Monday, August 29, 2022

TANZANIA NA QATAR ZAJADILI AJIRA WAKATI WA KOMBE LA DUNIA

Tanzania imeihakikishia Qatar kuwa ipo tayari kutoa vijana watakaoweza  kufanya kazi nchini humo, hususan katika kipindi hiki ambacho mahitaji ya nguvukazi ni makubwa kutokana na nchi hiyo kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Mpira wa Miguu wa  Kombe la Dunia yatakayochezwa mwezi Novemba 2022.

Hayo yameelezwa wakati wa mazungumzo baina ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, Dkt. Ahmad Hassan Al-Hamadi yaliyofanyika kwenye Ofisi za Wizara hiyo Jijini Doha, Qatar tarehe 28 Agosti 2022. 

Mazungumzo hayo yamefanyika ikiwa ni moja ya utekelezaji wa Mkataba wa Kazi uliosainiwa kati ya Tanzania na Qatar mwaka 2014.

“Tunawapongeza Qatar kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la FIFA litakaloanza mwezi Novemba mwaka huu. Aidha, napenda kukufahamisha kuwa Tanzania imewaandaa vijana wake  wenye ujuzi na hivyo tunaomba kupata nafasi za ajira na za viza (visa allocation) kwa ajili ya Watanzania kuweza kuja kufanya kazi huku hasa wakati huu wa kombe la dunia,” aliongeza Balozi Fatma 

Katika Kikao hicho, viongozi hao pia wamesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano mzuri uliopo kati ya nchi hizi mbili hususan katika maeneo ya uwekezaji na biashara. Balozi Fatma alieleza kuwa Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanya maboresho makubwa ya mazingira ya uwekezaji na biashara, hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara wa Qatar kuja kuwekeza nchini katika maeneo mbalimbali kama vile utalii, kilimo, madini, maliasili, uvuvi na utamaduni.

“Napenda kukuhakikishia kuwa Tanzania inazo fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji na tunawakaribisha Serikali ya Qatar pamoja na wananchi wenu kuja kuwekeza nchini hususan katika sekta za utalii, madini, biashara na uwekezaji,” ameeleza Balozi Fatma.

Mkutano huo ulioandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, pia umehudhuriwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu,  Prof. Jamal Katundu, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemed Mgaza na Mkuu wa Utawala wa Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar, Bi Patricia Kiswaga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, Dkt. Ahmad Hassan Al-Hamadi akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika Ofisi za Wizara hiyo Jijini Doha, Qatar

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, Dkt. Ahmad Hassan Al-Hamadi akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika Ofisi za Wizara hiyo Jijini Doha, Qatar. Wengine pichani ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu,  Prof. Jamal Katundu, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemed Mgaza na Mkuu wa Utawala wa Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar, Bi Patricia Kiswaga.



Sunday, August 28, 2022

JAPAN YATOA DOLA BILIONI 30 KUSAIDIA NCHI ZA AFRIKA


Serikali ya Japan imetangaza kutoa kiasi cha Dola za Marekani bilioni 30 katika kipindi cha miaka mitatu (2022 – 2025) kwa Nchi za Bara la Afrika ili kuziwezesha kutekeleza programu na miradi ya maendeleo itakayoleta mageuzi ya kiuchumi barani humo. 

Kiasi hicho cha fedha kimetangazwa kutolewa na Waziri Mkuu wa Japan Mhe. Fumio Kishida wakati wa mkutano wa 8 wa Wakuu wa Nchi na Serikali kati ya Japan na Nchi za Afrika kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (Tokyo International Conference on African Development – TICAD 8 Summit) uliofanyika mjini Tunis nchini Tunisia terehe 27 - 28 Agosti 2022.

Kupitia Mkutano huo Mhe. Fumio amezihakijishia nchi za Afrika kuwa Serikali ya Japan itaendelea kushirikiana nao kwa karibu kwa kuchangia maendeleo kupitia programu na miradi mbalimbali.

