Thursday, March 1, 2018

Waziri Mahiga akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Augustine Mahiga akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Alain Aime Nyamitwe alipomtembelea Wizarani, tarehe 1 Machi,2018, Dar es Salaam.

 Mhe. Waziri Mahiga,(Kulia) akizungumza jambo na Mhe. Waziri Nyamitwe katika mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Wizara, Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine walizungumzia jinsi ya kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na nchi ya Burundi.
Balozi wa Burundi nchini Mhe. Balozi Gervais Abayeho (wa kwanza kushoto), akifuatilia mazungumzo hayo, wengine wanaofuatilia mazungumzo, kutoka kulia  ni , Bw. Suleiman Saleh, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika. Bw. Wilbroad Kayombo na Bw. Erick Ngilangwa, Maafisa Mambo ya Nje,  na mwisho ni Katibu wa Waziri, Bw. Magabilo Murobi wakifuatilia mazungumzo hayo

Waziri Mahiga akiagana na mgeni wake Waziri Nyamitwe  baada ya kumaliza mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.