Wednesday, January 11, 2023

DKT. TAX AKUTANA NA BALOZI WA INDIA, DPRK NA MWAKILISHI WA HUAWEI-TANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax amekutana kwa mazungumzo kwa nyakati tofauti na wageni kadhaa waliomtembelea ofisini kwake Mtumba  jijini Dodoma.

Wageni hao ni Balozi wa India nchini, Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea, Mhe. Kim Young Su na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian.

Akizungumza na Balozi wa India nchini Mhe. Dkt. Tax amemshukuru Balozi huyo kwa kutenga muda wa kumtembelea kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kwenye wadhifa huo na kueleza kwamba ziara hiyo itamwezesha kuelewa kwa kina hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ushirikiano kati ya Tanzania na India na pia kubadilishana  mawazo ya namna ya kufanikisha masuala mbalimbali yaliyokubalika katika ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.

Amesema Tanzania na India zinashirikiana katika Sekta mbalimbali zenye umuhimu kwa  wananchi ikiwemo Sekta ya maji, elimu, teknolojia na  afya na kwamba ni wakati sasa kwa nchi hizi mbili kuendelea kutekeleza kwa kasi makubaliano mbalimbali ambayo tayari yamefikiwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 “Ushirikiano wetu unaenda vizuri na mambo tunayokubaliana kushirikiana na kufanyia kazi kwa pamoja yanaenda, zaidi tuongeze kasi kuyatekeleza. Niwahakikishie kuwa tutaaendelea kushirikiana ili kuendeleza uhusiano wetu ambao ni wa kidugu na kihistoria, ambao umekuwepo kwa miaka mingi,” amesema Dkt. Tax.

Naye Balozi wa India Mhe. Binaya Pradhan  ameeleza kuridhishwa kwake na ushirikiano anaoupata nchini katika kutekeleza majukumu yake na kueleza kwamba Serikali ya India kupitia Hospitali ya Apolo wamekubali kushirikiana na Hospitali ya Muhimbili kupitia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Hospitali ya Bugando ya jijini Mwanza na Taasisi ya Saratani ya Ocean  Road ya jijini Dar es Salaam katika kutoa huduma na kuwajengea uwezo watumishi katika hospitali hizo ili kusaidia wananchi wa Tanzania.

Kuhusu sekta ya elimu,  Balozi huyo amesema wamekuwa wakishirikiana na Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam (DIT) katika kukiboresha ili kukiwezesha kuwa Kituo bora cha utoaji wa huduma za teknolojia ya habari na mawasiliano nchini.

Akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea Mhe. Dkt. Tax amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi hiyo katika sekta kama kilimo, elimu afya na teknolojia ya habari na mawasiliano.

Kwa upande wake, Balozi Kim Young Su amempongeza Mhe. Dkt. Tax kwa kuteuliwa kwenye wadhifa huo ikiwa ni mara yake ya kwanza kukutana naye na kumwahidi ushirikiano. Pia amesema kuwa, Nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali.

Akizungumza na Naibu Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania Mhe. Tax ameipongeza kampuni hiyo kwa uwekezaji wao katika masuala ya Teknolojia hususan kupitia mradi wao wa kusambaza huduma za kidigitali vijijini.

“ Huawei ni Kampuni kubwa na tunathamini uwepo wenu hapa nchini. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ni mingoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo tutaendelea kushirikiana nanyi hususan kwenye kusambaza huduma za kidigitali vijijini na vyuoni ili hatimaye tuweze kufikia ndoto yetu ya kuwa kitovu cha kidigitali,” alisema Mhe. Dkt. Tax.

Kwa upande wake, Bw. Tao Mian alieleza kwamba hapa nchini Kampuni hiyo imetengeneza ajira zaidi ya 1000 ambapo zaidi ya asilimia 70 ya ajira ni za watanzania.Kadhalika Kampuni hiyo inashirikiana na  zaidi ya kampuni 70 za ndani, Wahandisi wa TEHAMA zaidi ya 2000 nchi nzima pamoja na vyuo zaidi ya 19 nchini. Aidha, Kampuni hiyo inaendesha mafunzo ya TEHAMA kwa zaidi ya wanafunzi 2000, kuhudumia zaidi ya asilimia 75 ya watanzania na kwamba imekuwa mchangiaji mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya TEHAMA nchini.

“Tunaridhishwa na uungwaji mkono wa Kampuni yetu hapa Tanzania na tunaahidi kuendelea kuchapa kazi ili kuhakikisha huduma za kidigitali zinawafikia wananchi wengi kwa wakati mmoja hususan wale wa vijijini” alisema Bw. Mian.

Pia alimueleza Mhe. Dkt Tax juu ya Mpango kabambe wa kuboresha mawasiliano ya TEHAMA vijijini ambao ni sehemu ya Mkataba wa ushirikiano uliosainiwa baina ya Tanzania na China ambao unatarajiwa kutekelezwa na Kampuni hiyo. Katika mradi huo kutakuwa na jumla ya miradi 19 ya kipaumbele, uboreshaji wa mawasiliano vijijini, usambazaji wa umeme Kaskazini Mashariki mwa Tanzania pamoja na miradi 9 ya msaada ambayo itatekelezwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA) na Hospitali ya Zanzibar.

Kampuni ya Huawei Tanzania ambayo imewekeza kwa zaidi miaka 15 nchini, inashirikiana na Kampuni ya Mawasiliano ya Simu Tanzania (TTCL) kusambaza Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ili kuwezesha huduma za kidigitali kupatikana kwa urahisi nchi nzima ambapo hadi sasa mkongo huo umesambaa kwa zaidi ya kilomita 15,000 nchi nzima.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa India nchini Mhe Binaya Pradhan, alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma hivi karibuni.


Mhe. Dkt. Tax akimsikiliza Balozi Mhe Binaya Pradhan wakati wa mazungumzo kati yao yaliyofanyika ofisini kwake jijini Dodoma. Kushoto ni Kaimu mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Halmenshi Lunyumbu.

Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa India nchini (kulia) akiwa na Naibu Balozi wa Ubalozi huo wakati wa mazungumzo kati yake na Mhe. Dkt. Tax

Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa India nchini akimkabidhi Mhe. Dkt. Tax zawadi ya kasha la kuhifadhia vitu.
Mhe. Dkt. Tax akiagana na Balozi Mhe Binaya Pradhan mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao
Mhe. Dkt. Tax na Mhe. Balozi Mhe Binaya Pradhan wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki mazungumzo yao 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea nchini, Mhe.  Kim Young Su alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma hivi karibuni

Mhe. Dkt. Tax akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Kim Young Su 

Mhe. Dkt. Tax akiagana na Mhe. Kim Young Su mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao

Picha ya pamoja
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe hivi karibuni

Mhe. Dkt. Tax akiendelea na mazungumzo na  Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian. Walioketi kushoto kwa Mhe. Waziri ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Magabilo Murobi na Afisa katika Idara hiyo, Bw. Herman Berege.

Picha ya pamoja
Mhe. Dkt. Tax akiagana na Bw. Tao Mian mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao

 

VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE SOUTHERN AFRICAN DEVELOPMENT COMMUNITY






 

Tuesday, January 10, 2023

DKT. TAX AKUTANA NA BALOZI WA INDIA, DPRK NA MWAKILISHI WA HUAWEI-TANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax amekutana kwa mazungumzo kwa nyakati tofauti na wageni kadhaa waliomtembelea ofisini kwake Mtumba  jijini Dodoma.

Wageni hao ni Balozi wa India nchini, Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea, Mhe. Kim Young Su na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian.

Akizungumza na Balozi wa India nchini Mhe. Dkt. Tax amemshukuru Balozi huyo kwa kutenga muda wa kumtembelea kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kwenye wadhifa huo na kueleza kwamba ziara hiyo itamwezesha kuelewa kwa kina hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ushirikiano kati ya Tanzania na India na pia kubadilishana  mawazo ya namna ya kufanikisha masuala mbalimbali yaliyokubalika katika ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.

Amesema Tanzania na India zinashirikiana katika Sekta mbalimbali zenye umuhimu kwa  wananchi ikiwemo Sekta ya maji, elimu, teknolojia na  afya na kwamba ni wakati sasa kwa nchi hizi mbili kuendelea kutekeleza kwa kasi makubaliano mbalimbali ambayo tayari yamefikiwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 “Ushirikiano wetu unaenda vizuri na mambo tunayokubaliana kushirikiana na kufanyia kazi kwa pamoja yanaenda, zaidi tuongeze kasi kuyatekeleza. Niwahakikishie kuwa tutaaendelea kushirikiana ili kuendeleza uhusiano wetu ambao ni wa kidugu na kihistoria, ambao umekuwepo kwa miaka mingi,” amesema Dkt. Tax.

Naye Balozi wa India Mhe. Binaya Pradhan  ameeleza kuridhishwa kwake na ushirikiano anaoupata nchini katika kutekeleza majukumu yake na kueleza kwamba Serikali ya India kupitia Hospitali ya Apolo wamekubali kushirikiana na Hospitali ya Muhimbili kupitia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Hospitali ya Bugando ya jijini Mwanza na Taasisi ya Saratani ya Ocean  Road ya jijini Dar es Salaam katika kutoa huduma na kuwajengea uwezo watumishi katika hospitali hizo ili kusaidia wananchi wa Tanzania.

Kuhusu sekta ya elimu,  Balozi huyo amesema wamekuwa wakishirikiana na Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam (DIT) katika kukiboresha ili kukiwezesha kuwa Kituo bora cha utoaji wa huduma za teknolojia ya habari na mawasiliano nchini.

Akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea Mhe. Dkt. Tax amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi hiyo katika sekta mbalimbali ambazo tayari nchi hizi mbili zinashirikiana ikiwemo kilimo, elimu afya na teknolojia ya habari na mawasiliano na utamaduni.

Kwa upande wake, Balozi Kim Young Su amempongeza Mhe. Dkt. Tax kwa kuteuliwa kwenye wadhifa huo ikiwa ni mara yake ya kwanza kukutana naye na kumwahidi ushirikiano. Pia amesema kuwa, Nchi yake itaendelea kushirkiana na  Tanzania katika sekta mbalimbali na kwamba ushirikiano wa kihistoria uliopo ambao umejengwa katika misingi iliyoachwa na waasisi wa mataifa mataifa haya utaendelezwa.

Akizungumza na Naibu Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania Mhe. Tax ameipongeza kampuni hiyo kwa uwekezaji wao katika masuala ya Teknolojia hususan kupitia mradi wao wa kusambaza huduma za kidigitali vijijini.

“ Huawei ni Kampuni kubwa na tunathamini uwepo wenu hapa nchini. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ni mingoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo tutaendelea kushirikiana nanyi hususan kwenye kusambaza huduma za kidigitali vijijini na vyuoni ili hatimaye tuweze kufikia ndoto yetu ya kuwa kitovu cha kidigitali,” alisema Mhe. Dkt. Tax.

Kwa upande wake, Bw. Tao Mian alieleza kwamba hapa nchini Kampuni hiyo imetengeneza ajira zaidi ya 1000 ambapo zaidi ya asilimia 70 ya ajira ni za watanzania.Kadhalika Kampuni hiyo inashirikiana na  zaidi ya kampuni 70 za ndani, Wahandisi wa TEHAMA zaidi ya 2000 nchi nzima pamoja na vyuo zaidi ya 19 nchini. Aidha, Kampuni hiyo inaendesha mafunzo ya TEHAMA kwa zaidi ya wanafunzi 2000, kuhudumia zaidi ya asilimia 75 ya watanzania na kwamba imekuwa mchangiaji mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya TEHAMA nchini.

“Tunaridhishwa na uungwaji mkono wa Kampuni yetu hapa Tanzania na tunaahidi kuendelea kuchapa kazi ili kuhakikisha huduma za kidigitali zinawafikia wananchi wengi kwa wakati mmoja hususan wale wa vijijini” alisema Bw. Mian.

Pia alimueleza Mhe. Dkt Tax juu ya Mpango kabambe wa kuboresha mawasiliano ya TEHAMA vijijini ambao ni sehemu ya Mkataba wa ushirikiano uliosainiwa baina ya Tanzania na China ambao unatarajiwa kutekelezwa na Kampuni hiyo. Katika mradi huo kutakuwa na jumla ya miradi 19 ya kipaumbele, uboreshaji wa mawasiliano vijijini, usambazaji wa umeme Kaskazini Mashariki mwa Tanzania pamoja na miradi 9 ya msaada ambayo itatekelezwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA) na Hospitali ya Zanzibar.

Kampuni ya Huawei Tanzania ambayo imewekeza kwa zaidi miaka 15 nchini, inashirikiana na Kampuni ya Mawasiliano ya Simu Tanzania (TTCL) kusambaza Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ili kuwezesha huduma za kidigitali kupatikana kwa urahisi nchi nzima ambapo hadi sasa mkongo huo umesambaa kwa zaidi ya kilomita 15,000 nchi nzima.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa India nchini Mhe Binaya Pradhan, alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 10 Januari 2023
Mhe. Dkt. Tax akimsikiliza Balozi Mhe Binaya Pradhan wakati wa mazungumzo kati yao yaliyofanyika ofisini kwake jijini Dodoma. Kushoto ni Kaimu mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Halmenshi Lunyumbu.
Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa India nchini (kulia) akiwa na Naibu Balozi wa Ubalozi huo wakati wa mazungumzo kati yake na Mhe. Dkt. Tax
Mhe Binaya Pradhan, Balozi wa India nchini akimkabidhi Mhe. Dkt. Tax zawadi ya kasha la kuhifadhia vitu.
Mhe. Dkt. Tax akiagana na Balozi Mhe Binaya Pradhan mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao 
Mhe. Dkt. Tax na Mhe. Balozi Mhe Binaya Pradhan wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki mazungumzo yao 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea nchini, Mhe.  Kim Young Su alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 10 Januari 2023
Mhe. Dkt. Tax akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Kim Young Su 
Mazungumzo yakiendelea
Mhe. Dkt. Tax akiagana na Mhe. Kim Young Su mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao
Picha ya pamoja
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 10 Januari 2023
Mhe. Dkt. Tax akiendelea na mazungumzo na  Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Huawei Tanzania Bw. Tao Mian. Walioketi kushoto kwa Mhe. Waziri ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Magabilo Murobi na Afisa katika Idara hiyo, Bw. Herman Berege.
Picha ya pamoja
Mhe. Dkt. Tax akiagana na Bw. Tao Mian mar abaada ya kukamilisha mazungumzo yao



 

VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE AFRICAN UNION COMMISSION


 



Monday, January 9, 2023

DKT. TAX AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UFARANSA NA WAWAKILISHI WA MASHIRIKA YA KIMATAIFA YALIYOPO NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax   leo tarehe 09 Januari 2023 amekutana kwa mazungumzo kwa nyakati tofauti na wageni mbalimbali waliomtembelea ofisini kwake Mtumba  jijini Dodoma

Wageni hao ni Balozi wa Ufaransa nchini,  Mhe. Nabil Hajlaoui; Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi. Mahoua Parums; Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Bianadamu na Watu, Mhe. Jaji Iman Aboud na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna.

Akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Dkt. Tax amempongeza Mhe. Balozi Nabil Hajlaoui kwa hatua ya Ubalozi huo kufungua ofisi jijini Dodoma ikiwa ni ishara ya Ufaransa katika kuuunga mkono harakati za Serikali ya Tanzania za kuimarisha makao makuu ya nchi Dodoma.

“Mhe. Balozi nchi zetu zimekuwa na uhusiano wa kirafiki uliodumu tangu Tanzania ilipopata uhuru wake, na tumeendelea kuungana mkono katika ngazi ya nchi na hata kimataifa, na kwa hili mnalolifanya hapa Dodoma linadhihirisha kuimarika kwa ushirikiano wetu,” alisema Dkt. Tax

Akizungumza katika kikao hicho Balozi wa Ufaransa alisema nchi yake imeamua kufungua ofisi ya ubalozi jijini Dodoma kama njia mojawapo ya kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Ufaransa pamoja kuunga mkono hatua ya Serikali ya kuhamishia makao makuu yake jijini humo.

Ameongeza kusema mwezi Juni 2023 Ufaransa inatarajia kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Paris hadi Dar es Salaam kupitia Zanzibar. Itakumbukwa kuwa mwaka 2021 Shirika hilo lilianzisha safari zake Zanzibar kupitia Nairobi, Kenya.

Amesema kuanzishwa kwa safari hizo za moja kwa moja zitawawezesha watalii kutoka Ufaransa kuja moja kwa moja nchini na hivyo kupunguza urefu wa safari na hivyo kufanya watalii na wafanybiashara wengi kuja kuangalia fursa na kutembelea vivutio vya utalii nchini kwa urahisi.

Mhe. Balozi pia amesema Ubalozi pia utaendeloea kutoa mafunzo ya lugha ya kifaransa kwa watumishi wa umma ambapo ikwa kuanzia wanaendelea na mafunzo hayo kwa watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Ulinzi na katika Chuo cha Idara ya Uhamiaji mjini Moshi.

Mhe. Balozi pia ameongelea nia ya nchi yake kuunganisha nguvu na Tanzania katika sekta ya nishati mbadala ili kuiwezesha Tanzania kujitosheleza na nishati hiyo nchini na hivyo kukuza uchumi wake.

Katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi. Mahoua Parums, Mhe. Dkt. Tax amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na Shirika hilo katika zoezi linaloendelea la kuwarejesha kwa hiari wakimbizi kwenye nchi zao za asili.

Kwa upande wake, Bi. Parums ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuhifadhi wakimbizi licha ya changamoto mbalimbali zilizopo. Amesema Shirika lake linathamini mchango huo wa kibinadamu wa Tanzania kwa wakimbizi hao na kwamba litaendelea kushirikiana na Serikali katika kuwarejesha kwa hiari wakimbizi wa Burundi.

Akizungumza na Mhe. Jaji Iman wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Bianadamu na Watu, Mhe. Dkt. Tax amesema Serikali ya Tanzania kama mwenyeji wa Mahakama hiyo iliyopo Arusha itaendelea kutekeleza makubaliano ya mkataba wa uenyeji kama ulivyoainisha.

Naye Jaji Iman amemhakikishia ushirikiano Dkt. Tax na kwamba wanaipongeza Serikali kwa kuendelea kutekeleza makubaliano ya mkataba wa uenyeji ambapo  hadi sasa Mahakama hiyo imepatiwa eneo la ukubwa wa ekari 25 kwa ajili ya kujenga ofisi zake za kudumu jijini Arusha.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa UNICEF nchini ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kusimamia na kutekeleza kikamilifu mikataba mbalimbali ya Kimataifa inayohusu masuala ya haki za watoto ikiwemo afya, elimu na kuwalinda dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui pamoja na wajumbe walioambatana nao kwenye mazungumzo kati yao yaliyofanyika ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi. Bi. Mahoua Parums alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Mhe. Dkt. Tax akipokea zawadi ya machapisho mbalimbali kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi. Bi. Mahoua Parums alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Bianadamu na Watu, Mhe. Jaji Iman Aboud alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Mhe. Dkt. Tax akiwa katika mazungumzo na Mhe. Jaji Iman
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma tarehe 09 Januari 2023
Sehemu ya ujumbe wa Mhe. Dkt. Tax ukifuatilia mazungumzo kati yake na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna akimpatia Mhe. Dkt. Tax maelezo ya zawadi ya picha kabla ya kumkabidhi 

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna akimkabidhi Mhe. Dkt. Tax zawadi ya picha ya watoto kama ishara ya kuonesha mchango wa shirika hilo katika kuwahudumia watoto hapa nchini












































 

VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE COMMONWEALTH SECRETARIAT


 

NAFASI ZA MASOMO NCHINI JAPAN


 

Saturday, January 7, 2023

DKT. TAX AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO LA WIZARA MTUMBA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), ametembelea na kujionea namna ujenzi wa jengo la Wizara katika mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma  unavyoendelea.


Katika ziara hiyo ya ukaguzi Mhe. Dkt. Tax amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa jengo hilo kuongeza kasi ili ujenzi ukamilike kwa wakati.


“Nimetembelea hapa, nimejionea kazi ilipofika, kazi bado ni kubwa inabidi muongeze bidii zaidi ili Mungu akijaalia mwezi Oktoba mwaka huu badala ya Desemba ujenzi uwe umekamilika na tuone tunajipanga namna gani,” amesema Dkt. Tax.


Amesema Wizara ina uhitaji mkubwa wa jengo hilo kwa kuwa watumishi wametawanyika katika maeneo matatu tofauti na inakuwa ngumu  kukutana kwa haraka pale inapobidi.


Amesema kukamilika kwa jengo Hilo kutatoa ahueni kwa watumishi wa wizara na kuwawezesha kuwa sehemu moja na hivyo kurahisisha utendaji kazi wa Wizara.


Katika ziara hiyo Mhe. Waziri Dkt. Tax aliambatana na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine na watendaji wengine wa Wizara.


Ujenzi wa jengo la Wizara ulianza mwezi Januari 2022 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2023. Ujenzi huo utagharimu kiasi cha Shilingi  bilioni 22.9 ambazo zimetolewa na Serikali ili kuziwezesha Wizara na Taasisi za Serikali kuwa na majengo ya kudumu katika mji wa Serikali.


Ujenzi huo unafanywa na Umoja wa makampuni ya Sole works na mshauri elekezi ambaye ni Chuo Kikuu cha Ardhi. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisaini kitabu cha wageni alipowasili kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 07 Januari 2023

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisaini kitabu cha wageni akiwa ameambatana na Mhe. Dkt. Tax kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 07 Januari 2023

Mhe. Dkt. Tax akizungumza na wakandarasi wa jengo la  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipofika kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambapo aliwahimiza kuongeza kasi ya ujenzi wa jengo hilo.
Mhe. Dkt. Tax akizungumza na wakandarasi wa jengo la  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipofika kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambapo aliwahimiza kuongeza kasi ya ujenzi wa jengo hilo.


Sehemu ya Wakurugenzi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wamsikiliza Mhe. Dkt. Tax wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara katika Mji wa Serijkali Mtumba

Sehemu ya Wakurugenzi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wamsikiliza Mhe. Dkt. Tax wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara katika Mji wa Serijkali Mtumba

Sehemu ya Wakandarasi wanaosimamia ujenzi wa Jengo la Wizara wakimsikiliza Mhe. Dkt. Tax alipotembelea jengo la Wizara kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi
Mkandarasi anayesimamia ujenzi wa Jengo la Wizara akitoa maelezo kuhusu hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa jengo hilo ambapo kwa sasa limekamilika kwa asilimia 55.
Mkandarasi wa Jengo la Wizara akifafanua jambo kwa Mhe. Dkt. Tax kuhusu hatua mbalimbali za ujenzi wa jengo hilo kwa kuonesha picha
Mhandisi wa Wizara, Bw. John Kiswaga naye akitoa ufafanuzi kwa Mhe. Waziri Tax kuhusu maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara
Mhe. Balozi Mbarouk akiangalia sampuli ya fremu za milango na kusisitiza ujenzi huo uzingatie ubora wa hali ya juu wa vifaa vyote vitakavyotumika kama, mbao, vigae na marumaru.
Mhe. Balozi Mbarouk akisisitiza jambo kwa wakandarasi kabla ya kuanza ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara
Mhe. Dkt. Tax kwa pamoja na Mhe. Balozi Mbarouk wakiingia kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara lililopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma

Mhe. Dkt. Tax akipanda ngazi kuelekea ghorofa za juu za jengo hilo ili kukagua maendeleo ya ujenzi

Mhe. Dkt. Tax akimsikiliza Mkandarasi wa Wizara, Bw. Kiswaga wakati akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya ujenzi wa jengo la Wizara


Mhe. Dkt. Tax akitoa maelekezo kwa wakandarasi na kuwataka kuongeza kasi na kuzingatia ubora na viwango katika ujenzi wa jengo la Wizara
Mwonekano wa jengo la Wizara linaloendelea kujengwa katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma