Friday, May 17, 2019

Fursa za ajira

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NAFASI ZA AJIRA KATIKA SEKRETARIETI YA JUMUIYA YA MADOLA, LONDON, UINGEREZA.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inawahamasisha Watanzania wenye sifa kuomba nafasi ya ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, London, Uingereza.

Ajira hizo ni :-

Afisa Msaidizi Programu ya Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (Assistant Programmes Officer – Monitoring and Evaluation Unit) na

Meneja Utafiti wa masuala ya Uchumi, Vijana na Maendeleo Endelevu (Research Manager-Economic, Youth and Sustainable Development).

Taarifa zote muhimu kuhusu fursa hizo za ajira zinapatikana kwa kupitia  tovuti  http://thecommonwealth.org.jobs.

Mwisho wa kutuma maombi ya nafasi hizo ni tarehe 23 Mei, 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.