Saturday, May 18, 2024

MKUTANO WA 16 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI WA FEDHA WA EAC WAFANYIKA ARUSHA

Mkutano wa 16 Wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki umefanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha Tanzania. Mkutano huo ulitanguliwa na mikutano ya ngazi ya watalaam na Mkutano wa Makatibu Wakuu iliyofanyika kuanzia tarehe 13 hadi 16 Mei 2024.


Mkutano wa SCFCEA ulifanyika sambamba na mkutano wa Mashauriano ya Kibajeti wa Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha. Mwenyekiti wa Mkutano huo alikuwa Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb.), Waziri wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mhe. Saadah Mkuya (Mb.), Waziri wa Nchi. Ofisi ya Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kuhudhuriwa pia na Mhe. Stephen Byabato (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki.


Mkutano huo ulipokea na kujadili taarifa ya Utekelezaji wa maamuzi ya mkutano wa 15 wa (SCFEA) pamoja na masuala mbalimbali. Aidha, Nchi Wanachama ziliwasilisha Miongozo ya Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Kaulimbiu za bajeti kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 ambapo Mkutano huo pia ulipitisha Kaulimbiu ya bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2024/2025 na kupitisha tarehe 13 Juni 2024 kuwa tarehe ya kusoma bajeti za nchi wanachama.


Vilevile, Mkutano huo ulipitisha Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili baina ya Nchi Wanachama na Mkataba Kifani wa Kuongoza Majadiliano baina ya Nchi za EAC na nchi nyingine



Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (katikati) akiongoza  Mkutano wa Mashauriano ya Kibajeti wa Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  uliofanyika sambasamba na  Mkutano wa 16 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha. Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa SCFEA uliongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Mhe. Saada Mkuya na kumshirikisha pia Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Alphayo Kidata na viongozi wengine waandamizi wa Serikali

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (katikati) akichangia jambo wakati wa  Mkutano wa 16 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha. Kushoto ni kiongozi wa ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo, Mhe. Waziri Mkuya na kulia ni Dkt. Mwamba

Mkutano ukiendelea

Viongozi wakiwa wamesimama wakati wa ufunguiz wa mkutano

Wajumbe wa mkutano wakifuatilia

Mkutano ukiendelea

Wajume wakifuatilia mkutano

Picha ya pamoja


 

Friday, May 17, 2024

TANZANIA, CHINA ZAINGIA ZAMA MPYA KIDIPLOMASIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. WANG Yi walipokutana Ofini kwakwe jijini Beijing kwa mazungumzo. Terehe 17 Mei 2024

  • Nia ni kujenga dunia yenye usawa 
  • China yafuta machozi waathirika wa mafuriko
  • Yamwalika Rais Samia Septemba
  • Hadhi ya Chuo cha Dk. Salim kupanda
BAADA ya miaka 60 ya uhusiano wa kihistoria, Tanzania na China leo zimetangaza kuingia katika zama mpya za uhusiano wa kidiplomasia ambao lengo lake ni kujenga dunia iliyo bora zaidi, yenye maendeleo zaidi na usalama zaidi.

Katika mkutano wa pamoja uliofanyika jijini Beijing, China, leo Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, alimweleza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba, kwamba katika miaka 60 iliyopita tangu kuanza kwa uhusiano nchi hizi mbili, Tanzania imejipambanua kama rafiki wa kwenye shida na raha.

“Tanzania mara zote amekuwa rafiki za China. Kwa China, miaka 60 ina maana kubwa sana kwenye uhusiano. Hatua inayofuata sasa baada ya hapa ni kuendeleza uhusiano huu katika zama mpya za kujenga dunia yenye maendeleo, ya haki na iliyo na usalama kwa watu wote” alisema Wang.

Waziri Makamba yuko nchini China kwa ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa mwenzake huyo na alitumia nafasi hiyo pia kueleza namna Tanzania inavyothamini mchango wa taifa hilo la bara la Asia katika maendeleo yake na kwamba wakati umefika sasa wa kuingia katika zama mpya kuendana na changamoto za dunia ya sasa.

“China ni rafiki zetu kwenye nyakati zote. Ni rafiki ambaye anatabirika na habadilikibadiliki wakati wote. Baada ya miaka hii 60 ya uhusiano uliotukuka, sasa tuingie katika zama mpya za uhusiano ambao utazingatia changamoto zilizopo kwenye kujenga dunia bora zaidi kuliko ile iliyokuwepo wakati wa waasisi wa uhusiano huu” alisema.

Katika kuonyesha uhusiano wa karibu baina ya wananchi wa mataifa hayo, Waziri Wang alisema China inatoa mchango wa dola 500,000 za Marekani, sawa na shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko ya mvua yaliyoikumba Tanzania mwaka huu.

Maeneo kadhaa ya Tanzania yameathiriwa na mvua kubwa za masika zilizochanganyika na zile za El Nino na Waziri huyo wa China alisema Wachina wamesikia kuhusu athari hizo na wametoa mchango huo ili kusaidia waathirika kuanza upya maisha yao. Waziri Makamba alishukuru kwa mchango huo akisema ni ushahidi mwingine wa urafiki wa kipekee baina ya nchi hizo mbili.

Katika hatua nyingine, Serikali ya China leo imetoa mwaliko rasmi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhudhuria mkutano wa masuala ya usalama baina ya China na Afrika (FOCAC) uliopangwa kufanyika Septemba mwaka huu.

Mkutano wa FOCAC hufanyika kila baada ya miaka mitatu na katika miaka ya karibuni umekuwa ni miongoni mwa mikutano muhimu kwenye uhusiano wa kimkakati baina ya nchi za Afrika na China.

Kadhalika, China imekubali ombi la Tanzania la kufanya maboresho ya Chuo cha Diplomasia cha Dkt. Salim Ahmed Salim ikiwemo kuongeza majengo, kuongeza mitaala na kukifanya kuwa cha kutengeneza ajenda kwa ajili ya masuala ya kimkakati ya kubadili mfumo wa uendeshaji wa dunia.

Dk. Salim ni mmoja wa wana diplomasia wa Tanzania wenye heshima kubwa nchini China na uamuzi wa kuongeza hadhi ya chuo hicho umezingatia hadhi yake kidiplomasia na umuhimu wake kwa nchi hizi mbili.

Katika ziara yake hiyo inayoendelea nchini China, Makamba ambaye ameambatana na Mhe. Zahor Haji Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), alitembelea na kufanya mazungumzo na taasisi na viongozi wa mashirika yanayohusika na misaada kwa Tanzania ikiwemo benki ya EXIM ambayo imeahidi kuendelea kukopesha kwenye miradi ya kimkakati.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akisalimiana na Rais wa Benki ya Exim ya China Bw. Ren Shengjun walipokuna kwa mazungumzo jijini Beijing, China
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akisalimiana na Mwenyekiti wa Shirika la Ushikiano wa Maendeleo ya Kimataifa (CIDCA) Bw. Luo Zhaohui walipokutana kwa mazungumzo Ofini kwakwe jijini Beijing, China.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. WANG Yi na ujumbe wao wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika jijini Beijini, China. 
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. WANG Yi akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba yaliyofanyika jijini Beijing, China.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba na Mwenyekiti wa Shirika la Ushikiano wa Maendeleo ya Kimataifa (CIDCA) Bw. Luo Zhaohui na ujumbe wao wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika jijini Beijing, China.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Rais wa Benki ya Exim ya China Bw. Ren Shengjun yaliyofanyika jijini Beijing, China
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. WANG Yi yaliyofanyika jijini Beijing, China
azungumzo kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba na Rais wa Benki ya Exim ya China Bw. Ren Shengjun yakiendela jijini Beijing, China
Picha ya pamoja

ETHIOPIA YAFUNGUA NJIA UJENZI WA UBALOZI DODOMA

Serikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia katika Mji wa Serikali Dodoma ya kuwa nchi ya kwanza kujenga majengo ya Ofisi na Makazi ya Balozi na kuzitolea wito nchi nyingine kuiga mfano huo.

 

Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethipia, Mhe, Birtukan Ayano ambapo kwa pamoja waliweka Jiwe la Msingi la ujenzi huo kwa niaba ya Serikali zao katika hafla iliyofanyika jijini Dodoma leo Mei 17, 2024.

 

Balozi Mbarouk alieleza kuwa uwekaji wa jiwe la msingi huo ni kielelezo tosha cha kuimarika kwa ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Ethiopia ambao ulianza tangu enzi za waasisi wa mataifa haya, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Haile Selassie.

 

Balozi Mbarouk alisisitiza umuhimu wa kukuza biashara baina ya nchi hizi mbili kwa kuwa kiwango cha biashara kinachofanyika hivi sasa hakiakisi uhusio mzuri uliopo baina ya mataifa hayo mawili.

 

Kwa upande wake, Mhe. Ayano alisema uwekaji wa jiwe la msingi huo ni ishara ya ushirikiano mzuri uliopo baina ya nchi hizi mbili na dhamira ya dhati ya Serikali ya Ethiopia ya kuuimarisha zaidi, hususan katika nyanja ya biashara na uwekezaji.

 

Hafla ya uwekaji jiwe la msingi ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule ambapo aliwahakikishia jumuiya ya wanadiplomasia nchini kuwa Dodoma ipo tayari kuwapokea na miundombinu ya kijamii ikwemo maji, elimu, afya na usafirishaji, Serikali inaendelea kuijenga na kuiboresha iliyopo. 

 

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Nderiananga; Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Vicent Mbogo, Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Mussa, Meya wa Halimashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe na viongozi waandamizi wa Serikali

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Mhe. Balozi Birtukan Anayo wakifungua kitambaa kuonesha jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kuweka jiwe hilo huku wakishuhudiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida, Makamu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama na viongozi wengine wa Chama na Serikali.
 
Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Mhe. Balozi Birtukan Anayo wakionesha jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kuweka jiwe hilo huku wakishuhudiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida, Makamu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama Mhe. Vicent Mbogo na viongozi wengine wa Chama na Serikali. 
Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Balozi wa Ethiopia nchini Tanzania Mhe. Shibru Memo Kadida akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma
 
Wajumbe wa Meza kuu wakifuatilia hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa (kushoto) na Meya wa Jiji la Dodoma prof. Davis Mwamfupe wakifuatilia hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama Mhe. Vicent Mbogo, (kulia) Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (wa pili kulia)  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga (katikati) Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Balozi Birtukan Ayano na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule wakimsikiliza mtaalamu wa kampui iiyoandaa mchoro wa jengo la Ubalozi wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa jengo hilo katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Mhe. Balozi Birtukan Anayo katika picha ya wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kuweka jiwe hilo wengine ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida, Makamu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama na viongozi wengine wa Chama na Serikali.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Mhe. Balozi Birtukan Anayo katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kuweka jiwe hilo huku wakishuhudiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida, Makamu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama na viongozi wengine wa Chama na Serikali.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) akiagana na Naibu Waziri Mambo ya Nje Ethiopia Mhe. Balozi Birtukan Anayo baada ya kukamilika kwa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Ethiopia katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kuweka jiwe hilo huku wakishuhudiwa na Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa.

 

Thursday, May 16, 2024

BALOZI MBAROUK AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA ETHIOPIA JIJINI DODOMA


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.



Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano alipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugeni wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ali Sakila Mbarouk akimpokea Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano alipowasili Wizarani  katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

 

Mkurugeni wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ali Sakila akimkaribisha Balozi wa Ethiopia nchin Mhe. Shibru Mamo alipowasili Wizarani  katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

 

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekutana na kuzungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Birtukan Ayano ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Ethiopia kwa manufaa ya pande zote mbili.

Akizungumza na mgeni wake Mhe. Balozi Mbarouk amesema Tanzania inajivunia kuwa na uhusiano na ushirikiano imara na Ethiopia hali ambayo inazifanya nchi hizo kuendelea kushirikiana katika sekta za usafiri wa anga, nishati, Kilimo, Mifugo, Utalii, Ulinzi na Uhamiaji

Balozi Mbarouk amesema Tanzania itatumia uhusiano wake na Ethiopia kukuza biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili.

Balozi Mbarouk pia ameipongeza Ethiopia kwa kuwa nchi ya kwanza kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi zake za Ubalozi na makazi ya Balozi katika eneo ambalo Serikali ya Ethiopia ilipewa na Serikali ya Tanzania.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Balozi Ayano amesema Ethiopia inaiona Tanzania Kama mdau mühimu wa kushirikiana naye kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji  na kuendeleza uhusiano uliopo.

Amesema amekuja Tanzania kwa kazi ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Ubalozi  na makazi ya Balozi wao katika makao makuu ya Tanzania jijini Dodoma.

“Ethiopia ni makao makuu ya Umoja wa Afrika , sisi ni viongozi na tunataka kuendelea kuwa mfano kwa nchi za Afrika na nyingine kwa kuwa wakwanza kuwa na jengo letu hapa Mtumba,” alisema Balozi Ayano.

Ameongeza kuwa Ethiopia inaamini kuwa kitendo cha wao kuweka jiwe la msingi na kuanza Ujenzi wa majengo hayo kutaendelea kuimarisha uhusiano wake na Tanzania.

Mhe Balozi Ayano yuko nchini kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanja cha Ubalozi kilichopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Ethiopia inakuwa nchi ya kwanza kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi za Ubalozi na makazi ya  Balozi tangu Serikali ya Tanzania ilipohamia jijini Dodoma Makao Makuu ya Serikali mwaka 2017.

China, Ujerumani, Ufaransa, Uingereza , Marekani na Umoja wa Mataifa na Mashirika yake yana Ofisi ndogo jijini Dodoma zilizofunguliwa baada ya Serikali kuhamia jijini Dodoma.