Wednesday, March 25, 2020

BALOZI KANALI IBUGE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAIMU BALOZI WA PAKISTAN

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akisalimiana na Kaimu Balozi wa Pakistan nchi Bw. Mohammad Saleem alipowasili katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma. Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali ya kudumisha na kukuza uhusiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge na Kaimu Balozi wa Pakistan nchi Bw. Mohammad Saleem wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye Ofisi za Wizara jijini Dodoma. Wengine ni  Caesar C. Waitara Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia (Wa kwanza kulia) na Afisa kutoka Ubalozi wa Pakistan nchini (Wa nne kushoto). 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akielezea jambo kwa Kaimu Balozi wa Pakistan nchi Bw. Mohammad Saleem walipo kutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akimsikiliza Kaimu Balozi wa Pakistan nchi Bw. Mohammad Saleem walipo kutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma
Mazungumzo yakiwa yanaendelea

Friday, March 20, 2020

WIZARA YAKUTANA NA KAMATI YA BUNGE YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI KWA MWAKA 2019/2020


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Wizara ya Mpango wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha wa 2019/2020 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama katika moja ya kumbi za Bunge jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Salim Mwinyi Rehani (mwenye suti nyeusi) wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi hayupo pichani aliyekuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Wizara ya mwaka 2019/2020


 WIZARA YAKUTANA NA KAMATI YA BUNGE YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI KWA MWAKA 2019/2020

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha wa 2019/2020.

Akiwasilisha taarifa ya Wizara, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi amesema Wizara katika kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuzingatia maoni na ushauri wa Kamati ya Bunge imeanzisha Kitengo cha Usimamizi wa Majengo ambacho kitakuwa chini ya Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu.

Amesema pamoja na kuanzishwa kwa Kitengo hicho Wizara imeendelea kushirikiana na Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA) katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi huku wakifuata sheria na taratibu zilizopo.

Amesema uamuzi wa kuanzishwa kwa kitengo hicho unatokana na ushauri uliotolewa na Kamati hiyo uliyoitaka Wizara kuhakikisha mipango ya ujenzi wa majengo ya ofisi na makazi ya Balozi mbalimbali nje ya nchi unasimamiwa kitaalamu na kwa ufanisi mkubwa.

“Uamuzi huu umetokana na ushauri ambao Kamati hii iliutoa kwa Wizara katika kuhakikisha suala la ujenzi wa majengo ya Balozi zetu unasimamiwa kitaalamu na kwa ufanisi,” alisema Prof. Kabudi.

Mhe. Waziri amesema Wizara inaendelea na mipango ya kuwashirikisha Watanzania waishio ughaibuni katika mipango na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchininikiwa ni pamoja na kuwawekea mazingira rafiki ya kuchangia maendeleo na kusaidia ndugu na jamaa zao waliopo nchini na kufanya uchambuzi wa mazingira ya ushirikishwaji wao na kuangalia masuala ya kisheria, kitaasisi ushirikiano na sekta binafsi takwimu za Watanzania waishio ughaibuni na uwezo na hamasa ya kuchangia maendeleo ya nchi.



Wednesday, March 18, 2020

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA SADC

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akifungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika uliofanyika kwa njia ya video kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Machi 2020.

Mhe. Waziri Mkuu akitoa salamu kwa Nchi Wanachama wa SADC ambao ni wajumbe wa Mkutano huo unaoongozwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa jumuiya hiyo.
Pamoja na salamu hizo za ufunguzi Mhe. Waziri Mkuu alipongeza jitihada zinazofanywa na Nchi Wanachama katika kukabiliana na majanga mbalimbali ikiwemo la ugonjwa wa virusi vya CORONA ambao umewezesha nchi wanachama kushirikiana kutafuta namna bora ya kuendelea na shughuli za utekelezaji kwa ustawi wa kanda na watu wake.

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, Mhe. Palamagamba John Kabudi akitoa hotuba ya utangulizi kumkaribisha Waziri Mkuu ili aweze kufungua mkutano wa wa Baraza hilo uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jinini Dar es Salaam.

Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC, Dkt. Stergomena Tax akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu ya jumuiya hiyo wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC.

Wajumbe wa Mkutano huo ambao ni Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine waandamizi wakifuatilia hafla ya ufunguzi. 


Tuesday, March 17, 2020

DKT. NDUMBARO AKUTANA NA BALOZI WA UBELGIJI, SWEDEN


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker pamoja na Balozi wa Sweden nchini Mhe. Anders Sjoberg leo jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo ya Mhe. Naibu Waziri, Dkt. Ndumbaro pamoja na Balozi wa Ubelgiji yalijikita katika masuala mbalimbali ikiwemo masuala ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ubelgiji hasa kwenye sekta za Kilimo na Madini.

Balozi wa Ubelgiji, Mhe. Acker amesema kuwa Ubelgiji itaendelea kuwekeza katika kilimo cha maharage mkoani Kigoma, na kilimo cha Tumbako katika mikoa ya Tabora, Ruvuma, Katavi na Rukwa.

"kupitia uwekezaji wa kilimo nchi zetu mbili (Tanzania na Ubelgiji) zimekuwa zikinufaika sawa hivyo ni rai yangu kuona uwekezaji huu unaendelea kutoa fursa za ajira kwa mataifa haya mawili," Amesema Balozi Acker.

Aidha, Dkt. Ndumbaro amesema kuwa Tanzania itaendelea kuhakikisha inazidi kuimarisha Uhusiano wake na Ubelgiji katika sekta ya Kilimo, Uwekezaji na Biashara ili kuendelea kutoa fursa za ajira na kukuza uwekezaji nchini.

Katika nyingine, Naibu Waziri Dkt. Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Sweden nchini Mhe. Anders Sjoberg, ambapo mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia.  

Pamoja na mambo mengine, Balozi wa Sweeden nchini Mhe. Sjoberg amemuahidi Naibu Waziri kuwa Sweeden itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha kuwa nchi hizi mbili zinapiga hatua katika maendeleo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Kwa upande wake Mhe. Naibu Waziri amemhakikishia Balozi Sjoberg kwamba Tanzania itaendelea kukuza na kuimarisha Ushirikiano na Uhusiano wake na Sweden kwani uhusiano huo wa muda mrefu umekuwa na manufaa kwa nchi zote mbili.


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisalimiana na Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker kabla ya kuanza kwa mazungumzo yao jijini Dar es Salaam



Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker akiongea na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati wa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam



Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akimfafanulia jambo Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker wakati wa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam



Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Balozi wa Sweeden nchini Mhe. Anders Sjoberg wakisalimiana bila kushikana mikono kabla ya kuanza kwa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam



Balozi wa Sweeden nchini Mhe. Anders Sjoberg akiongea na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati wa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam



Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akimueleza jambo Balozi wa Sweeden nchini Mhe. Anders Sjoberg wakati wa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam




Monday, March 16, 2020

TEKNOLOJIA YAWEZESHA MKUTANO WA MAAFISA WAANDAMIZI WA SADC KUEPUKA CORONA ( COVID-19)

Mkutano wa Maafisa Waandamizi ambao ni mkutano wa awali wa maandalizi ya Baraza la Mawaziri la nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajia kufanyika tarehe 18 Machi 2020 umefunguliwa rasmi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini  Dar es Salaam.

Akifungua mkutano huu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafisa Waandamizi wa SADC, Balozi Kanali Wilbert Ibuge amewashukuru wajumbe wote kutoka nchi wanachama pamoja na wataalamu wa TEHAMA kwa jitihata walizoonesha kuhakikisha mkutano huu kwa mara ya kwanza unafanyika kwa mfumo wa Video. “ Hii ni uthibitisho siyo tu wa namna ambavyo Teknolojia ya Habari na Mawasilisno imebadilisha na itaendelea kutubadilisha namna tunavyowasiliana bali pia ambavyo matishio ya majanga ya kidunia kama ugonjwa wa Virusi vya CORONA (COVID 19) yanavyotulazimisha kutafuta mbinu mbadala za kufanya mambo yetu kikanda na kidunia pamoja na kuendelea kuimarisha ushirikiano bila kuonana ana kwa ana” alisema Balozi Ibuge
Mkutano huu unahudhuriwa na Maafisa Waandamizi kutoka nchi 16 za Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika (SADC) wenye dhamana ya masuala ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Fedha, Uchumi, Mipango pamoja na Viwanda na Biashara.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu unaongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masharikia na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafisa Waandamizi wa SADC, Balozi Kanali Wilbert Ibuge ambaye ameambatana na maafisa wengine waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Fedha na Mipango Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Wizara ya Viwanda na Biashara Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Maafisa wengine waandamizi walioshiriki ni pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Mambo ya Ndani. Vilevile mkutano huu umehudhuriwa na baadhi ya Mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha katika nchi za SADC ambao ni pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Jamhuri ya Afrika Kusini.

Mkutano huu utajadili ajenda chache za muhimu kwa wakati huu ambazo ni: Taarifa ya Maandalizi ya Dira ya SADC ya 2050; Mpango Mkakati wa Maendeleo wa SADC 2020-2030; Maadhimisho ya miaka 40 ya SADC tangu kuanzishwa kwake mwaka 1980; Utekelezaji wa maazimio ya vikao vilivyopita; Hali ya michango na kifedha kwa ujumla ya SADC; na Kupokea taarifa ya ukaguzi wa shughuli mbalimbali za Sekretarieti SADC.


Awali mkutano katika ngazi ya Maafisa Waandamizi ulipangwa kufanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Machi 2020 na kufuatiwa na Mkutano wa Baraza la Mawaziri tarehe 17 na 18 Machi 2020. Hata hivyo, kufuatia ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na Mawaziri wa Afya kutoka Nchi Wanachama wa SADC walipokutana kwa dharura tarehe 9 Machi, 2020. Mkutano huo ulijadili na kupendekeza kwa Nchi Wanachama namna ya kuzuia maambukizi ya mlipuko wa ugonjwa hatari wa virusi vya Corona (COVID 19) unaosambaa kwa kasi na kuleta athari kubwa duniani tangu kubainika kwakwe mwezi Desemba.

===================================================================


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafisa Waandamizi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Balozi Kanali Wilbert Ibuge, akifungua mkutano wa Maafisa Waandamizi ambao ni mkutano wa awali wa maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakaofanyika Machi 18, 2020, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafisa Waandamizi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Balozi Kanali Wilbert Ibuge, akifungua mkutano wa Maafisa Waandamizi wa SADC unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, Tanzania. Ufunguzi wa Mkutano huo umefanyika kwa njia ya video kuepuka maambukizi ya Virusi vya ugonjwa CORONA (COVID 19)

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafisa Waandamizi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Balozi Kanali Wilbert Ibuge, akitoa hotuba ya ufunguzi ambapo alitumua nafasi hii kueleza agenda zitakazojadiliwa na wajumbe wa mkutano kutoka nchi wanachama. Pia aliishukuru Sekretariet ya SADC,wajumbe kutoka nchi wanachama, wataalamu wa TEHAMA kutoka nchi za SADC pamoja, na wajumbe wengine kwa ushirikiano wao uliowezesha kufanyika kwa mkutano huo kwa njia ya video. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC, Dr. Stergomena Tax.

Maafisa Waandamizi wa nchi za SADC  wakifuatilia ufunguzi wa mkutano huo uliokuwa ukiendelea kupitia mfumo wa video, unaofanyika katika kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, Tanzania 

Maafisa Waandamizi wa nchi za SADC  wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa mkutano kutokea nchini Tanzania kupitia mfumo wa video  

Mkutano ukiendelea.


Sunday, March 15, 2020

KAMATI YA BUNGE YA NJE, ULINZI NA USALAMA YATEMBELEA OFISI ZA WIZARA YA MAMBO YA NJE ZILIZOPO MTUMBA JIJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Victor Mwambalaswa (Mb.) akizungumza wakati wa ziara ya Wajumbe wa Kamati hiyo walipotembelea Jengo la Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Machi 2020. Lengo la ziara hiyo lilikuwa ni kukagua miradi inayosimamiwa na Kamati hiyo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama walipofanya ziara ya kikazi kwenye Jengo la Wizara lililopo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Machi 2020
Mhe. Prof. Kabudi akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya NUU
Wajumbe wa Kamati ya NUU akiwemo Mhe. Vuai Nahodha (kulia) wakimsikiliza Prof. Kabudi (hayupo pichani). Kushoto ni Mhe. Augustino Masele.
Wajumbe wengine wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Bonnah Kaluwa na Sophia Mwakagenda nao wakimsikiliza Mhe. Prof. Kabudi ambaye hayupo pichani
Mhe. Masoud Abdalla Salim, Mjumbe wa Kamati akichangia hoja wakati wa ziara yao kwenye Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba, Dodoma
Mhe. Prof. Kabudi akimsikiliza Mjumbe wa Kamati, Mhe. Silafu Maufi alipotoa ushauri kwa Wizara kuhusu kuboresha maeneo kadhaa ya Jengo walilotembelea
Mhe. Almas Maige, Mjumbe wa Kamati naye akizungumza. Kulia ni Mhe. Ruth Mollel na Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge (kushoto)
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Issa Ng'imba akitoa taarifa kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (hawapo pichani) kuhusu ujenzi wa Jengo la Wizara lililopo Mtumba
Sehemu ya Wakuuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Bw. Ng'imba ambaye hayupo pichani
Msimamizi wa Miradi ya Majengo ya Wizara, Mhandisi John Kiswaga  akijibu hoja kadhaa zilizowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakati wa ziara yao Wizarani
Mhe. Mwakagenda akizungumza wakati wa ziara yao 
Mhe. Prof. Kabudi akiwaeleza jambo Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama walipotembelea chumba cha ofisi yake wakati wa ziara yao kwenye jengo la Wizara lililopo Mtumba jijini Dodoma


Mhe. Prof. Kabudi akimwonesha Mhe. Mwambalaswa mandhari ya nje ya jengo akiwa ndani ya ofisi yake
Mhe. Prof. Kabudi akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama chumba cha wageni mashuhuri kilichopo kwenye Jengo la Wizara lililopo Mtumba

Wajumbe wa Kamati wakipita pembeni mwa eneo la kiwanja cha Wizara kama inavyoonekana
Mhe. Prof. Kabudi akiwaonesha eneo la nje la Jengo la Wizara
Mhe. Mwambalaswa akimweleza jambo Mhe. Prof. Kabudi
Jengo la Wizara kama linavyoonekana
Mhe. Prof. Kabudi akiwaongoza Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama kurejea ndani mara baada ya kutembelea eneo la nje la Jengo la Wizara lililopo Mtumba jijini Dodoma
Mhe. Prof. Kabudi akijadiliana jambo na  Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama mara baada ya kukamilisha ziara yao.
Mhe. Prof. Kabudi akiagana na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama mara baada ya kukamilisha ziara yao kwenye Jengo la Wizara lililopo Mtumba jijini Dodoma
====================================================


WAJUMBE WA KAMATI YA BUNGE YA  NJE, ULINZI NA USALAMA WATEMBELEA JENGO LA WIZARA LILILOPO MTUMBA

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakiongozwa na Mhe. Victor Mwambalaswa (Mb.), Mwenyekiti wa Kamati hiyo wamefanya ziara ya kikazi kwenye Jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo kwenye Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 15 Machi 2020.

Wajumbe hao ambao wapo kwenye program ya kukagua miradi iliyopo kwenye Wizara zinazosimamiwa na Kamati hiyo, wamepokelewa na mwenyeji wao Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mara baada ya kuwasili.

Wakizungumza wakati wa ziara hiyo, baadhi ya Wajumbe hao, wameipongeza Wizara kwa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo kwa wakati ikiwa ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhamia Dodoma. Pia wameishauri Wizara kuendelea kuboresha maeneo kadhaa katika jengo hilo ikiwa ni pamoja na kuweka uzio kuzunguka jengo hilo na kukamilisha mfumo wa TEHAMA kwa ajili ya kuboresha mawasiliano. Vilevile, Wajumbe wa Kamati hiyo wameitaka Wizara kuzingatia kanuni za ujenzi wa majengo ya Ofisi za Mambo ya Nje pale Wizara itakapoanza ujenzi wa jengo lake la kudumu katika siku zijazo.

Kwa upande wake, Mhe. Prof. Kabudi aliahidi kutekeleza ushauri uliotolewa na Wajumbe wa Kamati hiyo na kuwahakikishia kuwa, mapungufu kadhaa yaliyopo yatafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo.

Aidha, akitoa taarifa fupi kuhusu ugonjwa wa Corona kwa Wajumbe wa Kamati hiyo, Mhe. Prof. Kabudi alisema kuwa, Serikali ya Tanzania imechukua hatua madhubuti kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo endapo utaingia nchini. Hatua hizo ni pamoja na mikutano ya kikanda kuanza kufanyika kwa njia ya video ukiwemo Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika nchini kuanzia tarehe 16 hadi 18 Machi 2020.

Pia Kamati ya Kitaifa inayojumuisha Sekta mbalimbali imeundwa kwa ajili ya kuandaa mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ugonjwa huo. Kadhalika vifaa, wataalam na maeneo ya karantini tayari yametengwa kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo.

“Tanzania inaendelea kuchukua tahadhari mbalimbali kuhusu ugonjwa wa Corona ambao hadi sasa haujaingia nchini. Hatua hizo ni pamoja na kuandaa mikutano ya kikanda ambayo itafanyika kwa njia ya video. Katika kutekeleza hilo, Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC unaoanza tarehe 16 Machi mwaka huu utafanyika kwa njia ya video na utafuata taratibu zote za mikutano ya kikanda wakati wa ufunguzi” alisisitiza Prof. Kabudi.

Jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambalo lipo Mtumba jijini Dodoma lina ukubwa wa Mita za Mraba 1,002 na vyumba 17 vyenye matumizi mbalimbali zikiwemo Ofisi. Jengo hilo lilianza kujengwa mwezi Desemba 2018 na kukamilika mwezi Machi 2019.


Saturday, March 14, 2020

PROF. KABUDI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE KUJITOA MHANGA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara lililofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina jijini Dodoma tarehe 14 Machi, 2020. Pamoja na mambo mengine, Mhe. Prof. Kabudi amewataka Wafanyakazi wa Wizara hiyo kutekeleza majukumu yao kwa kujituma na kutanguliza mbele maslahi ya Taifa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara, Bw. Issa Ng'imba wakati wa ufunguzi wa  Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika jijini Dodoma

Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara hiyo uliofanyika jijini Dodoma
Sehemu nyingine ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara hiyo uliofanyika jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Ibuge naye akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika jijini Dodoma
Mhe. Prof. Kabudi na wajumbe wengine wakimsikiliza Katibu Mkuu, Balozi Kanali Ibuge (hayupo pichani)
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Baraza hilo
Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Amani Simon Msuya akiwa na Mwakilishi wa TUGHE-Dodoma wakifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Wajumbe wa Baraza la Wafanayakazi wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano wa Baraza hilo
Wajumbe wa Baraza wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano
Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Msuya nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Msuya (hayupo pichani)

Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Baraza
Mjumbe wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Zanzibar, Balozi Mohammed Hamza akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo wakati wa ufunguzi 


Sehemu ya Wajumbe wa Baraza wakimsikiliza Balozi Hamza (hayupo pichani)
Wajumbe wa Baraza
Wajumbe wengine wa Baraza
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu, Balozi Ibuge na Wajumbe wa TUGHE-Taifa na Wizarani
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ambao pia ni Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi mara baada ya kufungua rasmi Mkutano wa Baraza hilo
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wote wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki