Sunday, January 19, 2020

TANZANIA YAWASILISHA SALAM ZA RAMBI RAMBI NA PONGEZI - OMAN

Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwasilisha Salam za rambirambi kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Mhe. Yusuf bin Alawi kufuatia kifo cha Sultan wa Oman - Sultan Qaboos bin Said Al Said pia Salaam za pongezi kwa kiongozi mpya wa Oman Mtukufu Haitham bin Tariq bin Taimur Al Said, Muscat,Oman


Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Mhe. Yusuf bin Alawi akizungumza mara baada ya kupokea salam za rambirambi kufuatia kifo cha Sultan wa Oman - Sultan Qaboos bin Said Al Said pia Salaam za pongezi kwa kiongozi mpya wa Oman Mtukufu Haitham bin Tariq bin Taimur Al Said, Muscat,Oman

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Mhe. Yusuf bin Alawi,mara baada ya  kuwasilisha salam za rambirambi kufuatia kifo cha Sultan wa Oman - Sultan Qaboos bin Said Al Said pia Salaam za pongezi kwa kiongozi mpya wa Oman Mtukufu Haitham bin Tariq bin Taimur Al Said, Muscat,Oman. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Oman Balozi Abdallah Abasi Kilima.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Mhe. Yusuf bin Alawi,mara baada ya  kuwasilisha salam za rambirambi kufuatia kifo cha Sultan wa Oman - Sultan Qaboos bin Said Al Said pia Salaam za pongezi kwa kiongozi mpya wa Oman Mtukufu Haitham bin Tariq bin Taimur Al Said, Muscat,Oman.

UJUMBE MAALUM WA RAIS DKT MAGUFULI WAWASILI MUSCAT - OMAN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa na Mshauri Maalum wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Dkt. Salim bin Nassir Al Ismaili. Prof. Kabudi yuko Muscat - Oman kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufuatia kifo cha Sultan wa Oman, Sultan Qaboos  Bin Said Al Said aliyefariki Januari 10, 2020, pia kuwasilisha Salam za pongezi kwa Sultan Mpya wa Oman Mtukufu Haitham bin Tariq bin Taimur Al Said

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamgamba John Kabudi (Mb) akiwa na Mshauri Maalum wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Dkt. Salim bin Nassir Al Ismaili. Prof. Kabudi yuko Muscat - Oman. Kushoto ni Balozi wa Tanzania Nchini Oman Balozi Abdallah Abasi Kilima.

Saturday, January 18, 2020

TANZANIA YATANGAZA UTALII UHOLANZI

Ubalozi wa Tanzania nchini Uholanzi na wadau wengine; Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA) pamoja na makampuni binafsi kama vile, Sea-Cliff Resort & Spa Ltd, Natures Land Safari’s & Rentals na Mbalageti Safari wanashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Utalii (Holiday Fair 2020) yanayofanyika katika mji wa Utretch, Uholanzi kuanzia tarehe 16 hadi 19 Januari 2020.

Hii ni fursa nyingine muhimu kwa Tanzania kujitangaza na kuzidi kuvutia wadau zaidi katika Sekta ya Utalii, kuja kutembelea na kufanya biashara na Tanzania. Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene F. M. Kasyanju tayari amekutana na wadau wote waliofika Uholanzi, kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika ipasavyo na maonesho hayo.

Maonesho hayo ambayo kwa lugha ya kidachi yanajulikana kama “Vakantiebeurs 2020” hufanyika mwezi Januari kila mwaka na yanahudhuriwa na mataifa mbalimbali duniani kwa lengo la kutangaza na kuuza vivutio vya Utalii na Burudani 
Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya wawakilishi wa taasisi za Tanzania wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Utalii nchini Uholanzi. Kutoka kushoto ni Bw. Michael Christian Makombe kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Bibi Alistidia Karaze kutoka Bodi ya Utalii Tanzania na Bw. Gerald Mono kutoka TANAPA. 
Balozi Irene Kasyanju ( wa pili kulia) akiwa na wawakilishi wa TTB na Kampuni ya MAKASA Safaris kutoka Moshi, Kilimanjaro.

Balozi Irene Kasyanju akipokea zawadi ya Kalenda za 2020 kutoka kwa Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania kwenye Maonesho hayo, Bibi Alistidia Karaze ambaye ni Afisa Mkuu wa Utafiti na Maendeleo kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).

Balozi Kasyanju akiwa na wawakilishi kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, TTB, TANAPA; pamoja na Kampuni binafsi yaani, Nature’s Land Safaris & Rentals;  na Mbalageti Safari zote kutoka Mwanza, Tanzania na Sea-cliff ya Dar es Salaam.

Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi akiwa na Balozi wa Uganda nchini humo Mhe. Miriam Blaak ambaye alitembelea  kwenye Banda la Tanzania.
Mandhari ya Banda la Tanzania likionesha wateja mbalimbali wanavyolitembelea. Wateja wanaotembelea licha ya kujionea vivutio vya utalii, wanaonjeshwa pia vyakula vitamu vya Tanzania kama vile vitumbua na mandazi.

Friday, January 17, 2020

KAMPUNI YA ALRIFAI YA KUWAIT YATEMBELEA TANZANIA, KUANGALIA FURSA ZA UWEKEZAJI


Na Mwandishi wetu,

Kampuni ya Alrifai inayojihusisha na biashara ya mazao mchanganyiko iko nchini kwa lengo la kuangalia fursa za uwekezaji hususani kununua zao la korosho na kahawa na kuangalia uwezekano wa kujenga kiwanda cha kuchakata zao la korosho nchini.

Ujumbe wa watu watatu (3) ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud, Meneja Viwango Bwn. Ahmed Mohamed Bahie pamoja na Meneja wa Manunuzi Bwn. M. K Hussin uko nchini tangu tarehe 13 Januari, 2020 kwa lengo kuu la kuangalia uwezekano wa Kununua korosho zilizokwisha chakatwa pamoja na kahawa zilizokobolewa na pia kuona maeneo ambayo wanaweza kuwekeza katika kiwanda cha kuchakata korosho.

Ujumbe huo ulifanya kikako na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bodi ya Kahawa (TCB), Mamlaka ya Maendeieo ya Biashara Tanzania (TanTrade) pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko na kuweza kupata fursa ya kufahamu kwa undani juu ya taratibu za ununuzi wa mazao hayo pamoja na taratibu za uwekezaji wa kiwanda cha kuchakata korosho hapa nchini.

Akitoa maelezo juu ya uzalishwaji wa zao la Korosho nchini, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa TanTrade, Bi. Twilumba Mlelwa alisema kuwa korosho ghafi kwa mwaka huzalishwa kati ya tani 250,000 na tani 300,000 ambapo kiasi kikubwa huzalishwa Mtwara, Lindi, Ruvuma (Tunduru), Pwani (Mkuranga na Kibaha) pamoja na Tanga.

"Naomba niwatoe shaka juu ya zao la korosho kwani kwa sasa viwanda vya korosho ni 18 ambapo vinauwezo wa huhifadhi tani 63,000 za korosho lakini kwa sasa vinavyofanya kazi ni 13 na vina uwezo wa kubangua tani 43,000" Amesema Bi. Mlelwa

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud,ameushukuru Ubalozi wa Tanzania nchini Kuwait kwa ushirikiano alioupata kutoka ubalozini hadi kwa viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje kwa kuweza kuratibu zoezi la kukuagua zao la Korosho, kahawa pamoja na karafuu.

"Binafsi nashukuru kwa ushirikiano nilioupata kwa viongozi wa Mkoa wa Lindi na Mtwara, Bodi ya Mazao Mchanganyiko, TIC, TanTrade, Bodi ya Kahawa pamoja na Balozi Mhandisi Aisha Amour kwa namna alivyolisimamia jambo hili tangu likiwa wazo mpaka sasa tunapoelekea kwenye utekelezaji niwaahidi tu kuwa utekelezaji wa kununua mazao haya utaanza mara moja mara tu baada ya kufanya maamuzi na mikataba itasainiwa kwa mujibu wa sheria," amesema Bwn. Foaud

Aidha, mbali na maelezo ya uzalishaji wa zao la Korosho nchini, ujumbe huo pia ulipata fursa ya kuona zao la korosho lililohifadhiwa katika ghala la Serikali eneo la Kurasini jijini Dar es Salaam na uliridhishwa na zao hilo na kuahidi kuwekeza nchini kwani korosho zinzazalishwa ni nzuri na bora.

Meneja Viwango Bwn. Ahmed Mohamed Bahie amesema "tumejionea wenyewe ubora wa korosho, kahawa na karafuu kwa kweli ni nzuri sana na sote tumeridhika na ubora huo. Tutajitahidi kukamilisha taratibu zote muhimu na kuanza mara moja uagizaji wa korosho na baadae kujenga kiwanda cha kuchakata korosho hapa Tanzania,".  

Ujumbe huo ulipata fursa ya kutembelea maeneo kadhaa kwa lengo la kupata maelezo kuhusu taratibu na fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini, maeneo hayo ni pamoja na mikoa ya Lindi, Mtwara na Kilimanjaro pamoja na Zanzibar ambapo waliweza kuona uzalishaji wa Karafuu.

Ujio wa kampuni hiyo ni matokeo ya juhudi za Ubalozi wa Tanzania nchini Kuwait ambapo ulifanya mazungumzo na Kampuni ya Alrifai inayojihusisha na biashara ya mazao mchanganyiko kuhusu nia yao ya kununua zao la korosho na kahawa na kuangalia uwezekano wa kujenga kiwanda cha kuchakata zao la korosho nchini Tanzania.
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya kahawa nchini(TCB),Primus Kimaryo akiwaelezea jambo viongozi wa Kampuni Alrifai juu ya upatikanaji wa zao la kahawa nchini

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud, akiongea na viongozi kutoka TIC, TCB, TanTrade pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wakati walipokutana katika mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam

Add caption

Meneja Viwango Bwn. Ahmed Mohamed Bahie akikagua korosho zinazozalishwa hapa nchini, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko, Dkt. Anselm Moshi na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Biashara TanTrade, Bi. Twilumba Mlelwa



Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud pamoja na Meneja wa Manunuzi Bwn. Hussain wakikagua korosho zilizohifadhiwa kwenye moja ya ghala hapa nchini, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko, Dkt. Anselm Moshi

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko, Dkt. Anselm Moshi akimuonyesha Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud jinsi korosho zinavyohifadhiwa


 Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko, Dkt. Anselm Moshi akimfafanulia jambo Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud pamoja na Meneja Viwango Bwn. Ahmed Mohamed Bahie


Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Alrifai, Bwn. Abdellah Foaud akiuliza kitu wakati alipotembelea moja kati ya viwanda vya kubangua korosho Mkoani Mtwara


Ujumbe wa Kampuni ya Alrifai ukiwa katika moja ya kiwanda cha kubangua korosho mkoani Mtwara
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bwn. Gelasius Byakanwa (kulia) akiwa ofisini kwake na Ujumbe wa Kampuni ya Alrifai ambapo ujumbe huo ulitembelea pia chuo cha utafiti wa Korosho Nariendele na baadhi ya viwanda vya kubangua korosho

Ujumbe wa Kampuni ya Alrifai ukiwa katika moja ya duka la kuuza karafuu Mjini Zanzibar 

Thursday, January 16, 2020

PROF. KABUDI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA SULTAN WA OMAN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokelewa na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi katika ubalozi wa Oman - Tanzania. Prof. Kabudi amekwenda ubalozini hapo kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Sultan wa  Oman, Sultan Qaboos bin Said.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Oman uliopo Jijini Dar es Salaam kufutia kifo cha Sultan wa Oman, Sultan Qaboos bin Said. Waliosimama ni Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Ramadhan Muombwa Mwinyi.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Oman uliopo Jijini Dar es Salaam kufutia kifo cha Sultan wa Oman, Sultan Qaboos bin Said. 
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Ramadhan Muombwa Mwinyi na viongozi wa Ubalozi wa Oman hapa Nchini pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi,mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Sultan wa Oman,Sultan Qaboos bin Said.

Wednesday, January 15, 2020

SERIKALI YAAGIZA CHUO CHA DIPLOMASIA KUTOA ELIMU KWA VITENDO ZAIDI

Serikali imekitaka Chuo cha Diplomasia kutoa taaluma ya vitendo kwa wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho ili kuwawezesha wahitimu kuwa na mchango katika Taifa hususani wakati huu wa utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya Uchumi.

Akihutubia mahafali ya 22 ya Chuo cha Diplomasia, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ambaye ni Mgeni Rasmi katika mhafali hayo, amesema Serikali itafurahi kusikia chuo kinatoa mafunzo ya stratejia, jiopolitiki na demokrasia pamoja na haki za binadamu hasa kwa muktadha wa kiafrika.

Waziri Kabudi ameongeza kuwa taaluma inayotolewa na Chuo hicho isiwe ya nadharia pekee bali iambatane na vitendo ili elimu hiyo itumike kusaidia kufafanua masuala ya Kidiplomasia na uhusiano wa Kimataifa yanayotokea duniani.

"Nakiagiza Chuo kuandaa mpango mkakati wa mafunzo kwa vitendo ili tuangalie ni jinsi gani Wizara inaweza kusaidia. Aidha, Chuo kipitie mitaala yake mara kwa mara kama ilivyopendekezwa ili kisipitwe na wakati. Dunia inabadilika kwa kasi. Nasi hatuna budi kwenda kwa kasi hiyo," Amesema Prof. Kabudi.  


Prof. Kabudi ameongeza kuwa, ni vyema Chuo kikawa mstari wa mbele kutoa mafunzo hayo kwa wanadiplomasia, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, na wafanyabiashara waliopo hapa nchini.

"Nimefarijika kusikia kuwa mmefanya mazungumzo na Chuo cha ISRI cha Angola kwa nia ya kufikia makubaliano ya kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili nchini Angola ambapo rasimu ya Hati ya Makubaliano imeandaliwa na inasubiri kusainiwa," Amesema Prof. Kabudi.

Prof. Kabudi aliongeza kuwa, Serikali inatambua kwamba Balozi za Iran, Libya, Urusi, Indonesia na China zimekuwa zikitumia wigo huu wa ushirikiano na kubadilishana uzoefu, kutoa mada mbalimbali chuoni hapo. Aidha, alitumia fursa hiyo kuzikaribisha ofisi nyingine za kibalozi hapa nchini kutembelea Chuo cha Diplomasia na kutoa uzoefu wao kwa vinafunzi pamoja na wakufunzi. Hivyo basi, ni vyema menejimenti ya Chuo kutoa mwaliko kwa Balozi zote na wawakilishi wa kudumu wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini kuja kutoa uzoefu wao kwani nayo itakuwa sehemu ya diplomasia ya ulimwengu.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Drkt. Faraji Mnyepe amesema wahitimu 453 wametunikiwa vyeti baada ya kupata mafunzo na kufuzu ambapo kati yao 98 ni wa ngazi ya Astashahada ya Msingi, 119 ni wa Stashahada ya kawaida, 130 ni wa Shahada, 83 ni wa Stashahada ya Uzamili, 45 Stashahada ya uzamili wa diplomasia ya uchumi.

"Nina imani kuwa wahitimu wa leo kama wale wa miaka ya iliyopita, wameiva ipasavyo katika fani za mahusiano ya kimataifa, Diplomasia na Stratejia. Naamin pia kuwa mtakuwa rasilimali kubwa kwa Taifa letu katika fani mlizosomea" Amesema Dkt. Mnyepe.

Dkt. Mnyepe ameongeza kuwa, katika mwaka wa masomo 2019/20 chuo kimeweza kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka 1029 kwa 2018/19 hadi kufikia 1275 kwa mwaka wa masomo 2019/20 ambapo pamoja na mambo mengine juhudi zinaendelea katika kutanua wigo wa udahili kwa kuanziasha udahili wa mwezi Machi pamoja na kuanzisha program mpya.

 "Katika mwaka wa masomo 2019/20 chuo pia kimeweza kupanua mawanda ya program zake kwa kuongeza idadi ya program za muda mrefu. Chuo kimeanzisha Stashahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Amani na Udhibiti wa Migogoro ambapo kwa sasa program hii inaendeshwa Dar es Salaam na Dodoma," Amesema Dkt. Mnyepe.

Chuo cha Diplomasia kilianzishwa rasmi tarehe 13 Januari 1978 kwa kusainiwa Makubaliano yaliyofanywa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi zetu mbili wa wakati huo, Mhe. Benjamini William Mkapa wa Tanzania na Mhe. Joaquim Chissano wa Msumbiji. Kwa miaka yote hiyo, Chuo cha Diplomasia kimejikita kuwaandaa wanadiplomasia, wanastratejia na wabobezi wengi wa masuala ya Uhusiano wa Kimataifa.

Chuo kilitumika kuwaandaa wapigania uhuru wa nchi ya Msumbiji na baadae kilipanua huduma zake na kutumika kuwaandaa pia wapigania uhuru wa nchi za Angola, Zimbabwe, Namibia n.k.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), ambaye pia alikua mgeni rasmi wa Mahafali ya 22 ya Chuo cha Diplomasia, Dar es Salaam, akifungua rasmi Mahafali hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho Kurasini Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika MasharikiDkt. Faraji Mnyepe akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Chuo, Dkt. Jeremia Ponera.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), (katikati) akiwa katika picha ya ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika MasharikiDkt. Faraji Mnyepe na Kaimu Mkurugenzi wa Chuo, Dkt. Jeremia  pamoja na wanafunzi walifaulu vizuri masomo yao


Mgeni Rasmi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Faraji Mnyepe wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa Mahafali ya 22 ya chuo cha Diplomasia. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Chuo, Dkt. Jeremia Ponera

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), ambaye pia alikua mgeni rasmi wa Mahafali ya 22 ya Chuo cha Diplomasia, Dar es Salaam, akitoa hutuba yake wakati wa mhafali yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho Kurasini Jijini Dar es Salaam
Baadhi ya wanafunzi wakisubiri kutunikiwa 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe akisoma hotuba yake kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi
Kaimu Mkurugenzi wa Chuo, Dkt. Jeremia Ponera akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe ili amkaribishe mgeni rasmi kufungua mahafali ya 22 ya chuo

Baadhi ya wahadhiri wa Chuo cha Diplomasia wakiwa wamesimama  huku wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa mahafali
Baadhi ya Mabalozi na viongozi waandamizi wa Serikali wakiwa wanaimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa Mahafali ya 22 ya chuo cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), akimkabidhi zawadi mmoja kati ya wanafunzi walifaulu vizuri masomo yake


 













Tuesday, January 14, 2020

NAIBU WAZIRI DKT NDUMBARO AFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI MKAZI WA ICRC

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam,ambapo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua na kuthamini mchango wa ICRC  katika utoaji wa huduma na misaada ya kibinadamu hapa nchini hasa katika kambi za wakimbizi zilizopo hapa Nchini.

Amesisitiza kuwa Tanzania ikiwa ni mwanachama hai wa ICRC itaendelea kutimiza wajibu wake wa Kitaifa na Kimataifa na kwa kuzingatia Sheria za kimataifa  zilizopo chini ya ICRC,sheria za Tanzania na mkataba wa uenyeji (Head Quarter Agreement) kati ya Tanzania na ICRC uliosainiwa mwaka 2001.

Kwa upande wake Bw. Dubois ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuishirikisha ICRC katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali hususani ile inayohusu utoaji wa misaada ya kibinadamu (Humanitarian assistance) kwa kushirikiana na Chama cha Msalaba Mwekundu – Tanzania (Tanzania Red Cross Society – TRCS).

Ameongeza kuwa ICRC itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wadau wengine katika utoaji wa huduma kwa wakimbizi walioko hapa nchini,wafungwa/mahabusu waliopo magerezani,mafunzo kwa vyombo vya ulinzi na usalama hususani wakati wa ulinzi wa amani (Training on International Humanitarian Law during peace keeping mission).

Bw. Dubois ameambatana na Bi. Andrea Heath mwakilishi Mkaazi wa ICRC – Tanzania. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akimsikiliza Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois.

Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) 

Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) Hayupo pichani. Pembeni yake anayeandika ni Bi. Andrea Heath mwakilishi Mkaazi wa ICRC – Tanzania

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi (Head of Regional Delegation) wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Committee of the Red Cross – ICRC) katika Nchi za Tanzania,Kenya na Djibouti Bw. Olivier Dubois. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam

Thursday, January 9, 2020

SERIKALI YAWATAKA MABALOZI KUZINGATIA SHERIA, TARATIBU ZA NCHI


Tanzania imewataka Mabalozi, Makaimu Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa kuzingatia sheria za nchi pamoja na mikataba ya kimataifa ili kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao nchini kwa ufanisi na ufasaha.

Akiongea katika mkutano na Mabalozi, Makaimu Mabalozi pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa mahusiano ya Tanzania na nchi nyingine yanajengwa katika misingi ya mkataba wa Viena, Mkataba wa umoja wa mataifa na sheria mbalimbali, hivyo ni vizuri mabalozi kuzingatia taratibu hizo.

"Sisi kama tumesisitiza kuwa ni vyema mabalozi na wawakilishi wa nchi zao wakafuata taratibu, mila pamoja na desturi zilizopo katika mikataba hiyo ili kuhakikisha shughuli zao ndani ya Tanzania zinaendana na kufuatana na mkataba wa Viena, mkataba wa umoja wa mataifa lakini pia kunga, mila na desturi za kibalozi," Amesema Prof. Kabudi.

Aidha, Waziri Kabudi aliongeza kuwa Tanzania kupitia mkutano huo imeanza ukurasa mpya wa mahusiano na uendeshaji wa shughuli za Serikali na balozi pamoja na mashirika ya kimataifa yaliyopo Tanzania.

"………tunepata nguvu mpya baada ya mabalozi wote kueleza kuridhika kwao kwa hali ya juu sana na hatua ambazo Serikali ya Tanzania imechukua kupambana na rushwa, kupambana na ubadhirifu wa mali za umma, hatua ambazo Tanzania imechukua katika kuimarisha makusanyo ya kodi lakini pia kusimamia matumizi ya fedha za ndani pamoja na zile zinazotolewa na nchi mbalimbali katika maendeleo ya Tanzania,"  Amesema Prof. Kabudi.

Katika mkutano huo, Waziri Kabudi amewahamasisha mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini kuhusu kuhamia Makao Makuu ya Nchi Dodoma kwa kuwaeleza maendeleo yaliyofikiwa kuhusu ujenzi wa miundombinu mbalimbali muhimu na kwamba wakati umefika wa kuharakisha kuhamia Dodoma kwa wakati muafaka kwa kuwa maendeleo yaliyofikiwa nayatoa fursa ya kuwawezesha wao kuhamia jijini Dodoma.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mabalozi hao hapa Nchini ambae pia ni Balozi wa Comoro Dkt. Ahamada Mohamed ameipongeza Tanzania kwa kuitisha mkutano huo mapema ikiwa ni siku tisa tu tangu kuanza kwa mwaka mpya wa 2020 kwa nia ya kubadilishana mawazo na kusikiliza changamoto za mabalozi na wakuu wa mashirika ya kimataifa pia kuwaelezea hatua za utekelezaji za masuala ya maendeleo chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli jambo linalowapa fursa mabalozi hao kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi hapa nchini.

Nae balozi wa Kenya hapa Nchini Mhe. Dan Kazungu ambaye pia Kiongozi wa Mabalozi wa Bara la Afrika amesema wao kama mabalozi hawawezi kujua mipango, vipaumbele na changamoto za serikali bila ya kuelezwa na kutaka mikutano ya namna hiyo kufanyika mara kwa mara jambo ambalo linatoa uelewa na muelekeo wa utendaji kazi wa serikali  na hivyo kusaidia kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kwa kutambua fursa na changamoto zilizopo.

Awali akiwakaribisha mabalozi katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe, aliwataka mabalozi kuhakikisha kuwa wanazingatia taratibu na kanuni za nchi ili kuhakikisha shughuli zao ndani ya Tanzania zinaendana na kufuatana na mkataba wa Umoja wa Mataifa.

"Nawasihi sana tufanye kazi kwa kuzingatia taratibu za nchi pamoja na sheria na mikataba kwa manufaa ya nchi yetu (Tanzania) na nchi zenu ili tuweze kuendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina yetu kwa maendeleo endelevu" Amesema Dkt. Mnyepe

Mkutano huo umehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro,Katibu Mkuu Dkt Faraji Mnyepe na Mkuu wa Itifaki Balozi, Kanali Wilbert Ibuge, mabalozi 28, Makaimu Mabalozi 12 na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa 10.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe akiongea na mabalozi, (hawapo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na mabalozi, manaibu mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya mabalozi wakifuaatilia mkutano baina yao na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) leo jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (katikati), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb),Katibu Mkuu Dkt. Faraji Mnyepe na Mkuu wa Itifaki Balozi, Kanali Wilbert Ibuge wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi