![]() |
Picha ya pamoja |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
![]() |
Picha ya pamoja |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Makao Makuu Dodoma pamoja na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, wameungana na wanawake kutoka ofisi mbalimbali za umma na binafsi jijini Dodoma kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake duniani kwa mwaka 2025.
Maadhimisho hayo, ambayo hufanyika kila Machi
8, yameandaliwa kwa lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii na
kuhimiza usawa wa kijinsia.
Maadhimisho hayo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu isemayo: "Wanawake na Wasichana Tuimarishe Haki, Usawa na Uwekezaji."
Kaulimbiu hiyo inalenga kusherehekea mafanikio ya wanawake, kujadili changamoto wanazokabiliana nazo, na kutafuta njia za kuimarisha haki, usawa, na uwekezaji kwa maendeleo endelevu.
Mgeni rasmi katika
maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mheshimiwa Alhaj Jabir
Shekimweri, ambaye alisisitiza umuhimu wa haki za wanawake na ushiriki wao
katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
Aidha, alieleza kuwa serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha wanawake wanapata fursa sawa katika elimu, uchumi, na uongozi.
Mheshimiwa Shekimweri alitoa wito kwa jamii kuendelea kupinga ukatili wa kijinsia na kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi stahiki kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa taifa. “Tukiwekeza kwa wanawake na wasichana, tunaiwekeza jamii katika maendeleo endelevu. Haki na usawa si jambo la hiari bali ni msingi wa maendeleo ya taifa letu,” alisema Shekimweri.
Pia, amewahimiza wadau kushirikiana kuwawezesha wanawake kiuchumi na kielimu na kusisitiza kuwa haki inapaswa kwenda sambamba na wajibu, akiwataka wanawake na wasichana kuwa mstari wa mbele kutumia fursa zinazotolewa kwa nidhamu, bidii, na maadili mema.
Aliongeza kuwa matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ni muhimu katika kudumisha maadili ya Kitanzania, huku akihimiza jamii kutumia teknolojia kwa maendeleo chanya.
Katika maadhimisho hayo, wanawake kutoka sekta mbalimbali walishiriki uzoefu wao na kutoa hamasa kwa wenzao juu ya njia bora za kufanikisha malengo yao. Pia, vikundi vya ujasiriamali vilipata nafasi ya kuonyesha bidhaa zao, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha uwekezaji kwa wanawake na kuwawezesha kiuchumi.
Maadhimisho hayo yaliambatana na michezo mbalimbali, ambapo washindi walitunukiwa medali na vikombe kama ishara ya kutambua juhudi zao na mchango wao katika jamii. Kaulimbiu ya mwaka huu inaendelea kuwa mwangaza kwa wanawake na wasichana kote nchini, ikiwahimiza kuimarisha haki, usawa, na uwekezaji kwa ustawi wa jamii na maendeleo endelevu ya taifa.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mheshimiwa Alhaj Jabir Shekimweri, akitoa hotuba kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, yaliyofanyika kimkoa, jijini Dodoma, katika viwanja vya Chinangali Park.
Ujumbe wa Serikali ya Finland umetembelea Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma na kukagua kiwanja kilichotengwa kwa ujenzi wa ubalozi wa nchi hiyo katika eneo hilo la Mji wa Serikali.
Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Finland katika kuhakikisha inaimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati yake na Tanzania.
Ujumbe huo umeongozwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kusini katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland, Bi. Helena Airaksinen, ambaye aliambatana na Balozi wa Finland nchini Mhe. Theresa Zitting.
Baada ya ukaguzi wa eneo hilo, Bi. Airaksinen alieleza kuridhishwa kwake na mazingira ya kiwanja hicho, akibainisha kuwa kinatoa fursa kwa Finland kuendelea kuimarisha uwepo wake nchini Tanzania.
Aidha, alisifu jitihada za Serikali ya Tanzania katika kuboresha miundombinu ya Mji wa Serikali Mtumba ili kuwezesha shughuli za kidiplomasia na utoaji wa huduma mbalimbali za serikali.
Kwa upande wake, Mhe. Balozi Zitting alisisitiza dhamira ya Finland ya kuendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali, hususani katika sekta za maendeleo, biashara, na diplomasia.
Alieleza kuwa hatua ya nchi yake kujenga ubalozi makao Makuu ya Serikali Dodoma ni ishara ya ushirikiano imara kati ya nchi hizo mbili.
Katika ziara hiyo, ujumbe wa Finland pia ulitembelea maeneo mbalimbali katika Mji wa Serikali Mtumba zikiwemo ofisi za serikali na maeneo yanayoendelea kuendelezwa na hivyo kupata fursa ya kujionea kwa kina mwelekeo wa serikali katika kuimarisha utendaji wa taasisi zake.
Ujumbe wa Tanzania katika ziara hiyo ulijumuisha maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Ofisi ya Jiji la Dodoma.
Maafisa hao waliwasilisha taarifa kuhusu maendeleo ya Mji wa Serikali na juhudi zinazoendelea kufanywa ili kuhakikisha unakuwa kitovu cha shughuli za serikali na kidiplomasia nchini.
Ziara hii inaashiria hatua muhimu katika kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Finland, huku ujenzi wa ubalozi wa Finland jijini Dodoma ukitarajiwa kuimarisha zaidi ushirikiano wa kidiplomasia na maendeleo kati ya nchi hizo mbili.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kusini katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland, Bi. Hellena Airaksinen(Kushoto) na Balozi wa Finland nchini Mhe. Theresa Zitting (kulia).