Monday, August 12, 2019

BALOZI MTEULE WA DENMARK AKABIDHI NAKALA ZA HATI YA UTAMBULISHO KWA PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet alipofika katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukabidhi nakala za hati za utambulisho.August 12,2019

Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi nakala za hati za utambulisho. Tukio hilo limefanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.August 12,2019

Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet akiwatambulisha kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi baadhi ya maafisa aliongozana nao,wakati alipofika katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukabidhi nakala za hati za utambulisho. August 12,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet. Walioko pembeni ni baadhi ya wakurugenzi na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania. August 12,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Bw Jestas Nyamanga na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania. August 12,2019.

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Bw. Jestas Nyamanga wakipunga mkono kuagana na Balozi Mteule wa Denmark hapa Nchini,Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet. August 12,2019.






PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI AKAGUA PIKIPIKI MPYA KWA AJILI YA SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa anashuhudia namna mojawapo ya pikipiki mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya mapokezi na kuongoza misafara ya viongozi,Wakuu wa Nchi na Serikali watakaohudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea Jijini Dar es Salaam,Tanzania ikiunganishwa. Anayeshuhudia ni Afisa Usafirishaji – IKULU Bw. Zuberi Kachingwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa anafurahia mojawapo ya pikipiki mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya mapokezi na kuongoza misafara ya viongozi,Wakuu wa Nchi na Serikali watakaohudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea Jijini Dar es Salaam,Tanzania. Anayeshuhudia ni Afisa Usafirishaji – IKULU Bw. Zuberi Kachingwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa anajaribu moja ya pikipiki mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya mapokezi na kuongoza misafara ya viongozi,Wakuu wa Nchi na Serikali watakaohudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea Jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni Afisa Usafirishaji – IKULU Bw. Zuberi Kachingwa.

Baadhi ya pikipiki mpya zitakazotumika katika mapokezi na kuongoza misafara ya viongozi,Wakuu wa Nchi na Serikali watakaohudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea Jijini Dar es Salaam zikiwa tayari kwa mapokezi.

Thursday, August 8, 2019

TANZANIA IKO TAYARI KUWAPOKEA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI KWA AJILI YA MKUTANO WA 39 WA SADC

Bw. Zuberi Kachingwe Afisa Usafirisahaji, IKULU,(katikati) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akikagua magari yatakayotumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. Kulia ni Afisa Usafirishaji Msaidizi Bw. Athumani Natepe. August 8, 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akipewa maelezo na Bw. Zuberi Kachingwe Afisa Usafirisahaji, IKULU,wakati Prof Palamagamba John Kabudi akikagua magari yatakayotumiwa na viongozi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi ya wakuu wa Serikali na Nchi watakaohudhuria mkutano huo Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Zuberi Kachingwe Afisa Usafirisahaji, IKULU pamoja na Bw. Athumani Natepe Afisa Usafirishaji Msaidizi mara baada ya kumaliza kukagua magari yatakayotumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa amesimama mbele ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa ndani ya mojawapo ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

Baadhi ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi,wakuu wa Nchi na Serikali wakati wa mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utafanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

Baadhi ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi,wakuu wa Nchi na Serikali wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utafanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

CHINA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA OFISINI KWA AJILI YA SADC

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Wang Ke nyaraka za makabidhiano ya Masada wa vifaa vya ofisini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili kumi na saba vitakavyotumika wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC),August 08,2019

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Wang Ke nyaraka za makabidhiano ya Msaada wa vifaa vya ofisini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili kumi na saba vitakavyotumika wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Wanaoshuhudia ni maafisa kutoka Ubalozi wa China na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. August 08,2019. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akikabidiana nyaraka za Msaada wa vifaa vya ofisini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili kumi na saba vitakavyotumika wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Wanaoshuhudia ni maafisa kutoka Ubalozi wa China na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. August 08,2019. na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Mhe. Wang Ke 



Saturday, August 3, 2019

WATUMISHI WA UMMA NA MAAFISA ITIFAKI WAPATA MAFUNZO KUHUSU UTOAJI WA HUDUMA SADC

Wakufunzi wa mafunzo kwa watumishi wa umma na Maafisa Itifaki watakaotoa huduma kwa wageni watakaoshiriki Mkutano wa 39 wa SADC wakimsikiliza mtoa mada (hayupo pichani) wakati wa mafunzo hayo. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mkutano wa kimataifa wa Julius Nyerere,Dar es Salaam. 03 August,2019.

Baadhi ya watumishi wa umma na Maafisa Itifaki waliohudhuria mafunzo maalum ya namna yakuwahudumia wageni wa mkutano wa SADC wa 39 yaliyoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere,Dar es Salaam. 03 August 2019.

Baadhi ya watumishi wa umma na Maafisa Itifaki waliohudhuria mafunzo maalum kuhusu namna yakuwahudumia wageni wa mkutano wa SADC wa 39 wakifuatilia mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere,Dar es Salaam. 03 August 2019.

