Thursday, May 16, 2024

BALOZI MBAROUK AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA ETHIOPIA JIJINI DODOMA


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.



Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugeni wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ali Sakila Mbarouk akimpokea Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano alipowasili Wizarani  katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

 

Mkurugeni wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ali Sakila akimkaribisha Balozi wa Ethiopia nchin Mhe. Shibru Mamo alipowasili Wizarani  katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

 

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekutana na kuzungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Ethiopia kwa manufaa ya pande zote mbili.

Akizungumza na mgeni wake Mhe. Balozi Mbarouk amesema Tanzania inajivunia kuwa na uhusiano na ushirikiano imara na Ethiopia hali ambayo inazifanya nchi hizo kuendelea kushirikiana katika sekta za usafiri wa anga, nishati, Kilimo, Mifugo, Utalii, Ulinzi na Uhamiaji

Balozi Mbarouk amesema Tanzania itatumia uhusiano wake na Ethiopia kukuza biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili.

Balozi Mbarouk pia ameipongeza Ethiopia kwa kuwa nchi ya kwanza kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi zake za Ubalozi na makazi ya Balozi katika eneo ambalo Serikali ya Ethiopia ilipewa na Serikali ya Tanzania.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Ayano amesema Ethiopia inaiona Tanzania Kama mdau mühimu wa kushirikiana naye kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji  na kuendeleza uhusiano uliopo.

Amesema amekuja Tanzania kwa kazi ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Ubalozi  na makazi ya Balozi wao katika makao makuu ya Tanzania jijini Dodoma.

“Ethiopia ni makao makuu ya Umoja wa Afrika , sisi ni viongozi na tunataka kuendelea kuwa mfano kwa nchi za Afrika na nyingine kwa kuwa wakwanza kuwa na jengo letu hapa Mtumba,” alisema Balozi Ayano.

Ameongeza kuwa Ethiopia inaamini kuwa kitendo cha wao kuweka jiwe la msingi na kuanza Ujenzi wa majengo hayo kutaendelea kuimarisha uhusiano wake na Tanzania.

Mhe Balozi Ayano yuko nchini kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanja cha Ubalozi kilichopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Ethiopia inakuwa nchi ya kwanza kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi za Ubalozi na makazi ya  Balozi tangu Serikali ya Tanzania ilipohamia jijini Dodoma Makao Makuu ya Serikali mwaka 2017.

China, Ujerumani, Ufaransa, Uingereza , Marekani na Umoja wa Mataifa na Mashirika yake yana Ofisi ndogo jijini Dodoma zilizofunguliwa baada ya Serikali kuhamia jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.