Saturday, October 5, 2019

RAIS MAGUFULI AZINDUA KITUO CHA HUDUMA PAMOJA (OSBP) MPAKANI TUNDUMA/NAKONDE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.

Kituo hicho kimefunguliwa leo tarehe 5 Oktoba 2019, na 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu.

Wakizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika zoezi la uzinduzi wa kituo hicho, kwa nyakati tofauti Mhe. Dkt. Magufuli na Mhe. Lungu walieleza kuwa wataendelea kudumisha uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliodumu kwa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili (Tanzania na Zambia) kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha, Rais Magufuli alizungumzia umuhimu wa kuiongezea ufanisi Reli ya TAZARA ili kuchagiza kasi ya biashara baina ya Tanzania na Zambia.

Kadhalika, Mhe. Rais Magufuli amewahimiza Wananchi wa mji wa Tunduma kuulinda mpaka kwa kuepuka kujenga katika eneo la mpaka huo.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amewapongeza Wananchi wa Mji wa Tunduma kwa kuendelea kulinda na kudumisha amani mpakani hapo. Vilevile ametumia fursa hiyo kuwasihi kuendelea na juhudi za kukuza biashara baina yao na Zambia ili kuboresha maisha yao.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde kwa ajili ya ufunguzi.
Taswira ya Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.
Taswira ya Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli  akifuatilia maelezo kutoka  kwa Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) kabla ya kuanza kwa zoezi la ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde. 
Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  akizungumza na wananchi (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu ,wakiangalia jiwe la msingi wakati wa zoezi la ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde tarehe 5 Oktoba, 2019 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu, pamoja na Wafadhili wa Ujenzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde wakipanda mti katika zoezi la uzinduzi wa Kituo hicho 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu wakikata utepe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde tarehe 05 Oktoba, 2019.

Thursday, October 3, 2019

MAANDALIZI KUELEKEA UFUNGUZI WA KITUO CHA PAMOJA (OSBP) MPAKANI TUNDUMA/NAKONDE


UBALOZI WA TANZANIA, UHOLANZI WASHIRIKI KWA MAFANIKIO TAMASHA LA EMBASSY FESTIVAL

Balozi wa Tanzania, The Hague, Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju akitoa maelezo kwa mgeni aliyetembelea Banda la Tanzania wakati wa Tamasha maarufu kama Embassy Festival lililofanyika hivi karibuni. Tamasha hilo huandaliwa na Manispaa ya The Hague kwa kushirikiana na Balozi za nchi mbalimbali zenye Ofisi zake The Hague kwa lengo la kutangaza tamaduni za nchi hizo.
Balozi Irene Kasyanju (mwenye fulana kulia) pamoja na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Bibi Naomi Zegezege Mpemba (wa pili kushoto) wakitoa maelezo kuhusu Tanzania kwa wageni
waliotembelea Banda la Tanzania, huku Bw. Denis Baraka (wa kwanza kushoto)  ambaye ni Mtanzania na mdau wa shughuli za utalii ambaye kwa sasa anasoma nchini Ujerumani na ambaye kutokana na kupenda kutangaza utalii wa Nchi yake alisafiri kutoka Kiel, Ujerumani kuja Uholanzi kuungana na Ubalozi pamoja na Watanzania wengine kwenye Embassy Festival.
Mwonekano wa Banda la Tanzania na wageni waliotembelea.
Balozi Irene Kasyanju (wa tatu kushoto) akiwa na walishiriki wa maonesho ya mavazi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wakiwa wamevaa fulana za kuitangaza Tanzania ambao ni Bw. Issa Lupatu, Mwambata Fedha wa Ubalozi (wa pili kulia aliyevaa miwani) na Bw. John Appolo Kilasara,Katibu wa Chama cha Watanzania wanaoishi Uholanzi (Tanzanians in the Netherlands – TANE) ambaye pia ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha ISS nchini Uholanzi
Balozi Irene Kasyanju akiwa na Bi. Bahia Kihondo, Mtanzania aliyeandaa maonesho ya mavazi
pamoja na watoto ambao walifungua maonyesho hayo kwa kusoma shairi fupi kwa lugha ya Kidachi na Kiswahili. 
Watazamaji wa maonesho ya mavazi yaliyotangaza utamaduni wa Mtanzania walikusanyika kwa
wingi kutazama maonesho hayo

Mwonekano wa Banda la Tanzania kwa sehemu ya ndani, likiwa limefurika Diaspora waliofika
kulitembelea na kupata fursa ya kuzungumza na mmoja wa wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Uholanzi, Bi Linda Mkony (aliyevaa koti katikati) na Bw. Denis Baraka, wakiwa pia wamevaa
na fulana maalum za kuitangaza Tanzania
Washiriki wakionesha vazi lenye michoro ya wanyama “animal prints” wanaopatikana kwenye mbuga za Tanzania
kwa mtindo wa kisasa
Maonesho ya mavazi yakiendelea– vazi la khanga.

 Washiriki wa maonyesho ya mavazi wakiwa katika vazi la Kimasaai.
====================================================================================================

UBALOZI WA TANZANIA, UHOLANZI WASHIRIKI KWA MAFANIKIO
TAMASHA LIJULIKANALO KAMA “EMBASSY FESTIVALTHE HAGUE”

Ubalozi wa Tanzania The Hague, Uholanzi umeshiriki katika Tamasha maarufu la Embassy Festival lililofanyika mwezi Septemba, 2019. Tamasha hili huandaliwa na Manispaa ya The Hague kwa kushirikiana na Balozi za nchi mbalimbali zenye Ofisi zake nchini humo kwa lengo la kutangaza utamaduni wa nchi hizo.

Kama ilivyokuwa kwa balozi nyingine, Ubalozi wa Tanzania ulikuwa na banda lake kwa ajili ya kuonesha utamaduni wa Tanzania. Kwa kushirikiana na Watanzania wanaoishi Uholanzi (Diaspora), Ubalozi ulitumia fursa hiyo kutangaza utamaduni pamoja na vivutio vya utalii zikiwemo mbuga za wanyama.

Ubalozi uliandaa maonesho ya mavazi (fashion show) kwa kuonesha vazi la Kimasai (shuka na shanga, n.k.), pamoja na khanga. Aidha, Ubalozi uliandaa maonesho ya mavazi na vitambaa vyenye animal prints za Simba, Chui (The big five), Twiga na Pundamilia na kuvionesha kwa mtindo wa kisasa na hivyo kuvutia watu wengi.

Diaspora wajasiriamali walipata fursa ya kuuza bidhaa zao mbali mbali za asili kama vile khanga, chai, kahawa ya Tanzania, shanga, hereni, viatu na bangili. Watu wengi waliotembelea Banda la Tanzania walifurahia korosho, chai na kahawa vyote kutoka Tanzania vilivyokuwa vimeandaliwa mahsusi kwa ajili yao.

Ubalozi umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuitangazaTanzania kupitia tamasha hilo ambapo idadi kubwa ya watu walishiriki na kuchukua vipeperushi vya kutangaza utalii wa nchi.

PROF. KABUDI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU KATIBU KATIBU MKUU UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) akislimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Amina Mohammed katika ofisi za Umoja huo zilizopo New York Marekani.

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Amina Mohammed akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) hayupo pichani,wakati akimkaribisha kwa mazungumzo katika ofisi za Umoja huo zilizopo New York Marekani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Amina Mohammed (Hayupo pichani) wakati alipokwenda katika ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo New York Marekani.

Naibu katibu mkuu wa Umija wa Mataifa Dkt. Amina Mohammed na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na ujumbe wake (hawapo pichani) katika ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo New York Marekani.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Amina Mohammed na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na ujumbe wake. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo New York,Marekani.