Tuesday, July 23, 2024

MKUTANO WA 117 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA JUMUIYA YA NCHI ZA AFRIKA, CARIBBEAN NA PASIFIKI (OACPS) WAANZA JIJINI BRUSSELS

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo wa 117 ulioanza tarehe 23 Julai 2024, kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Bw. Msafiri Mbibo akifuatilia mkutano huo. 


Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 

Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 

Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 


Mkutano ukiendelea 

Mkutano ukiendelea  kutokea jijini Brussels


Mkutano ukiendelea  kutokea jijini Brussels



Mkutano wa 117 wa Baraza la Mawaziri la nchi za nchi za Jumuiya ya nchi za Afrika, Caribbean na Pasifiki (OACPS) Unachofanyika kwa mfumo wa mseto kuanzia tarehe 23 hadi 26 Julai 2024 umeanza jijini Brussels, Ubelgiji. 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede , anaongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo wa 117 ulioanza tarehe 23 Julai 2024. 

Mkutano huo pia unafuatiliwa kwa njia ya mtandao na Balozi wa Tanzania Brussels Mhe. Jestas Nyamanga na Maafisa waandamizi kutoka Wizara za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha, Viwanda na Biashara, Uvuvi, Mifugo, Madini, na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mkutano huo wa kwanza kwa mwaka huu unajadili maendeleo muhimu ya ushirikiano kati ya wanachama katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa pamoja na kuwa jukwaa la kuboresha mikakati ya kikanda na kimataifa ili kuimarisha maendeleo endelevu na ushirikiano wa kimaendeleo kati ya nchi za OACPS. 

Mkutano huo pia utatoa fursa ya kuimarisha uhusiano na Umoja wa Ulaya kupitia majadiliano ya Mkataba wa Ushirikiano wa Samoa ambao unalenga kuboresha biashara uwekezaji na ushirikiano wa kisiasa kati ya nchi za OACPS na Umoja wa Ulaya.

Mkutano huo unatarajiwa kujadili na kupitisha bajeti ya OACPS kwa mwaka 2024, kupitia na kujadili taarifa za fedha za OACPS ikiwemo taarifa ya uchaguzi wa hesabu za Jumuiya, kujadili utekelezaji wa Mkataba wa Ubia  kati ya OACPS na Umoja wa Ulaya kuhusu mkataba wa Samoa, kujadili taarifa ya ununuzi wa jengo jipya la Ofisi za OACPS na kujadili taarifa ya mkutano wa Mawaziri wa Madini na Nchi za OACPS uliofanyika Cameroun kuhusu uendelezaji wa madini ya kimkakati kwenye nchi wanachama.

Mkutano huo wa Baraza la Mawaziri hukutana mara mbili kwa mwaka kujadili na kuamua kuhusu masuala mbalimbali ya jumuiya ni jukwaa muhimu kwa Mawaziri wa nchi hizo kubadilishana mawazo na kufanya maamuzi kuhusu matukio na maendeleo muhimu yaliyotokea katika kipindi cha kuanzia Juni 2023 hadi Juni 2024 ambako masuala na fursa muhimu zinazohitaji uelewa wa pamoja na mwelekeo wa kimkakati wa Mawaziri wa OACPS yalitokea.

Wajumbe wa sasa wa Baraza hilo la Mawaziri linaundwa na nchi za Jamaica- Rais, Liberia- Rais anayeondoka, Jamhuri ya Kongo, Rais ajaye, Sudan- Inawakilisha Afrika Mashariki, Angola Inawakilisha Kusini mwa Afrika, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-Inawakilisha Afrika ya Kati, Burkina Faso, Inawakilisha Afrika Magharibi,Haiti Inawakilisha nchi za Karibiani na Vanuatu Inawakilisha nchi za Pasifiki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.