Friday, November 18, 2022

DKT. MWINYI: MABALOZI JENGENI UHUSIANO MZURI NA SEKTA ZA UMMA, BINAFSI

 



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwahutubia Mabalozi wa Tanzania Nje ya Nchi wakati wa mkutano uliofanyika Zanzibar 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasilisha salamu za Wizara kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa Mkutano wa mabalozi wa Tanzania Nje ya Nchi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wizara wakati wa mkutano kati ya Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi na Mabalozi 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akitoa neno la utangulizi  wakati wa mkutano kati ya Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi na Mabalozi 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga  akizungumza kama mshereheshaji wakati wa mkutano kati ya Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi na Mabalozi 

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia mkutano kati yao na Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia mkutano kati yao na Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi

Meza Kuu ikiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika picha ya pamoja Uongozi na Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi ya mkutano




MABALOZI WATEMBELEA BANDARI YA MALINDI


Amidi wa Mabalozi Tanzania Mhe.Dkt. Asha-Rose Migiro (aliyeshika Mic) akiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab (kushoto) akizungumza katika ziara ya kutembelea eneo la ujenzi wa bandari ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini wakati Mabalozi wa Tanzania walioko mkutanoni Zanzibar walipotembelea Shirika la Bandari Zanzibar ili kujionea shirika hilo linavyofanya kazi

Amidi wa Mabalozi Tanzania Mhe.Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtumishi wa Shirika la Bandari Zanzibar (hayuko pichani)  kwa Mabalozi wa Tanzania waliotembelea eneo la ujenzi wa bandari ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja  Zanzibar


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar Bw. Nahmat Mahfoudh akizungumza na Mabalozi Tanzania waliotembelea eneo la ujenzi wa bandari ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja 


Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohamed Mahmoud akizungumza na Mabalozi Tanzania waliotembelea eneo la ujenzi wa bandari ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja

 Mabalozi Tanzania wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab akiwa na mabalozi wa Tanzania wakisikiliza maelezo kutoka kwa Viongozi wa Shirika la Bandari Zanzibar walipotembelea eneo la ujenzi wa bandari ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja

 

Balozi wa Tanzania nchini Uhlonzi Mhe. Caroline Chipeta (katikati) akiwa na baadhi ya wajumbe wa Menejiment ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati Mabalozi wa Tanzania  walipotembelea eneo la Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja ambako Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepanga kujenga Bandari mpya  na ya kisasa
 


Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki Mkutano wa Mabalozi unaofanyika mjini Zanzibar wametembelea bandari ya Malindi leo tarehe 17 Novemba 2022 na kujionea jinsi bandari hiyo inavyofanya kazi.


Mabalozi hao pia wametembelea eneo la Mangapwani ambako Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepanga kujenga bandari kubwa mpya na ya kisasa ambayo itaipunguzia mzigo bandari ya Malindi.
Katika ziara hiyo iliyoongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab imewawezesha Mabalozi hao kujionea jinsi bandari ya Malindi inavyofanya kazi na hivyo kusaidia juhudi za kukuza uchumi wa Zanzibar

Akizungumza na mabalozi hao katika bandari ya Malindi na eneo la Mangapwani, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar Bw. Nahmat Mahfoudh amesema bandari ya Malindi kwa sasa imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya kupokea makontena mengi na makubwa na meli za kisasa kuliko uwezo wa bandari hiyo ambao ujenzi wake hauruhusu kupokea meli na contena hizo.

 ‘‘Bandari hii inakabiliwa na changamoto ya ufinyu wa nafasi na uwezo wa kuhudumia meli na makontena makubwa, kwa hiyo bandari hii itabakia kuwa bandari ya meli za abiria kati ya Zanzibar na Dar es Salaam, kiufupi hii itakuwa bandari ya kitalii’’, alisema Bw. Mahfoudh.

Amesema wameamua kujenga bandari ya mangapwani ili iweze kwenda na mahitaji ya nyakati hizi kwa kuwa uwezo wake ni kupokea Tus 80,000 lakini bandari mpya itakayojengwa Mangapwani itakuwa na uwezo wa kupokea Tus 800,000 hadi 1,800,000. 

Akiongelea changamoto zinazolikabili Shirika la Bandari Zanzibar Bw. Mahfoudh amesema bado wanapambana kuondokana na madhara yaliyotokana na janga la Covid 19 ambalo limelilitea shirika madhara makubwa.

Akizingumza katika ziara hiyo, Amidi wa Mabalozi nchini, Mhe.Dkt. Asha-Rose Migiro amelishukuru Shirika la Bandari kwa kuwapokea na kuzungumza nao na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya. 

Amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa utayari wake wa kuwa na Miradi ya kimkakati kama huo wa bandari ya Mangapwani uliopangwa kufanyika katika mkoa wa Kaskazini 

Amesema kwa niaba ya mabalozi wenzake wanaahidi kuwa Mabalozi wazuri ambao wataendelea na kazi ya kuwavutia na kuwashawishi wawekezaji wenye mitaji mikubwa ili kuweza kutimiza nia na dhamira ya kuiendeleza Zanzibar.

Thursday, November 17, 2022

MABALOZI WANAWAKE WAAHIDI KUIUNGA MKONO TAASISI YA ZMBF

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi amewahamasisha Mabalozi wanawake wa Tanzania kuiunga mkono Taasisi hiyo ili kuiwezesha kufikia malengo yake ya kuwasaidia watoto na kuwakwamua kiuchumi wanawake na vijana wa Zanzibar.

Mhe. Mama Mwinyi ametoa rai hiyo tarehe 17 Novemba, 2022 alipokutana na Mabalozi Wanawake wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi katika makazi yake mjini Zanzibar.

Amesema Taasisi hiyo ambayo aliianzisha mwezi Julai 2021 imejikita katika kutekeleza malengo makuu manne ambayo  ni Kuwainua Kiuchumi Wanawake wakulima wa zao la Mwani; Kuboresha upatikanaji wa Lishe bora kwa wanawake wajawazito na watoto;  Kuboresha mazingira ili kuwalinda wasichana na wavulana dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia; na Kuiimarisha taasisi ya ZMBF ili kuiwezesha kuwa endelevu na yenye matokeo chanya kwa jamii.

Ameongeza kuwa  ili kuwakwamua kiuchumi wanawake wakulima wa zao la mwani ambao ni asilimia 80 ya wakulima wote wa zao hilo, jitihada za pamoja zinahitajika ili kuliongezea thamani zao hilo ili liwanufaishe zaidi wakulima hao kuliko ilivyo hivi sasa.

Mhe. Mariam ameongeza kuwa, katika kuimarisha afya ya watoto wa kike pamoja na kukuza kiwango cha ufaulu kwa watoto hao, Taasisi hiyo imeanzisha Program ya hedhi salama kwa kutengeneza taulo za kike ambazo ni rafiki kwa mazingira.

“Taasisi yetu ina takribani mwaka mmoja tangu ianzishwe, tumejikita kuimarisha lishe kwa kina mama wajawazito na watoto na kuwasaidia wanawake wakulima wa mwani. Lakini pia tumejielekeza katika kuboresha elimu kwa watoto wa kike kwa kuwatengenezea taulo za kike ili kupunguza utoro mashuleni unaotokea wakati watoto hao wakiwa hedhi. Hivyo tunaomba mtuunge mkono nyinyi binafsi na kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kwenye maeneo yenu ya uwakilish ili tufikie malengo yetu” alisema Mhe. Mariam. 

Kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, Mhe. Mama Mwinyi amesema Taasisi yake hutoa elimu kwa wanawake ya namna ya kujilinda na kuwalinda watoto pamoja na kuwahamasisha kutoa taarifa ya matukio ya ukatili wanayofanyiwa ili sheria ichukue mkondo wake. Pia taasisi hiyo imeanzisha nyumba maalum ambayo huwasaidia wahanga wa matukio ya ukatili ambapo wakiwa hapo hujengewa uwezo kwa kupatiwa ujuzi wa fani mbalimbali ili kujikimu kimaisha pamoj ana kupatiwa msaada wa kisheria.

Kwa upande wao, Mabalozi hao walipongeza jitihada zinazofanywa na Mhe. Mama Mariam kupitia Taasisi hiyo na kueleza utayari wao wa kuisaidia ili kuiwezesha kutimiza malengo yake ambayo mengi ni miongoni mwa masuala yanayopewa kipaumbele katika majukwaa ya kikanda na kimataifa.

Mabalozi wa Tanzania wapo Zanzibar kushiriki Mkutano kati yao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan unaofanyika kisiwani humo kuanzia tarehe 14 hadi 21 Novemba, 2022.

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi akizungumza na Mabalozi wanawake wa Tanzania alipokutana nao ofisini kwake mjini Zanzibar

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi akizungumza na Mabalozi wanawake wa Tanzania alipokutana nao ofisini kwake mjini Zanzibar. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab. 

Balozi wa Tanzania na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa - Geneva, Mhe. Maimuna Tarishi akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Mabalozi na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi tarehe 17 Novemba, 2022  
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akieleza jambo katika Mkutano wa Mabalozi na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi tarehe 17 Novemba, 2022 

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme akichangia mada katika Mkutano wa Mabalozi na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi tarehe 17 Novemba, 2022 

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi akiagana na mabalozi baada ya kumaliza kikao baina yake na mabalozi hao 

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi katika picha ya pamoja na mabalozi wanawake

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora (ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi katika picha ya pamoja na mabalozi wanawake





TANZANIA, OMAN KUENDELEZA USHIRIKIANO

Tanzania imeahidi kuendelea kushirikiana na Oman katika kutekeleza makubaliano mbalimbali yaliyofikiwa  wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Samia Suluhu Hassan aliyoifanya nchini humo mwezi Juni 2022 ili kuimarisha ushirkiano baina ya nchi hizo mbili.

Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (MB.) alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan katika Ofisi za Wizara Zanzibar.

Wakati wa kikao hicho ambacho pamoja na mambo mengine, kilifanyika ili kutathmini utekelezaji wa makubaliano na maelekezo yaliyotolewa na viongozi wakuu wakati wa ziara hiyo, Mhe. Mbarouk amesema baadhi ya maeneo tayari yameanza kufanyiwa kazi ikiwemo maagizo ya kuandaa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Desemba 2022.

Kadhalika, Balozi Mbarouk ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuonesha utayari wa kuanza kuchimba visima 100 vya maji Tanzania Bara pamoja na  kujenga Hospitali katika eneo la Mahonda kwa upande wa Zanzibar ambapo kinachosubiriwa ni mchoro utakaowasilishwa kabla ya kuanza ujenzi wa hospitali hiyo.

Kwa upande wake, Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan amesema Oman imeweka utaratibu wa kuchimba visima 20 kila mwaka ambavyo vitaanza kuchimbwa katika kipindi cha miezi mitatu ijayo kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo.

Kukutana kwa viongozi hao kumelenga kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Oman pamoja na kufuatilia masuala waliyokubaliana wakuu wa nchi hizo mbili wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan nchini Oman mwezi Juni 2022.

Pia viongozi hao wamejadili utekelezaji wa mikataba mbalimbali iliyosainiwa na pande hizo mbili wakati wa ziara hiyo.

Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara - Zanzibar

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimfafanua jambo Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan  walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara - Zanzibar

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan katika Ofisi za Wizara - Zanzibar

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Oman uliongozwa na Balozi wa Oman nchini, Mhe. Saud bin Hilal bin Saud al Shidhan katika Ofisi za Wizara - Zanzibar



WAZIRI SORAGHA: ZANZIBAR NI ENEO BORA KWA UWEKEZAJI

    

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe akitoa neno kuhusu uwekezaji katika sekta ya uchumi wa buluu Zanzibar
Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea, Mhe. Togolany Mavura akichangia jambo kuhusu mada ya uwekezaji katika sekta ya uchumi wa buluu

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Abdallah Possi akichangia mada kuhusu uwekezaji katka uchumi wa buluu  Zanzibar.

Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Humphrey Polepole akitoa neno kuhusu uwekezaji katika uchumi wa buluu Zanzibar.



 



WIZARA KUSHIRIKIANA NA SMZ KUTEKELEZA AGENDA ZA KIKANDA, KIMATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amesema Wizara anayoiongoza itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kuhakikisha agenda mbalimbali za kikanda na kimataifa zinawanufaisha wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Mhe. Dkt. Tax ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Novemba, 2022 wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu, Mhe. Jamal Kassim Ali, Ikulu Zanzibar.

Mhe. Waziri Tax amemtembelea Mhe. Jamal, Ofisini kwake Ikulu Zanzibar kwa lengo la kumsalimia na kubadilishana naye mawazo ya namna ya kuimarisha ushirkikiano kati ya Wizara na Ofisi yake.

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Tax amemwahidi ushirikiano Waziri Jamal na kumshukuru kwa kupata fursa hiyo muhimu ambayo inalenga kuendelea kuboresha utekelezaji wa majukumu ya Wizara hususan katika masuala ya kikanda na kimataifa kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Waziri Tax ameongeza kuwa Wizara anayoiongoza inaendelea kutekeleza kikamilifu maelekezo yote yaliyotolewa kwao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuhusu kuzipa kipaumbele hoja za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye majukwa ya kikanda na kimataifa pamoja na kuwashirikisha Diaspora katika kuchangia maendeleo ya Taifa.

