Wednesday, November 18, 2020

BALOZI BRIGEDIA JENERALI WILBERT A. IBUGE ATOA SOMO KWA WABUNGE KUHUSU DIPLOMASIA NA ITIFAKI

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada mbele ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania kwa ajili ya kuwaweka sawa katika eneo la Itifaki na Diplomasia

Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiendelea kutoa mada kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania eneo la Itifaki na Diplomasia.

Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akitoa somo kwa Wabunge


Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiendelea kutoa somo kwa Wabunge



Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akitoa somo kwa Wabunge huku Naibu Spika Mhe. Dkt. Tulia Akson na Katibu wa Bunge Bw. Stephen Kigaigai wakimsikilizaa.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, ametoa somo la Diplomasia na Itifaki kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Balozi Ibuge ametoa somo hilo tarehe 16 Novemba 2020 katika semina iliyofanyika katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma.

Katika Semina hiyo, Balozi Brig. Gen. Ibuge aliwaeleza Wabunge hao kwa ujumla kuhusu dhana ya Itifaki; Itifaki ya Viongozi wa Kitaifa; Itifaki katika mawasiliano ya Viongozi; Itifaki ya mawasiliano rasmi na Balozi zilizopo hapa nchini.

Dhana nyingine ni pamoja na Itifaki ya upeperushaji Bendera na mipaka yake; Itifaki ya mavazi kwa viongozi pamoja na mambo mengine kuhusu Itifaki kwa Wabunge na Viongozi wote nchini.

Semina hiyo ililenga kuwajengea Wabunge uelewa mpana zaidi kuhusu masuala ya Diplomasia na Itifaki ikiwa ni moja ya masuala muhimu ya kuyafahamu kama zilivyo sheria na taratibu mbalimbali ambazo kwa namna moja ama nyingine watakutana nazo katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Kibunge.





Tuesday, November 17, 2020

WATUMISHI WA WIZARA WALIVYOMPOKEA WIZARANII MHE. PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI BAADA YA KUAPISHWA

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi baada ya kuwasili Wizarani Mtumba akitokea Ikulu ya Chamwino alipoapishwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili cha Serikali ya awamu ya Tano tarehe 16/11/2020

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akipokea shada la maua kutoka kwa mtumishi wa wizara alipokaribishwa Wizarani baada ya kuapishwa.


Matukio katika picha yakionesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi alipopokelewa na menejimenti na watumishi wa Wizara alipowasili Wizarani baada ya kuapishwa










 

 

 

 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Katibu Mkuu mara baada ya kuwasili
 

Katibu Mkuu  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi kuzungumza na menejimenti ya Wizara baada ya kukaribishwa Wizarani

 


 Kikao kikiendelea

Monday, November 16, 2020

PROFESA KABUDI AKIAPISHWA KUWA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

 

Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiapa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi na Mhe. Dkt. Philip Mpango wakiapa, Ikulu Chamwino jijini Dodoma. Mhe. Dkt. Philip Mpango ameapa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango

Saturday, November 14, 2020

BALOZI IBUGE AKUTANA NA BALOZI WA CHINA NCHINI

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke ofisini kwake jijini Dodoma.

Katika kikao hicho Katibu Mkuu, Balozi Ibuge na Balozi Wang Ke pamoja na mambo mengine wameongelea juu ya mapendekezo ya mabadiliko ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu nafasi za uwakilishi wa kudumu kwa Bara la Afrika.

katika Kikao hicho Balozi Ibuge amesisitiza msimamo wa Tanzania kuunga mkono nia ya Bara la Afrika kuwa na nafasi mbili za uwakilishi wa kudumu katika Baraza hilo. Nchi za Afrika zinataka uwakilishi huo uwe na nguvu ikiwa ni pamoja na kupata nafasi moja ya kura ya Veto kama walivyokubaliana katika mkutano wa Ezulwini  na Azimio la Sirte la mwaka 1999. 

Balozi Ibuge pia amezungumzia kuhusu utekelezaji wa mambo maalum ambayo yamo katika Hotuba ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli  aliyoitoa wakati wa kuzindua Bunge la 12, tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma, ambapo amemuomba Balozi Wang Ke kufikisha mambo yaliyomo katika hotuba hiyo kwa wawekezaji wa China ili kuwekeza nchini.

Balozi Ibuge amesema maono ya Mhe. Rais aliyoyasema katika hotuba yake ni utekelezaji wa moja ya kauli iliyowahi kutolewa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa "wakati wengine wanatembea Watanzania tunatakiwa tukimbie." ili kufikia maendeleo kwa haraka. 

Kwa Upande wake Balozi Wang Ke amemuhakikishia Balozi Ibuge, kwamba China iko pamoja na Bara la Afrika na kwamba wanaunga mkono  mapendekezo ya Bara la Afrika ya kuwa na nafasi mbili za kudumu katika Baraza hilo.

Balozi Wang Ke ameelezea kufurahishwa na maono ya Mhe. Rais yaliyobainishwa katika Hotuba hiyo na kuahidi kuendelea kuisaidia Tanzania ili kufanikisha maono hayo kwa vitendo na kuwaletea wananchi wa Tanzania maendeleo. 

Viongozi hao pia wamejadiliana na kukubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na kindugu baina ya Tanzania na China kwa faida ya pande zote mbili.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimkaribisha Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke alipokutana naye ofisini kwake jijini Dodoma.



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akizungumza na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke walipokutana ofisini kwake jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo hayo walipokutana ofisini kwake jijini Dodoma.


Balozi Wang Ke akizungumza katika kikao hicho 






Friday, November 13, 2020

WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI WAHIMIZWA KUTANGULIZA MASLAHI YA TANZANIA

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amekutana na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki na kuwahimiza kutanguliza  maslahi ya Tanzania katika kutekeleza majukumu yao.

Mhe. Ibuge amesema hayo jijini Dodoma alipokutana na Wabunge hao na kusisitiza kuwa maslahi ya Tanzania ni lazima yawe kipaumbele chao katika kutekeleza majukumu yao  ili kufanikisha ushiriki wa Tanzania kikamilifu katika mtangamano wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 “Endeleeni kushikilia msimamo wa kutanguliza maslahi ya Tanzania siku zote, muendelee kufanya kazi hiyo nzuri  kwenye masuala mengine yote yanayogusa maslahi ya nchi yetu,” amesema Balozi Ibuge na kuongeza kuwa nafasi yao kama wabunge wa Afrika Mashariki inatokana na uwepo wa jimbo lao ambalo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mtangamano huo.

Balozi Ibuge pia amewataka Wabunge hao kuwasiliana mara kwa mara na Serikali ili kupata maoni, ushauri na msimamo wa Serikali katika kujadili na kupitisha masuala mbalimbali ndani ya bunge hilo.

Balozi Ibuge amewataka wabunge hao kujiepusha na migogoro ndani ya Bunge na Jumuiya kwani kufanya hivyo kutaiwezesha Tanzania kujiweka sawa katika nyanja za siasa na diplomasia na kuwapongeza kwa utendaji kazi wao na hasa jinsi walivyoshughulikia suala la Muswada binafsi wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Wabunge hao Mhe. Adam Kimbisa aliishukuru Wizara kwa kukutana nao kuwapa muongozo wa namna ya kushughulikia mambo mbalimbali yanayoendelea ndani ya Bunge na Jumuiya kwa ujumla.

Mhe. Kimbisa alimuahakikishia Katibu Mkuu kuwa Wabunge hao  wataendelea kuhakikisha maslahi ya Tanzania yanazingatiwa katika hatua zote za mtangamano kupitia ushiriki wao katika Bunge la Afrika Mashariki.

 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akizungumza na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) ofisini kwake Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika Picha ya pamoja na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) walipomtembelea ofisini kwake Jijini Dodoma




SALAMU ZA PONGEZI




 

Tuesday, November 10, 2020

COMORO YAIPONGEZA TANZANIA KWA UCHAGUZI HURU, AMANI NA HAKI

Rais wa Visiwa vya Comoro Mheshimiwa Azali Assouman ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufanya uchaguzi huru, amani na haki.

Rais wa Visiwa vya Comoro ameipongeza Tanzania leo jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa tayari kuondoka nchini na kurejea Comoro baada ya kushuhudia hafla ya uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli uliofanyika Novemba 5 Jijini Dodoma.

Rais Assouman anasema Tanzania ni nchi ya Amani na utulivu wa kisiasa kwani wakati wote wa tukio la kuapishwa kwa Dkt Magufuli aliona mambo ambayo yanapaswa kuigwa na mataifa mengine hususan kwenye nyakati za uchaguzi.

"Kwa kweli tangu nimefika hapa Tanzania nimeona mambo mazuri na ambayo tunapaswa kuyaiga sisi viongozi wa mataifa mengine," Amesema Rais Assouman

Mbali na kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo ya uchaguzi, pia Rais Assouman ameliahidi ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika Nyanja za mbalimbali ikiwemo diplomasia ya uchumi, biashara, uwekezaji na utalii.

“Najisikia niko nyumbani kwa sababu uhusiano wetu umeimarishwa zaidi, mahusiano yetu yamekuwa katika masuala ya kijamii, utamaduni, biashara na mambo mengine mengi” Amebainisha Rais Assouman.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Sylvester Mabumba amesema kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Comoro katika kuhakikisha kuwa sera ya uchumi wa nchi zote mbili unakua zaidi.

"Sisi tuatendelea kushirikiana vyema na Comoro kibiashara ili kukuza sera ya 2025 tunaifikia ipasavyo kwa kuhakikisha kuwa uchumi wetu unafikia kiwango cha juu sana, naamini kuwa tunapokuwa na masoko ya uhakika Viswa vya Comoro uchumi wetu utakuwa zaidi," Amesema Balozi Mabumba.

Kwa Upande wake Balozi wa Visiwa Vya Comoro nchini Tanzania mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed amesema kuwa kuna fursa nyingi za kiuchumi ambazo Comoro na Tanzania zinaweza kushirikiana.

Rais Assouman aliwasili nchini Novemba 4 kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli uliofanyika Novemba 5 Jijini Dodoma ambapo baada ya shughuli hiyo alipata fursa ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ambapo na kujiona vivutio mbalimbali vya utalii nchini.

Serikali ya Tanzania na Visiwa Comoro zimekuwa zikishirikiana katika sekta mbalimbali ikiwemo, elimu, afya, biashara na uwekezaji.


Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman akiongea na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA),kabla ya kuondoka nchini na kurejea nchini Comoro. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe.Sylivester Mabunda  akifuatiwa na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed.   


Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman akiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA), baada ya kushuhudia hafla ya Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli iliyofanyika Novemba  5, 2020 Jijini Dodoma na Baadaye alitembelea Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro


Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman, akiangalia kikundi cha ngoma   kabla ya kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA), baada ya kushuhudia hafla ya Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli iliyofanyika Novemba 5, 2020, Jijini Dodoma na Baadaye alitembelea Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro

Kikundi cha Ngoma kikiburudisha katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere kabla ya kuondoka kwa Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman



Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman, akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe.Sylivester Mabunda katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA), Jijini Dar es Salaam


Rais wa Visiwa  vya Comoro, Mhe. Azali Assouman, akiaga tayari kwa  kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere(JNIA), kwa kutumia Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania)





Thursday, November 5, 2020

MHESHIMIWA DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AKILA KIAPO CHA URAIS

Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akila kiapo cha kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye sherehe za uapisho zilizofanyika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akila kiapo cha kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye sherehe za uapisho zilizofanyika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akihutubia hadhira iliyohudhuria sherehe ya uapisho katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, muda mfupi baada ya kula kiapo.