Thursday, April 15, 2021

BALOZI BRIGEDIA JENERALI IBUGE AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MKOANI MWANZA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge leo ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu Mkoani Mwanza. Ziara hii inalenga kufuatilia maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) katika Ukanda wa Ziwa Victoria. 

Akiwa mkoani Mwanza Balozi Brigedia Jenerali Ibuge ametembelea mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Victoria uliopo Walayani Magu, Mwanza. Utekelezaji wa mradi huu wa Kikanda unaratibiwa na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria chini ya ufadhili na Adaptation Fund (AF). Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu ambapo pia utahusisha Nchi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda.

Balozi Brigedia Jenerali Ibuge akiwa katika eneo la mradi ameeleza kuridhishwa na ubunifu wa mradi huo na kuwaeleza wananchi waliojitokeza kuwa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inafautilia utekelezaji wa mradi huo wa mazingira unaowanufanisha wakazi wa eneo hilo kwa sababu unatekelezwa chini ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na hivyo Wizara ndio yenye dhamana ya kuratibu masuala yote yanayohusu au kutokana na Jumuiya. “Hatuwezi tukawa tunaenda kwenye vikao na kuzungumzia kuhusu kutumia pesa za walipa kodi katika kutekeleza miradi bila sisi wenyewe kufika kuona na kujiridhisha juu ya ubora na maendeleo ya miradi husika; Niwahakikishie, haya yote yanafungamana na namna serikali mliyoichagua inavyowajali katika kuleta maendeleo yetu sote kwa pamoja” ameeleza Balozi Brigedia Jenerali Ibuge. 

Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Ally Said Matano kwa upande wake ameeleza kuwa, LVBC itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kubuni na kutekeleza miradi itakayo tatua changamoto katika jamii na kuchagiza maendeleo ya Nchi na watu wake.

Kabla ya kuanza kwa ziara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Ibuge alikutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Mwaza Mhe. John V.K. Mongela na Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Ally Said Matano ambaye pia aliambatana naye katika ziara ya kutembelea miradi. Balozi Brigedia Jenerali Ibuge ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanaitunza miradi hiyo na kuitumia ipasavyo ili kuboresha maisha yao kama ilivyokusidiwa kwenye malengo ya kuanzishwa kwake. 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge (kushoto) akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela wakiwa katika mazungumzo pamoja na watendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria na Wizara.
Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Eliabi Chodota, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela, Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) Dkt. Ally Said Matano na Mhandisi Hilda Luoga kutoka LVBC
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Magu.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe. Salum A. Kalli kwenye ukaguzi wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Victoria uliopo Walayani humo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiongea na baadhi ya wananchi wa Magu (hawapo pichani) waliojitokeza kwenye ziara yake ya ukaguzi wa mradi.


 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akielekeza jambo kwa Watendaji alipotembelea eneo la Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi uliopo wilayani Magu, Mwanza.

Thursday, April 8, 2021

MAPOKEZI YA NAIBU KATIBU MKUU KATIKA MAKAO MAKUU YA WIZARA – DODOMA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab leo amewasili katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara zilizopo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma na kupolewa na Watumishi na Menejimenti ya Wizara.

Balozi Fatma Rajab baada ya mapokezi hayo alipata wasaha wa kuongea na Wakuu wa Idara na Vitengo ambapo licha yakuwataka kuendelea kufanya kazi kwa weledi na juhudi amewaahidi ushirikiano katika kuteleza majumu yao ya kila siku. 

Balozi Fatma aliapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki tarehe 6 Aprili, 2021.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akipokelewa Wizarani Mtumba, jijini Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akisalimiana na Balozi Anisa Mbega alipowasili Wizarani. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akisalimiana na Balozi Stephen P. Mbundi wakati anapokelewa Wizarani.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi na Menejimenti ya Wizara mara baada ya mapokezi ya kukaribishwa Wizarani.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akisaini kitabu cha wageni alipowasili Wizarani
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab akiongea na Watumishi na Menejimenti ya Wizara (hawapo pichani) mara baada ya kuwasili Wizarani

Tuesday, April 6, 2021

MAPOKEZI YA KATIBU MKUU, NAIBU KATIBU MKUU KATIKA OFISI NDOGO ZA WIZARA - DAR

 Na Mwandishi wetu, Dar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameendelea kumuamini Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika nafasi ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Ibuge aliteuliwa Februari 06, 2020 kuwa katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki nafasi anayoendelea kuishikilia mpaka sasa.

Kabla ya wadhifa huo, Balozi Ibuge alikuwa Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocal) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuapisha Balozi Fatma Mohammed Rajab kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Fatma aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Qatar Desemba 03, 2016 nafasi aliyokuwa akiishikilia hadi alipoteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (Hayupo Pichani) akimuapisha Balozi Fatma Mohammed Rajab kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo Ikulu Jijini Dar es Salaam



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab wakipokelewa na baadhi ya watumishi katika Ofisi Ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab mara baada ya kuwasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Wizara wakati wa mapokezi katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 



  

 

Thursday, April 1, 2021

WAZIRI NA NAIBU WAKE WAWASILI WIZARANI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula akiwasili katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma muda mfupi baada kula kiapo cha kutumikia nafasi hiyo. Mhe. Balozi Mulamula na Naibu wake Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk wamepokelewa na Watumishi na Wakuu wa Idara na Vitengo wakiongozwa Katibu Mkuu Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula akikaribishwa Wizarani muda mfupi baada ya kula kiapo cha kutumikia nafasi hiyo

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akikaribishwa Wizarani muda mfupi baada ya kula kiapo cha kutumikia nafasi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula na Naibu wake Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk wakisikiliza maelezo ya Katibu Mkuu Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge mara baada ya kuwasili Wizarani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula akiongea na Watumishi na Menejimenti ya Wizara (hawapo pichani) mara baada ya kuwasili Wizarani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula akisaini kitabu cha wageni alipowasili Wizarani
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisaini kitabu cha wageni alipowasili Wizarani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula na Naibu wake Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi, Menejimenti na Viongozi wa Wizara mara baada ya mapokezi ya kuwakaribisha Wizarani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula na Naibu wake Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi, Menejimenti na Viongozi wa Wizara mara baada ya mapokezi ya kuwakaribisha Wizarani.

 

WAZIRI NA NAIBU WAZIRI WATEULE WAAPA KUWA WABUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA



Waziri Mteule wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberatha Mulamula akiapa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Naibu Waziri Mteule wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiapa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania