Waandishi
Waendesha Ofisi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
wametakiwa kutumia ujuzi walioupata kupitia mafunzo ya Ununuzi wa Umma kwa njia
ya Kielektroniki (NeST) kwa ufanisi na uwajibikaji ili kuboresha utendaji kazi
wao, kuongeza uwazi na kuimarisha mifumo ya ununuzi wa umma.
Kauli
hiyo imetolewa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Bw.
Kawina Kawina alipofunga mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara
Mtumba jijini Dodoma.
Bw.
Kawina amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha mfumo wa NeST unatumika
ipasavyo katika mchakato wa ununuzi wa vifaa na huduma mbalimbali wizarani.
Amefafanua kuwa serikali imewekeza katika mifumo ya kidijitali ili
kurahisisha utendaji kazi, kuongeza uwazi, na kupunguza mianya ya upotevu wa
rasilimali.
Vilevile amesisitiza kuwa maarifa waliyopewa hayapaswi kubaki kama nadharia pekee
bali wanapaswa kuyatumia kwa vitendo katika majukumu yao.
"Serikali
imewekeza katika mifumo hii kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji na kurahisisha
utendaji kazi. Hivyo ni muhimu kuhakikisha kuwa maarifa haya mliyoyapata
mnayatenda kwa vitendo ili kuongeza ufanisi wa ununuzi wa umma," alisema
Bw. Kawina
Aidha
amesisitiza kutumia mfumo huo kwa weledi, na kuwasihi kuwa mabalozi wazuri wa
NeST ndani ya wizara kwa kushirikiana na wenzao na kuhakikisha kuwa kila hatua
ya ununuzi inafuata taratibu na miongozo ya serikali.
Kwa
upande wao washiriki wa mafunzo hayo wameishukuru wizara kwa kuwawezesha kupata
ujuzi huo, na kuahidi kuutumia kwa ufanisi ili kuboresha utendaji wao wa kazi.
Washiriki
hao pia wamebainisha kuwa mafunzo hayo yamewapa uelewa wa kina kuhusu taratibu
za manunuzi kwa njia ya mtandao na namna ya kuhakikisha kila hatua inafuata
sheria.
Mafunzo
hayo ya siku tatu yamefanyika katika ukumbi wa Wizara, Dodoma kuanzia tarehe 18
hadi 20 Februari 2025.
Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Kawina Kawina akizungumza kwa niaba ya Menejimenti ya wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa hitimisho la mafunzo ya Manunuzi ya Umma ya Kielektroniki kwa Waandishi Waendesha Ofisi wa Wizara hiyo.
Picha ya pamoja
No comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.