Wednesday, May 26, 2021

TANZANIA, KENYA WAJADILI VIKWAZO VISIVYO VYA KIFORODHA

 Na Mwandishi wetu, Arusha

Timu ya wataalamu kutoka Tanzania imekutana na timu ya wataalamu kutoka Kenya Jijini Arusha kujadili njia za kuondoa vikwazo visivyo vya kibiasha baina ya Nchi hizo kwani vimekuwa vikiathiri biashara, mkutano wa leo Mei 26, 2021 ni maandalizi ya mkutano wa Mawaziri wa Biashara wa pande zote mbili utakaofanyika tarehe 29 Mei 2021.

Mkutano wa leo utafuatiwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 28 Mei 2021 na baadaye mkutano wa Mawaziri  tarehe 29 Mei 2021. Mkutano huo utahitimishwa kwa mawaziri wa Kenya na Tanzania kufanya ziara katika mpaka wa Namanga tarehe 30 Mei, 2021 kujionea shughuli za biashara zinavyofanyika katika mpaka huo.

Ujumbe wa Tanzania katika timu wataalam umeongozwa na Mkurugenzi wa Mtangamano wa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Ally Gugu wakati ujumbe wa Kenya umeongozwa na Bw. Michael Mandu, Mkuu wa Biashara baina ya Nchi na Nchi, Idara ya Maendeleo ya Biashara na Ujasiriamali.  

Mkutano wa wataalamu umetoa fursa ya kujadili masuala yote yanayokwamisha biashara baina ya pande zote mbili ambapo masuala yaliyowasilishwa na Kenya kujadiliwa ni pamoja na kutotoa upendeleo kwa sigara, maziwa, bidhaa za nyama, kutoka Kenya, tozo ya kuingia kwa wafanyabiashara (business pass) kufanya kazi za muda mfupi za kitaalamu. 

kwa upande wa Kenya, baadhi ya masuala ambayo Tanzania imewasilisha kujadiliwa ni kuongezwa bei ya vinywaji baridi (uplifting) kutoka Tanzania, kutoza ushuru wa forodha bidhaa za glass, kuzuia mahindi kutoka Tanzania, bei kubwa ya ushuru wa stempu katika bia, kubadili mfumo wa uingizaji mizigo mikubwa ambapo gharama za uingizaji mizigo Kenya zimeongezeka na kuathiri biashara.

Katika kutekeleza maagizo ya Wakuu wa nchi (Tanzania na Kenya) mawaziri wa seka husika kutoka watakutana na kujadili juu ya vikwazo hivyo katika mkutano wao utakaofanyika tarehe 29 Mei, 2021 jijini Arusha. 

Tarehe 4 – 5 Mei, 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alifanya ziara rasmi nchini Kenya ambapo katika ziara hiyo Mhe. Samia Hassan Suluhu na Mwenyeji wake Mhe. Uhuru Kenyatta pamoja na mambo mengine, walielekeza Mawaziri wa Biashara wa pande zote wakutane na kujadili vikwazo vya kibiashara ambavyo vinaathiri biashara kwa lengo la kuviondoa.

Mwenyekiti wa timu ya majadiliano ambae ni Mkurugenzi wa Mtangamano wa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara – Tanzania, Bw. Ally Gugu akiongea na washiriki (hawapo pichani) wakati wataalamu hao walipokutana leo Jijini Arusha kujadili njia za kuondoa vikwazo visivyo vya kibiasha baina ya Tanzania na Kenya. Kulia ni mwenyekiti mwenza kutoka Kenya ambae ni Mkuu Kitengo cha Biashara baina ya Nchi na Nchi, Idara ya Biashara na Maendeleo ya Ujasiriamali Bw. Michael Mandu.


Sehemu ya ujumbe wa Tanzania ukifutilia mkutano wa madajiliano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kiforodha


Sehemu ya ujumbe wa Tanzania ukifutilia mkutano wa madajiliano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kiforodha

Sehemu ya ujumbe wa Kenya ukifutilia mkutano wa madajiliano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kiforodha




Timu ya wataalam kutoka Tanzania na Kenya wakifuatilia mkutano wa madajiliano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kiforodha



Monday, May 24, 2021

MKUTANO WA SCTIFI WAANZA JIJINI ARUSHA

 Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda na Uwekezaji (SCTIFI) kwa ngazi ya wataalamu umeanza leo jijini Arusha ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa tarehe 28 Mei 2021.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo umetoa fursa kwa wataalamu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili utekelezaji wa maamuzi ya awali ya SCTIFI, ripoti ya baraza la mawaziri wa fedha, ripoti ya kamati ya sekta ya forodha na ripoti ya kamati ya kisekta ya biashara.

Mengine yaliyojadiliwa ni utekelezaji wa uamuzi wa mkutano juu ya EAC-EU EPA, ripoti ya kamati ya viwango ya Afrika Mashariki, ripoti  kuhusu masuala ya ushindani, ripoti ya kamati ya sekta ya uwekezaji pamoja na biashara nyingine.

Aidha, Mkutano wa Baraza la Mawaziri kwa ngazi ya wataalamu utafanyika kuanzia leo (Jumatatu 24 hadi 26 Mei, 2021 na kufuatiwa na mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu tarehe 27 Mei 2021 na baadae tarehe 28 Mei 2021 kufanyika mkutano wa Baraza la Mawaziri.


Mbali na mkutano wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la biashara, viwanda na uwekezaji (SCTIFI), pia Mkutano baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kenya utakaofanyika jijini Arusha, kuanzia 26 hadi 30 Mei, 2021 kwa lengo la kutatua Vikwazo vya Kibiashara.


Mkutano huu ni maelekezo ya Wakuu wa Nchi na Serikali katika ziara ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoifanya nchini Kenya tarehe 04 hadi 05 Mei, 2021.


Jumuiya ya Afrika Mashariki inaundwa na nchi wanachama sita ambazo ni Burundi, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Tanzania na Uganda.



Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda na Uwekezaji (SCTIFI) kwa ngazi ya wataalamu, ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi, Wizara ya Afrika Mashariki na Maendeleo ya Kikanda kutoka Kenya, Bw. Edward Owango akiongea na washiriki wa mkutano (hawapo pichani). Mkutano huo umeanza leo Jijini Arusha na kuhudhuriwa na wataalamu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Biashara,Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji, kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Benard Haule akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda na Uwekezaji (SCTIFI) kwa ngazi ya wataalamu 


Sehemu ya washiriki wakifuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda na Uwekezaji (SCTIFI) kwa ngazi ya wataalamu ulioanza leo Mei 24, 2021 jijini Arusha


Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda na Uwekezaji (SCTIFI) kwa ngazi ya wataalamu ulioanza leo jijini Arusha



Friday, May 21, 2021

MAONESHO YA PILI YA KAZI ZA SANAA ZA TANZANIA YAFUNGULIWA JIJINI HONG KONG, CHINA.

Maonesho ya Pili ya Kazi za Sanaa za Tanzania yamefunguliwa tarahe 21 Mei, 2021 jijini Hong Kong nchini China. Hafla ya ufunguzi wa maonesho hayo ilihudhuriwa na Jumuiya ya Wanadiplomasia na wafanyabiashara wa jijini Hong Kong


Katika hotuba yake ya Ufunguzi aliyoitoa kwa njia ya mtandao kutoka Beijing, Balozi wa Tanzania Nchini China ameeleza kwamba Tazania na China zimekubaliana kukuza mahusiano ya kitamaduni na sanaa na ili kuendelea kutoa fursa za kiuchumi kwa wasanii. 

Vilevile Balozi Kairuki ametumia fursa hiyo kuwaalika watalii kutoka China kutembelea Tanzania kujionea vivutio vya kiutamaduni na kazi za sanaa.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania jijini Hong Kong Ndugu Eddie Leung ameeleza kwamba Ofisi yake itaendelea kukuza mahusiano baina ya Tanzania na Hong Kong kupitia sanaa, utalii na biashara.

Aidha, Ndugu LEUNG ameahidi kuendelea kufadhili programu za mafunzo ya Uongozi kwa vijana wa kitanzania jijini Hong Kong. Mwaka 2019, Ndugu Leung alifadhili ziara ya mafunzo ya uongozi jijini Hong Kong kwa vijana 20 kutoka Tanzania.
Baadhi Wanadiplomasia na wafanyabiashara wa jijini Hong Kong wakikata utepe kwenye ufuguzi wa maonesho ya pili ya kazi ya sanaa za Tanzania zinazofanyika katika Jiji hilo.

Baadhi Wanadiplomasia na wafanyabiashara wa jijini Hong Kong wakiangalia kazi mbalimbali sanaa kwenye maonyesho yanayoendelea  jijini Hong Kong

Baadhi Wanadiplomasia na wafanyabiashara wa jijini Hong Kong wakisikiliza Hotuba ya Ufunguzi  ya Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki




RAIS MSTAAFU MHE. KIKWETE AONGOZA KONGAMANO LA MIAKA 40 YA SADC

Na Mwandishi wetu

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete ameongoza Kongamano la Maadhimisho ya miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kutoa uzoefu na mchango wa Tanzania katika Jumuiya hiyo.

Rais Kikwete amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa SADC ni kupunguza utegemezi, kukuza ushirikiano utakaojenga mtangamano wa kikanda, kuhamasisha utekelezaji wa sera za mipango ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za pamoja katika mpango wa maendeleo na mpango wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama.

“Maadhimisho haya yanaadhimishwa na nchi zote wanachama wa SADC kwa lengo la kutoa fursa ya kuangalia na kutambua malengo, mchango na fursa zilizopo katika nchi wananchama wa SADC,“ amesema Dkt. Kikwete.

Dkt. Kikwete ameongeza kuwa wapigania uhuru kutoka nchi nyingi za Afrika wanaendelea kuikumbuka Tanzania kutokana na mchango mkubwa wa kuanzisha harakati za kuzikomboa nchi nyingine kutoka katika utawala wa kikoloni ikiwa ni pamoja na Tanzania kuwapatia mbinu za kupambana na Wakoloni.

Awali, akiwasilisha salamu za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Mhe. Waziri, Balozi Liberata Mulamula (Mb), Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amesema kuwa maadhimisho ya miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja na masuala mengine, yanalenga kuenzi mchango mkubwa wa Viongozi Wakuu waanzilishi wa SADC ambao maono yao yaliweka msingi wa ukombozi wa kisiasa na kiuchumi kwa Kanda ya Kusini mwa Afrika; na Kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu mtangamano wa SADC na faida za uanachama wetu kwenye Jumuiya hii ikiwa ni pamoja na fursa zilizopo katika nyanja mbalimbali ili waweze kuzichangamkia.

“Tunapoadhimisha miaka 40 ya SADC hatuwezi kamwe kuepuka kuzungumzia mchango mkubwa uliotolewa na Tanzania kwenye Jumuiya hii.  Itakumbukukwa kuwa, Tanzania wakati wa uongozi wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilifanya kazi kubwa ya kusaidia harakati za ukombozi hususan kwa nchi za Kusini mwa Afrika. Kadhalika, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa Kwanza wakati wa SADCC kabla ya kubadilishwa kuwa SADC mwaka 1992,” amesema Balozi Sokoine.

Ameongeza kuwa, Uenyekiti wa Tanzania katika SADC kama ilivyokuwa kwa miaka ya nyuma, ulikuwa wa mafanikio kwa nchi na kwa Kanda kwa ujumla. Miongoni mwa mafanikio makubwa tunayojivunia ni kuridhiwa kwa Lugha yetu ya Taifa, Kiswahili kuwa miongoni mwa Lugha nne za SADC.

“Ili SADC itimize malengo iliyojiwekea ya kuwa Jumuiya yenye amani, usalama, ustawi na maendeleo kama ilivyoelezwa kwenye Dira ya SADC ya mwaka 2050  na Mpango Mkakati wa Maendeleo wa Kanda 2020 - 2030 kila mdau lazima atimize wajibu wake umpasao,” amesema Balozi Sokoine.

Nae Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda amesema kuwa nchi wanachama nyingine zinakiri na kutambua mchango wa Tanzania katika harakati za kuzikomboa kutoka kwenye utawala wa kikoloni.

“Nchi hizo zimekuwa zinakiri kuwa bila Tanzania kuzisaidia zingechelewa kupata uhuru ikiwemo Afrika Kusini ambayo katika jitihada za kutafuta Uhuru wake ilimwaga damu,” amesema Mhe. Makinda.

Pamoja na hayo Mhe. Makinda amesema kuwa mchango wa Hayati Mwalimu Julius Nyeyere utaendelea kukumbukwa daima na nchi wananchama wa SADC.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akiwasilisha mada kuu kwa washiriki (hawapo pichani) katika Kongamano la Maadhimisho ya miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika: Uzoefu wa Tanzania 


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwasilisha salamu za Wizara kwa washiriki (hawapo pichani) katika kongamano la maadhimisho ya miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula. Kongamano hilo limefanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 


Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akiwasilisha mada kuu kwa washiriki wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC): Uzoefu wa Tanzania 


Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda akichangia mchango wa Tanzania katika historia ya SADC wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam


Kongamano la miaka 40 ya SADC likiendelea


Washiriki wakifuatilia Kongamano la miaka 40 ya SADC likiendelea



Thursday, May 20, 2021

SERIKALI: MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI NI SALAMA

 Na Mwandishi wetu, Dar

Serikali imesema mwamko wa biashara na uwekezaji ni mkubwa kwa sasa baada ya baadhi ya makampuni na taasisi zilizokuwa zimefunga shughuli zao kuanza kurejea na kwamba serikali kwa sasa inapitia upya sera yake ya uwekezaji ili kuweka mazingira bora Zaidi ya biashara na uwekezaji.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul Jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kuhusu kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara yanakuwa rafiki.

“Mwamko wa biashara na uwekezaji ni mkubwa kwa sasa baada ya baadhi ya makampuni na taasisi zilizokuwa zimefunga shughuli zao kuanza kurejea na kwamba serikali kwa sasa inapitia upya sera yake ya uwekezaji ili kuweka mazingira bora na salama zaidi ya biashara na uwekezaji,” amesema Balozi Mulamula.

Balozi wa Uholanzi hapa Nchini Mhe Jeroen Verheul amekiri kuwa Tanzania ina fursa na rasilimali nyingi zinazohamasisha na kuvutia biashara na uwekezaji licha ya uwepo wa maeneo machache yanayohitaji maboresho ambayo yakifanyiwa kazi ipasavyo makampuni mengi kutoka Ulaya na mabara mengine yatakuja kuwekeza Nchini.

“Tanzania ina fursa na rasilimali nyingi za uwekezaji licha ya uwepo wa maeneo machache yanayohitaji maboresho ambayo yakifanyiwa kazi ipasavyo kampuni nyingi kutoka Ulaya na mabara mengine na hata hapa Tanzania zitakuja kuwekeza kwa wingi,” amesema Balozi Verheul 

Balozi huyo ameongeza kuwa kupitia kauli mbiu ya diplomasia ya uchumi nchi yake iko tayari kushirikiana na Tanzania katika kuangalia maeneo yenye changamoto na kuyatafutia ufumbuzi kwa maslahi ya pande zote mbili.

Katika tukio jingine, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amekabidhi ofisi kwa Katibu Mkuu mpya Mhe. Joseph Edward Sokoine ambapo tukio hilo limeshuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula. 

Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiteta jambo na Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul yakiendelea katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul yakiendelea katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika picha ya pamoja na Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mhe. Jeroen Verheul pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Hassan Mwamweta (mwenye tai nyekundu) na maafisa waandamizi kutoka wizarani pamoja na ubalozi wa Uholanzi



NAFASI ZA KAZI KATIKA KAMISHENI YA UMOJA WA MATAIFA INAYOSIMAMIA MASUALA YA UCHUMI BARANI AFRIKA (UNECA)

 


NAFASI ZA KAZI KWENYE KAMISHENI YA UMOJA WA AFRIKA (AUC)

 


MAKABIDHIANO YA OFISI KATI YA BALOZI BRIG. JENERALI IBUGE NA BALOZI JOSEPH SOKOINE

Na Mwandishi wetu, Dar

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambae kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amekabidhi Ofisi kwa Katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo Mhe. Balozi Joseph Edward Sokoine 

Makabidhiano ya ofisi yameshuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb).

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine akipokea ua kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati walipokuwa wanamkaribisha katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Bw. Alex Mfungo. 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine akitambulishwa kwa baadhi ya wakurugenzi wa Idara na Vitengo wa wizara na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Bw. Alex Mfungo wakati alipowasili katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine akiswasalimia baadhi ya wafanyakazi wa wizara katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkabidhi ua Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine mara baada ya kuwasili katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam kwa makabidhiano ya Ofisi. Kushoto ni aliyekuwa Katibu Mkuu Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine. katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimkabidhi ofisi Katibu Mkuu mpya Balozi Joseph Sokoine. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam. 


Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimkabidhi ofisi Katibu Mkuu mpya Balozi Joseph Sokoine. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam. 


Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge na  Katibu Mkuu mpya Balozi Joseph Sokoine wakiwa wameshikana mikono mara baada ya kukabidhiana ofisi  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Balozi Joseph Sokoine pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge mara baada ya makabidhiano ya ofisi

 

Wednesday, May 19, 2021

PAKISTAN, IRAN ZAAHIDI KUIMARISHA DIPLOMASIA YA UCHUMI

 Na Mwandishi wetu

Pakistan na Iran zimeahidi kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi mapana ya pande zote.

Ahadi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati Mabalozi wa Pakistan na Iran walipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mabalozi waliokutana na Waziri Mulamula ni Balozi wa Pakistani hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na Kaimu Balozi wa Irani hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh ambapo viongozi hao wamejadili masuala ya kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Nchi zao lakini pia kuimarisha na kuboresha diplomasia ya uchumi kwa maslahi mapana ya nchi zote.

Pamoja na mambo mengine, Balozi wa Pakistan Mhe. Saleem ameelezea kufurahishwa na uhusiano mzuri uliopo baina ya Iran na Tanzania na amepongeza hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Tanzania imeendelea kuzichukua katika kuimarisha diplomasia ya uchumi.

Nae Kaimu Balozi wa Iran amesisitiza juu ya uwekezaji na biashara ambapo amesema kuwa Serikali yake ipo tayari kufanya biashara na Tanzania na kuinua uchumi wa wananchi wan chi zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Liberata Mulamula (Mb) amewahakikishia mazingira salama ya biashara na uwekezaji na kuwaahidi ushirikiano wa kutosha kutoka Tanzania.

Kadhalika, Waziri Mulamula amesema ushirikiano wa diplomasia ya uchumi kati ya Tanzania na Pakistan unatoa fursa nyingi ikiwemo kukuza biashara hasa katika sekta ya kilimo ikiwemo chai, pamba, korosho, mbegu za mafuta, Madini ya Tanzanite, pamoja na uwekezaji.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkaribisha Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na ujumbe wake katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam


Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mhe. Mohammad Saleem akiongea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam


Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mhe. Mohammad Saleem akimuonesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula takwimu za ukuaji wa biashara kati ya Pakistan na Tanzania katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkaribisha Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh akimuelezea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimueezea jambo Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

Kikao kikiendelea 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wa Pakistan








WATANZANIA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOPATIKANA SADC


Watanzania wamehimizwa kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatina kwenye mtangamano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ikiwemo biashara, uwekezaji na soko la bidhaa mbalimbali za Tanzania ili kunufaika na Jumuiya hiyo.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 19 Mei 2021 na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe wakati akifungua rasmi Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini  mwa Afrika (SADC)  lililofanyika kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.

Mhe. Prof. Mwamfupe amesema kwamba, katika kipindi cha miaka 40 tangu kuanzishwa kwa SADC mwezi Aprili  1980, wigo wa fursa umeongezeka ambapo sasa Jumuiya imejikita katika kuwanufaisha  wananchi wake kiuchumi baada ya kukamilisha jukumu la kuzikomboa kisiasa  Nchi za Kusini mwa Afrika ambalo lilikuwa moja ya lengo la kuanzishwa kwa Jumuiya ya SADC.

Kadhalika alisema kuwa maadhimisho ya miaka 40 ambayo yamebeba kaulimbiu isemayo “Miaka 40 SADC ya Kuimarisha Amani na Usalama, Kuhamasisha Maendeleo na Ustahimilivu wa Changamoto Zinazoikabili Dunia” yanalenga pamoja na mambo mengine kuenzi mchango wa waaanzilishi wa SADC, lakini pia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu Mtangamano wa SADC na faida za uanachama wa Tanzania kwenye Jumuiya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwaeleza wananchi fursa zinazopatikana za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Pia aliongeza kuwa, maadhimisho haya yanalenga kuangazia mafanikio yaliyofikiwa pamoja na kuongeza hamasa kwa makundi mbalimbali kama vile wafanyabiashara, vijana, wanawake, makundi maalum na wananchi kwa ujumla kuchangamkia fursa za kiuchumi na kijamii zinazopatikana SADC.

“Leo tunaposherehekea miaka 40 ya SADC tunafungua wigo kwa wadau mbalimbali hususan wafanyabiasha na vijana kuwaonesha namna gani wanaweza kunufaika na Jumuiya hiyo kutoka ile ya kufundishwa darasani hadi SADC inayotuwezesha kupanga mipango yetu ya maendeleo kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara, vijana na makundi mengine. Hivyo tuna kazi kubwa moja ya kuhakikisha elimu kuhusu fursa zinazopatikana SADC inawafikia wananchi wote” alisema Prof. Mwamfupe.

Awali akizungumza kuwakaribisha Washiriki wa Kongamano hilo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Faustine Bee alisema anashukuru Chuo hicho kuwa sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya SADC kwani ni heshima kubwa kwao ambayo imewezesha wadau mbalimbali kukutana na kubadilisha mawazo ya namna ya kuiimarisha Jumuiya hiyo.

Aliongeza kusema kwamba, wakati Nchi Wanachama wa SADC zikiadhimisha miaka 40 ya Jumuiya hiyo, Chuo hicho kinatambua faida za SADC kwani tayari kinashirikiana na Nchi za Jumuiya hiyo ambapo Tanzania kwa sasa inapokea wanafunzi kupitia ushirikiano huo. Alisema mfano mzuri ni ule uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji ambazo tayari zinashirikiana katika kubadilishana wanafunzi kupitia utaratibu wa TAMOSE (Tanzania –Mozambique Students Exchange Program) ambapo tayari wanafunzi kutoka Msumbiji wanasoma UDOM na Vyuo vingine hapa nchini na vivyo hivyo wapo wanafunzi kutoka Tanzania wanaosoma nchini Msumbiji.

Kadhalika alisema, Chuo hicho ambacho kinapokea wanafunzi kutoka Nchi zingine za SADC kama Comoro, Afrika Kusini, Zambia, Malawi, DRC na zingine kimejiwekea malengo ya kuingia kwenye vyuo bora 20 katika Afrika kufikia mwaka 2030. Alisisitiza kuwa, lengo hilo litafanikiwa endapo Chuo kitapokea wanafunzi wengi kutoka nje ya nchi ikiwa ni moja ya kigezo  cha kupima ubora wa chuo na alitoa ombi kwa Serikali kukisaidia Chuo hicho kuongeza wanafunzi kupitia ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na nchi zingine na ule wa kikanda na kimataifa.

Wakati wa Kongamano hilo, ambalo limeandaliwa kwa uratibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa ikiwemo “Kuimarisha Amani na Usalama katika Kukabiliana na Changamoto za Ulimwengu” iliyowasilishwa na Mkuu wa Chuo cha Diplomasia Mstaafu, Dkt. Mohammed  Maundi na mada isemayo          “Kuhamasisha Maendeleo na Uhimilivu katika kukabiliana na Changamoto za Ulimwengu” ambayo iliwasilishwa na  Mhadhiri na Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Ajali Mustafa.

Viongozi wengine walioshiriki Kongamano hilo ni Mkuu wa Chuo cha Mipango, Prof. Hozen Mayaya, Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo, Dkt. Michael Msendekwa, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma anayeshughulikia Taaluma, Prof. Alexander Makulilo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agnes Kayola. Pia, kongamano lilihudhuriwa na Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Mipango na Chuo cha Serikali za Mitaa kilichopo Hombolo jijini Dodoma.


Mgeni Rasmi ambaye ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akifungua rasmi Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) tarehe 19 Mei 2021. Kongamano hilo ambalo liliandaliwa chini ya uratibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lilihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wanafunzi kutoka UDOM na Vyuo vingine vya Dodoma. 

Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma (UDOM), Prof. Faustine Bee akiwakaribisha Washiriki wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC Chuoni hapo

Mkuu wa Chuo cha Diplomasia Mstaafu, Dkt. Mohammed Maundi akiwasilisha mada kwa Washiriki kuhusu Kuimarisha Amani na Usalama katika Kukabiliana na Changamoto za Ulimwengu wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC lilifanyika UDOM

Mhadhiri Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Ajali Mustafa nae akiwasilisha mada kuhusu Kuhamasisha Maendeleo na Uhimilivu katika Kukabiliana na Changamoto za Ulimwengu wakati wa Kongamano la kuadhimisha miaka 40 ya SADC.

Sehemu ya Washiriki waliohuria Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Agnes Kayola, Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo, Dkt. Michael Msendekwa  na Mkuu wa Chuo cha Mipango, Prof. Hozen Mayaya 

Sehemu nyingine ya Washiriki wa Kongamano

Washiriki wa Kongamno wakiwemo wahadhiri wakifuatialia uwasilishwaji wa mada mbalimbali

Sehemu ya Wanafunzi wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 40 ya SADC

Sehemu nyingine ya Washiriki

Washiriki wa Kongamano la maadhimisho ya miaka 40 ya SADC kama wanavyoonekana pichani

Sehemu nyingine ya washiriki

Waandishi wa Habari wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 40 ya SADC

Washiriki kama wanavyoonekana pichani

Mmoja wa Wahadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma akichangia jambao wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC

Mmoja wa Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma akiuliza swali wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC

Mwanafunzi kutoka Chuo cha Mipango nae akichangia jambo wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 40 ya SADC

Picha ya pamoja

Meza Kuu katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali