Thursday, June 20, 2024

RAIS WA GUINEA BISSAU KUFANYA ZIARA RASMI NCHINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akitangaza rasmi ziara ya Rais wa Guinea Bissau, Mhe. Umaro Sissoco Embaro itakayofanyika nchini kuanzia tarehe 21 hadi 23 Juni 2024. Ziara hiyo pamoja na mambo mengine inalenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Guinea Bissau. Balozi Shelukindo ametangaza ziara wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofamyika jijini Dar es Salaam tarehe 20 Juni 2024

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ali Sakila (kulia) akifuatilia Mkutano kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Shelukindo (hayupo pichani) na Wandishi wa Habari akitangaza kuhusu ziara ya Rais wa Guinea Bissau, Mhe. Umaro Sissoco Embalo itakayofanyika nchini kuanzia tarehe 21 hadi 23 Juni 2024

Mkutano ukiendelea


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.