake ya vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Wizara kwa ajili ya kumuaga Balozi wa Denmark Mhe. Einar Hebogard Jensen na Balozi wa Switzerland Mhe. Florence  Tinguely Mattli hapa nchini ambao wamemaliza muda wao wa kazi. Hafla hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Hyatty Regency Jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Balozi wa Denmark Mhe. Einar Hebogard Jensen (wa pili kutoka kulia), Balozi wa Switzerland Mhe. Florence  Tinguely Mattli (wa pili kutoka kushoto), Balozi wa Uingereza Mhe. Sarah Cooke na Kaimu Balozi wa Marekani Bi. Inmi Petterson kwa pamoja wakimsikiliza kwa makini Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani)
Balozi wa Italy Mhe. Roberto Mengoni (wa kwanza kushoto) na Katibu wa Waziri Bw. Charles Mbando wakimsikiliza kwa makini Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani)
Switzerland Mhe. Florence  Tinguely Mattli naye alitoa neno la shukrani kwa ushirikiano alioupata wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake akiwa hapa nchini. ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na kuitangaza vyema Tanzania 
Balozi wa Denmark Mhe. Einar Hebogard Jensen naye alishukuru kwa ushirikiano alioupata wakati wote katika kutekeleza majukumu yake akiwa hapa nchini. Hata hivyo hakusita kumpongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kupambana na Rushwa pamoja na kujenga miundombinu mizuri hapa nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati), kiongozi wa Mabalozi nchini Tanzania Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoul Mohamed (wakwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Jestas Nyamanga wakiwasikiliza Balozi wa Sweden na Denmark (hawapo pichani) walipokuwa wakizungumza.
Kiongozi wa Mabalozi nchini Tanzania Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoul Mohamed naye akizungumza neno wakati wa hafla ya kuwaaga Mabalozi wa Switzerland na Denmark (hawapo pichani)  







Dkt. Ndumbaro azungumza na Mkuu wa Timu ya kujitegemea ya Umoja wa Mataifa Bw. Youssef Mahmoud.


Prof. Kabudi apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa India, Mhe. Sanjiv Kohli. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Balozi mteule Sanjiv Kohli mara baada ya kupokea nakala zake
Mazungumzo yakiendelea
Prof. Palamagamba John Kabudi akiagana na Balozi Mteule Mhe. Sanjiv Kohli mara baada ya kumalizaka kwa hafla hiyo




Ubalozi wa Tanzania nchini India wafanikisha hafla ya uzinduzi wa safari za Air Tanzania mjini Mumbai

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwele akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa safari za  Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania) katika mji wa Mumbai nchini India. Uzinduzi huo ulifanyika katika Hoteli ya Bandra Kurla mjini Mumbai tarehe 18 Julai 2019
Waziri wa Elimu, Michezo na Ustawi wa Vijana wa India ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi rasmi wa safari za a Shirika la Ndege la Tanzania mjini Mumbai nae akizungumza kwenye hafla hiyo
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa safari za ndege za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai nchini India
Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Ndege ya Tanzania, Mhandisi Emmanuel Korosso nae akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa safari za Air Tanzania mjini Mumbai, India
Wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akiwa tayari kukata utepe kuashiria kuanza rasmi kwa safari za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai, India
Mhe. Kamwele akiwa na Viongozi wengine kutoka Tanzania na India wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa safari za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akikata keki maalum kuashiria kuanza rasmi kwa safari za Ndege za Air Tanzania mjini Mumbai, India
Matukio mbalmbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na India wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za Air Tanzania mjini Mumbai
Mhe. Waziri Kamwelwe akipokea Jarida la Travel ambalo ambalo huandika taarifa kuhusu masuala ya usafirishaji na uchukuzi kwa ujumla
Mhe. Waziri Kamwelwe (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (wa tatu kushoto), viongozi mbalimbali kutoka Tanzania na India pamoja na Marubani waliofamikisha ndege ya kwanza ya Air Tanzania kutua Mumbai kwa ajili ya safari za kibiashara 
Mhe. Balozi Luvanda katika picha ya pamoja na wadau walioshiriki uzinduzi wa safari za ndege ya Air Tanzania mjini Mumbai. Kushoto ni Bw. Kheri Goloka, Afisa wa Ubalozi Mwandamizi.

Wafanyabiasha kutoka China ziarani nchini kutafuta fursa za biashara



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wafanyabiashara kutoka Jimbo la Zhejiang, China kuja nchini kutafuta fursa za biashara

Ujumbe wa wafanyabiashara 25 kutoka Kampuni kubwa 15 za Jimbo la Zhejiang nchini China ukiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Bunge la Jimbo hilo, Mhe. Bi. GE Huijun utafanya ziara nchini kuanzia tarehe 20 hadi 23 Julai 2019 kwa lengo la kukutana na kufanya mazungumzo na wadau mbalimbali kuhusu fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini.

Ziara hiyo inalenga kukuza mahusiano ya kiuchumi baina ya Jimbo la Zhejiang na Tanzania katika sekta mbalimbali za maendeleo kama vile teknolojia, mawasiliano, ujenzi na uchukuzi, afya na madini.

Mhe. GE Huijun pia atafuatana na viongozi 13 wa Serikali ya Zhejiang kwenye ziara hiyo ambayo itaanzia Zanzibar tarehe 20 Julai 2019.

Ujumbe huo ukiwa nchini, pamoja na masuala mengine, unategemea kukutana na Viongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar kwa ajili ya kujadiliana nao kuhusu fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zilizopo nchini.

Ukiwa Zanzibar, ujumbe huo utatembelea maeneo ya viwanda ya Amani na Fumba kwa ajili ya kujionea fursa za uwekezaji. Aidha, ujumbe huo utakutana na Mamlaka ya Uwekezaji na Uendelezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) pamoja na kukutana na wafanyabiashara wa Zanzibar kwa madhumuni ya kuanzisha ushirikiano.

Kadhalika ujumbe huo utashiriki ufunguzi wa Kongamano la Biashara kati ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Wafanyabiashara kutoka Zhejiang utakaofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 22 Julai 2019.

Ujumbe huo unategemea kukamilisha ziara yao nchini tarehe 23 Julai, 2019.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
19 Julai 2019


Thursday, July 18, 2019

VACANCY ANNOUNCEMENT


PRESS RELEASE

VACANCY ANNOUNCEMENT FROM THE INTERNATIONAL TELECOMMUNICATION UNION (ITU)

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received Vacancy Notice No. 21D-2019/BDT-DDR/External/D2 from the International Telecommunication Union (ITU) inviting qualified Tanzanians to apply for the post of  Deputy to the Director and Chief of the Administration and Operations Coordination Department (DDR).

Application details can be found through the ITU website: http://www.itu.int/employment/Recruitment/index.html.

Closing date for application is Sunday 25th August 2019.


Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
18th July 2019.


Wednesday, July 17, 2019

Prof. Kabudi akutana na Mabalozi wa Nchi za SADC


Prof. Kabudi azungumza na Mabalozi wastaafu wa Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani kwa nia ya kupata ushauri na maoni yao kuhusu maandalizi ya Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo Prof. Palamagamba John Kabudi ameongozana na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), Katibu Mkuu Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (wa kwanza kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (wa kwanza kulia).  
Juu na Chini ni sehemu ya Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakimsikiliza Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani). 


Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani) 
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), Naibu Waziri Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), Katibu Mkuu Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Mwinyi wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani