Friday, October 7, 2022

DKT. TAX AWATAKA WATUMISHI KUCHAPA KAZI KWA BIDII NA KUSHIRIKIANA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa amepokea shada la maua kutoka kwa Bi. Theresia Msendo mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine alipowasili katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz alipowasili katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma

Naibu Waziri  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) akizungumza katika kikao cha katika kikao cha makabidhiano ya Ofisi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (hawapo pichani) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akizungumza katika kikao cha makabidhiano ya Ofisi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula. Kushoto ni Mhe. Balozi Mbarouk, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akizungumza katika kikao cha makabidhiano ya Ofisi kati yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza katika kikao cha makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula kilichofanyika mtumba jijini Dodoma


Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Alex Mfungo akizungumza katika kikao cha makabidhiano ya Ofisi kati ya Mhe. Dkt. Tax na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mulamula kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akikibidhi rasmi Ofisi kwa  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar Bi Mariam Haji Mrisho akitoa neno la shukurani katika hafla ya Makabidhino ya Ofisi kwa  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma
Baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara wakifuatilia hafla ya Makabidhino ya Ofisi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na mtangulizi wake Balozi Mulamula (hawapo pichani) iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara wakifuatilia hafla ya Makabidhino ya Ofisi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na mtangulizi wake Balozi Mulamula (hawapo pichani) iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na mtangulizi wake Balozi Mulamula wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara baada ya kukamilika kwa hafla ya Makabidhino ya Ofisi iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na mtangulizi wake Balozi Mulamula katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara baada ya kukamilika kwa hafla ya Makabidhino ya Ofisi iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma

 

 

 

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amewataka watumishi wa Wizara kuendelea kuchapa kazi kwa bidii, ufanisi na kushirikiana ili kufikia matarajio ya serikali na wananchi kwa ujumla.

Dkt. Tax ametoa rai hiyo leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dodoma mara baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula.

Dkt. Tax amesema watumishi wa Wizara wanatakiwa kuhakikisha wanatumia weledi na kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu ya Wizara ili kuleta tija na ufanisi wakati wote.

“Sisi ni timu ya ushindi, tuendelee kuchapa kazi, nitashirikiana na watumishi wote wa Wizara, kuhakikisha tunatekeleza majukumu yetu kwa viwango na kwa muda sahihi, tuwe wabunifu na tujitahidi kufanya kazi kama timu ili kufikia matarajio ya Serikali yetu na wananchi wote kwa ujumla,” alisema Dkt. Tax

Ameongeza kuwa kazi ya kukuza uhusiano kati ya Tanzania na nchi mbalimbali, Jumuiya za kikanda na kimataifa haiwezi kufanikiwa ikiwa watumishi hawatashirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kama timu huku wakizingatia weledi, uzalendo na ubunifu kwa maslahi mapana ya taifa.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Balozi Liberata Mulamula amewashukuru Watumishi wa Wizara kwa ushirikiano waliompatia alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambao ulimuwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

“Nimeacha timu imara nawashukuru wote kwa ushirikiano mlionipatia na niwaombe muendelee na moyo huohuo katika kufanikisha majukumu ya wizara,” alisema Balozi Mulamula.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbrouk Nassor Mbarouk amemshukuru Balozi Mulamula kwa ushirikiano aliompatia katika kipindi chake na kumsihi aendelee kushirikiana nao kwa kuzingatia hazina kubwa ya uzoefu na ujuzi alionao katika sekta ya mambo ya nje.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine alisema Wizara imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kumuahidi Dkt. Tax kuwa watumishi wako imara na wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni na hivyo kuleta tija kwa wizara na taifa kwa ujumla









Thursday, October 6, 2022

TANZANIA, INDIA KUIMARISHA SEKTA YA UCHUMI

Tanzania na India zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika sekta ya uchumi hususan kuendeleza miradi ya maendeleo ya kiuchumi, kuongeza thamani ya bidhaa za kilimo pamoja na ujenzi wa viwanda.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine alipokutana kwa Mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

“Tumekubaliana kuwa ni wakati muafaka wa kuongeza ushirikiano wa kiuchumi, hasa kwa kuwa na miradi ya ushirikiano wa sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), kuongeza thamani ya bidhaa za kilimo kuwa na viwanda vitakavyojengwa nchini na kuanza kuzalisha bidhaa mbalimbali ambazo awali zilikuwa zinapatikana nchini India,” amesema Balozi Sokoine.

Viongozi hao pia wamejadili namna ya kuwekeza katika maeneo maalumu ya kibiashara ambapo kutakuwa na uzalishaji wa bidhaa kwa masoko ya nje na ya ndani na kuendeleza falsafa ya Tanzania ya Viwanda. 

“Tanzania inamakubaliano na India ya kushirikiana katika masuala ya teknolojia hususan Tehama ambapo hadi sasa India imekubali kuanzisha tawi la Taasisi ya Tehama nchini Tanzania na taasisi hiyo inategemewa kuanza kutoa mafunzo mwakani, ameongeza Balozi Sokoine.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi amesema wamekubaliana namna ya kushirikiana na kuimarisha sekta ya uchumi hususan biashara na uwekezaji kwa maslahi ya pande zote mbili.

Serikali ya India inaamini kuwa Tanzania inaweza kuisaidia katika uwekezaji wa viwanda vikubwa zaidi lakini pia kwa kuwekeza Tanzania, ni rahisi ya kulifikia soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki…….“tunataka kuwaleta wawekezaji kutoka India na kuja kuwekeza katika viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa Tanzania,” amesema Mhe. Ravi

Mhe. Ravi ameongeza kuwa endapo Serikali ya Tanzania itawapatia eneo maalumu la biashara (Special Economic Zone) la uwekezaji ambalo litasaidia kushawishi wawekezaji kutoka India kuja kuwekeza nchini.  

Mwezi Agosti, 2022, Tanzania na India ziliahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano ikiwemo kuhakikisha sekta za afya na nyingine zinaimarika ikiwemo kilimo.

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi akizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akimueleza jambo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mazungumzo baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi yakiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine katika picha ya pamoja na Ujumbe wa India unaoongozwa na  Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje India, Mhe. Dammu Ravi katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Tuesday, October 4, 2022

PAPA FRANCIS AMTUNUKU MTANZANIA NISHANI YA HESHIMA

Baba Mtakatifu Papa Francis amtunuku Padre Richard Mjigwa, C.PP.S., kutoka Tanzania Nishani ya Msalaba wa Kanisa na Papa kutokana na huduma ya mawasiliano ya Kanisa kupitia Radio Vatican Idhaa ya Kiswahili.

Padre Mjigwa pia anahudumu katika Baraza la Kipapa la Mawasiliano kupitia Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican ni mtanzania wa pili kutunukiwa Nishani hiyo baada ya miaka 6 tangu Mtanzania wa kwanza aliyehudumu katika Baraza hilo, Mama Thabita Janeth Mhella kutunukiwa Nishani hiyo mwezi Septemba 2016. 

Padre Mjigwa ambaye ni Mwanashirika wa Shirika la Damu Azizi, alikabidhiwa Nishani hiyo na Mhariri Mkuu wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano la Kipapa, Dkt. Andrea Tornielli kwa niaba ya Papa Francis kufuatia juhudi zake za kuhudumia jamii katika kueneza sauti na miongozo ya Papa katika lugha ya Kiswahili kupitia Radio Vatican kwenye mataifa yanayozungumza lugha hiyo. 

Padre Mjigwa aliyezaliwa Tanzania mwaka 1964 alianza shughuli ya huduma ya uandishi wa habari kama mshirika mnamo mwaka 1994 hadi 1999 na baadaye kuanza rasmi katika Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican kuanzia mwaka 2008 hadi sasa. 

Katika hatua nyingine, Padre Mjigwa kwa niaba ya Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican alipokea Nishani ya maadhimisho ya miaka 30 ya Idhaa hiyo ambayo ilianzishwa rasmi Tarehe 27 Septemba 1992. Tuzo hiyo ameipokea wakati muafaka ambapo Lugha ya Kiswahili imeendelea kutambulika duniani kama lugha kuu mojawapo ya mawasiliano. 

Utangazaji katika lugha ya Kiswahili kwenye Radio Vatican ulianza mapema mwezi Novemba 1961 baada ya Wamisionari wa Afrika (White Fathers) kuanza kuandaa makala kwa lugha ya Kiswahili kufuatia uzinduzi uliofanywa na Papa Mtakatifu Yohane XXIII na kupelekea kurushwa matangazo hayo ya kila siku kwa Afrika.


Mhariri Mkuu wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano la Kipapa, Dkt. Andrea Tornielli akimkabidhi Nishani ya Msalaba wa Kanisa na Papa, Padre Richard Mjigwa, (C.PP.S.) kutoka Tanzania kutokana na huduma ya mawasiliano ya Kanisa kupitia Radio Vatican Idhaa ya Kiswahili

Mhariri Mkuu wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano la Kipapa, Dkt. Andrea Tornielli akimpongeza Padre Richard Mjigwa, (C.PP.S.) kutoka Tanzania baada ya kupokea Nishani ya Msalaba wa Kanisa na Papa, kutokana na huduma ya mawasiliano ya Kanisa kupitia Radio Vatican Idhaa ya Kiswahili

Picha ya pamoja 



TANZANIA YACHAGULIWA MJUMBE WA BARAZA LA ITU

Tanzania imefanikiwa kushinda kwa kishindo katika uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Shirika la Mawasiliano Duniani (ITU) katika uchaguzi uliofanyika wakati wa mkutano mkuu wa ITU jijini Bucharest, Romania leo, tarehe 3 Oktoba 2022. Tanzania imepata kura 141 kati ya kura 180 zilizopigwa na nchi wanachama wa Shirika hilo. 

Baraza la ITU husimamia shughuli za Shirika katika kipindi cha kati ya mikutano mikuu ambayo hufanyika kila baada ya miaka 4.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu uliongozwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Mnauye (Mb) na kujumuisha maofisa waandamizi wengine kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mashirika na Taasisi za Mawasiliano nchini.

Kwa kuchaguliwa kwake, Tanzania sasa itakuwa mjumbe wa Baraza la ITU kwa kipindi cha miaka 4 ijayo. Ushindi huu ni mafanikio makubwa kwa Tanzania na ni kielelezo cha kazi nzuri anayoifanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan katika medani ya kimataifa na hivyo kuifanya nchi iweze kukubalika na kuaminiwa. 

Ushindi huu pia ni matokeo ya kampeni ya kimkakati iliyoendeshwa na Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania, Umoja wa Mataifa - Geneva. Aidha, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Taasisi zilizopo chini yake zilizifanya kazi kubwa ya kampeni na kutoa raslimali muhimu kwa ajili hii. 

Itakumbukwa kuwa Tanzania iliwahi kuwa mjumbe wa Baraza hili kabla ya kushindwa katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2018, Dubai UAE.

Miongoni mwa faida za kuwa mjumbe wa Baraza la ITU ni pamoja na:

• Kuwa katika nafasi nzuri ya kutambua fursa zilizopo na hatimaye kunufaika na misaada na huduma zinazotolewa na Mashirika na pia kupata taarifa muhimu za miradi na shughuli za ITU kwa urahisi na haraka

• Kujua na kuratibu mwenendo wa teknolojia mpya ili kuandaa njia za utatuzi wa changamoto zake.

• Kukuza uwezo wa kiutendaji wa wataalamu nchini wanaoshiriki katika shughuli za Baraza ikiwa ni pamoja na kubadilishana ujuzi na uzoefu na nchi nyingine katika masuala mbalimbali.

• Kupata fursa ya kupokea na kuchambua taarifa mbalimbali za utendaji wa ITU, kutoa mapendekezo na kuboresha mwenendo wa Umoja. 

• Kuwasilisha mapendekezo ya nchi juu ya uendeshaji wa ITU.

• Kushawishi maamuzi yatolewayo na Baraza yasiwe na matokeo hasi kwa sekta ya mawasiliano.

• Kuitangaza nchi na kuchangia maendeleo ya sekta ya mawasiliano barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Mnauye (wa pili kutoka kulia) ukisubiri kutangazwa kwa matokeo ya kura ya uchaguzi wa Baraza la Shirika la Mawasiliano (ITU). Wengine katika picha, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza na kushoto kwa Mhe. Waziri Nape ni Katibu Mkuu wa Wizara ya  Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Ujumbe wa Tanzania ukishangilia ushindi baada ya kutangazwa kwa matokeo
Picha ys pamoja ya ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano Mkuu wa ITU, Bucharest, Romania


 

Monday, October 3, 2022

TANZANIA, CZECH KUIMARISHA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Jamhuri ya Czech zimekubaliana kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano hususan utalii, biashara na uwekezaji ili kukuza na kuimarisha misingi ya diplomasia iliyopo baina ya mataifa hayo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.), amebainisha hayo alipozungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Balozi Mbarouk amesema Tanzania ilisaini mkataba wa ushirikiano na Jamhuri ya Czech mwaka 2006 hivyo ni wakati muafaka wa kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano.

“Ni muda tangu tuliposaini mkataba wa makubaliano hivyo kwa sasa ni wakati muafaka baina yetu kuingia mkataba wa makubaliano katika maeneo mapya ya ushirikiano hususan katika sekta biashara na uwekezaji, Utalii,” amesema Balozi Mbarouk

Balozi Mbarouk ameongeza kuwa katika sekta ya utalii, miaka ya nyuma Tanzania ilikuwa inapokea watalii 6,000 kutoka Jamhuri ya Czech, na kwa kuwa maambuzi ya uviko 19 yamepungua duniani, Tanzania imeboresha mazingira ya utalii, biashara na uwekezaji.

Amewasihi watalii na wawekezaji kutoka Czech kuja kutalii na kuwekeza Tanzania.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa amesema Czech inajivunia ushirikiano wake imara na wa muda mrefu na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuahidi kuwa Czech itaendelea kudumisha ushirikiano huo.

“Nakuahidi kuwa tutaendelea kuwahamasisha watalii, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Czech kuja kutalii na kuwekeza Tanzania…..ni jukumu letu kuhakikisha kuwa sekta ya biashara na uwekezaji inakuwa na kunufaisha mataifa yote mawili,” amesema Mhe. Tlapa

Mhe. Tlapa ameahidi kuwa Czech itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mengine ya ushirikiano kama vile elimu, afya, kilimo, utamaduni na michezo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Tlapa yupo nchini kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 2 – 4, Oktoba 2022.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk  katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa  katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na ujumbe wa Jamhuri ya Czech unaoongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa  

DKT. TAX AWASILI WIZARANI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amewasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Naibu Waziri, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.), Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara.

Dkt. Tax ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Oktoba 2022 na kuapishwa tarehe 03 Oktoba 2022 Ikulu Jijini Dar es Salaam. 

Dkt. Tax amechukua nafasi ya Balozi Liberata Mulamula baada ya Mhe. Rais kufanya mabadiliko madogo kwenye Baraza la Mawaziri. 

Akizungumza baada ya kuwasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam, Mhe  Dkt. Tax amesema atashirikiana na watumishi wote wa Wizara katika kila ngazi ili kuhakikisha malengo ya Wizara yanatekelezwa kikamilifu.

“Nipo tayari kufanya kazi na nyinyi, na kujifunza kutoka kwenu ili kutekeleza majukumu yangu….. Taasisi yoyote ili iweze kufanikiwa lazima ifanye kazi kwa pamoja na kuwa na ushirikiano,” amesema Dkt. Tax

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokelewa na  Naibu Waziri, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipowasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na mmoja wa watumishi wa Wizara alipowasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Waziri, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk  na Katibu Mkuu, Balozi Joseph Sokoine. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Naibu Waziri, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk  wakimsikilza Katibu Mkuu, Balozi Joseph Sokoine alipokuwa akimkaribisha Dkt. Tax katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu, Balozi Joseph Sokoine katika picha ya pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu, Balozi Joseph Sokoine, Wakurugenzi wa Idara mbalimbali katika Wizara na baadhi ya watumishi katika picha ya pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika 
Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Sunday, October 2, 2022

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE CZECH AWASILI NCHINI KWA ZIARA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa amewasili nchi leo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 2 hadi 4 Oktoba 2022.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, Mhe. Tlapa amepokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na Balozi wa Tanzania nchi Ujerumani ambaye pia anawakilisha Jamhuri ya Czech, Mhe. Dkt. Abdallah Possi.

Akiwa nchini, Mhe. Tlapa kwa nyakati tofauti, atakutana kwa mazungumzo na Waziri wa Nchi-Tamisemi,  Waziri wa Afya,  Waziri wa Viwanda na Biashara, pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) pamoja na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Hospitali ya Jeshi la Wananchi (JWTZ).  

Tanzania na Czech zimekuwa zikishirikiana katika sekta za elimu,utamaduni, afya, biashara na uwekezaji.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa amewasili nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Tanzania nchi Ujerumani ambaye pia anawakilisha Jamhuri ya Czech, Mhe. Dkt. Abdallah Possi (wa kwanza kushoto) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa walipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa walipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme



TANZANIA, KOREA KUIMARISHA MISINGI YA USHIRIKIANO

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeeleza dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea ili kuimarisha zaidi misingi ya uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati ya nchi hizo.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) katika maadhimisho ya siku ya kuanzishwa kwa Taifa hill iliyofanyika  Jijini Dar es Salaam tarehe 1 Oktoba, 2022.

Mhe. Waziri Mulamula aliongeza kuwa Tanzania imekusudia kuendelea kuimarisha misingi ya uhusiano wake wa kidiplomasia uliopo kati yake na Jamhuri ya Korea kwa kuongeza maeneo ya ushirikiano katika sekta za maji, teknolojia, afya, elimu, nishati, usafirishaji na uchukuzi, pamoja na biashara na uwekezaji. 

“Mwaka huu tunatimiza miaka 30 ya uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano kati yetu, kudumu kwa ushirikiano huu muda wote ni ishara ya uhusiano mzuri uliopo baina yetu, tutaendelea kuulinda na kuuthamini ushirikiano huu nyakati zote kwa maslahi mapana ya nchi zetu mbili,” amesema Mhe. Balozi Mulamula

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Waziri Mulamula ameongeza kuwa Jamhuri ya Korea imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo kwa Tanzania kwa kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Ameongeza kuwa, Wakala wa Kukuza Biashara na Uwekezaji wa Korea (KOTRA), Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Korea (KOICA) pamoja na Benki ya EXIM ya Korea ni Taasisi ambazo zinashiriki katika harakati za kuchangia maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Naye Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini, Mhe. Kim Sun-Pyo amesema Tanzania imekuwa mdau mkubwa wa Jamhuri ya Korea kwa nyakati zote na kuahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa manufaa ya mataifa yote mawili.

“Tumekuwa tukishirikiana katika nyanja mbalimbali kama vile nishati, elimu, afya, maji na miundombinu hivyo ni matarajio yetu kuwa tutaendelea kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano hususan katika nyanja za biashara na uwekezaji ili kukuza uchumi wa mataifa yetu,” amesema Mhe. Balozi Sun-Pyo.

Mhe. Balozi Sun-Pyo amesema takwimu za biashara zinaonesha kuwa ujazo wa biashara kati ya Korea na Tanzania umeongezeka lakini bado tumekusudia kuongeza maeneo ya ushirikiano ili kuwawezesha wafanyabiashara na wawekezaji wa mataifa yote mawili kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika mataifa haya.

Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha misingi ya uhusiano wa muda mrefu uliopo kati yake.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akitoa hotuba yake ya ufunguzi wakati wa maadhimisho ya siku ya kuanzishwa kwa Taifa hill iliyofanyika  Jijini Dar es Salaam tarehe 1 Oktoba, 2022

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akitoa hotuba yake ya ufunguzi wakati wa maadhimisho ya siku ya kuanzishwa kwa Taifa hill iliyofanyika  Jijini Dar es Salaam tarehe 1 Oktoba, 2022








BIASHARA TANZANIA, NIGERIA YAONGEZEKA

Biashara kati ya Tanzania na Nigeria imeongezeka kutoka shilingi bilioni 23 mwaka 2020 hadi shilingi bilioni 24 mwaka 2021. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb.) alipokuwa akishiriki katika hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Nigeria yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam

Balozi Mulamula ameongeza kuwa takwimu za biashara na uwekezaji zinatia moyo kuona kiwango cha biashara kati ya nchi zetu mbili kimeendelea kuongezeka, kutoka shilingi bilioni 23 mwaka 2020 hadi shilingi bilioni 24 mwaka 2021. Kuhusu uwekezaji, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesajili Kampuni 23 za Nigeria ambazo zimewekeza Tanzania kwa uwekezaji wa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 466.50 na kutoa takriban ajira 1,734.

“Nangependa kutumia fursa hii kuhimiza jumuiya zetu za wafanyabiashara kuangalia fursa za biashara zinazopatikana katika nchi hizi mbili (Tanzania na Nigeria). Serikali ya Tanzania imefungua milango yake kwa mtu yeyote karibuni kuwekeza,” amesema Balozi Mulamula

Tanzania na Nigeria zinashirikiana kwa karibu kukuza Ajenda ya mwaka 2030 ya Umoja wa Afrika. Hii inalazimu, miongoni mwa mambo mengine, kukuzwa kwa jamii zenye amani, usawa, na ajenda ya maendeleo ya bara la Afrika na watu wake.

Kwa Upande wake Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Hamisu Umar Takalmawa amesema kuwa Nigeria inajivunia kuwa rafiki wa Tanzania kwani mataifa haya yamekuwa yakishirikiana kijamii katika masuala ya utamaduni, muziki, nyimbo na tamthilia....n.k

“Ushirikiano na umoja baina ya Nigeria na Tanzania umekuwa na misingi imara ya kukuza na kuimarisha diplomasia baina ya mataifa yetu mawili,” amesema Balozi Takalmawa

Balozi Takalmawa ameongeza kuwa biashara kati ya Nigeria na Tanzania imeongezeka ikilinganishwa na miaka iliyopita, kadhalika uwekezaji nao umeongezaka jambo ambalo linaashiria mazingira bora ya biashara na uwekezaji. Mbali na kuadhimisha siku ya Uhuru wa Nigeria, pia Waziri Mulamula alizindua maktaba katika ofisi za Ubalozi wa Nigeria hapa nchini. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Hamisu Umar Takalmawa katika Ofisi za Ubalozi wa Nigeria Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwasilisha hotuba yake wakati wa maadhimisho ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Nigeria yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula pamoja na Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Hamisu Umar Takalmawa wakikata utepe wa kufungua maktaba ya ubalozi wa Nigeria katika Ofisi za ubalozi huo Jijini Dar es Salaam



Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Hamisu Umar Takalmawa akikabidhi nakala ya kitabu kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula baada ya kufungua maktaba ya ubalozi huo Jijini Dar es Salaam

Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na baadhi ya mabalozi walioshiriki katika maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Nigeria yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam 





Saturday, October 1, 2022

TANZANIA YAJIVUNIA USHIRIKIANO WAKE NA CHINA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema inaendelea kujivunia ushirikiano wake na Serikali ya Watu wa China kwa vitendo zaidi kwa maslahi ya pande zote mbili. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula, (Mb.) katika hafla ya maadhimisho ya miaka 73 ya uhuru wa China iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Katika maadhimishio hayo, Balozi Mulamula na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian, walipanda miti katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam ikiwa ni ishara ya ushirikiano mzuri uliopo baina ya mataifa hayo. 

Balozi Mulamula pamoja na mambo mengine, amesema kuwa Tanzania iko tayari kufanya kazi na China ili kuendeleza na kutekeleza kikamilifu Mpango wa Maendeleo wa Ulimwengu na Mpango wa Usalama wa Ulimwengu katika kuimarisha ushirikiano wa pande zote.

“Tunapoadhimisha miaka 73 ya kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China, tunaadhimisha miaka 61 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi zetu mbili. Tanzania na China ni marafiki wa wakati wote, katika shida na raha,” amesema Balozi Mulamula.

Kwa upande wake, Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Chen Mingjian amesema uhusiano wa China na Tanzania umekuwa ukiendelea kukua kwa kasi na kufikia viwango vya juu kutokana na misingi imara inayosimamiwa na Viongozi wa mataifa haya mawili.

Viongozi wetu, Rais wa China Mhe. Xi Jinping na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wanajali na kuongoza maendeleo ya uhusiano wa mataifa yao kwa maslahi ya pande zote mbili.

“China na Tanzania zimekuwa zikifurahia uhusiano ulioasisiwa na Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa China na Baba wa Taifa hilo Hayati Mao Zedong,” amesema Balozi Mingjean

Balozi Mingjean ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka 73 ya uhuru wa China, kumekuwa na ongezeko la miradi ya ushirikiano baina ya China na Tanzania ambapo ongezeko hilo limekuwa chachu ya maendeleo.

Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana katika nyanja mbalimbali zikiwemo, afya, mawasiliano, elimu, uchumi wa kidijitali, biashara na uwekezaji, miundombinu pamoja na utekelezaji wa miradi midogo ya kujikimu kimaisha inayoweza kuwanufaisha wananchi. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula pamoja na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian wakimwagilia maji kwenye mti walioupanda katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian wakipanda mti katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea katika hafla ya upandaji mti katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja