Friday, June 25, 2021

MKUTANO WA 14 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI WA KILIMO NA USALAMA WA CHAKULA WA EAC WAFANYIKA ARUSHA

Mkutano wa 14 Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umefanyika leo tarehe 25 Juni 2021 jijini Arusha huku Mawaziri wakikubaliana kuendelea kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali ya kilimo ili kujihakikishia usalama wa chakula kwa wananchi wote Afrika Mashariki.

 

Mkutano huo ambao ulitanguliwa na mikutano ya Wataalam na Makatibu Wakuu iliyofanyika jijini hapa kuanzia tarehe 21 hadi 24 Juni 2021, ulilenga kupitia na kujadili utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya Baraza la Mawaziri wa Jumuiya pamoja na kupitia na kujadili masuala mbalimbali  muhimu ya kisera, kimkakati, miradi na program zinazotekelezwa katika sekta ya kilimo.

 

Aidha, Mawaziri hao wamepokea na kujadili agenda mbalimbali zilizowasilishwa kwao na Makatibu Wakuu kama vile Taarifa ya Usalama wa Chakula ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; Taarifa kuhusu Mradi wa Afrika wa Kilimo cha Ushindani cha Mpunga kwa Kanda ya Afrika Mashariki; Taarifa kuhusu Maendeleo ya Mifugo; Taarifa kuhusu Mradi wa Kuzuia na Kudhibiti Sumukuvu; Taarifa kuhusu Maendeleo ya Uvuvi; na Taarifa kuhusu Uhamasishaji wa Uchangiaji Rasilimali.

 

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Mawaziri umeongozwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Prof. Adolf Mkenda na kuhudhuriwa pia na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki, Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Mhe. Soud Nahodha Hassan, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Andrew Massawe, Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatama pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Sekta mbalimbali zinazojishughulisha na masuala ya kilimo na usalama wa chakula hapa nchini. 

Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza  wakati wa Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021
Mhe. Prof. Mkenda akisaini Ripoti ya Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021


Mhe. Prof. Mkenda (kushoto) akiwa na Mawaziri wengine wa Tanzania walioshiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021. Kulia ni Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Mhe. Soud Nahodha Hassan na katikati ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Mawaziri ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Ushirika wa Kenya, Mhe. Lawrence Angolo akizungumza wakati wa Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Ujumbe wa Burundi ukishiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Sehemu ya ujumbe wa Kenya ukiwa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Kenya katika Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu Tanzania, Bw. Patrick Ngwediadi akiwa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021 

Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Benjamin Mwesiga akishiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021 pamoja na Bibi Jackline Mpuya kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa

Sehemu ya washiriki wakifuatilia Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Sehemu ya ujumbe wa Tanzania wakishiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Mtendaji Mkuu wa Mpango wa Kuboresha Kilimo Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini (SAGCOT), Bw. Geoffrey Kirenga (kulia) akiwa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Mkutano ukiendelea

Maafisa Waandamizi wakiwa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha tarehe 25 Juni 2021

Picha ya pamoja



 

Thursday, June 24, 2021

MAKATIBU WAKUU WA EAC WANAOSIMAMIA SEKTA YA UCHUKUZI, MAWASILIANO, NA HALI YA HEWA WAKUTANA DAR ES SALAAM.


Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano, na Hali ya Hewa (TCM) la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu umefanyika leo tarehe 24 Juni, 2021 jijini Dar es Salaam. Makatibu Wakuu hao wamekutana, sambamba na masuala mengine kukamilisha maandalizi ya mwisho kuelekea Mkutano wa Mawaziri unaotarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 25 Juni, 2021. 

Katika Mkutano huo Mkatibu Wakuu, wamepokea, kupitia na kujadili taarifa ya utekelezaji wa programu, mikakati, miradi, maelekezo na maauzi yaliyotolewa katika Mikutano ya awali ya Sekta hiyo. Vilevile, Makatibu Wakuu hao wamepitia na kujadili agenda zitakazo jadiliwa na Mawaziri katika mkutano wao unaotarajiwa kufanyika hapo kesho. Agenda hizo ni pamo na; kujadili kuhusu mapendekezo ya Taasisi ya Afrika Mashariki juu kuratibu programu za maendeleo katika Sekta ya Mawasiliano; kuangalia hatua ya maendeleo iliyofikiwa ya utekelezaji wa miradi na programu katika sekta ndogo ya barabara, reli, usafiri wa anga, usafiri wa majini, hali ya hewa na mawasiliano. 

Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Mwenyekiti ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Miundombinu na Huduma kutoka Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki ya nchini Kenya Bw. Charles Ngunjiri amesema Jumuiya ya Afrika imepiga hatua kubwa katika ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa biashara na kurahisha upatikanaji wa huduma mbalimbali katika ya Jumuiya. Aliongeza kutoa rai kwa wajumbe wa mkutano kutumia vyema mkutano huo kutoa michango ya kujenga zaidi itakayo endelea kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Jumuiya katika sekta ya Uchukuzi, Mawasiliano, na Hali ya Hewa. 

Katika Mkutano huu wa ngazi ya Makatibu Wakuu, kwa upande wa Tanzania umehudhuriwa na Ndg. Mussa Haji Ali, Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais – Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Zanzibar na Ndg. Amour Hamil Bakari, Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Zanzibar.

Mkutano ukiendelea

Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Bw. Eliabi Chodota akifuatilia Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano, na Hali ya Hewa ngazi ya Makatibu Wakuu uliokuwa ukiendelea katika Hoteli ya Four Points jijini Dar es Salaam.
Meza kuu ikiongoza majadilino kwenye Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano, na Hali ya Hewa ngazi ya Makatibu Wakuu uliokuwa ukiendelea katika Hoteli ya Four Points jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania wakifuatilia Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano, na Hali ya Hewa ngazi ya Makatibu Wakuu uliokuwa ukiendelea katika Hoteli ya Four Points jijini Dar es Salaam


MAKATIBU WAKUU WA SEKTA YA KILIMO NA USALAMA WA CHAKULA WA EAC WAKUTANA JIJINI ARUSHA

Mkutano wa 14 Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Ngazi ya Makatibu Wakuu umefanyika leo tarehe 24 Juni 2021  jijini Arusha ikiwa ni maandalizi ya mwisho kuelekea Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika jijini hapa tarehe 25 Juni 2021.

 

Lengo la Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo  na Usalama wa Chakula pamoja na mambo mengine ni kupitia na kujadili utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya Baraza la Mawaziri wa Jumuiya pamoja na kupitia na kujadili masuala mbalimbali  muhimu ya kisera, kimkakati, miradi na program zinazotekelezwa katika sekta ya kilimo.

 

Katika Mkutano wao, Makatibu Wakuu, pamoja na mambo mengine wamepokea na kupjadili agenda mbalimbali zilizowasilishwa kwao na Wataalam ikiwemo, Taarifa ya Usalama wa Chakula ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; Taarifa kuhusu Mradi wa Afrika wa Kilimo cha Ushindani cha Mpunga kwa Kanda ya Afrika Mashariki; Taarifa kuhusu Maendeleo ya Mifugo; Taarifa kuhusu Mradi wa Kuzuia na Kudhibiti Sumukuvu; Taarifa kuhusu Maendeleo ya Uvuvi; na Taarifa kuhusu Uhamasishaji wa Uchangiaji Rasilimali.

 

Awali akifungua Mkutano huo, Mwenyekiti ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Ushirika wa Kenya, Prof. Hamadi Iddi Boga ametoa rai kwa wajumbe wa mkutano huo kuendelea kushirikiana katika kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo kwenye jumuiya  ili kujihakikishia usalama wa chakula.   

 

Amesema kuwa changamoto nyingi za kilimo zinazozikabili nchi wanachama  zinafanana hivyo ni vizuri nchi zote zikajikita kufanyia kazi changamoto hizo pamoja na kutekeleza program na maazimio yanayofikiwa kwenye mikutano mbalimbali ili hatimaye kuboresha sekta ya kilimo na usalama wa chakula ambayo ni muhimu kwa ustawi wa wananchi.

“Nawashukuru sana kwa kuja na kushiriki kwenye mkutano huu muhimu. Naelewa kwamba usalama wa chakula ni jukumu letu sote kama nchi wanachama na kwa vile tunapitia changamoto zinazofanana ikiwemo mabadiliko ya tabianchi na corona ni vizuri tukaja na mbinu za pamoja kuzikabili changamoto hizo na kuendeleza sekta hii muhimu ya kilimo” alisema Prof. Boga.

 

Katika hotuba yake ililiyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Sekta za Uzalishaji katika Sekretarieti, Bw. Jean Havugimana,  Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughilikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Mhe. Christophe Bazivamo amewashauri wafanyabiashara wa mazao ya kilimo katika Nchi Wanachama kushirikiana na mamlaka zinazosimamia usalama wa chakula na viwango ili kupata ushauri wa kitaalam kwa ajili ya kuzalisha bidhaa salama na zenye ushindani katika soko. Kadhalika ameshauri elimu kuhusu kilimo itiliwe mkazo kwa nchi wanachama ili kuzalisha wataalam wengi kwenye sekta hii na pia kukuza ajira kwa vijana ambao ni kundi kubwa zaidi katika nchi wanachama.

 

Kwa upande wake, mwenyeji wa Mkutano huo ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo wa Tanzania, Dkt. Andrew Massawe amewakaribisha na kuwashukuru wajumbe waliosafiri kutoka kwenye nchi zao hadi jijini Arusha licha ya changamoto ya ugonjwa wa Corona  na kuwatakia mkutano mwema na wenye manufaa kwa wananchi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Ngazi ya Makatibu Wakuu umeongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Andrew Massawe na kuhudhuriwa pia na Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatama pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Sekta mbalimbali zinazojishughulisha na masuala ya kilimo na usalama wa chakula hapa nchini. 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Andrew Massawe (kushoto) akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika jijini Arusha tarehe 24 Juni 2021 kwa ajili ya kuandaa Mkutano wa 14 wa Baraza la Kiseikta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika jijini hapa tarehe 25 Juni 2021.  Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatama.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Makatibu Wakuu ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Ushirika wa Kenya, Prof. Hamadi Iddi Boga akifungua Mkutano huo uliofanyika jijini Arusha tarehe 24 Juni 2021 kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya Mkutano wa 14 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika tarehe 25 Juni 2021.

Mkurugenzi wa Sekta ya Uzalishaji katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Jean Havugimana akizungumza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Mhe. Christophe Bazivamo wakati wa Mkutano wa Makatibu Wakuu

Sehemu ya ujumbe wa Kenya ukishiriki Mkutano wa Makatibu Wakuu 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Andrew Massawe akiwa kwenye Mkutano wa Makatibu Wakuu. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatama na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu Tanzania, Bw. Partick Ngwediadi

Kiongozi wa ujumbe wa Burundi kama anavyoonekana puchani

Sehemu ya ujumbe wa sekretarieti katika mkutano

Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Benjamin Mwesiga akishiriki Mkutano wa Makatibu Wakuu pamoja na Bibi Jackline Mpuya kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa.

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania wakishiriki mkutano wa Makatibu Wakuu wanaoshughulikia sekt aya kilimo na usalama wa chakula

Ujumbe wa Tanzania wakiwa kwenye mkutano

Mkutano ukiendelea

Wajumbe wakifuatilia matukio mbalimbli kwenye Mkutano

Wajumbe kutoka Sekta za kilimo na usalama wa chakula wakishiriki Mkutano wa Makatibu Wakuu 

Mkutano ukiendelea

Wadau wa kilimo wakiwa kwenye mkutano 

Mkutano ukiendelea

 

Wednesday, June 23, 2021

BALOZI MBAROUK AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA POLAND

 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (katikati) akisalimiana na Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski alipowasili ofisini kwake jijini Dodoma

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (katikati)  akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski (kushoto) wakizungumza kulia ni  Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Abdallah Possi .

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski walipokutana kwa  mazungumzo ofisini kwake jijini Dodoma

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk walipokutana kwa mazungumzo ofisini kwake jijini Dodoma

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Abdallah Possi (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika Bw. Hassan Mwamwetta waifuatilia mazungumzo kati ya Mawaziri hao.

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk walipokutana kwa mazungumzo ofisini kwake jijini Dodoma. Kulia kwa Mhe. Waziri Mbarouk wakishuhudia massikilizo hayo ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Abdallah Possi na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika Bw. Hassan Mwamwetta.




Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayeshughulikia na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski ofisini kwake jijini Dodoma.

Akiongelea kikao hicho Balozi Mbarouk amesema kuwa wamejadiliana juu ya kuimarisha mahusiano yaaliyopo kati ya Tanzania na Poland ikiwa ni pamoja na kuanzisha uwekezaji mpya nchini, kuwezesha wanafunzi na wataalamu wetuu kujifunza na kupata utaalmu hasa katika matibabu ya moyo, masikio, pua na Koo.

“Tumekutana hapa na Mhe Naibu Waziri kutoka nchini Poland, tumezungumza na kujadliana juu ya namna bora za kuendelea kuimarisha mahusiano baina ya nchi zetu , tuna maeneo mengi ambayo tunashirikiana baina ya nchi zetu, lakini pia nimewaomba kuanzisha uwekezaji mpya nchini, ikiwa ni pamoja na kutoa nafasi za masomo kwa ameneo ya matibabu ya moyo, masikio,pua na koo”, amesema Balozi Mbarouk.

Amesema kuwa wamejadiliana juu ya kuhakikisha ujenzi wa Kiwanda cha matrekta cha Kibaha na ujenzi wa maghala ya kuhifadhia nafaka na kuongeza kuwa ujio wa Naibu Waziri huyo utawezesha kukwamua miradi hiyo na hivyo kuikamilisha kama ilivyopangwa

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri huyo ameelezea utayari wa Poland katika kuhakikisha mahusiano kati ya Poland na Tanzania yanaimarika na kuendelea kuisaidia Tanzania katika sekta za elimu, kilimo hasa ikizingatiwa kuwa Poland imeendelea kwa kiasi kikubwa kupitia kilimo.

Amesema Poland iko tayari kuisaidia Tanzania kaatika maeneo ya elimu kwa kutoa nafasi za masomo nchin Poland ikiwa ni pamoja na ufadhili kwa wanafunzii wa Kitanzania, uwepo wa mifumo ya kisasa ya kutolea maji taka, kilimo na maendeleo ya usalama wa chakula.

Naibu Waziri huyo. Mhe. Powel yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku nne ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dkt. Abdallah Possi pamoja na Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka nchni Poland waliobobea katika maeneo ya teknolojia ya kisasa katika sekta za kibenki (smart teknologies) teknolojia ya kisasa katika sekta ya umeme (smart technologies for electricity sector -smart meter connection and lighting systems) na ulipaji kwa kutumia teknolojia za kisasa (smart payment apps).

Naibu Waziri huyo na timu wanatarajia kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Shirika la Umeme nchii (TANESCO) Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Benki za CRDB na NMB na Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF).



Ziara ya naaibu Waziri huyo imefuatia mwaliko uliotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Idara ya Ulaya na Marekani




NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE WA POLAND MHE.PAWEL JABLONSKI AWASILI JIJINI DODOMA




Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski awasili jijini Dodoma kwa ziara ya kikazi.



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumaani Mhe. Dkt. Abdallaah Possi katika uwanja wa ndege jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akiwa na Balozi wa Poland nchini Mhe. Krzysztof Buzalski

Ujumbe wa wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchii Poland ulioambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika ambaye yuko nchni kwa ziara ya kikazi kufuatiaa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski awasili jijini Dodoma kwa ziara ya kikazi.

Mhe. Powel  ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dkt. Abdallah Possi pamoja na Balozi wa Poland hapa nchini Mhe. Krzysztof Buzalski. 

Naibu Waziri huyo atakutana na kufanya mazungumzo ya pamoja na watendaji wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maji, Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Uwekezaji, Kilimo na Fedha na Mipango hapa jijini Dodoma. 

Naibu Waziri huyo ameambatana na timu ya wawekezaji na wafanyabiashara  waliobobea katika maeneo ya teknolojia ya kisasa katika sekta za kibenki (smart teknologies) teknolojia ya kisasa katika sekta ya umeme (smart technologies for electricity sector -smart meter connection and lighting systems) na ulipaji kwa kutumia teknolojia za kisasa ( smart payment apps). 

Wataalamu hao wakiwa jijini Dar es Salaam watakutana na Ofisi ya Mkuu wa  Mkoa wa Dar es Salaam, TANESCO, TPSF, Benki za CRDB, NMB na NSSF



Tuesday, June 22, 2021

MKUTANO WA SADC WA BARAZA LA MAWAZIRI SADC WAENDELEA MAPUTO - MSUMBIJI


Katibu Mkuu Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine(katikati) muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC Mjini Maputo,Msumbiji. Kushoto kwa Balozi Sokoine ni Balozi Grace Martni na kulia ni Balozi Mteule Agnes Kayola 

Katibu Mkuu Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt. Stergomena Tax akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC Mjini Maputo,Msumbiji. . Kulia kwa Dkt. Tax ni Balozi Grace Martini na kushoto kwa Balozi Sokine ni Balozi Mteule Agnes Kayola
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine akifuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC unaoendelea Maputo,Msumbiji . Nyuma ya Balozi Sokoine kulia ni Balozi Grace Martini na kushoto ni Balozi Mteule Agnes Kayola

 Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ukiwa unaendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Joachim Chissano Maputo,Nchini Msumbiji