Mhe. Fumio pia amezihakikishia nchi hizo kuwa Serikali ya Japan itaendelea kushiriki kikamilifu katika kukabiliana na changamoto zinazokwamisha juhudi za Afrika za kujikwamua kiuchumi. Amezitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kama vile milipuko ya magonjwa, mabadiliko ya Tabia Nchi na upungufu wa chakula.

Akizungumzia kuhusu kiasi cha fedha kilichotelewa, Mhe. Fumio amesema kupitia mpango wa TICAD sekta binafsi za pande zote mbili (Japan na Afrika) zimeendelea kustawi, hivyo Serikari yake itaendelea kuhamasisha Kampuni za Japan kuendelea kuwekeza Afrika katika sekta mbalimbali ikiwemo ujenzi wa viwanda, kilimo, Afya, nishati ya umeme na teknolojia. 

Kuhusu mgawanyo wa fedha hizo Mhe. Fumio amesema kuwa pamoja na TICAD kufanikiwa katika maeneo mengi ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, afya na elimu, Japan katika kipindi cha miaka miatatu ijayo (2022/23-24/25) itaangazia pia maeneo muhimu yanayogusa maisha ya watu ya kila siku. 

Ameyataja maeneo hayo kuwa ni mapinduzi ya kijani, Mabadiliko ya tabia nchi, kukuza uwekezaji, kuendeleza hali ya maisha ya Waafrika, ambapo kiasi cha Dola za Marekani bilioni 5 zitatolewa kufanikisha mpango huo. 

Maeneo mengine ni Afya na maendeleo ya rasilimali watu. Katika sekta ya afya Japan itachangia kiasi Dola za Marekani bilioni 1.08 kuiwezesha Afrika kukabiliana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria. Mhe. Fumio aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ijayo Serikali yake inatarajia kuwajengea uwezo zaidi ya watu 300,000 kutoka bara la Afrika katika sekta ya viwanda, afya, elimu, sheria na utawala.

Akizungumza katika mkutano huo Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ambaye amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameeleza umuhimu wa Bara la Afrika kuendelea kushikirikiana na Jumuiya ya Kimataifa katika kutatua changamoto zinazolikabili bara hilo katika ukuzaji wa uchumi. 

Mhe. Mjaliwa akiongelea madhara yaliyo sababishwa na athari za UVIKO 19 na Vita vya Urisi na Ukraine ikiwemo mfumuko wa bei wa bidhaa, ametoa rai kwa Jumuiya ya Kimataifa kuendelea kushirikiana na nchi za Afrika katika jitihada zake za kujigemea kiuchumi, ili kuhakikisha zinaendelea kutoa huduma bora na muhimu kwa wananchi wake na kuwawezesha wananchi katika shughuli zao zinazowagusa moja kwa moja kama vile kuendeleza kilimo na utalii.

Naye Rais wa Tunisia Mhe. Kais Saied ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Mkutano wa TICAD 8, akifungua mkutano huo amesema Japan ni mbia wa kweli wa maendeleo ya Afrika kwa kuwa wakati wote imekuwa mstari wa mbele kushirikiana na Afrika katika kutafuta suluhu ya changamoto zinazolikabili bara hilo, na kuchangia katika kundeleza sekta mhimu kama vile elimu, kilimo, teknolojia, ujenzi wa miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji, mabadiliko ya tabia nchi sambamba na kutoa mikopo yenye riba ndogo na masharti nafuu. 

Mkutano wa 8 wa TICAD umehudhuriwa na zaidi ya washiriki 3000 kutoka nchi 55 za Bara la Afrika na Mashirika mbalimbali ya Kimataifa, umebeba kauli mbiu isemayo “Kukuza Maendeleo Endelevu ya Afrika kwa ajili ya Waafrika” (“Promoting Africa-led, African-owned sustainable development”)
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) akifuatilia Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8) unaoendelea mjini Tunis, nchini Tunisia. Waliopo karibu naye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Mbarouk (kulia) na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba (kushoto)
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akisalimiana na Rais wa Tunisia Mhe. Kais Saied alipokuwa akiwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Palais de Congres mjini Tunis nchini Tunisia
Viongozi wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika, Ujumbe wa Serikali ya Japan, watendaji na wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya kimataifa walioshiriki mkutano wa TICAD8 wakiwa katika picha ya pamoja. 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa na Rais wa Tunisia Mhe. Kais Saied wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa TICAD8.

Saturday, August 27, 2022

MKUTANO WA NANE WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA TICAD WAANZA MJINI TUNIS, TUNISIA

Mkutano wa 8 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (Tokyo International Conference on African Development – TICAD 8 Summit) umeanza leo tarehe 27 Agosti 2022 mjini Tunis, Tunisia. Hii ni mara ya pili kwa mkutano huu kufanyika Barani Afrika tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993 baada ya ule wa Kenya (TICAD 6) uliofanyika mwaka 2016. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anawakilishwa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) katika Mkutano huu. 

Mkutano huo wa TICAD 8 utafanyika kwa siku mbili tarehe 27 na 28 Agosti 2022; na umetanguliwa na Kikao cha Maafisa Waandamizi wakiwemo Mabalozi wanaoziwakilisha nchi za Afrika nchini Japan, kilichofanyika tarehe 25 Agosti 2022. Pamoja na masuala mengine, Mkutano huu unatarajiwa kukubaliana kuhusu namna ya kuiwezesha Afrika kukabiliana na changamoto zinazoikabili Dunia ili kuiwezesha kufikia Agenda ya Maendeleo ya Umoja wa Afrika (Agenda 2063). 

Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na janga la UVIKO 19, amani na usalama, mabadiliko ya tabia nchi, upatikanaji mgumu wa malighafi na mfumuko wa bei kwa bidhaa zinazotegemewa na nchi za Afrika kama vile gesi, mafuta na pembejeo za kilimo ambazo ni muhimu katika ukuaji wa uchumi wa Bara la Afrika. 

Agenda 2063 ilikubaliwa na viongozi wa Afrika wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika kwa lengo la kuliunganisha Bara la Afrika katika masuala ya kukuza uchumi; kuhamasisha utawala bora na utawala wa sheria; kuhakikisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja; kuhakikisha amani na usalama unaimarika na kuiweka Afrika katika nafasi ya mchangiaji mkuu wa uchumi duniani

Mhe. Kassim Majaliwa katika mkutano huu anatarajiwa kuwa na mazungumzo ya pembezoni na Waziri Mkuu wa Japan, Mheshimiwa Fumio Kishida na watendaji wakuu wa kampuni na taasisi za Japan ikiwemo Shirika la Maendeleo la Japan (JICA); Kampuni ya Mitsubishi; Bodi ya Japan Tobacco Inc (JT Group); na Taasisi ya Japan inayojishughulisha na masuala ya Uchumi na Maendeleo ya Afrika (Association of African Economy and Development - AFRECO). 

Tangu kuanza kufanyika kwa mikutano ya TICAD, Japan imekuwa ikiongeza kiasi cha fedha za mkopo wa masharti nafuu na msaada katika kuchangia maendeleo ya Afrika kutoka Dola za Marekani bilioni 0.6 kwa mwaka 1993 (TICAD 1) hadi kufikia Dola za Marekani bilioni 20 kwa mwaka 2019 (TICAD 7). Kwa upande wa Tanzania misaada na mikopo ya masharti nafuu kutoka Japan imesaidia katika utekelezaji wa programu na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, maji, afya, nishati ya umeme, kilimo na elimu.

Ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Japan unazingatia mwongozo wa Agenda ya Umoja wa Mataifa ya Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu inayojikita kwenye kupunguza umasikini na kukuza maendeleo. Japan ni miongoni mwa washirika wakubwa wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini Tanzania kupitia JICAkuanzia mwaka 1962. Tanzania ni nchi pekee inayoshirikiana na Japan katika maeneo matatu ya ushirikiano yaliyopewa kipaumbele na nchi hiyo ikiwemo, ushirikiano katika misaada na mikopo ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo; ujuzi na uzoefu kupitia program ya wajapani ya kujitolea chini ya Japan Overseas Cooperation Agreement; na fursa za mafunzo na masomo

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akifuatilia Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8) unaoendelea mjini Tunis, nchini Tunisia.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Tunisia Mhe. Najla Bouden alipowasili katika uwanja ndege wa kimtaifa wa Carthage mjini Tunis nchini Tunisia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa  kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8) ulio anza kufanyika leo tarehe 27 Agosti 2022.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu wa Tunisia Mhe. Najla Bouden alipowasili mjini Tunis, Tunisia.

Friday, August 26, 2022

TANZANIA NA IRAN ZAAHIDI KUONGEZA MAENEO MAPYA YA USHIRIKIANO

Tanzania na Iran zimekubaliana kuibua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za biashara, kilimo, masoko, utalii, uwekezaji, afya, madini, nishati na utaalamu.

Hayo yamefikiwa wakati wa mazungumzo kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian yaliyofanyika jijini Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.

Waziri Mulamula ameeleza kuwa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran nchini imekuja wakati muafaka ambapo, mataifa hayo mawili yenye uhusiano wa kihistoria yanatimiza miaka 40 tokea kuanzishwa kwa uhusianao wa kidiplomasia.

‘’Ziara hii inatupa muendelezo mzuri katika kuimarisha uhusiano wetu na kuangalia maeneo mapya ya kukubaliana kushirikiana” alisema Waziri Mulamula.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mhe. Hossein Amirabdollahian alieleza utayari wa nchi yake kushirikiana na Tanzania katika kubadilishana utaalamu na uzoefu katika sekta mbalimbali za maendeleo ili uhusiano uliopo ulete faida za kiuchumi kwa manufaa ya mataifa hayo mawili. 

“Tumefungua ukurasa mpya wa uhusiano wa kidiplomasia kwa mataifa yetu, hivyo naamini kupitia ziara hii kutapatikana mafanikio yanayoonekana kwa maslahi ya mataifa yetu. 

Mhe. Hossein Amirabdollahian yupo nchini kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 24 hadi 26 Agosti 2022  akiambatana na ujumbe wa Wafanyabiashara, Wamiliki wa Viwanda na Maafisa Waandamizi ambao pamoja na mambo mengine walishiriki kongamano la biashara lililofanyika Dar Es Salaam tarehe 25 Agosti 2022.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.

Picha ya pamoja, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian  pamoja na ujumbe waliombatana nao katika mazungumzo yao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimuaga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian mara baada ya kumaliza mazungumzo katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha mmoja wa mjumbe aliyeambatana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mhe. Hossein Amirabdollahian katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 26 Agosti 2022.

 

NSSF YACHANGIA M.50 KUTENGENEZA KANZIDATA YA DIASPORA


Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (wa pili kulia) na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah (wa pili kushoto) wakiwa na wanasheria wao wakisaini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (kulia) na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah wakipongezana baada ya kusaini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

 

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (wa pili kulia) na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah (wa pili kushoto) na wanasheria wao wakionesha kabrasha lenye makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

 

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana akizungumza katika hafla ya utiaji saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah akizungumza baada ya hafla ya utiaji, saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam, aliyekaa kushoto ni Mkurugenzi wa Diaspora Wizarani Balozi James Bwana akimsikiliza.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Semeni Nandonde akizungumza katika hafla ya utiaji saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.


Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah baada ya kutia saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii  (NSSF) katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana baada ya kutia saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii  (NSSF) katika picha ya pamoja katika hafla ya kutia saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.


 



Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii  (NSSF) umesaini makubaliano na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub).

Makubaliano hayo yamesainiwa leo kati ya Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora Balozi James Bwana kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mkurugenzi wa Uthaminishaji, Takwimu na Usimamizi wa Hadhari, Bw. Ibrahim Maftah kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo, Balozi Bwana amesema kukamilika kwa mfumo huo wa kidigitali kutaiwezesha Serikali kuwasajili, kuwatambua na kurahisisha shughuli za kuwaratibu Diaspora na kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya Taifa.

“Leo hii tumeshuhudia utiaji saini wa makubaliano ambayo yataiwezesha NSSF kutoa Shilingi Milioni 50 ambazo zitaiwezesha Wizara kutengeneza Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, kitendo hiki ni mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu ambao Wizara umekuwa nao na NSSF, ni matarajio ya Wizara kuwa NSSF itahuisha program yao ya Diaspora na kubuni programu mpya ili kutoa huduma kwa Diaspora wetu na wao kunufaika zaidi na programu hizo,” alisema Balozi Bwana.

Balozi Bwana aliongeza kuwa Diaspora ni eneo muhimu  la uwekezaji kwa maendeleo ya taifa hasa ikizingatiwa kuwa kwa mwaka 2021 Diaspora waliwekeza jumla ya Shilingi Bilioni 3.9 katika mpango wa UTT Amis na kutuma nchini Shilingi Milioni 569.3 kwa ndugu na jamaa zao hapa nchini.

“Serikali inategemea mfumo utakaowatambua, kuwasajili na kuwawezesha Diaspora wa Tanzania Duniani kote kupata huduma nyingi na muhimu wanazohitaji na kushiriki kidijitali katika shughuli mbalimbali za maendeleo biashara, uchumi na uwekezaji hapa nchini,” aliongeza Balozi Bwana.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Ibrahim Maftah ameipongeza Wizara kwa kuja na wazo la kuanzisha mfumo huo na kuihakikishia Wizara kuwa NSSF itaendelea kushirikiana na Wizara kuhakikisha mfumo wa kidigitali wa Diaspora Digital Hub unakamilika na kutumika katika maeneo yote yenye tija kwao na kwa taifa kwa ujumla.

“Kitendo cha NSSF kusaini makubaliano hayo kinaonesha utayari na muelekeo wetu katika kutumia fursa mbalimbali zinazopatikana katika eneo la Diaspora,” alisema Bw. Maftah.

Awali mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Semeni Nandonde amesema kukamilika kwa mfumo huo kutaiwezesha Serikali kufahamu kwa ufasaha idadi ya diaspora wake, ujuzi walionao, elimu zao .

Ameongeza kuwa mfumo huo utakapokamilika diaspora wataweza kupata huduma maalum zitakazoandaliwa kwa ajili ya mahitaji yao kama vile huduma za kibenki, hifadhi ya jamii, bima ya afya kwa wategemezi wao waliopo hapa nyumbani, taarifa za fursa za uwekezaji, biashara na masoko, masuala ya uhamiaji, vitambuklkisho vya taifa na huduma nyinginezo.

KAMISHINA MKUU WA UNHCR ATUA DODOMA

Kamishina Mkuu wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), Bw. Filippo Grandi yupo nchini tokea tarehe 24 Agosti 2022 kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine, atafanya mazungumzo na viongozi wakuu wa Serikali na kutembelea Kambi za Wakimbizi mkoani Kigoma.


Bw. Grandi ambaye leo tarehe 25 Agosti ametembelea Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu ya mkoani Kigoma na baadaye kuwasili mkoani Dodoma na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula ameelezea kuridhishwa kwake na  huduma bora zinazotolewa kwa Wakimbizi ukilinganisha na miaka mitatu iliyopita alipofanya ziara kama hiyo mwaka 2019. 

Kwenye Kambi ya Nyarugusu, ambayo inahifadhi Wakimbizi zaidi ya 130,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Burundi, Bw. Grandi alijionea hali halisi ya maisha ya wakimbizi hao na kusikiliza maelezo ya wawakilishi wao pamoja na taasisi mbalimbali zinazohudumia wakimbizi.

Baada ya kusikiliza maelezo, Bw  Grandi aliahidi kuwa UNHCR itaendelea kushirikiana na wadau ikiwemo Serikali Ili kuboresha maisha ya wakimbizi pamoja na kukabiliana na athari zitokanazo na shughuli za wakimbizi kama vile uharibifu wa mazingira. 

Ziara ya Bw. Grandi nchini imekuja kufuatia mazungumzo yake aliyofanya na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan jijini New York wakati wa Kikao cha 76 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2021.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana kwa bashasha na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bw. Filippo Grandi kwenye Uwanja wa Ndege wa Dodoma. Bw. Grandi yupo nchini kwa ziara ya kikazi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bw. Filippo Grand kwenye chumba cha wageni maalum cha Uwanja wa Ndege wa Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendeguza na kushoto ni Mkurugenzi wa UNHCR wa Kanda ya Afrika Mashariki, Pembe ya Afrika na Maziwa Makuu, Bibi  Clementine Awu Nkweta



 

Thursday, August 25, 2022

TANZANIA YAIHAKIKISHIA IRAN MAZINGIRA SALAMA YA BIASHARA, UWEKEZAJI

 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mhe. Amir Abdollahian akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk walipokutana kwenye ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Iran lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk akifungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Iran lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam


Meza kuu ikiwa katika picha ya pamoja wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Iran lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam







WIZARA NA BENKI YA NMB WASAINI HATI YA MAKUBALIANO

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana akizungumza katika hafla ya utiaji saini hati za makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) kati ya Wizara na Benki ya NMB PLC  katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam


Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Semeni Nandonde (aliyesimama kukulia) akizungumza wakati wa hafla ya kusaini  hati za makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) kati ya Wizara na Benki ya NMB katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam .




Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (kulia) na Mwakalishi wa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bw. Alfred Shao (kushoto) wakisaini hati za makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) walizosaini katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam .


Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (kulia) na Mwakalishi wa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bw. Alfred Shao (kushoto) wakionesha hati za makubaliano walizosaini ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) walizosaini katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam .

Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bw. Alfred Shao akizungumza katika hafla ya kusaini Hati ya Makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) na Benki ya NMB PLC.



 
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja baada ya kusaini Hati ya Makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) na Benki ya NMB PLC.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Watumishi wa Benki ya NMB Plc katika picha ya pamoja baada ya kusaini Hati ya Makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub).

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Benki ya NMB Plc wamesaini Hati ya Makubaliano ya kutengeneza Mfumo wa Kanzi Data wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub).

Makubaliano hayo yamesainiwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora Balozi James Bwana kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine  na Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali wa Benki ya NMB, Bw. Alfred Shao kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Akiongea katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo Balozi Bwana amesema mfumo huo wa kidigitali utaisaidia Serikali kuwatambua, kuwasajili na kuwawezesha Diaspora wa Tanzania waliopo sehemu mbalimbali ulimwenguni kupata huduma mbalimbali na kushiriki kidigitali katika shughuli mbalimbali za maendeleo, biashara, uchumi na uwekezaji nchini.

“Ushirikiano wa Wizara na Benki ya NMB Plc ni wa muda mrefu na wenye mafanikio mengi katika kuendelea kusukuma gurudumu la maendeleo ya Tanzania. Wizara ina imani kuwa kupitia udhamini huu wa shilingi milioni 100 kutoka Benki ya NMB, fedha hizo zitawezesha kukamilisha matengenezo ya mfumo wa Diaspora Digital Hub na hivyo kuboresha huduma zenye kukidhi mahitaji ya Diaspora wote ulimwenguni,” amesema Balozi Bwana

Balozi Bwana ameongeza kuwa, mfumo huo pamoja na mambo mengine, utafungua uwezekano wa fursa zaidi za ushirikiano kati ya Wizara na Benki hiyo utawezesha utunzaji wa taarifa mbalimbali za Diaspora wa Tanzania popote walipo ulimwenguni na hivyo kurahisisha kazi ya uratibu wa Diaspora.

Balozi Bwana amesema Serikali inategemea kuwa kukamilika kwa  mfumo huo kutaweza kuwatambua, kuwasajili na kuwawezesha Diaspora wa Tanzania Duniani kote kupata huduma nyingi na muhimu wanazohitaji na kushiriki kidijitali katika shughuli mbalimbali za maendeleo biashara, uchumi na uwekezaji hapa nchini.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bw. Alfred Shao  amesema benki yao inaamini kuwa kukamilika kwa mfumo huo kutawawezesha Diaspora wa Tanzania kuungana, kutambulika na kuiwezesha Serikali kuwa na Kanzi Data ya uhakika na kuwafikia diaspora wengi kwa wakati mmoja na hivyo kuleta mafanikio makubwa kwa Taifa na Mtanzania mmoja mmoja anayeishi nje ya nchi.

"Sisi NMB tunaamini kuwa mfumo huu, utawaunganisha, utawatambua na kuiwezesha Serikali kuwa na Kanzidata ya Diaspora wake, ni wazi kuwa mfumo huu utaleta maendeleo makubwa kwa Taifa na Mtanzania mmoja mmoja wanaoishi nje ya nchi," alisema Bw. Shao

Aliahidi kuwa NMB itaendelea kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika kuhakikisha mfumo wa kidigitali wa Diaspora Digital Hub unakamilika kwa wakati.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Semeni Nandonde amesema makubaliano yaliyoingiwa kati ya Wizara na Benki ya NMB yanaashiria utayari wao katika kulifadhili na kuliwezesha wazo la Wizara la kuwa na mfumo wa kutunza taarifa za Diaspora na kuwawezesha dispora kunufaika na huduma mbalimbali pindi mfumo huo utakapokamilika.



 

JPC YA TANZANIA NA YAMALIZIKA


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk akimkabidhi zawadi ya picha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Jamhuri ya Msumbiji Balozi  Manuel Gonçalves mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 15 wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji unaofanyika jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Jamhuri ya Msumbiji Balozi  Manuel Gonçalves akimkabidhi zawadi Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 15 wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji unaofanyika jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk akishikana mikono na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Jamhuri ya Msumbiji Balozi  Manuel Gonçalves baada ya kumkabidhi zawadi mgeni wake walipomaliza Mkutano wa 15 wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji unaofanyika jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk aliyeshikana mkono na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Jamhuri ya Msumbiji Balozi  Manuel Gonçalves baada kumalizika kwa Mkutano wa 15 wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji unaofanyika jijini Dar es Salaam


 



WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA IRANI AWASILI TANZANIA KWA ZIARA YA KIKAZI

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mhe. Amir Abdollahian aliwasili nchini jana usiku kwa ziara ya kikazi ya siku tatu na kupokelewa na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam 

Mara baada ya kuwasili nchini, Mhe. Abdollahian alisema, lengo la ziara yake nchini Tanzania ni kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Iran na Tanzania katika sekta za kisiasa na kiuchumi.

Nae Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula alimueleza nia ya Serikali ya Tanzania ni kuendelea kudumisha uhusiano wa kihistoria uliopo baina ya mataifa hayo na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya sita imejidhatiti katika kukuza na kuendeleza Diplomasia ya Uchumi hivyo ni matumaini yake kuwa ujio wake hapa nchini utachangia kuendeleza diplomasia ya uchumi kati ya Tanzania na Iran.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mhe. Amir Abdollahian katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.  Mhe. Abdollahian aliwasili nchini jana usiku kwa ziara ya kikazi ya siku tatu. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mhe. Amir Abdollahian katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam baada ya kuwasili nchini jana usiku kwa ziara ya kikazi ya siku tatu


Mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mhe. Amir Abdollahian yakiendelea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemedi Mgaza.