Friday, August 20, 2021

MKUTANO WA NNE WA TUME YA PAMOJA YA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA KENYA WAFANYIKA NAIROBI, KENYA.


Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya umeanza kufanyika leo tarehe 19 Agosti 2021 Jijini Nairobi, Kenya. Mkutano huu utakaofanyika kwa kipindi cha siku sita kuanzia tarehe 19 hadi 24 Agosti, 2021 unalenga kujadili mambo mbalimbali muhimu ya ushirikiano ikiwemo Mahusiano ya Kidiplomasia, Ulinzi na Utawala Bora, Uchumi na Biashara, na Masuala ya Kijamii sambamba na kuibua maeneo mapya ya ushikiano kwa lengo la kuchagiza maendeleo baina ya Tanzania na Kenya. 

Mkutano huu muhimu katika ustawi wa ushirikiano na maendeleo baina ya mataifa haya mawili, unafanyika ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya Nchini Kenya mwezi Mei, 2021, kuwa Nchi hizi mbili zifanye Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano. 

Akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano huo katika ngazi ya Wataalamu, Balozi Naimi S.H. Azizi, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amebainisha kuwa mkutano huo umetoa fursa hadhimu kwa pande zote mbili kukutana ili kuweka mipango na mikakati ya pamoja itakayoimarisha ushirikiano kwenye utekelezaji wa vipaumbele vya shughuli za maendeleo katika sekta mbalimbali kwa manufaa ya pande zote mbili. “Natambua vyema kuwa tokea Mkutano wa Mwisho wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano ulipofanyika, mengi mazuri yamefanyika baina ya Nchi zetu (Tanzania na Kenya) na kwa kupitia miogozo ya Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mathalani nilifarijka sana pale timu yetu ya Wataalamu ya Pamoja ya kudhibiti Mipaka ilipofanya Mkutano wao kwa mafanikio Juni 2021, Jijini Mombasa, Kenya. Hili linaendelea kudhihirisha utayari wa Serikali zetu wa kudumisha amani na kuleta maendeleo”. Alisema Balozi Naimi S.H. Azizi. 

Balozi Naimi S.H. Azizi aliongeza kusema kuwa ni muhimu wajumbe wa mkutano wajikite katika kujadili masuala muhimu yenye maslahi kwa pande zote mbili ili kukidhi matarajio ya Wakuu wa Nchi hizi mbili, ya kuona Wataalamu katika Serikali wanazoziongoza wanaendelea kuwajibika ipasavyo katika kuwaletea maendeleo wananchi. 

Mkutano huu umejumuisha Viongozi, Watendaji na Maafisa mbalimbali wa Serikali kutoka Tanzania na Kenya. 

Balozi Naimi S.H. Azizi (kulia) Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya   Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya uliokuwa ukiendela katika Hoteli ya Movenpick Jijini Nairobi, Kenya. 
Balozi Naimi S.H. Azizi Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya unofanyika Jijini Nairobi Kenya
Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Mhe. Dkt. John Simbachawene akifuatilia Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya uliokuwa ukiendela katika Hoteli ya Movenpic Jijini Nairobi, Kenya.
Meza Kuu wakifuatilia Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya uliokuwa ukiendela katika Hoteli ya Movenpick Jijini Nairobi, Kenya
Sehemu ya Wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya uliokuwa ukiendela katika Hoteli ya Movenpick Jijini Nairobi, Kenya

Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya ukiendelea.

Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya unaendelea Jijini Nairobi, Kenya wakiwa katika picha ya pamoja.
Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya ukiendelea.
Mhe. Ababu Namwamba, Katibu Mkuu wa Utawala katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Nne wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya unofanyika Jijini Nairobi Kenya

Monday, August 16, 2021

ISRAEL YAKOSHWA NA VIVUTIO VYA UTALII TANZANIA

 Na Waandishi wetu, Arusha

Mamia ya watalii kutoka Israel waendelea kuja nchini kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii licha ya changamoto ya Ugonjwa wa UVIKO-19 ambao umeikumba dunia hivi sasa.

Kuja kwa watalii hao kunatokana na sio tu Tanzania kubarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, bali pia hatua za tahadhali zinachokuliwa na Serikali dhidi ya maambukizi ya virusi vya UVIKO-19.

Hatua hizo ambazo zimewejengea imani watalii kuendelea kuja nchini zimetambuliwa na Baraza la Wasafiri na Utalii Duniani (World Travels and Tourism Council-WTTC) ambapo Mwezi Agosti 2020 baraza hilo liliitangaza Tanzania kuwa nchi salama ya kuitembelea.   

Akizungumza Jijini Arusha, wakati wa hafla ya kuwapokea watalii takribani 100 kutoka Israel na wengine 150 waliokuwa wanaagwa, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemedi Mgaza amesema ujio wa watalii hao umetokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Wizara ya Mambo ya Nje, kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Israel na wadau wengine wa utalii za kutangaza vivutio vya utalii nchini humo.

Juhudi hizo ni pamoja na kushiriki maonesho ya utalii yanayofanyika kila mwaka nchini Israel ambapo kwa mwaka huu yamepangwa kufanyika mwezi Oktoba, kushiriki katika vyombo vya habari mbalimbali nchini humo pamoja na kuwatumia mawakala wa utalii, kampuni za kuongoza watalii na waandishi wa habari.

Mmoja wa watalii waliokuwa wanaagwa leo, Bw. Lior Ziegler aliwahakikishia Watanzania kuwa Watalii kutoka Israel wataendelea kuja nchini kwa sababu Tanzania imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, huduma bora ikiwemo na mapokezi mazuri ya kuridhisha.

“Nimefurahia kutalii katika vivutio mbalimbali vya utalii hapa Tanzania kwa kweli ni vizuri sana…..nitaendelea kuhamasisha Waisrael kuja kutembea hapa na kujionea wenyewe vivutio hivyo adhimu,” Amesema Bw. Ziegler

Kauli hiyo imeungwa mkono na Afisa Masoko Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Bw. Michael Makombe ambapo alieleza kuwa watalii hao wamevutiwa na Bonde la Ngorongoro kutokana na mazingira yake ya upekee, wanyama kuonekana kwa urahisi pamoja na historia ya Olduvai Gorge ambapo ni eneo linaloaminika kuwa fuvu la mtu wa kale zaidi duniani limegunduliwa.

Kwa upande wa Kaimu Meneja Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bi. Christina Kamuzola amesema TTB kwa kushirikiana na Serikali na wadau kutoka sekta binafsi itaongeza juhudi za kutangaza vivutio vya utalii ili kufikia malengo ya Serikali ya kuleta watalii milioni tano na mapato ya Dola za Marekani bilioni 600 kwa mwaka ifikapo mwaka 2025 kama ilivyoainishwa katika Ilani ya CCM ya 2020-2025.

Juhudi hizi ni utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa Tarehe 27 Julai, 2021 akiwaapisha mabalozi wapya 13 na kuwaagiza pamoja na mambo mengine, kutangaza vivutio vya utalii, fursa za kiuchumi pamoja na uwekezaji zinazopatikana nchini. 

Baadhi ya watalii kutoka Israel wakipita kuangalia kikundi cha utamaduni kutoka kabila la Wamasai katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kabla ya kuondoka kurejea Israel


Baadhi ya watalii kutoka Israel wakipita kuangalia kikundi cha utamaduni kutoka kabila la Wamasai katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kabla ya kuondoka kurejea Israel


Baadhi ya watalii kutoka Israel wakipita kuangalia kikundi cha utamaduni kutoka kabila la Wamasai katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kabla ya kuondoka kurejea Israel


Baadhi ya watalii kutoka Israel wakipita kuangalia kikundi cha utamaduni kutoka kabila la Wamasai katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kabla ya kuondoka kurejea Israel


Baadhi ya watalii kutoka Israel wakiwa katika eneo la kuondokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kabla ya kuondoka kurejea Israel


Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemedi Mgaza akiongea na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) baada ya watalii kuondoka kuelekea Israel


Kaimu Meneja Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bi. Christina Kamuzola akiongea na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) baada ya watalii kuondoka kuelekea Israel

Afisa Masoko Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Bw. Michael Makombe akiongea na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) baada ya watalii kuondoka kuelekea Israel


 

Wednesday, August 11, 2021

BALOZI AGNES KAYOLA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE KIKAO CHA KAMATI YA KUDUMU YA MAKATIBU WAKUU WA SADC

 

Mratibu Mkuu wa Kitaifa wa masuala ya SADC na Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola akifuatilia majadiliano katika kikao cha Kamati ya kudumu ya Makatibu Wakuu kitakachomalizika leo jijini Lilongwe, Malawi. Nyuma yake kushoto ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Evaristo Longopa na kulia ni Bw. Edward Komba Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

 

Na mwandishi wetu , Lilongwe


Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu ni miongoni mwa vikao vya awali kuelekea Mkutano wa 41 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 hadi 18 Agosti 2021 jijini Lilongwe, Malawi.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu unaongozwa na Mratibu Mkuu wa Kitaifa wa masuala ya SADC, Balozi Agnes Kayola ambaye amemuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine.

Viongozi wengine walioambatana na  Balozi Kayola kwenye mkutano huo ni pamoja na: Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaaban ambaye ameongoza Kikao cha Kamati ya Fedha katika kikao hicho cha Makatibu Wakuu; na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Evaristo Longopa.

Aidha, mkutano huu utafuatiwa na mikutano mingine ya awali ikiwamo Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utafanyika tarehe 13 hadi 14 Agosti, 2021 na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC utakaofanyika tarehe 16 Agosti 2021 ambao utajadili hali ya ulinzi na usalama katika kanda kwa kipindi cha Agosti 2020 hadi Agosti 2021. Mkutano huu utahusisha nchi tatu (3) za SADC Organ Troika ambazo wajumbe wake ni Botswana, Mwenyekiti wa sasa wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama; Afrika Kusini, Mwenyekiti ajaye wa Organ; na Zimbabwe, Mjumbe aliyemaliza muda wa uenyekiti wa Asasi.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa ngazi ya Mawaziri utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ambaye ataambatana na Waziri wa Fedha na Mipango, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mwakilishi kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mikutano hii ya awali pamoja na mambo mengine inajukumu la kuandaa, kupitia na kuwasilisha mapendekezo ya masuala mbalimbali ya kikanda yatakayofanyiwa maamuzi kwenye Mkutano wa 41 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika utakaofanyika tarehe 17-18 Agosti 2021 jijini Lilongwe.

Mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu ulianza tarehe 9 Agosti 2021 na unatarajiwa kumalizika leo tarehe 11 Agosti 2021. Kumalizika kwa mkutano huu kunaruhusu kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).


TANZANIA KUJIPANGA KUNUNUA DOZI MILIONI 17 ZA UVIKO - 19 ILIZOTENGEWA NA UMOJA WA AFRIKA

Umoja wa Afrika umeitengea Tanzania dozi milioni 17 za chanjo za UVIKO- 19 kupitia mpango wa Umoja huo wa kuzisaidia Nchi wanachama kupata chanjo kwa ajili ya Wananchi wake.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameyasema hayo Addis Ababa Nchini Ethiopia alipokutana kwa mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania waishio Nchini Ethiopia (Diaspora) waliotaka kufahamu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na UVIKO -19 ikiwa ni pamoja na suala la chanjo.

 

Aidha Balozi Mulamula amewataka Watanzania wanaofanya kazi katika Mashirika na Taasisi mbalimbali za Kimataifa kusaidia upatikanaji dozi nyingine za chanjo ya UVIKO 19 ili kuwawezesha Watanzania wengi  kupata chanjo hiyo kutokana na  mwamko wa Watanzania kuongezeka mara  baada ya kuzinduliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Katika tukio jingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Ethiopia Mhe Sahle – Work Zewde Addis Ababa nchini Ethiopia ambapo Tanzania na Ethiopia zimekubalina kuendelea kutumia ndege za shirika la Ethiopia kutangaza vivutio na kusafirisha Watalii kutoka mataifa mbalimbali kuja Tanzania.

 

Aidha Balozi Mulamula amemhakikishia Rais Sahle – Work Zewde kuwa Tanzania itaendelea kutekeleza maeneo yote ya ushirikiano ambayo Rais Zewde alikubaliana na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ziara ya Rais huyo Chato nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na suala la kuwarejesha Nchini Ethiopia wahamiaji wanaoshikiliwa katika magereza mbalimbali.

 

Kwa upande wake Rais wa Ethiopia  Mhe. Sahle – Work Zewde amesisitiza kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Nchi hiyo hususani katika kutatua changamoto zinazozuia maendeleo miongoni mwa Mataifa hayo.

RAIS WA ETHIOPIA MHE. SAHLE - WORK ZEWDE AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI MULAMULA ADDIS ABABA - ETHIOPIA

Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle – Work Zewde akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula(Mb).

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Rais Zewde, Addis Ababa, Ethiopia 11 Agosti,2021.


Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle – Work Zewde akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula(Mb) mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi za Rais Zewde, Addis Ababa, Ethiopia 11 Agosti,2021.

Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle – Work Zewde akiwa katika ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula(Mb) mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi za Rais Zewde, Addis Ababa, Ethiopia. 11 Agosti,2021. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Naimi Azizi na Kushoto kwa Rais Zewde ni Kaimu Balozi wa Ethiopia Bi Elizabeth.
 

Tuesday, August 10, 2021

TANZANIA YASAINI MKATABA WA UANZISHWAJI WA TAASISI YA UDHIBITI WA DAWA YA UMOJA WA AFRIKA (AMA)


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Monica Nsanzabaganwa wakionesha mkataba wa Tanzania wa kukubali kuanzishwa kwa Taasisi ya Udhibiti wa Dawa ya Umoja wa Afrika (African Medicines Agency (AMA)) mara baada ya kusaini Mkataba huo tarehe 10 Agosti,2021 katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika  Addis Ababa, Ethiopia.Tanzania inakuwa Nchi ya 22 kusaini Mkataba huo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) panoja na  Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Monica Nsanzabaganwa wakionesha Mkataba wa Tanzania wa kukubali kuanzishwa kwa Taasisi ya Udhibiti wa Dawa ya Umoja wa Afrika (African Medicines Agency (AMA)) mara baada ya kusaini Mkataba huo tarehe 10 Agosti,2021 katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika  Addis Ababa, Ethiopia.Tanzania inakuwa Nchi ya 22 kusaini Mkataba huo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Monica Nsanzabaganwa wakionesha Mkataba wa Tanzania wa kukubali kuanzishwa kwa Taasisi ya Udhibiti wa Dawa ya Umoja wa Afrika (African Medicines Agency (AMA)) mara baada ya kusaini Mkataba huo tarehe 10 Agosti,2021 katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika  Addis Ababa, Ethiopia.Tanzania inakuwa Nchi ya 22 kusaini Mkataba huo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Monica Nsanzabaganwa pamoja na baadhi wajumbe kabla ya kusaini mkataba wa Tanzania wa kukubali kuanzishwa kwa Taasisi ya Udhibiti wa Dawa ya Umoja wa Afrika (African Medicines Agency (AMA)) 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe alioongozana nao katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika zilizopo Addis Ababa nchini Ethiopia mara baada ya kusaini mkataba wa Tanzania wa kukubali kuanzishwa kwa Taasisi ya Udhibiti wa Dawa ya Umoja wa Afrika (African Medicines Agency (AMA)) Tarehe 10 Agosti,2021. Tanzania inakuwa Nchi ya 22 kusaini Mkataba huo

Monday, August 9, 2021

WAZIRI MULAMULA AMUAGA BALOZI WA OMAN

  Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amemuaga Balozi wa Oman nchini, Mhe. Ally Abdallah Almahruqi katika ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini.

Balozi Mulamula amempongeza Balozi Almahruqi kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kudumisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Oman na Tanzania wakati wote wa uwakilishi wake hapa nchini.

“Tanzania tunashukuru zaidi kwa ushirikiano uliotuonesha wakati wote ulipokuwa hapa kama Balozi na tunakuahidi kuudumisha na kuuendeleza ushirikiano huo kwa maslahi ya nchi zetu mbili (Tanzania na Oman)," amesema Balozi Mulamula

Kwa upande wake Balozi wa Oman aliyemaliza muda wake wa uwakili hapa Nchini Mhe. Ally Abdallah Almahruqi ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano alioupata wakati wote alipokuwa akitekeleza majukumu yake.

“Nawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipatia wakati wote niliokuwa hapa nikitekeleza majukumu yangu kama Balozi, hakika nilifarijika sana……….naahidi kuwa nitakuwa balozi mwema kwa Serikali ya Tanzania,” amesema Balozi Almahruqi  

Pia Balozi ameipongeza Tanzania kwa hatua inazochukua za kupambana na virusi vya korona ikiwemo kuungana na mataifa mengine duniani kuchanja chanjo ya Ugonjwa wa Virusi vya Korona, UVIKO-19.

Tanzania na Oman zimekuwa zikishirikiana katika sekta mbalimbali ikiwemo uwekezaji katika madini, mafuta, gesi, kilimo, usafirishaji, utalii pamoja na biashara. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Balozi wa Oman nchini, Mhe. Ally Abdallah Almahruqi katika hafla ya kumuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Hafla ya kumuaga imefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Oman aliyemaliza muda wake wa uwakilishi nchini, Mhe. Ally Abdallah Almahruqi akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro Balozi wa Oman aliyemaliza muda wake wa uwakilishi nchini, Mhe. Ally Abdallah Almahruqi  


Thursday, August 5, 2021

BALOZI MULAMULA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA QATAR

 Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Qatar nchini Tanzania Mhe. Hussain Ahmad Al Homaid leo Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walijadili masuala ya kuimraisha uhusiano wa kidiplomasia, kuendeleza biashara na uwekezaji katika sekta za sekta za Madini, Utalii, pamoja na Mafuta na Gesi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al Homaid leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

   Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al Homaid yakiendelea

  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al Homaid leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula pamoja na Balozi wa Qatar nchini Mhe. Hussain Ahmad Al Homaid wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara pamoja na Ubalozi wa Qatar


WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA NJE YA NCHI

Na Mwandishi wetu, Dar

Watanzania wamepewa changamoto ya kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana Nje ya Nchi ili waweze kuinua uchumi wao pamoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Changamoto hiyo imetokewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakati alipofanya ziara ya kutembelea Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd leo Jijini Dar es Salaam.

Balozi Mulamula amewasihi watanzania kuchangamkia fursa za masomo, masoko pamoja na biashara na uwekezaji na endapo kuna mtanzania anakwama basi asisite kuwasiliana na Wizara ili asaidiwe kupata ufumbuzi wa changamoto inayomkabili na kumwezesha kupata fursa husika.

“Fursa mbalimbali zimekuwa zikitangazwa katika Mashirika na Asasi za Kimataifa lakini watanzania wamekuwa wazito kiasi flani kuchangamkia fursa hizo, mfano fursa ya kufundisha lugha ya Kiswahili nje ya nchi, fursa ya kuuza bidhaa za kilimo nje ya nchi na nyingine nyingi………rai yangu kwa watanzania tuchangamkie fursa hizi ili tuweze kuinua kipato na uchumi wetu na taifa kwa ujumla,” amesema Balozi Mulamula

Pia Balozi Mulamula amewahakikishia ‘Diaspora’ kuwa serikali inatambua na kuthamini mchango wao na kwa sasa inaendelea kuandaa Sera ya Mambo ya Nje ili kuwawekea mazingira bora na salama ya uwekezaji nchini.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula ameipongeza Kampuni ya Mwananchi kwa kuhabarisha na kuelimisha jamii kwa weledi wa taaluma ambao umekuwa ukiwawezesha wananchi kufahamu mambo mbalimbali yanayoendela nchini.

“Vyombo vya habari vya Mwananchi ni mdau muhimu sana kwani vimekuwa vikihabarisha na kuelimisha wadau mbalimbali mambo mazuri yanayotekelezwa na Serikali ya Tanzania,” amesema Balozi Mulamula

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyombo vya habari katika kuhakikisha kuwa vinaitambulisha vyema Serikali ya Tanzania vyema katika mataifa mbalimbali.

Balozi Mulamula ametembelea Kampuni ya Mwananchi Communications Limited wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti na kujionea shughuli zinavyofanyika pamoja na kuongea na wahariri wa Magazeti hayo. 

Tarehe 04 Juni, 2021 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula alifanya ziara yake ya kwanza katika vyombo vya habari vya habari vya IPP ambavyo ni ‘The Guardian Ltd’ inayozalisha magazeti ya The Guardian na Nipashe, Radio One, Capital radio, East Africa radio, ITV, Capital TV pamoja na East Africa TV.

1.  Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi Communications Limited Bw. Bakari Machumu akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi za Mwananchi Communications Ltd Jijini Dar es Salaam. Mwingine ni Naibu Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi, Bw. Rashid Kejo 


1.  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwaelezea jambo Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi Communications Limited Bw. Bakari Machumu pamoja na Naibu Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi, Bw. Rashid Kejo 


1.  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiangalia gazeti la Mwananchi wakati wa kikao


1.  Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi Communications Limited Bw. Bakari Machumu akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nakala za Magazeti ya Mwananchi, The Citizen pamoja na Mwanaspoti


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza mmoja kati ya wafanyakazi wa mwananchi   

1.  Naibu Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi, Bw. Rashid Kejo akimuonesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula namna magazeti yanavyohifadhiwa katika jalada maalum


Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na wahariri wa Mwananchi Communications Limited kikiendelea 

1.  Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na wahariri wa Mwananchi Communications Limited kikiendelea  



Wednesday, August 4, 2021

BALOZI MULAMULA: ZIARA YA RAIS SAMIA RWANDA IMEIMARISHA UHUSIANO WA KIDIPLOMASIA

 Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amesema moja ya mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan nchini Rwanda ni kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia, kukuza biashara na uwekezaji pamoja na kuimarisha sekta ya uchukuzi baina ya Tanzania na Rwanda.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri Mulamula amesema kuwa mbali na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, pia ziara ya Mhe. Rais nchini Rwanda nchini Rwanda ziara hiyo imekuwa kielelezo kizuri cha ujirani mwema, na imeweka msingi mzuri wa ushirikiano baina ya nchi zetu mbili katika siku za usoni na walionesha kuridhishwa kwao na hali ya uhusiano uliopo.

Pamoja na mambo mengine, Waheshimiwa Marais walikubaliana kuharakisha majadiliano kuhusu Rwanda kuongeza matumizi yake ya Mkongo wa Taifa wa Tanzania.

“Nchi zetu zilikubaliana kuhakikisha kwamba upembuzi yakinifu unaofanywa kuhusu kuanzisha kiwanda cha maziwa Mkoani Mwanza unakamilika ifikapo mwezi Septemba, 2021. Kukamilika kwa mchakato huo na kuanza kwa uwekezaji kutatoa fursa za ajira kwa vijana wetu, lakini pia kutaongeza soko kwa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa katika Kanda ya Ziwa,” amesema Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Waheshimiwa Marais wamebaini fursa mbalimbali za ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda ambazo zitakuwa na manufaa kwa Serikali na wananchi ikiwemo sekta za biashara na uwekezaji na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.  

“Ziara ya Mhe. Rais Samia nchini Rwanda ililenga pia kuimarisha ushirikiano katika uendelezaji wa miundombinu ya ushoroba wa kati ambapo Serikali ya Tanzania inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuimarisha uchukuzi kupitia ushoroba wa Dar es Salaam chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, ikiwemo uboreshaji wa Bandari za Dar es Salaam na Tanga na ujenzi wa miundombinu ya reli. Jitihada hizo zinalenga kurahisisha na kupunguza muda na gharama za usafirishaji. Hivyo, Mhe. Rais aliwakaribisha wafanyabiashara na wasafirishaji kutoka Rwanda kuendelea kutumia Bandari za Tanzania, ameongeza Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula pamoja na Mambo mengine amesema kuwa katika ziara hiyo, Mhe. Samia akiwa na mwenyeji wake Mhe. Paul Kagame walishuhudia utiaji saini wa Hati za Makubaliano ya Ushirikiano nne (4) ambazo ni ati ya Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta ya Elimu, Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta ya TEHAMA, Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta ya Uhamiaji pamoja na Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta ya Usimamizi wa Bidhaa za Dawa.

“Waheshimiwa Marais walishuhudia pia uwekaji saini wa Tamko la Pamoja la Ziara (Joint Communique) linaloainisha maeneo ya ushirikiano yaliyokubaliwa na kutoa mwongozo wa utekelezaji,” amesema Balozi Mulamula.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mulamula ameongeza kuwa, Rais Samia alitembelea kiwanda cha kutengeneza maji, maziwa na juisi cha Inyange, kutembelea eneo la Makumbusho la Mauaji ya Kimbari yaliyotokea nchini Rwanda Mwaka 1994 ambapo aliweka Shada la Maua kama ishara ya kumbukumbu kwawote waliopoteza maisha.

Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Paul Kagame alielezea utayari wa Rwanda kuanza kufundisha lugha ya Kiswahili katika shule zake na hivyo watahitaji walimu wa lugha ya kiswahili.  

Katika Tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Nam Tien.

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo ya viongozi hao yalilenga kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia uliopo baina ya Tanzania na Vietnam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari (Hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam. kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz.  


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz.  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Nam Tien katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

 


Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Nam Tien kikiendelea


BALOZI MULAMULA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE MAREKANI

 Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anaeshughulikia masuala ya Siasa Mhe. Victoria Nuland Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo ya viongozi hao yalilenga kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia uliopo baina ya Tanzania na Marekani.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anaeshughulikia masuala ya Siasa Mhe. Victoria Nuland akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimuelezea jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anaeshughulikia masuala ya Siasa Mhe. Victoria Nuland katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anaeshughulikia masuala ya Siasa Mhe. Victoria Nuland kikiendelea   


Kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anaeshughulikia masuala ya Siasa Mhe. Victoria Nuland kikiendelea