Tuesday, August 27, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI ASHIRIKI MKUTANO WA MAWAZIRI WA TICAD JIJINI YOKOHAMA, JAPAN


Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe.Kono Taro (mwenye tai ya rangi ya chungwa) akifungua rasmi Mkutano wa Mawaziri wa maandalizi ya Mkutano wa Saba wa Kimataifa kuhusu Mandeleo ya Afrika (TICAD 7) . Ufunguzi huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Pacifico jijini Yokohama, Japan  tarehe 27 Agosti 2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (wa tatu kushoto kwenye meza nyeupe) akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa TICAD wa Mawaziri uliofanyika Yokohama, Japan tarehe 27 Agosti 2019

Mkutano ukiendelea

===========================================================


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAANDALIZI YA MKUTANO WA SABA WA TOKYO KUHUSU MAENDELEO YA AFRIKA (TICAD 7) WAFANYIKA JIJINI YOKOHAMA, JAPAN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi leo tarehe 27 Agosti 2019 ameshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Maandalizi ya Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD 7) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Pacifico jijini Yokohama, Japan.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine unatarajiwa kupitia na kupitisha rasimu ya Azimio la Yokohama na Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Azimio hilo litakalowasilishwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaoanza tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019 kwa ajili ya kuridhiwa.

Akifungungua mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Kono Taro amezipongeza nchi za Afrika kwa kupiga hatua katika maendeleo kupitia ushirikiano na Japan na kwamba nchi yake itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na nchi hizo ili kuziwezesha kufikia malengo ikiwemo mapinduzi ya viwanda.

Mhe. Taro alisema kuwa, ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia mpango wa TICAD umeendelea kuimarika tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 1993 na kwamba ni matarajio yake Mkutano wa Saba utakuwa wa tija zaidi kwa pande hizo mbili.

“Nawakaribisha Mawaziri wenzangu Yokohama ambapo maandalizi ya mkutano wa saba wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika yanaendelea. Jukumu letu ni kupitia na kupitisha rasimu ya Azimio la Yokohama na Mpango kazi wake ili hatimaye litunufaishe sote pale litakapopitishwa na Wakuu wa nchi” alisema Mhe. Taro.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano huo, Mhe. Sameh Shoukry ameipongeza Japan kwa kuendelea kuandaa mikutano hiyo ambayo ina nia ya kuifikisha Afrika katika mapinduzi ya viwanda na kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana na umaskini.

Kwa upande wake, Naibu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ambao ni miongoni mwa waandaaji wa Mkutano wa Saba wa TICAD, Bw. Kwesi Quartey amesema kuwa, mkutano huo unafanyika wakati Umoja wa Afrika unaendelea kutekeleza agenda 2063. Agenda hiyo pamoja na mambo mengine inalenga kuziwezesha nchi za Afrika kufikia maendeleo ya hali ya juu kwenye sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu, teknolojia na miundombinu.

Kadhalika Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Kanda ya Afrika kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Afrika, Bw. Lamin Manneh alisema kuwa ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia TICAD umekuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo ya Bara la Afrika. Aliongeza kuwsema kuwa, Shirika lake ambalo linasimamia maendeleo linaridhishwa na ushirikiano uliopo kati ya Japan na Afrika ambao kwa kiasi kikubwa umefanikiwa.

Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Ushirikiano na Afrika pamoja na mambo mengine unatoa fursa ya kupanga mikakati ya ushirikiano na agenda za kimaendeleo zitakazotelezwa kati ya Japan na Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Agenda za mkutano wa mwaka huu zinalenga kujadili mageuzi ya kiuchumi na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kukuza sekta na uvumbuzi. Pia kuimarisha usalama na ustahimilivu endelevu kwenye jamii pamoja na kuendeleza jitihada za kuimarisha amani na usalama barani Afrika. Agenda za Mkutano wa Saba zinaenda sambamba na agenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine ya kimataifa kama Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Mkutano huu ambao umewashirikisha Mawaziri kutoka nchi za Afrika, na wadau mbalimbali wa maendeleo unafanyika ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Yokohama, Japan.
27 Agosti 2019


Monday, August 26, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI (MB) ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA ULIOPO TOKYO NCHINI JAPAN.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwasili katika Ubalozi wa Tanzania uliopo Tokyo,Japan. Katikati ni Kaimu Balozi wa Tanzania Nchini Japan Bw. John Kambona akifuatiwa na Bi. Edda Magembe Afisa Ubalozi. August 26,2019. 

Kaimu Balozi wa Tanzania Nchini Japan Bw. John Kambona (katikati) akitoa ufafanuzi wa jambo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) mara baada ya kuwasili katika Ubalozi wa Tanzania uliopo Tokyo,Japna anayefuatia ni  Bi. Edda Magembe Afisa Ubalozi. August 26,2019.  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akitoa maelekezo kwa Kaimu Balozi wa Tanzania Tokyo,Japan Bw. John Kambona akiwa na Afisa Ubalozi Bi. Edda Magembe. August 26,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa anaingia katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania uliopo Tokyo,Japan. August 26,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika moja ya Maktaba ya vitabu iliyopo katika Ubalozi wa Tanzania - Tokyo,Japan. August 26,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akikagua aina  ya vitabu vilivyopo katika Maktaba ya Ubalozi wa Tanzania Nchini Japan. August,26,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika ofisi ya Balozi wa Tanzania Nchini Japan. August 26,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongoza kikao kazi cha ujumbe wa Tanzania uliopo Yakohama Nchini Japan kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika 2019 (TICAD7 YOKOHAMA 2019). August 26,2019.

Kaimu Balozi wa Tokyo - Japan Bw. John Kambona akiwa anatoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na baadhi ya ujumbe uliopo Yakohama, Japan kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika 2019 (TICAD7 YOKOHAMA 2019). August 26,2019.

Baadhi ya wajumbe waliopo Yakohama-Japan kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika 2019 (TICAD7 YOKOHAMA 2019) wakiwa katika kikao kazi cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi(hayupo Pichani). August 26,2019.

================================================================


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKUTANO WA SABA WA TOKYO KUHUSU MAENDELEO YA AFRIKA (TICAD 7)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi amewasili jijini Yokohama, Japan tarehe 26 Agosti kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 7 wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD 7) utakaofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.

Mkutano huu wa Saba utatanguliwa na kikao cha Maafisa Waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu na Mabalozi tarehe 25 na 26 Agosti 2019 ukifuatiwa na kikao cha Mawaziri tarehe 27 Agosti, 2019 na utahitimiswa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019. Kauli mbiu ya Mkutano huu ni “Kuendeleza Maendeleo ya Afrika kupitia Watu, Teknolojia na Uvumbuzi”.

Mkutano wa Saba pamoja na mambo mengine unatoa fursa ya kupanga mikakati ya ushirikiano na agenda za kimaendeleo zitakazotelezwa kati ya Japan na Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Agenda za mkutano wa mwaka huu zinalenga kujadili mageuzi ya kiuchumi na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kukuza sekta na uvumbuzi. Pia kuimarisha usalama na ustahimilivu endelevu kwenye jamii pamoja na kuendeleza jitihada za kuimarisha amani na usalama barani Afrika. Agenda za Mkutano wa Saba zinaenda sambamba na agenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine ya kimataifa kama Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Kutokana na mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya kiuchumi barani Afrika, Mkutano wa TICAD 7 umeandaa ratiba maalum itakayozishirikisha taasisi binafsi na za umma kwenye majadiliano ya kibiashara yatakayofanyika tarehe 29 Agosti 2019. Lengo la majadiliano hayo ni kuwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa Serikali wamiliki wa Kampuni, wafanyabiashara na wawekezaji ili kujadili kwa pamoja masuala mbalimbali ya kukuza baishara, uwekezaji na utalii kati ya Japan na Afrika.

Kadhalika  wakati wa mkutano wa saba nchi zote za Afrika zimepatiwa nafasi ya kushiriki katika shughuli mbalimbali kwa lengo la kutangaza fursa za biashara, uwekezaji na vivutio vya utalii za nchi husika. Tanzania kupitia Bodi ya Utalii (TTB) imejipanga kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini wakati wa mkutano huo.

Mkutano wa Saba wa TICAD utahitimishwa kwa Wakuu wa Nchi kupitisha Azimio la Yokohama na Mpango Kazi wa utekelezaji wa Azimio hilo. Serikali ya Japan ilianzisha jukwaa la majadiliano kati yake na nchi za Afrika mwaka 1993 kwa ajili ya kujadili maendeleo na nchi hizo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ataongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Yokohama, Japan.
26 Agosti 2019

Friday, August 23, 2019

Naibu Waziri Mhe.Dkt Damas Ndumbaro afanya mazungumzo na Mabalozi


Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mhe.Yonas Yosef Sanbe Balozi wa Ethiopia nchini Tanzania yaliyofanyika katika ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam Agosti 23, 2019

Baloz Sanbe katika mazungumzo hayo ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuna kuganishwa Mkunao wa SADC HAPA
Mhe. Dkt Ndumbaro Naibu Waziri akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Sanbe walipokutana kwa mazungumzo.
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akimsikiliza Mhe. Mousa Farhang Balozi wa Iran nchini, walipokutana kwa mazungumzo ofisi ndogo za Wizara jiji Dar es Salaam.

 Katika mazungumzo yao, waliwili hao walijikita kujadili masuala mbalimbali ya kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili. 
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akisalimiana na  Mhe. Mousa Farhang Balozi wa Iran nchini Tanzania
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akimsikiliza Mhe. Abdelilah Benryane Balozi wa Morocco nchini Tanzania
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati akifanya mazungumzo  na Balozi wa Morocco Mhe. Abdelilah Benryane
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akisalimia na Mhe. Abdelilah BenryaneBalozi wa Morocco

Wakati huohuo Mhe. Pro. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Tanzania  Mhe. Wang Ke
Sehemu ya Wafanyakazi wa Ubalozi wa China wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea

Mhe. Pro. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki akiwa katika mzungumzo na Balozi wa China nchini Tanzania  Mhe. Wang Ke yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Agosti 23, 2019

Thursday, August 22, 2019

WAZIRI KABUDI AMUAGA MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA NCHINI

Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akizungumza katika hafla fupi ya kumuaga Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alvaro Rodriguez iliyofanyika hoteli ya Hyatt jijini Dar es Salaam.

Waziri Kabudi katika hotuba yake amempongeza Bwana Rodriguez kwa utumishi wake uliotukuka katika kipindi chote akiwa nchini. Aidha, amemshukuru kwa kushirikiana na Serikali na kujitoa kwa dhati katika kuchangia juhudi kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa Serikali nchini.

Bwana Rodriguez amemaliza muda wake wa kuhudumu nchini Tanzania ambapo amefanya kazi kwa kipindi cha miaka mitano.
Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Kulia) na Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto) Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, anayemaliza muda wake wa kuhudumu nchi wakifurahia jambo wakati wa hafla fupi ya kumuaga
Bw. Deusdedit Kaganda Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akizungumza kwenye hafla fupi ya kumuaga Bw. Rodriguez Maratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini ambaye amemaliza muda wake wa kuhudumu nchini 
Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) na Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto) Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini wakishirikishana jambo  wakati wa hafla hiyo
Bi.Ramla Khamis Afisa Mambo ya Nje Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza katika hafla ya kumuaga Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini
Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) akikabidhi zawadi kwa Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto) Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini ambaye amemaliza muda wake wa kuhudumu
Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Bw. Alvaro Rodriguez Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini ambaye amemaliza muda wa kuhudumu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi kutoka wizarani na Ofisi ya Umoja wa Mataifa.

Wednesday, August 21, 2019

WAZIRI KABUDI AFANYA MKUTANO NA WANAHABARI


Mhe. Prof. Paramagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Waziri Kabudi katika Mkutano wake na wanahabari amewashukuru nakuwapongeza waandishi wa habari na vyombo vya habari, kwa ushirikiano mkubwa 
na uzalendo waliouonyesha katika kuutangaza Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo  Kusini mwa Afrika (SADC).

Waziri Kabudi alitumia fursa hiyo kutoa rai kwa waandishi wa habari kuendelea kufuatilia na kuuhabarisha umma masuala mbalimbali yanayojiri kweny ya Jumuiya SADC.

Tanzania itaendelea kuwa mwenyeji wa Mikutano mbalimbali ya kisekta ya SADC katika kipindi cha hiki cha mwaka mmoja cha Uenyekiti wake.
Bw. Emmanuel Buhohela Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  akizungumza wakati wa Mkutano na Wanahabari uliofanyika katika Ukumbi wa  Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2019.


Bibi Agnes Kayola Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda akizungumza wakati wa Mkutano na waandishi wa habari

Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mkutano

Meza kuu ikifuatilia Mkutano uliokuwa ukiendelea.


Wakati huohuo Waziri Kabudi amepokea ujumbe wa wawaendesha baiskeli unaojumuisha washiriki kutoka nchi wanachama wa Jamuiya ya Afrika Mashariki. Ziara hii ya waendesha baiskeli imeandaliwa na asasi ya kiraia "Camp fire" ya nchini Uganda. Ziara yao inahusisha kuzunguka nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa lengo la kukuza umoja na ushirikiano wa kikanda.

 Akizungumza kiongozi wa waendesha baiskeli hao bwana John Balongo ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapa ushirikiano na mapokezi mazuri katika kipindi chote walichokuwa nchini. 
Msafara wa waendesha Baiskeli wakiwasili katika viunga vya Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2019 

Waziri Kabudi akisalimiana na ujumbe wa waendesha baiskeli kutoka nchi wanachama za Afrika Mashariki walipowasili katika viunga vya Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere
Waziri Kabudi akimkabidhi bendera ya Taifa mwakilishi wa Tanzania katika ziara ya baiskeli ya Afrika Mashariki, mara baada ya kuwapokea katika viunga vya Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Waziri Kabudi akizungumza wakati wa mapokezi ya msafara wa ujumbe wa waendesha baiskeli wa Afrika Mashariki
Bw. Eliabi Chodota, Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Kijamii (mwenye tai nyekundu) Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akizungumza wakati wa mapokezi ya msafara wa waendesha baiskeli kutoka nchi wanachama wa Afrika Mashariki 
Bw. John Barongo, Kiongozi wa msafara wa waendesha baiskeli wa Afrika Mashariki akizungumza baada ya mapokezi
Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nchi za Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa waendesha baiskeli 

Tuesday, August 20, 2019

WAZIRI KABUDI AFUNGUA KIKAO KAZI MAALUMU CHA MABALOZI WA TANZANIA



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Waziri Kabudi afungua rasmi kikao kazi maalum cha Mabalozi 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi amewataka Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje kuongeza jitihada katika kuhamasisha wawekezaji, wafanyabiashara na watalii kuja nchini ikiwa ni utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi. 
Waziri Kabudi ameyasema hayo tarehe 20 Agosti 2019 wakati akifungua rasmi  kikao kazi maalum cha Mabalozi kinachofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere  jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 20 hadi  23 Agosti 2019.
Mhe. Waziri Kabudi alisema kuwa, Mabalozi ambao wana jukumu kubwa la kusimamia maslahi ya Tanzania kwenye nchi mbalimbali duniani, wameendelea kufanya kazi nzuri katika  kuhakikisha dhana ya diplomasia ya uchumi inafikiwa na kwamba matokeo ya jitihada hizo ni pamoja na kuongezeka kwa watalii, wawekezaji na wafanyabiashara nchini. Pia kumekuwa na ongezeko la fursa za ufadhili wa masomo na ajira kwa Watanzania kwenye nchi mbalimbali.
“Hii ni mara yangu ya kwanza kukutana nanyi Waheshimiwa Mabalozi tangu niteuliwe na Mhe. Rais kwenye wadhifa huu. Nazipongeza jitihada zenu katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi kwani matokeo tunayaona kwa biashara kuongezeka hapa nchini watalii na hata wawekezaji. Hivyo nataka mwongeze jitihada zaidi ili nchi yetu ifikie azma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025” alisema Mhe. Kabudi”.
Aidha, Mhe. Waziri Kabudi alitoa rai kwa Mabalozi kuendelea kuwahamasisha Watanzania waishio nje (Diaspora) kujiandikisha na kuanzisha jumuiya zao ili kwa namna moja au nyingine na wao washiriki kuchangia maendeleo hapa nchini.
Akizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili Mabalozi hao ikiwa ni pamoja na uchakavu wa baadhi ya majengo ya balozi, Mhe. Kabudi alieleza kuwa Wizara inaendelea kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto hizo.
Akizungumza kwa niaba ya Mabalozi, Kiongozi wa Mabalozi hao, Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia alipongeza jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuanzisha na kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo Mabalozi walipata fursa ya kuitembelea. Alisema kuwa, miradi hiyo ni chachu ya maendeleo katika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. 
"Tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati. Tumepata fursa ya kuiona miradi hiyo ikiwemo ile ya ujenzi wa barabara, reli na umeme. Kimsingi miradi hii inalenga kumwondolea umaskini Mtanzania kwa vile pamoja na mambo mengine itarahisha usafirishaji na kumwezesha mkulima kusafirisha kwa urahisi mazao yake kutoka sehemu moja kwenda nyingine kupitia miundombinu hiyo", alisema Balozi Aziz.
Pia aliipongeza Serikali kupitia Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kuandaa na kufanikisha Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kufanyika nchini kwa mafaniko makubwa.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
20 Agosti 2019

Mhe. Prof. Paramagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi cha Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam Agosti 20,2019

Lengo la kikao hicho ni kujadili masula mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa diplomasia ya uchumi. 
Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizumgumza kwenye kikao na Mabalozi wa wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani. 

Mabalozi na Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya ufunguzi iliyo kuwa ikitolewa na  Waziri Mhe. Prof Kabudi (Hayupo pichani).
Sehemu ya Watendaji wa Wizara wakifuatilia kikao
Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Wakuu wa Wizara mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi cha Mabalozi
Viongozi Wakuu wa Wizara wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi Wanawake
Viongozi Wakuu wa Wizara  wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mara baada ya ufunguzi wa Kikao kazi maalum.
Mhe. Naimi Aziz Balozi wa Tanzania Addis Ababa, Ethiopia akitoa hutuba kwenye ufunguzi wa Kikoa kazi cha Mabalozi kinachoendelea katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam