Thursday, May 10, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Japan nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Aldof Mkenda akisisitiza jambo katika mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Mhe.Masaharn Yoshida alipomtembelea na ujumbe wake Wizarani tarehe 10 May,2018, Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kuendelea kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Japan. Aidha, alimsisitiza Balozi kwa nafasi yake kuendelea kuhamasisha wawekezaji kutoka Japan kuendelea kuwekeza hapa nchini, alimhakikishia ushirikiano kutoka Serikalini iwapo watakuja kuwekeza hapa nchini.

Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan Idara inayosimamia masuala ya Afrika, Bi. Mariko Kaneko akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu katika mazungumzo hayo. Bi. Kaneko alisema Japan inafurahishwa na ukuaji wa haraka wa uchumi wa Tanzania hivyo nchi yake itaendelea kuiunga mkono Tanzania hasa kwa upande wa maendeleo ya Viwanda na miradi mbalimbali.


Mazungumzo yakiendelea


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.