“Mhe. Waziri leo nimekuja kwa ajili ya kukusalimia kwa vile nipo hapa Zanzibar na Mabalozi wa Tanzania wote tukiendelea na Mkutano. Nakuahidi kufanya kazi kwa pamoja kwa nguvu mpya ili kuhakikisha hoja zote za kipaumbele za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinakuwa na tija katika majukwaa ya kikanda na kimataifa kwa manufaa ya pande zote na bila kuwasahau Diaspora wetu” amesema Dkt. Tax.

Kwa upande wake, Mhe. Jamal ambaye Ofisi yake pamoja na mambo mengine, ina jukumu la kusimamia masuala ya kikanda na kimataifa amemshukuru Dkt. Tax kwa kutenga muda na kumtembelea na kwa namna ya pekee alishukuru ushirikiano anaoupata kutoka Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ya Zanzibar.

Pia alieleza kuwa, ipo haja ya kuimarisha zaidi ushirikiano ulipo ili kupeleka maazimio ya pamoja kwenye majukwaa ya kikanda na kimataifa na kwamba Ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano wote utakaohitajika.

Kuhusu Diaspora alisema tayari Ofisi yake imeandaa Sheria na sasa wanaendelea na zoezi la kuwatambua. Hivyo aliomba kuendeleza ushirikiano wa pamoja ili kuendelea kuwatambua, kuwasimamia na kuwaratibu ili kuwawezesha kuchangia kikamilifu maendeleo ya Taifa.

“Naomba tuendelee na ushirikiano huu ili tuweze kuwaunganisha pamoja Diaspora wetu pamoja na kuwatambua kwa usahihi ili kuweza kuwasimamia na kuwaratibu katika kuchangia maendeleo ya taifa letu,” amesema Mhe. Jamal

Dkt. Tax yupo Zanzibar kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Sita wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mabalozi wa Tanzania unaofanyika Kisiwani humo kuanzia tarehe 14 hadi 21 Novemba 2022. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu, Mhe. Jamal Kassim Ali akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax wakati  alipomtembelea Ofisini kwake Ikulu Zanzibar 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu, Mhe. Jamal Kassim Ali akieleza jambo wakati wa kikao chake na mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax Ofisini kwake Ikulu Zanzibar 

Kikao baina ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu, Mhe. Jamal Kassim Ali na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax kikiendelea 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akieleza jambo wakati wa kikao chake na mwenyeji wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu, Mhe. Jamal Kassim Ali, Ikulu - Zanzibar 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akieleza jambo wakati wa kikao chake na mwenyeji wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu - Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu - Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali akimsindikiza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kumaliza kikao chao Ikulu, Zanzibar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu - Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali akiagana na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kumaliza kikao chao Ikulu, Zanzibar



DKT. TAX AIPONGEZA SERIKALI YA UAE KWA KUFUNGUA UBALOZI MDOGO ZANZIBAR

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena  Tax amepongeza uamuzi wa Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) wa kufungua Konseli Kuu (Ubalozi Mdogo) Visiwani Zanzibar na kutoa wito kwa Wananchi kutumia uwepo wa Konseli hiyo kuboresha ushirikiano katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, utalii na masoko kwa bidhaa za Tanzania.

 

Mhe. Dkt. Tax ametoa pongezi hizo hivi karibuni wakati akipokea Hati za Utambulisho za Konseli Mkuu wa UAE, Zanzibar   Mhe. Balozi Saleh Ahmed Alhemeiri katika hafla fupi iliyofanyika katika Ofisi za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Zanzibar.

 

Amesema hatua hiyo ni muhimu sana katika kuimarisha ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na UAE kwani  sasa fursa nyingi zilizopo Zanzibar ikiwemo utalii, uchumi wa buluu na biashara vitashamiri zaidi na kukua.



Ameongeza kusema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali  ya Awamu ya Nane ya Zanzibar chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  zimeendelea kuimarisha ushirikiano na nchi mbalimbali pamoja na kutafuta fursa za biashara, utalii, uwekezaji  na masoko kwa bidhaa za Tanzania ili kuiwainua kiuchumi watanzania wote.

 

Ameongeza kwamba kufunguliwa kwa Konseli Kuu hiyo ni matokeo ya ziara mbalimbali za viongozi hao nchini humo ikiwemo ile ya Mhe. Rais Samia aliyoifanya nchini UAE mwezi Februari 2022 wakati wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dubai Expo 2020.

 

Pia amesema wakati wa ziara hiyo, pamoja na mambo mengine, Mikataba na Hati za Makubaliano mbalimbali  zilisainiwa kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

 

"Napongeza kwa dhati uamuzi wa Serikali ya UAE wa kufungua Konseli Kuu au Ubalozi mdogo hapa Zanzibar. Ni imani yangu kuwa, uwepo wa Konseli Kuu hii utasaidia kuharakisha utekelezaji wa masuala mbalimbali ya ushirikiano ambayo tayari yamekubalika kwa manufaa ya pande hizi mbili" alisema Dkt. Tax.

 

Akitaja maeneo ya kipaumbele ya ushirikiano kwa upande wa Zanzibar, Mhe. Waziri Tax amesema ni pamoja na Uchumi wa Buluu hususan katika uvuvi wa bahari kuu, utalii, biashara na uwekezaji kwa ujumla.



Pia Mhe. Dkt Tax amemhakikishia ushirikiano Balozi huyo na kwamba ana imani kuwa kupitia yeye masuala mengi yatakamilika.

 

" Tutashirikiana na wewe kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa kati ya nchi hizi mbili hususan kwa upande wa Zanzibar yanatekelezwa na kama ulivyosema awali kwa kiasi fulani Zanzibar inafanana na Dubai, basi tujielekeze kuigeuza  Zanzibar  kuwa  Dubai ya Afrika" alisema Dkt. Tax.

 

Kwa upande wake, Mhe.  Alhemeiri amesema amefarijika kuwepo Zanzibar na kwamba yupo tayari kushirikiana na Serikali hiyo katika kukuza biashara, kilimo, elimu, na uchumi wa buluu kwani zipo fursa lukuki katika Kisiwa hiki zinazohitaji kuendelezwa.

 

"Nia yetu ni kushirikiana na Serikali kukiendeleza Kisiwa kizuri cha  Zanzibar. Nimeona zipo fursa nyingi za kufanyia kazi. Nitajikita zaidi kwenye masuala ya utalii, biashara, elimu, uchumi wa buluu na usafirishaji kwa kuzishawishi mamlaka za UAE kuongeza safari za moja kwa moja za Mashirika ya Ndege ya UAE kuja Zanzibar ili kukuza utalii, alisema Mhe. Alhemeiri. 



Mhe. Dkt. Tax yupo mjini Zanzibar kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Sita wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mabalozi wa Tanzania unaofanyika Kisiwanio humo kuanzia tarehe 14 hadi 21 Novemba 2022. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Visiwani Zanzibar, Mhe. Balozi Saleh Ahmed Alhemeiri. Hafla hiyo fupi imefanyika hivi karibuni katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Zanzibar. Mhe. Dkt. Tax yupo mjini Zanzibar kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Sita wa Mabalozi wa Tanzania unaoendelea mjini hapo kuanzia tarehe 14 hadi 21 Novemba 2022

Mhe. Dkt. Tax akizungumza na Mhe. Alhemeiri mara baada ya kupokea hati za utambulisho. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Dkt. Tax alipongeza uamuzi wa Serikali wa kufungua Konseli Kuu Zanzibar na kutoa wito kwa watanzania kutumia uwepo wa Ofisi hiyo kuimarisha ushirikiano

Mhe. Dkt. Tax akiagana na Mhe. Alhemeiri mara baada ya kumaliza mazungumzo.

Mhe. Dkt. Tax na Mhe. Alhemeiri wakiwa kati picha ya pamoja
Mhe. Dkt. Tax na Mhe. Alhemeiri wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemed Mgaza (kulia) na Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mariam Mrisho (kushoto)

Picha ya pamoja







 

Wednesday, November 16, 2022

MABALOZI WAAINISHA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI





Sehemu ya waheshimiwa mabalozi wakifuatilia majadiliano katika Mkutano wa Mheshimiwa Rais na Mabalozi unaofanyika tarehe 14 – 21 Novemba, 2022 Zanzibar.

Sehemu nyingine ya Waheshimiwa mabalozi wakifuatilia majadiliano katika Mkutano wa Mheshimiwa Rais na Mabalozi unaofanyika tarehe 14 – 21 Novemba, 2022 Zanzibar.

Viongozi Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na mabalozi wakifuatilia kikao katika Mkutano wa Mheshimiwa Rais na Mabalozi unaondelea Zanzibar.

Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ukiongozwa na Waziri Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Fatma Rajab katika picha ya pamoja na mabalozi wa Tanzania Nje ya nchi