Thursday, February 10, 2022

WATANZANIA WAASWA KUILINDA NCHI

Imeelezwa kuwa jukumu la kulinda nchi ni la kila Mtanzania na vijana wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kwa kuwa wao ni chachu ya ukuaji uchumi wa nchi na viongozi watarajiwa wa Taifa hili.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola wakati alipokuwa anafungua semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma.

Balozi Kayola alisema Wizara imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu kwa wanafunzi ili wao kama vijana wawe na elimu stahiki kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa ambayo yatawawezesha kushiriki kikamilifu katika kutumia fursa za mtangamano ukiwemo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ( EAC).

Alieleza kuwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, vijana wametambuliwa kama kundi muhimu kwa maendeleo ya jumuiya hiyo, hivyo utoaji wa elimu hiyo ni muhimu ili vijana wafahamu fursa zilizopo katika nyanja mbalimbali za uchumi, utamaduni, elimu na siasa na namna na ya kuzichangamkia. 

Aliwambia wanafunzi hao kuwa Sera ya Vijana ya EAC imeweka bayana haki za vijana kuwa na uhuru wa kutembea na kuweka makazi kwenye nchi yoyote ya Jumuiya kwa madhumuni mbalimbali kama kutafuta elimu, ajira au kufanya biashara, hivyo ni muhimu kwa vijana hao wanapoelekea kuhitimisha masomo yao ya sekondari ni vyema wakaweka mipango ya kuchangamkia furza za EAC.

Balozi Kayola alihitimisha hotuba yake kwa kuwasihi vijana hao kuwa mabalozi waźuri wa Tanzania katika safari yao ya maisha na kuwaelimisha wanafunzi wenzao na jamii kwa ujumla ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kupata elimu hiyo.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imejiwekea utaratibu wa kuelimisha makundi mbalimbali katika Jumuiya yakiwemo ya wanafunzi kuhusu Sera ya Mambo ya Nje. Na katika semina hiyo wanafunzi hao walielimishwa kuhusu majukumu ya Wizara, utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje, hatua za mtangamano wa EAC na fursa zake pamoja mchakato wa kuelekea shirikisho la kisiasa la EAC.

Semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma masuala mbalimbali ya Mtangamo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiendelea 

Sehemu ya wadau wakifuatilia semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma iliyofanyika kwenye ukumbi wa informatics katika Chuo Kikuu cha Dodoma

Picha ya patoja
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Balozi Agness Kayola akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Bw. Emmanuel Buhohela. Wote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Semina ikiendelea
Semina ikiendelea

Tuesday, February 8, 2022

RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AFDB) DKT. ADESINA AWASILI DODOMA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki BaloziLiberata Mulamula (katikati) akizungumza na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (kushoto) huku Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) akiwasikiliza wakati Dkt. Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.


Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (wa pili kushoto) akizungumza na wenyeji wake waliompokea katika Uwanja wa ndege Dodoma alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma huku Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (kulia) wakifuatilia mazungumzo hayo.




Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina awasili jijini Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini. Katika uwanja wa ndege wa Dodoma Dkt. Adesina amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba.

Dkt. Adesina yuko nchini kwa ziara ya siku tatu ambapo tarehe 09 February 2022 atashiriki katika uzinduzi wa ujenzi wa barabara za mzunguko zinazojengwa katika jiji la Dodoma utakaofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Ujenzi wa barabara hizo za mzunguko zenye urefu wa kilomita 112.3 unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na benki hiyo. Ujenzi wa barabara hizo utalifanya jiji la Dodoma kuwa na barabara za aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

MKUTANO WA 15 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA KISEKTA LA NISHATI LA EAC WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA KATIKA NGAZI YA WATAALAMU

Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki umefunguliwa leo tarehe 8 Februari 2022 jijini Arusha, Tanzania katika ngazi ya Wataalamu.


Mkutano huu utafanyika katika ngazi tatu ambapo umeanza na; Mkutano Ngazi ya Wataalamu unaofanyika tarehe 8 hadi 9 Februari 2022, utafuatiwa na Mkutano Ngazi wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 10 Februari 2022 na utamalizika kwa Mkutano Ngazi ya Mawaziri utaofanyika tarehe 11 Februari 2022.


Lengo la Mkutano huu ni kupitia na kuandaa taarifa ya hali ya utekelezaji wa Maamuzi/Maagizo ya mikutano iliyopita; Hatua iliyofikiwa hadi sasa katika sekta za Nishati Umeme, Nishati Mafuta, na Nishati Jadidifu; pamoja na Utekelezaji wa Miradi/Programu mbalimbali za Kitaifa na Kikanda ya Sekta za Nishati inayotekelezwa ndani ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.


Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano Ngazi ya Wataalamu unaongozwa na Kamishna Msaidizi Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila ambaye ameambatana na Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota, Mkurugenzi Idara ya Nishati na Madini kutoka Wizara ya Nishati na Madini Zanzibar, Mhandisi Said H. Mdungi pamoja na maafisa wengine Waandamizi kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye dhamana katika sekta ya nishati.


Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Ngazi ya Makatibu Wakuu ni sehemu ya mikutano ya awali kwaajili ya maandalizi ya Mkutano wa  Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki utaofanyika tarehe 11 Februari 2022. 


Kushoto ni Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme katika Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifafanua jambo wakati wa majadiliano ya mkutano huo.

Mwenyekiti wa Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu kutoka Jamhuri ya Kenya, Mhandisi Benson Mwakina (Kushoto) akiongoza majadiliano, kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Bw. Christophe Bazivamo. 

Kushoto ni Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Mgeta Sabe na wajumbe wengine wa Tanzania wakifatilia majadiliano.
Mkutano ukiendelea

Ujumbe wa Tanzania.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Tanzania.



WAZIRI MULAMULA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA 46 WA DHARURA WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, akiwa jijini Dodoma ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki katika Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Mkutano huu wa dharura umeitishwa kwa lengo la kujadili ripoti ya majadiliano yaliyofanyika tarehe 15 hadi 24 Januari 2022 jijini Nairobi, Kenya kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuhusu Nchi hiyo kujiunga na Jumuiya. 

Pamoja na muasula mengine yaliyojadiliwa Mkutano umekubaliana kuendelea kufanyia kazi kwa wakati hoja za pande zote mbili za majadiliano (EAC na Congo DRC), na kuandaa taarifa itakayowasilishwa kwa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ili kuharakisha uridhiaji wa maombi ya DRC

Mkutano huu wa dharura ambao umefanyika kwa njia ya mtandao umehudhuriwa na Nchi zote wanachama wa Jumuiya na kuongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Waziri anayesimamia masuala ya Mtangamano wa Afrika Mashariki Mhe. Adam Mohamed kutoka nchini Kenya. 

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliwasilisha maombi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 4 Juni 2019. 
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine (katika) na Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama Balozi Stephen Mbundi wa Wizara hiyo wakifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendele
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akichangia hoja kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao.

Monday, February 7, 2022

WAZIRI MULAMULA: TUTAENDELEA KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA NISHATI NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amesema Wizara kwa kushirikiana na Wizara zingine, Mashirika na Taasisi za Serikali na Sekta binafsi itaendelea kuweka jitihada katika kutangaza fursa za uwekezaji zinazotokana na sekta ya nishati. 

Waziri Mulamula ameeleza haya wakati wa mazungumzo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ocean Business Partners Tanzania Ltd Bw. Abdulsamad Abdulrahim na Makamu wa Rais, wa Kampuni ya dmg event ya nchini Uingereza Bw. Damian Howard yaliyofanyika Ofisini kwake jijini Dodoma. “Licha ya hazina kubwa tuliyonayo katika sekta ya nishati, serikali pamoja sekta binafsi bado tunakazi kubwa ya kuendelea kutangaza na kutafuta wawekezaji ili kukuza uwekezaji na mapato katika sekta hii. Waziri Mulamula. 

Bwana Abdulsamad na Bw. Howard wamepongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi madhubuti wa Mhe.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini. Waliongeza kusema Makampuni yao yataendelea kuunga mkono jitihada za serikali katika kutangaza fursa za uwekezaji zinazotokana na sekta ya nishati nje ya mipaka ya Tanzania. 


Katika tukio jingine Waziri Mulamula amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma. 

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Edwin Rutageruka (wa kwanza kusho), Mkurugenzi wa Diplomasia Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Makamu wa Rais wa Kampuni ya dmg event ya nchini Uingereza Bw. Damian Howard (wa pili kushoto) na Bw. Abdulsamad Abdulrahim (kulia) Mkurugenzi wa Kampuni ya Ocean Business Partners Tanzania Ltd walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.
Mazungumzo yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma

Friday, February 4, 2022

FURSA ZA AJIRA NA USHAURI ELEKEZI KATIKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA

Fursa za ajira na ushauri elekezi kwa Watanzania katika benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)



 

MAAFISA JWTZ WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ITALIA

Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiongozwa na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira pamoja na Col. Abdallah Khalfan wametembelea Ubalozi wa Tanzania Jijini Roma, Italia.

Wakiwa Ubalozini walipokelewa na mwenyeji wao Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo ambapo pamoja na mambo megine wamezungumzia masuala ya ushirikiano. Maafisa hao walikuwepo nchini Italia kwa shughuli za kikazi. 

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Italia 


Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira na Col. Abdallah Khalfan   


Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira, Col. Abdallah Khalfan pamoja na baadhi ya watumishi wa Ubalozi    


 

Thursday, February 3, 2022

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE WA SERIKALI YA URUSI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Masuala ya Kibinadamu kutoka nchini Urusi Bw. Yevgeny Primakov leo tarehe 03 Februari 2022 katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Bw. Primakov ameambatana na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Yuri Popov pamoja na Mjumbe kutoka Serikali ya Urusi, Bw. Egor Utkin.

Wawakilishi hao kutoka Serikali ya Shirikisho la Urusi waliwasilisha ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimirovich Putin.

Pamoja na mambo mengine viongozi hao walijadili juu ya kuimarisha ushirikiano uliopo na kwamba kwa sasa Tanzania na Urusi zinajikita zaidi katika kufungua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii na masuala mengine ya kiuchumi kwa maslahi mapana ya mataifa hayo.

Waziri Mulamula alieleza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano mzuri na wa kihistoria ambao uliasisiwa na Waasisi wa Mataifa hayo mawili.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kushoto) akipokea ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia)kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimirovich Putin

Mazungumzo yakiendelea. 

Picha ya pamoja Mhe. Waziri na Ujumbe kutoka Serikali ya Urusi.
Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, na Kulia kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Fredrick Kibuta.
 Kutoka kulia kwa Mhe. Waziri ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Urusi, Bw. Evgeny Primakov, Balozi wa Urusi nchini,
 Mhe. Yuri Popov pamoja na Mjumbe kutoka serikali ya Shirikisho la Urusi, Bw. Egor Utkin.

Waziri Mulamula akikabidhi shajara.
                                                                                      
Picha ya Pamoja.

Wednesday, February 2, 2022

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA SAUDIA ARABIA

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.Kikao hicho kilifanyika ofisini kwa Mhe. Waziri Mttumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia (walioko kushoto) wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini (katikati) katika kikao na Wawekezaji kutoka nchini Saudi Arabia(hawapo pichani) kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Hemedi Mgaza na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi Balozi Edwin Rutageruka wakati wa kikao na wawkezaji hao



Waziri Mulamula (katikati) katika picha ya pamoja na ujumbe wa  wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia waliokuja nchini kuangalia fursa za biashara na uwekezaji baada ya kumalizika kwa kikao chao jijini Dodoma

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini akiwa nje ya jengo la Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba akizungumza na wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia aliokuja nao Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji baada ya kumalizika kwa kikao chao na Mhe Waziri Mulamulajijini Dodoma


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

 

Mhe. Waziri Mulamula amekutana na Ujumbe wa wawekezaji hao ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 02 February 2022. Ujumbe wa wawekezaji hao umeongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia Mhe. Ali Mwadini umeelezea utayari wao wa kuja kuwekeza nchini.

Akizungumza katika kikao hicho Balozi Mulamula amewakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia mazingira rafiki ya uwekezaji nchini na kwamba Tanzania iko tayari kuwapokea.

Amesema Tanzania na Saudia zina uhusiano wa muda mrefu ambao una historia ya aina yake na kwamba uwekezaji kutoka kwa kampuni hiyo ni sehemu ya kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia.

Kampuni hiyo inayomiliki viwanda mbalimbali nchini Saudi Arabia inajishughulisha na uzalishaji wa pembejeo za Killimo hususan, mbolea za kupandia na kukuzia mimea pamoja na dawa (pesticides) aina ya ‘phosphorus, nitrogen, potassium na sulfur’.

Mbali na uzalishaji wa mbolea na dawa, Kampuni hiyo pia inazalisha vifaa vya kilimo vya plastiki ikiwa ni pamoja na khusambaza bidhaa katika nchini za Saudi Arabia, ukanda wa Mashariki ya Kati na duniani kote.

 

Wawekezaji hao waliwasili nchini Januari 28, 2022  wametembelea Mikoa ya Mtwara, Lindi Mtwara na Dodoma na kukutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Mikoa hiyo, wadau wa sekta binafsi na wakulima wa korosho kuzungumzia biashara na uwekezaji katika nyanja hizo. 

Wawekezaji hao wamemuhakikishia Mhe. Waziri Mulamula juu ya nia yao ya kuja kuwekeza Tanzania na kutaja maeneo ambayo ni kipaumbele chao kuwa ni madini, biashara, kilimo na mifugo

 

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Donald Wright leo tarehe 2 Februari 2022 jijini Dodoma.
Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani katika sekta za afya, uwekezaji, biashara na uhusiano wa kimataifa. 


Kushoto ni afisa kutoka Ubalozi wa Marekani, Bi. Kristin Mencer akifuatilia mazungumzo.

Kutoka kulia ni Katibu wa Waziri, Bw. Seif Kamtunda na Afisa Mambo ya Nje Bi. Talha Waziri wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya Pamoja.



 

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA ALFA CARE GROUP LIMITED

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kati) amekutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Alfa Care Group Limited Bw. Dadkarim Mulla (wa kwanza kushoto) ambaye aliambatana na  Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Mrisho Gambo (wa pili kushoto) walipomtembelea Wizarani tarehe 1 Februari 2022 jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Edwin Rutageruka (mwenye tai) na Katibu wa Waziri, Bw. Seif Kamtunda.

Katika Mazungumzo yao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kwa lengo ya kuyafikia malengo ya kitaifa kwa ufanisi.

Vilevile wamejadili namna ya kuongeza uwekezaji katika miradi ya maendeleo husasani sekta ya afya, miundombinu, teknolojia, utalii sambamba na kukuza ajira kwa watanzania.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya pamoja
Mhe. Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Gambo Calenda na Shajara za Wizara.

Mhe. Waziri akimkabidhi pia Bw. Mulla calenda ya Wizara