Add caption

Friday, August 2, 2019

RAIS,DKT MAGUFULI ATIMIZA AHADI YAKE KWA RAIS WA KENYA,MHE.UHURU KENYATTA

Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. Pindi Chana akimkabidhi Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta nyaraka ya zawadi maalum ya ndege aina ya Tausi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. August 02,2019

Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta akizungumza mara baada ya kupokea ndege aina ya Tausi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.Aliyesimama pembeni mwa Rais Kenyatta ni Balozi wa Tanzania Nchini Kenya, Dkt Pindi Chana. August 02,2019

Rais wa Kenya,Mhe. Uhuru Kenyatta akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya,Balozi Pindi Chana mbele ya Zawadi ya ndege aina ya Tausi mara baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo. August 02,2019

Ndege aina ya Tausi ambao wamekabidhiwa kwa Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta ikiwa ni zawadi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Tausi hao wamekabidhiwa kwa Rais Kenyatta na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. Pindi Chana. August 02,2019

Watoa Huduma Mkutano wa SADC wapigwa msasa

Naibu Kamishna na Mkuu wa Mafunzo ya Jeshi la Polisi Tanzania Ali Lugendo akihutubia kwenye ufunguzi wa mafunzo ya wanafunzi watakao hudumia kwenye Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajiwa kufanyika nchini mwezi Agosti. Katika Hotuba yake Kamishna Lugendo amewataka wanafunzi hao kuzingatia mafunzo watakayopewa ili kutoa huduma bora na nzuri kwa wageni watakaohudhuria mkutano huo. Ufunguzi huo umehudhuriwa na Mratibu Mkuu wa Itifaki Bw. Batholomeo Jungu (wa pili kutoka kushoto) na Umefanyika katika chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es Salaam
Juu na Chini ni sehemu ya Wanafunzi hao wakimsikiliza kwa makini Kamishna Lugendo (hayupo pichani)

Sehemu ya wakufunzi wakimsikiliza kwa makini Kamishna Lugendo


Wanafunzi wanaotarajiwa kupewa mafunzo ya namna ya kuhudumia kwenye Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajiwa kufanyika nchini mwezi Agosti wakifanya mazoezi 
Kamishna Ali Lugendo akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa chuo hicho, Mratibu Mkuu wa Itifaki, Bw. Batholomeo Jungu (wanne kutoka kushoto) pamoja na wanafuzi mara bade ya ufunguzi wa Mafunzo ya kutoa huduma bora na nzuri, kwa Wageni watakao hudhuria Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajiwa kufanyika nchini mwezi Agosti





TANZANIA NA ZIMBABWE ZASAINI HATI 5 ZA MAKUBALIANO YA PAMOJA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) na Waziri wa mambo ya Nje wa Zimbabwe Luten Jenerali Mstaafu Sibusiso Moyo wakisaini hati za makubaliano ya pamoja (MoU) katika Nyanja mbalimbali. Tukio hilo limefanyika Harare,Zimbabwe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) na Waziri wa mambo ya wanawake,Jinsia na Maendeleo ya Jamii Mhe. Sithembiso Gile Nyoni wakisaini hati za makubaliano ya pamoja (MoU) katika Nyanja ya jinsia na kuwawezesha wanawake  Tukio hilo limefanyika Harare,Zimbabwe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) na Waziri wa mambo ya Nje wa Zimbabwe Luten Jenerali Mstaafu Sibusiso Moyo wakisaini hati za makubaliano ya pamoja (MoU) wakionesha kwa furaha hati za makubaliano ya pamoja (MoU) kati ya Tanzania na Zimbabwe mara bade ya kusaini hati hizo. Tokio hilo limefanyika Harare,Zimbabwe.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Zimbabwe (JPCC). Mkutano huo umefanyika Harare,Zimbabwe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) na Waziri wa mambo ya Nje wa Zimbabwe Luten Jenerali Mstaafu Sibusiso Moyo,wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe judoka Tanzania na Zimbabwe mara bade ya kumalizika Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Zimbabwe. Mkutano huoumefanyika Harare,Zimbabwe





Thursday, August 1, 2019

WFP wasafirisha shehena ya mzigo kwa kutumia MV. Umoja

Meli ya mizigo ya MV Umoja iliyobeba mabehewa ya treni yenye shehena ya mzigo wa Shirika la Programu ya Chakula Duniani (World Food Program-WFP) kutoka Mwanza kwenda Uganda iliwasili bandari ya Portbell, Uganda tarehe 31 Julai 2019.

Katika Halfa ya mapokezi ya meli hiyo, Serikali ya Uganda iliwakilishwa na Waziri wa Nchi-Uchukuzi, Mhe. General Katumba Wamala na kwa Upande wa Tanzania, Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Dkt. Aziz Mlima alimwakilisha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe.

Njia hii ya usafiri wa reli kutoka Dar Es Salaam hadi Port Bell (Kampala) Uganda, inapunguza gharama kwa asilimia zaidi ya 50 na pia inachukuwa siku 5 tu kwa mzigo kusafiri kutoka bandari ya Dar Es Salaam hadi Kampala.

Kwa mwaka jana WFP walisafirisha tani 40,000 na kwa kutumia njia hii wameokoa zaidi ya Dola za Marekani milioni 2.

Ujumbe uliosafiri na meli ya MV Umoja iliyobeba mabehewa hayo yenye mizigo ya WFP ulijumuisha Mkurugenzi Mtendaji wa TRC, Bw. Masanja Kadogosa; Mkurugenzi wa Uchukuzi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Johnson Kisaka ambao waliambatana na Mkurugenzi wa WFP-Tanzania, Bw. Michael 


Meli ya MV. Umoja iliyobeba shehena ya mzigo, mali ya WFP kutoka Dar Es Salaam ikiwasili katika Bandari ya Port Bell jijini Kampala tarehe 31 Julai 2019.

Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz Mlima akitoa neno wakati wa hafla ya mapokezi ya meli ya Mv. Umoja jijini Kampala, Uganda.


Balozi Mlima akiongea na wanahabari kuhusu zoezi hilo.