Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) na uongozi wa Chuo hicho umetembelea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Ziara hiyo ya mafunzo imelenga kutoa nafasi kwa Wanafunzi hao kujifunza kuhusu historia ya Wizara , Sera ya Mambo ya Nje na majukumu yanayotekelezwa na Wizara kwa wakati huu.
Akizungumza wakati wa kuwakaribisha Wanafunzi hao Wizarani Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo alielezea juu ya mabadiliko ya Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 ambayo alieleza kuwa yamefanyika ili kuiwezesha Sera hiyo kuendana na mahitaji ya wakati uliopo na huku ikikidhi mahitaji ya wakati ujao.
“Tunayo Sera ya Mambo ya Nje ambayo tulitengeneza mwaka 2001 lakini sera hiyo sasa tumeifanyia maboresho ili iweze kuendana na mabadiliko mbalimbali ambayo yametokea duniani" alisema Balozi Shelukindo.
Alisema maboresho hayo yataiwezesha Sera ya Mambo ya Nje kukidhi mahitaji ya wakati huu na wakati ujao.
Balozi Shelukindo pia alisisitiza kuwa pamoja na maboresho hayo bado Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania imeendelea kusimamia katika misingi yake ile ile ya ujirani mwema, kutokufungamana na upande wowote, kutokuonea wanyonge, kuwa na Afrika yenye Umoja, na kutekeleza malengo ya Maendeleo ya Umoja wa mataifa.
Balozi Shelukindo ametumia nafasi hiyo kuihakikishia NDC kuwa Wizara itaendelea kushirikiana nao wakati wote ili kuhakikisha NDC inaendelea kuwa kituo bora cha mafunzo nchini na kutoa Wanafunzi mahiri kwa manufaa ya Taifa.
Akizungumza wakati wa utambulisho wa wanachuo hao Mkuu wa Chuo cha NDC Meja Jenerali Balozi Wilbert Ibuge alisema wanafunzi waliotembelea Wizarani ni wa kozi ya 13 kwa mwaka 2024/2025 ambapo 40 wanatoka Jeshini na katika Wizara, Idara na Taasisi za Umma nchini na Wengine 21 wanatoka katika nchi rafiki za Bangladesh, Botswana, Burundi-2, Ethiopia, Misri-2, India, Kenya-2, Malawi, Namibia,Nigeria,Rwanda-2, Sierra Leone, Afrika Kusini, Uganda, Zambia-2 na Zimbabwe.
Amesema ziara ya wanafunzi hao Wizarani imelenga kuwapatia wanachuo hao mafunzo kwa vitendo ikizingatiwa kuwa masuala ya mambo ya nje na sera ya mambo ya nje ni miongoni mwa masuala Makuu ambayo wanafundishwa chuoni hapo.
“Chuo chetu katika kozi hizo za Ulinzi na Strategia focus yetu kubwa ni kuhusu masuala ya ulinzi na mambo ya nje na hapa wamekubaliana Leo ili asilia kutoka kwa wahusika ambao wanatekeleza majukumu hayo kwa vitendo".
![]() |
Picha ya pamoja |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
Sehemu ya Wanafunzi wa kozi ya 13 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) |
![]() |
No comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.