Saturday, July 25, 2020

MABALOZI 'WAMLILIA' RAIS MSTAAFU MZEE MKAPA


Baadhi ya mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, wamejitokeza kusaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa aliyeaga dunia Tarehe 24 Julai, 2020 jijini Dar es Salaam 'wakimlila' na kumuelezea kwa mema mengi aliyoyafanya wakati wa uhai wake.

Mabalozi hao walianza kuwasili nyumbani kwa Mzee Mkapa kwa nyakati tofauti ambapo mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo baadhi yao wakaelezea walivyoguswa na msiba.

Balozi wa Misri chini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abulwafa amemuelezea Mzee Mkapa kuwa alikuwa mtu makini na aliyependa    masuala ya kidiplomasia.   

"Nimekuja hapa kwa niaba ya Serikali ya Misri kuja kutoa pole kwa kuondokewa na Mzee Mkapa kiongozi mchapakazi kwa taifa la Tanzania na alikuwa kiongozi aliyeinua uchumi wa taifa ambapo chini ya uongozi wake Tanzania iliingia katika ubinafsishaji na utandawazi", Amesema Balozi Abulwafa.

Ameoneza kuwa Mzee Mkapa atakumbukwa na wanadiplomasia wengi duniani kwani alikuwa kiongozi aliyependa amani ambapo enzi za uhai wake alisuluhisha mauaji ya kimbari katika nchi za Rwanda na Burundi pamoja na kurejesa amani katika nci za Sudan, Kongo DRC, Zimbabwe na Kenya.

"Tutamkumbuka kwa upendo na uchapakazi wake uliokuwa umetukuka na kuonesha matunda ya amani na mandeleo kwa Tanzania na Afrika Mashariki", Amesema Balozi Abulwafa.

Kwa upande wake mwakilisi wa Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Adrian Fitzgerald amemuelezea Rais Mstaafu Mzee Mkapa kuwa alikuwa rafiki mkubwa wa Ireland, na ambaye aliyeendeleza na kudumisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Ireland ambao hadi sasa upo imara.

"Kwetu sisi kama Serikali ya Ireland tumeguswa sana na msiba huu, kwa kuondokewa na kiongozi mchapakazi na mpenda amani….daima tutamkumbuka kwa mema yaka na uchapaji kazi wake ulioiletea Tanzania maendeleo. Tulimfaamu vizuri alikuwa kionozi mpenda maendeleo na amani……kwetu sisi ni pigo kubwa sana kwa kifo chake" Amesema Fitzgerald

Baadhi ya mabalozi waliofika na kusaini kitabu cha maombolezo ni Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Shinichi Goto, Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Tanzania, Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi, Balozi wa Misri chini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abulwafa, Balozi wa Finland chini Tanzania, Mhe. Riitta Swan, Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi.


Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Balozi Shinichi Goto akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin Mkapa aliyeaga dunia Tarehe 24 Julai, 2020 jijini Dar es Salaam  

Balozi wa Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Tanzania, Balozi, Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Marehemu Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam  

Balozi wa Misri chini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abulwafa akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin Mkapa nyumbani kwa Marehemu jijini Dar es Salaam  


Balozi wa Finland chini Tanzania, Mhe. Riitta Swan akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Marehemu Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin Mkapa


Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin Mkapa nyumbani kwa marehemu jijini Dar es Salaam  

Mwakilisi wa Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Adrian Fitzgerald akiwaelezea waandishi wa habari jinsi alivyomfahamu Rais Mstaafu Mzee Mkapa wakati alipokuwa nyumbani kwa marehemu jijini Dar es Salaam

PROF. KABUDI AMLILIA MZEE MKAPA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa. Mhe. Benjamin William Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia Ijumaa ya Julai 24,2020 Jijini Dar Es Salaam na anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Lupaso,Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Jumatano ya Julai 29,2020

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa. Mhe. Benjamin William Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia Ijumaa ya Julai 24,2020 Jijini Dar Es Salaam na anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Lupaso,Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Jumatano ya Julai 29,2020

Thursday, July 23, 2020

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MISRI AKARIBISHA KIWANDA CHA NYAYA CHA CAIRO KUWEKEZA NCHINI

Balozi wa Tanzania nchini Misri, Mhe. Meja Generali (Mst.) Anselm Shigongo Bahati akifanya mazungumzo na uongozi wa Kampuni ya Giza Power kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya pande mbili. Kampuni hiyo inamiliki kiwanda kikubwa cha kutengeneza nyaya za umeme kwa matumizi mbalimbali.  Kadhalika, Mhe. Balozi Bahati alitembelea kiwanda hicho na kujionea uwezo wa uzalishaji wa kiwanda hicho  na kujadili na uongozi wa kiwanda hicho kuhusu kuja kuwekeza Tanzania. Kiwanda cha Giza Power kinafanya biashara ya nyaya za umeme na nchi za Ulaya, Mashariki ya Kati na Afrika.
Mhe. Balozi Bahati akipata maelezo kutoka kwa mtaalam alipokitembelea kiwanda kikubwa cha kutengeneza nyaya za umeme kwa matumizi mbalimbali. Kwenye ziara hiyo Mhe. Balozi Bahati alijionea uwezo wa uzalishaji wa kiwanda hicho. Kiwanda cha Giza Power kinafanya biashara ya nyaya za umeme na nchi za Ulaya, Mashariki ya Kati na Afrika.

Tuesday, July 21, 2020

Naibu Katibu Mkuu Dkt Haji akaribishwa rasmi Wizarani



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Mwinyi Talib Haji katika ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma,  mara baada ya kuapishwa tarehe 20 Julai 2020.

Menejimenti ya Wizara wakiwa wamejipanga kumkaribisha ofisini Naibu Katibu Mkuu Dkt Haji ofisini Mtumba.

Naibu Katibu Mkuu akisalimiana na sehemu ya Menejimenti

Naibu Katibu Mkuu akisalimiana na sehemu ya Wakurugenzi, kulia ni Katibu Mkuu Balozi Ibuge akiwa emeongozana nae. 



                      Naibu Katibu Mkuu akisalimiana na sehemu ya Wakurugenzi

Katibu Mkuu Balozi Ibuge akiwa katika mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu alipomkaribisha ofisini kwake Mtumba, Dodoma.





Thursday, July 16, 2020

DKT. NDUMBARO AFANYA MAZUNGUMZO NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA MKOA WA RUVUMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Wilaya hiyo Mhe. Christina Mndeme ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo.

Mazungumzo hayo yamefanyika baada kuhitimisha ziara iliyofanywa na Dkt. Ndumbaro ya kutembelea mipaka inayoinganisha Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji iliyopo katika Mkoa wa Ruvuma. 

Dkt. Ndumbaro kwa nyakati tofauti katika mwaka huu amefanya ziara maalumu katika mpaka wa Magazini uliopo Wilayani Namtumbo-Ruvuma, Wenje uliopo Wilayani Tunduru-Ruvuma, Chiwindi uliopo Wilayani Nyasa-Ruvuma  na baadaye mpaka wa Mkenda uliopo Wilaya ya Songea Vijijini. Mipaka yote inaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji. 

Lengo la kufanya ziara ilikuwa ni kubaini na kutatua changamoto zinazokabili maeneo ya mipakani sambamba na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi. Katika ziara hizo Dkt. Ndumbaro alikutana na kuafanya mazungumzo na baadhi ya wananchi na watumishi katika mipaka husika. Sambamba na changamoto kadhaa alizozibaini aliridhishwa na utendaji wa Watumishi waliopo mpakani na kuwahimiza kundelea kufanyakazi kwa bidii,ubunifu na kwa kuzingatia maadali.

Aidha, Dkt. Ndumbaro katika kikao chake na Kamati ya Ulinzi ya Mkoa wa Ruma amebainisha kuwa changamoto nyingi zilizoelezwa mipakani zikiwemo ukosefu wa umeme, barabara za kiwango cha lami, mawasiliano na Vituo vya kutoa huduma Pamoja Mpakani (OSBP), Serikali chini ya usimamizi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tayari zimeanza kufanyiwa kazi.

Dkt. Ndumbaro kwa upande wake amehimiza umuhimu wa Mamlaka za Mkoa hasa zilizopo maeneo ya Mipakani kuendelea kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika kutekeleza Diplomasia ya Uchumi, kudumisha na kulinda uhusiano wa kidiplomasia na nchi jirani.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mhe. Christina Mndeme kwa niaba ya Kamati ya Ulinzi ya Mkoa, amempongeza Naibu Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro kwa ziara hiyo na jitihada anazifanya katika kuhakikisha Diplomasia ya Uchumi inaendelea kutekelezwa kwa mafanikio makubwa. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Mhe. Christina Mndeme wakisalimia walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Makao Makuu ya Mkoa huo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisaini kitabu cha Wageni alipo wasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mideme
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akifafanua jambo alipokutana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Ruvuma.

Kikao kikiendelea

Wednesday, July 15, 2020

DKT. NDUMBARO AFANYA ZIARA KATIKA MPAKA WA MKENDA, RUVUMA


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amefanya ziara katika eneo la mpaka wa Mkenda uliopo Wilaya ya Songea Vijijini Mkoani Ruvuma unaoinguanisha Tanzania na nchi Jirani ya Msumbiji. Ziara hii inalenga kibaini na kutatua changamoto mbalimbali ili kukuza biashara na uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji. Katika ziara hiyo Dkt. Ndumbaro aliambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi ya Wilaya ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Vijijini Mhe. Pololet Mgema. 

Akiwa mpakani hapo Dkt. Ndumbaro amefanya mazungumzo na watumishi wa Idara mbalimbali za Serikali walipo katika ofisi za mpaka huo kwa lengo la kusikiliza changamoto na mapendekezo yanayolenga kuboresha namna ya utoaji huduma kwa wakazi wa eneo la mpaka na watumiaji wa mpaka huo. Aidha, Dkt. Ndumbaro pamoja na kutoa ufumbuzi wa baadhi ya changamoto, na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizosalia amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa ubunifu, jitihada na uaminifu.

Dkt. Ndumbaro pia ametembelea Ofisi za mpakani kwa upande wa Nchi jirani ya Msumbiji na kufanya mazungumzo na Watumishi walipo katika Ofisi hizo. 

Mheshimiwa Ndumbaro, amewaeleza wakazi na watumishi waliopo mpakani humo kuwa Serikali inaendelea na hatua za kuzitatua changamoto kubwa zinazo changia ugumu wa utekelezaji wa majukumu ya kilasiku na kuadhiri mwenendo wa biashara mpakani hapo, ikiwemo ukosefu wa umeme, huduma ya mawasiliano na barabara ya kiwango cha lami na ujenzi wa Kitu cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP)

Dkt. Ndumbaro amewapongeza Watumishi walipo mpakani kwa kazi nzuri wanayoifanya na amewahimiza Watumishi hao kuendelea kutekeleza Dilomasia ya Uchumi, kuendeleza uhusiano mwema na kushughulikia suala la Diaspora

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisaini kitabu cha Wageni alipotembelea Ofisi ya Uhamiaji katika mpaka wa Mkenda uliopo Wilaya ya Songea Vijijini, Mkoani Ruvuma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza na Wafanyakaozi wanahudumu katika mpaka wa Mkenda. Kushoto ni Mhe. Pololet Mgema Mkuu wa Wilaya ya Songea Vijijini. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Mkuu wa Wilaya ya Songea Vijijini Mhe. Pololet Mgema wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya wakazi wa mpakani Mkenda 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akipokelewa na Maafisa Uhamiaji wa upande wa Msumbiji alipotembelea ofisi za mpakani Mkenda za nchi hiyo wakati wa ziara.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisaini kitabu cha Wageni alipotembelea Ofisi ya Uhamiaji za Msumbiji zilizopo mpakani Mkenda, Ruvuma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Mkuu wa Wilaya ya Songea Vijijini Mhe. Pololet Mgema wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya Watumishi wa Mpakani kutoka Tanzania na Msumbiji 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiendelea na ziara katika maeneo mbalimbali ya mpaka

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisisitiza jambo wakati wa mazunguzo na daadhi Wananchi waliojitokeza wakati wa ziara

Friday, July 10, 2020

TANZANIA, CHINA ZAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO, KUKUZA MAENDELEO


Tanzania na China zimeahidi kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia ili kuhakikisha kuwa nchi hizo zinakuwa na maendeleo endelevu. 

Makubaliano hayo yamefanywa na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke, wakati alipokutana kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge leo jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Ibuge amesema kuwa wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo suala la namna ya kutekeleza nia ya Viongozi Wakuu wa nchii za China na Tanzania (Rais wa China, Mhe. Xi Jinping pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Joseph Pombe Maufuli) ya kupunguza madhara yatokanayo na ugonjwa wa COVID 19 ikiwemo kufutiwa na kusamehewa madeni.

Naishukuru Serikali ya China kwa uhusiano na ushirikiano ambao imekuwa ikionesha kwa Tanzania. Uhusiano huo umeendelezwa na viongozi wa pande zote mbili ambao umekuwa ukiimarika siku hadi siku na kuahidi kuwa serikali ya Tanzania itaendela kudumisha ushirikiano wake wa kidiplomasia kati yake na China.

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo yalijadili masuala ya biashara na uwekezaji, mradi wa nyumba 25 za wataalum wa Afya zilizopo Osterbay jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Balozi Wang Ke pamoja na mambo mengine, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada ilizochukua katika kukukuza uchumi wake hadi kufikia uchumi wa kati, pamoja na mapambano dhidi ya COVID 19.

"Leo nimekutana na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Balozi Brigedia Jenerali Ibuge na kuongea mambo mbalimbali ya ushirikiano na tunaipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada  ilizochukua katika kufanya kazi kwa bidii na kukuza uchumi wake hadi kufikia uchumi wa kati, pamoja na hatua ilizochukua katika kupambana na janga la COVID 19 ambapo tumefurahishwa kuona janga la COVID 19 limeisha," Amesema Balozi Ke.

Balozi Ke ameongeza kuwa wamekubaliana katika maongezi hayo pia kuendeleza ushirikiano wa kufanya kazi kwa pamoja kwa manufaa ya mataifa mawili (Tanzania na China) ili kuhakikisha uhusiano na ushirikiano unazidi kukua na kuimarika.

 Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana katika sekta za kilimo, biashara na uwekezaji, miradi ya mikopo nafuu na misaada, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Uchukuzi, Afya, Utalii na utamaduni. 

China na Tanzania zilianzisha mahusiano rasmi ya kidiplomasia mwaka 1964.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiongea na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke, wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam

Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge wakati Walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam 



Tuesday, July 7, 2020

NUMBER OF FRENCH TOURISTS SURGE TO 56,000

The number of French tourists visiting Tanzania increased from 21,000 in 2016 to 56,000 last year, thanks to the Tanganyika Expeditions Agency and Axium by Parker operators, who have been organising trips.

Speaking at a meeting with French tour operators and tourism professionals in Paris recently, Tanzanian Ambassador to France Samwel Shelukindo told participants that the government of Tanzania had lifted restrictions on commercial flights and quarantine measures imposed on travellers since May 18, this year.

He noted that international airlines, including Ethiopian Airlines, Qatar Airways and KLM had already resumed flights to Tanzania.
"As it is the case in other countries, Tanzania was also affected by the Covid-19 pandemic, but now coronavirus cases have dropped significantly, thanks to the commitment and efforts made by the government under the leadership of our President John Magufuli and Tanzanian people who understood the challenge and complied with preventive measures to fight against the covid-19 pandemic," said the ambassador.

He added that the Ministry of Natural Resources and Tourism had developed national standard operating procedures (SOPs) for the management of Covid-19 in tourism business and invited potential tourists to consult the embassy.

"In this respect, I would like to underline that Tanzania has started receiving tourists. All precautions and preventive measures are taken to receive tourists and enable them to have an unforgettable stay. The government has also created an enabling environment to attract tourists." 

French tour operators listening to Tanzanian Ambassador's  speech   
Tanzanian Ambassador to France H.E Samwel Shelukindo addressing French tour operators during a meeting that took place in Paris, France recently.
Participants listening to Ambassador Shelukindo's  speech during a meeting with French Tour Operators that took place in Paris recently.  

Monday, July 6, 2020

KATIBU MKUU BALOZI BRIGEDIA JENERALI IBUGE ATEMBELEA BANDA LA WIZARA SABASABA


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, ametembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Wizara Balozi Ibuge amewataka Watanzania kuendelea kuchapa kazi zaidi ili kuyaona matunda ya nchi kuwa katika kundi la uchumi wa kati.

''Sasa nchi yetu imeingia katika uchumi wa kati ambao unamaanisha kila mtu aendelee kupiga juhudi zaidi ya pale alivyokuwa anafanya ili tuendelee kupaa kuliko hivi ambavyo tumefikia sasa'' amesema Balozi Ibuge.

Amesema Tanzania sasa ina Balozi 43 na Balozi ndogo tatu na ni mwenyeji wa Balozi 63 na Mashirika ya Kimataifa 30 ikiwa ni namna ya kuipeleka Tanzania katika anga za kimataifa tukionyesha mafanikio vivutio vyetu na vitu vingine vyote tunavyovifanya ili kujiletea maendeleo huku tukiimarisha mahusiano ya kimataifa.

Akiwa katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Balozi Ibuge ametembelea banda la Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) na makampuni matatu ya Kigeni yanayoshiriki maonesho hayo.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akizungumza na watumishi alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akiangalia jarida linaloelezea utekelezaji wa dipolomasia ya uchumi linalochapishwa na Wizara alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, katika picha ya pamoja na watumishi walioko kwenye banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba)

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akijadili jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dkt. Ave Maria Semakafu walipotembelea moja ya banda kwenye maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dkt. Ave Maria Semakafu wakimsikiliza mfanyabiashara kutoka Siria anayeshiriki maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

Nafasi ya Kazi katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola


Sunday, July 5, 2020

DKT. NDUMBARO ATEMBELEA BANDA LA WIZARA SABASABA


Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, ametembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Wizara Dkt. Ndumbaro amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi ili kuiletea sifa Serikali na kuendelea kuimarisha mahusiano ya kimataifa.

"Kwa kuwa sisi tunafanya kazi ya kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Nje na kuhakikisha mahusiano ya kimataifa yanaimarika hatuna budi kufanya kazi kwa bidii na maarifa yetu yote, hili ni jukumu letu hivyo ni lazima tuhakikishe tunalitekeleza kwa ufanisi na ufasaha," Amesema Dkt. Ndumbaro

Akiwa katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Dkt. Ndumbaro ametembelea pia banda la Bunge, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Dodoma na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.


Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.




Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Ndumbaro, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.




Thursday, July 2, 2020

PROF. KABUDI ATETA NA MJUMBE MAALUM WA MAZIWA MAKUU



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Prof. Kabudi ateta na Mjumbe Maalum wa Maziwa Makuu

Dodoma, 2 Julai 2020
Tanzania inaamini katika umoja wa jumuiya ya kimataifa kwenye kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia ikiwemo mlipuko wa ugonjwa wa Corona.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) alipofanya mazungumzo kwa njia ya mtandao na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye eneo la Maziwa Makuu, Balozi Huang Xia.

Viongozi hao walitumia fursa hiyo kubadilishana mawazo katika masuala mbalimbali yanayotokea duniani, ikiwa ni pamoja na mikakati na mbinu bora za kukabiliana na janga la ugonjwa wa Corona na athari zake katika uchumi kwenye eneo la Maziwa Makuu.   

Balozi Huang alielezea hatua mbalimbali anazozichukua zikiwemo kuongea na taasisi za kimataifa za fedha na wadau wengine kwa ajili ya kuzihimiza kutoa misaada kwa nchi za Maziwa Makuu ili ziweze kukabiliana na janga la ugonjwa wa Corona na athari zake za kiuchumi na kijamii. Licha ya kukutana na taasisi hizo, Balozi Huang pia amefanya mashauriano na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Maziwa Makuu kuhusu janga la Corona. Kwenye mashauriano hayo Mawaziri wamesisitiza umuhimu wa kuandaa mkutano wa Mawaziri kwa njia ya mtandao ili kujadili, pamoja na mambo mengine mikakati ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona na hali ya usalama katika eneo la Maziwa Makuu.

Kwa upande wake, Prof. Kabudi aliunga mkono wazo la kuwa na mkutano wa Mawaziri wa nchi za Maziwa Makuu na kuelezea matumaini yake kuwa, mkutano huo utatoa mawazo mazuri yatakayosaidia ufumbuzi katika changamoto zinazoikabili dunia ukiwemo ugonjwa wa Corona.

Aidha, Prof. Kabudi alitoa maelezo kuhusu mikakati iliyochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kudhibiti ugonjwa wa Corona. Alisema moja ya mikakati hiyo ni tangazo la maombi ya siku tatu kwa nchi nzima lililotolewa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, maombi ambayo yaliyohusisha imani zote.  Tangazo hilo  lilionekana ni jambo geni kwa watu wengi duniani lakini kwa Tanzania, nchi yenye waislamu na wakristo takribani nusu kwa nusu, lilikuwa ni muhimu na uamuzi huo haukuifanya Tanzania kupuuza maelekezo mengine yanayotolewa na wataalam wa afya.   

Mazungumzo hayo yalihitimishwa kwa Mhe. Waziri kuahidi kuwa, Tanzania itashirikiana kwa karibu na ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika uamuzi wake wa kuandaa mkakati maalum wa kuzuia migogoro na kuimarisha amani na utulivu kwenye eneo la nchi za maziwa makuu.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akizungumza kwa njia ya mtandao na Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu, Mhe. Balozi Huang Xia kuhusu ushirikiano katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona na masuala ya amani na usalama katika ukanda huo. Mazungumzo hayo yalifanyika Prof. Kabudi akiwa jijini Dodoma huku Balozi Huang Xia akiwa jijini Nairobi, Kenya.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Prof. Kabudi ukifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Kabudi na Balozi Huang Xia (hawapo pichani). Kulia ni Bw. Magabilo Murobi, Katibu wa Waziri na Bw. Ali Ubwa, Afisa Mambo ya Nje.