Tuesday, June 26, 2018

Waziri Mahiga akutana kwa pamoja na Balozi wa Uingereza na Kaimu Balozi wa Marekani nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akisalimiana na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Dkt. Inmi Patterson akiwa amefuatana na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Sarah Cooke mara walipomtembelea na kufanya nae mazungumzo kwenye Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje zilizopo Jijini Dar es Salaam 
Dkt. Mahiga akisalimiana na Mhe. Balozi Cooke.
Dkt. Mahiga akimsikiliza Mhe. Balozi Cooke alipokuwa akimweleza jambo wakati wa mazungumzo yao
Sehemu ya ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe Waziri Mahiga na Balozi Cooke (hawapo pichani). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya  Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga, Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu ( kulia) pamoja na Anthony Mtafya, Afisa Mambo ya Nje
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Dkt. Patterson ( kulia) pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Ubalozi wa Marekani na Uingereza nchini wakisikiliza kwa makini mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Cooke (hawapo pichani).
Mkutano ukiendelea.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.